Mahakama yabatilisha makubaliano ya mgawanyo mirathi ya Mengi

Mahakama yabatilisha makubaliano ya mgawanyo mirathi ya Mengi

Kama hujui sheria uliza wanaozijua wakusaidie kwa ukweli.

kisheria, hasa sheria za Mirathi kwa Tanzania, Kinachoangaliwa ni Mali alizoacha Marehemu na warithi wa Marehemu basi.

Nitatoa mfano. Mkikaa kikao cha Mirathi, cha kwanza mtajadili Mali alizoacha Marehemu na warithi wake. Sasa sifa ya warithi haitegemei umri na mchango wake kwenye mali za marehemu.

Warithi halali ,unaanza na Mke wa Marehemu, Watoto wa Marehemu na wazazi wa Marehemu. Sasa haijalishi huyo Mke umemwoa lini na ukiwa na mali kiasi gani. Kinachoangaliwa ni hadhi yake kama ni Mke wa marehemu basi.

Anaweza kuwa Mke umemuoa ndani ya mwaka mmoja na amekuta karibu mali zote umechuma mwenyewe, Ukifa anapata mgawo wake safi kama mrithi wa Marehemu....... Msichanganye mambo ya Mirathi na sheria za ndoa katika mgawanyo wa mali pale ndoa zinapovunjika.
Aliyekuambia mm nimejikita kwenye sheria ni nani? Kama sheria ingekuwa kila kitu huko magerezani pasingekuwepo na wafungwa walioonewa.
 
Kwenye pesa hata wasaidizi wanajitokeza wa kutosha...hapo haishangazi kukuta kuna jopo la Watu zaidi ya kumi wanapiga kazi.
😂😂😂😂😂😂 wanajua kesi ikiisha ni hela ndefu sana
 
Tsh jifunze hapo. Mkishafika mahakamani maamuzi binafsi yanabaki moyoni mwako.
911 mm sijali sheria inasemaje. Nimetoa angalizo kuwa linapokuja suala la mali, umakini wa maamuzi unahitajika. Sheria inaweza mbeba asiyestahili anayestahili akaaply sheria binafsi.
 
Naona mahakama inataka kurefusha shauri. Hii kitu ipo wazi na wala haina haja ya kuanza kurumbana mahakamani. Sijui kwa sheria zetu zimekaaje lakini kwa akili ya kawaida, mali isiyo ya marehemu haihusiki katika mirathi ya marehemu. Yaani huwezi kurithi kisicho halali yako!
Tatizo dah! Mother yule wa kwanza hawajafikia makubaliano ya kulipana ila kiuhalisia wamepambana na kutoka mbali sana ivi mahakama ni za kimchongo zaidi bora waangalie zaidi jinsi watagawanya vip Mali kwa mke wa kwanza kisheria then asilimia za mengi ndo jack apate na wanae...Hapa naona ujanja wa wanasheria kuleta mlolongo mrefu ila kupiga pesa ndo kazi yao
 
Huyu dada sidhani kama ana hiyo IQ ya kurisk kukwapua jasho la watu ambalo yeye hakuwa sehemu ya kulitafuta. Kuna watu huenda wanamtumia. Tatizo la kutumiwa ni pale unapoachwa mwenyewe.

Anatumika vipi.. kwani mengi alitumwa amtongoze jack. Ama alishikiwa bunduki amzalishe watoto na kufunga nae ndoa.

Sasa mke halali akubali mali za mumewe zibebwe na wachache
 
Anatumika vipi.. kwani mengi alitumwa amtongoze jack. Ama alishikiwa bunduki amzalishe watoto na kufunga nae ndoa.

Sasa mke halali akubali mali za mumewe zibebwe na wachache
Kama ww ndiyo jackie ujumbe umeshauelewa maana unajua unachofanya.
 
Anatumika vipi.. kwani mengi alitumwa amtongoze jack. Ama alishikiwa bunduki amzalishe watoto na kufunga nae ndoa.

