DOKEZO Mahakama yavunja ndoa ya Davis Mosha na mkewe aliyeishi naye miaka 28, anyimwa mali. Mosha adai kuibiwa $ milioni 1.4 na jaribio la kupewa sumu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Hii ni komesha kwa wanawake wote wanaoolewa kwa kukimbilia mali huku wakiwaacha watakaowapenda kwa dhati maisha yao yote mpaka kifo kiwatenganishe. Kumeibuka mtindo wa wanaume kutowajumuisha wake zao katika mali zao. Hali kadhalika wanawake nao wameanza kuwa na mali nje na ndoa, wanafanya miradi kwao bila kuwashirikisha waume zao wakijihami ikitokea ndoa kusambaratika tayari mali wanazo nje ya ndoa. Ndoa zimeingiliwa na changamoto za kuvunjika mapema kutokana na ubinafsi na usaliti
 
hivi wanawake wa kaskazini hawana mbinu mbadala ili wamililki mali za mme kama mahaba na kukata kiuno hadi watumie ya kuua mme!
kuuua! kuuua! kuuua!
unatafuta kwa mbinde alaf unakufa kisa kamnofu kadogo hivi ...k
(natoa ofa kwa mwanamke wa kaskazin anayetaka kumalizana na mmewe bila kuacha shaka. kuanzia ni steelwire method na/au unga wa kinyonga!)
 
Nimeona huu mjadala wa Kesi ya Davis Mosha na Mke wake lakini naweza Nami changia kwa kifupi:-Ni Hivi Huyo mwanamke Nancy alipogundua moja Pesa nyingii alizoiba Kwenye kampuni alikuwa anagawia Waumme zake hasa Mtabibu Mitimingi ili ajengee Gorofa na mbaya zaidi alimuajili Huyo Mpenzi wake Kwenye moja ya Taasisi ya Davis pale Mbezi Afrikana, Hiyo mwanamke alimfanya Mtabibu Huyo kuwa controller wa kila kitu bila kampuni kujua, masuala ya Supermarket NK Lakini pia kuanza kuzicontrol kampuni kiganga, Huku Mkurugenzi akiwa nje ya nchi au popote kusaka fursa za kampuni na kampuni mpya.

Lakini Mbaya zaidi Huyo mwanamke alitaka kuua Mtoto wa Mkurugenzi kimya kimya kwa kumtumia mfanyakazi wa ndani huko arusha akisaidiana na Dada mmoja ambaye Kesi yake iliiendeshwa Nairobi Kenya na kufungwa, Sasa Nancy Baada ya kushtukiwa meseji zile Baada ya Mfanyakazi wa nyumbani huko Arusha kukosea meseji badala ya kumtumia Nancy kuwa Zoezi la kumuua Mtoto litafanyika Usiku akamtumia Mama wa Mtoto.
Ile Meseji ya mauaji ilipokosea njia Nancy akaamua kukimbia kwake kwa Aibu ya Watoto wake na kutamba Mitandaoni kuwa amenunua Apartment Masaki hababaishwi.

Baadaye watu wakamshika masikio, Kesi Kesi Mara Kesi kaamua kwa Hiari yake afute Kesi alipogundua mabilioni ya Mafuta ya kampuni aliyoiba PUMA, CARMEL NK,

Sasa Leo Tena Naona andiko hili kuwa amezulumiwa kwa Hiyo mwanamke akiolewa na mtu Mwenye Pesa Basi mme wake pesa ikizidi anakimbia Halafu anadai Mali kweli?
Basi Matajiri wako mbioni kutooa kama Dangote, Kumbe wanawake Ni staili, Kama Ya Hakimi aiseee.

Pia nimeshangaa Nancy kuweka ili andishi Huku la hukumu Wakati aliitoa Kesi mwenyewe inasikitisha sana, Naona anguko la wanawake kuolewa na Matajiri kabisa,
 
Na Kweli hiyu mwanamme nae akiamua kuwafinyia majaji rufani fungu ndefu mosha lazma adondoshe

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Kwa facts zipi?? Ameulizwa maswali kashindwa kujibu huko mahakama ya rufaa ataenda kujibu nini? Na hata akijibu ataulizwa kwanini haya alishindwa kuyajibu mahakama kuu??
 
Kwa mawazo yako, nini kilimstahili kama alifanya jaribio la Kumuua Mumewe??.


Kwa Sheria za Tanzania, Mwanamke ukiishi naye miezi sita tu ni Mkeo .


Wewe ulivyopigwa Chini na The Bold, mlokaa miaka zaidi ya 5..

Kuna Mali amekugawia???.
 
Sasa kashaiba zaidi ya 5B unataka apewe nini tena?? Ebu acheni unafki basi

Ebu jiweke wewe kwenye position ya Mosha alafu useme ungefanyaje. Mke kaiba 5B, Mke anachepuka na bado akataka kukuua isitoshe akakimbia tena nyumbani na pesa nyingi na akaacha ujumbe kila mtu aishi kivyake. How would you have mercy on that??
 
😂😂😂Sawa kaiba ila alikuwa na ngao ya kuwa kama mke ndio tatizo ,kama ingekuwa mtu baki sio rahisi uchote zote hizo .
 
Mwendazake Jiwe kabla ya mauti kumkuta alitoa AMRI hukumu zote ziwe kwa lugha ya kiswahili, inakua kuaje hawa bado wanatumia lugha ya MALKIA?
Ni maajabu tumekusomesha kwa kodi zetu shule za Kingereza and still upo hapa unalalamikia Kingereza?

KWahiyo tulipoteza kodi zetu?

Tumekusomesha ukatusaidie ku-negotiate na wazungu huko mahakama za duniani wasituibie ardhi yetuand still unalalamika hapa?

Kwahiyo tumechoma hela zetu?

Hasara tupu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…