Sasa mke halali akubali mali za mumewe zibebwe na wachache
Hapo sasa.
Mengi hakuwa underage alipomtongoza, kuzaa naye na kumuoa Jack.
Na bila shaka alijua consequences akianza kufa yeye.
Kuna jamaa mmoja wa Kaskazini siku moja nazungumza naye kwa hasira sana anasema Mengi wanatoka naye sehemu moja na anamheshimu sana Mzee Mengi halafu anasema 'huyo malaya hatakiwi kupata kitu'.
Nikamwambia acha mihemko ya kijinga, kama unamheshimu Mzee Mengi ulipaswa umheshimu pia Mke wake. Huwezi kusema unamheshimu Mtu halafu unamtukana mke wake, na kama alikuwa anaona mke wa Mzee Mengi malaya angepaswa ayaseme hayo kwa Mzee akiwa hai.
 
Hili la kukaa nje ya mahakama na kukubaliana ndilo la msingi.
Huko nyuma nilikuwa nawaambia Watu hili jambo si rahisi wanavyofikiria. Wengi walikuwa wanachangia kwa mihemko, kwamba Jack hakuchuma mali kwa hiyo akae kando Watoto wake watatunzwa na Watoto wakubwa wa Mengi.

1. Wanachosahau ni kuwa Jack ni mke halali wa Mengi (ndiyo maana katika mashauri yote hakuna mahali limepingwa)

2. Jack amezaa na Mengi watoto wawili. Watoto ambao ni haki yao kurithi mali za Baba yao ambaye ni Mzee Mengi

3. Na kwa kuwa Watoto wa Jack ni Watoto halali wa Mzee Mengi na hawajafikisha umri wa miaka 18 mnaweza kujua nani anastahili kusimamia haki zao.

Wosia uliodaiwa kuandikwa na Mengi ulitupiliwa mbali na mahakama. Kwa hiyo hapa mambo yanaanza upya ndiyo maana wakili wa Jack kaanza na kuhakikisha mali zote ambazo zilikuwa hazijagawanywa zinarudishwa pamoja halafu kesi ya mgao ianze upya. Hapa hata kama humpendi lakini huyo dada katumia mawakili wazuri.

Naona hapo la msingi wakae pamoja kwa kushirikiana na Wazee wenye busara na mgao ufanyike tu. Hata kama Jaclk hatapata kama ilivyosemwa kwenye ule wosia uliokataliwa, lakini obvious ataondoka na mgao mkubwa si haba.

Halafu sisi maskini humu JF acheni habari ya kuzungumzia kuhusu kuuliwa Jack.
Mzee Mengi hakuwa na historia ya aina hiyo. Wakati anamtongoza na kumuoa Jack, alifanya hayo yote akiwa na akili timamu na Mtu mzima. Tusitie kinyongo kwa mali zisizotuhusu.
Usiite watu maskini au matajiri, jisemee tu mwenyewe. Ulichoongea ni sahihi kabisa na sidhani kama huyu dada anatakiwa kuzulumiwa, angalizo ni yeye asije akawa anataka kuzulumu, na hilo lilionekana kwenye wosia wa kwanza. Kuhusu kuuwawa si mara ya kwanza kwa matukio kama hayo kutokea, Umakini unahitajika ili kuzuia mambo kama hayo yasitokee.
 
Ni hivi mkuu...kuna mgawo ambao tayar wanandoa walikubaliana wagawane 2015 lkn hawakufikia tamati...ambapo marehemu mke WA mengi ilishajulika angepata asilimia 35 ya mali....lkn wapalestina wakatKa bimkubwa apate 50 kitu ambacho kinakiuka makubaliano ya awali....hapo haki ya marehemu mke mkubwa ni 35....inayobakia unarudi Kwa mengi tayar Kwa mgao!
Niliwahi kumsikia Jacqueline akihojiwa na Ayo tv kama sikosei alidai Mengi na mtalaka walishagawana hisa zao na watoto walipewa 10% kila mmoja na hisa za Mercy zilikuja kurithiwa na wanawe ndipo Mzee Mengi aliamua kuacha wosia kwamba mali zake zigawanywe kwa Watoto wake aliozaa na Jacqueline pamoja na Jacqueline mwenyewe,sasa mbona sasa kuna maelezo tofauti?
 
Wazee wengi walio oa kwenye Umri wao wa Uzee, wengi baada ya kipindi Cha Chini ya Miaka 2 hupoteza Maisha. Tuna mifano mingi ikiwemo wa Juzi wa Mzee Mrema.

Baada ya hapo kinachofatia ni mgogoro wa Mali i.e Mirathi. Kuna wakati ukifikiri nje ya boksi ni kama Wanawake wanaokubali kuolewa na Wazee hawa huwa wanalenga kunufaika na Urithi wa Mali zako wakiamini hautachukua round lazima Ufe.

Anyways, Ngoja tuone mgawanyo wa Mali Kwa Uwiano sawa kati ya Walioanza kuzichuma miake Ile 1990 na hawa walioingia Wakikuta Mzee tayari ni Bilionea 🙌
 
Niliwahi kumsikia Jacqueline akihojiwa na Ayo tv kama sikosei alidai Mengi na mtalaka walishagawana hisa zao na watoto walipewa 10% kila mmoja na hisa za Mercy zilikuja kurithiwa na wanawe ndipo Mzee Mengi aliamua kuacha wosia kwamba mali zake zigawanywe kwa Watoto wa aliozaa na Jacqueline pamoja na Jacqueline mwenyewe,sasa mbona sasa kuna maelezo tofauti?
Kwanza kuongelea family issue kwenye TV tayari hill ni tatizo.

Wanaomdanganya Jack wanampoteza, angekuwa na busara hiyo issue mnamaliza nyumbani na bado atapata mgao mzuri tu, ila akijifanya mjuwaji Kwa jina la Mke imekula kwake, Jackkine hakumpenda Mengi Bali alifuata pesa, Sasa pesa zikimfanya awe kipofu atazilia kuzimu.
 
Naona Jackline anakitafuta kifo Kwa bidii kubwa.

Anaharibu future ya hao Watoto, huwezi kurithi tu utajiri Kwa MTU umemkuta na Mali zake na ana Watoto wakubwa, hakuna MTU anaweza kukubali upuuzi huu.
Akifa tuanze na nani
 
Naona jaji amekosea katika uamuzi wake, haiwezekani mgao wa Mke wa zamani wa Mzee Mengi Bi Mercy ambao ni hisa 35 zirudi kwenye mali za Mzee Mengi eti kwa vile tu walikuwa hawajakakamilisha hilo zoezi la kugawana wakati uamuzi ulishatolewa na mahakama na kuwa hukumu iliyokubaliwa na pande zote mbili (Mengi na Mercy.

Ni dhahiri kuna harufu ya rushwa.
 
Unaambiwa kabla hujafa andika wosia, unaandika wosia ukifa wosia unapingwa na watu wengine kwa hoja kwamba wakati unauandika hukua na akili tomamu na watu wengine wakuamulia nje ya uamuzi uliouacha wewe mwenyewe, wosia una maana gani sasa?
Unaweza kuandika wosia na wakaubadilisha vile vile, muhimu ukiwe njema kula maisha tu usijinyime ili kuwekeza alafu ukifa unaacha ugomvi
 
Kwani kuuwa mtu ni lazima apigwe risasi?

Kuna Russian mafia wanauwa bila kuacha any tressing, unaijuwa Polonium poison?
Naihitaji sana inapatikana wapi? Naomba namba ya mwakyembe
 
Niliwahi kumsikia Jacqueline akihojiwa na Ayo tv kama sikosei alidai Mengi na mtalaka walishagawana hisa zao na watoto walipewa 10% kila mmoja na hisa za Mercy zilikuja kurithiwa na wanawe ndipo Mzee Mengi aliamua kuacha wosia kwamba mali zake zigawanywe kwa Watoto wake aliozaa na Jacqueline pamoja na Jacqueline mwenyewe,sasa mbona sasa kuna maelezo tofauti?
Ndo hivyo hata Mimi niliona Ile interview...upande WA mengi ulileta hoja kuwa...Wakati mengi anaandika huo wosia alikuwa anaumwa na hakuwa na uwezo kutoa maamuzi sahihi au yenye Busara...na walitoa lawama Kwa jackline kuwa alimshinikiza mengi kuandika huo wosia...
 
Back
Top Bottom