Vichaa wengi mjini ni kesi za mirathi,ndugu wakisema tyuze nyuma we kubali tu,ukikataa unapewa uchizi tuNaogopa kweli...hapa nilipo nasubiriwa na kesi kama hii basi naogopa mnoo maana complications ni nyingi mnoo. Mirathi ni mbaya sana.
Mungu atutetee.
Ngoja nikimbie jukwaa Pendwa.Yah. Kama Kawa.
kesi za mirathi zimesababisha maeneo ya tandale,magomeni,na temeke kuwa na machizi wengi sanaNyie haya mambo yapo sana tu ila watu wanabisha.
Balaa jingine lipo kwenye kesi za mirathi, kuna wilaya moja kwenye mahakama fulani ya mwanzo kulikua na kesi ya mirathi ambayo kila ikikaribia siku ya hukumu inaondoka na hakimu mkazi anaehusika na hiyo kesi. Wakaamua waifute tu maana iligharimu sana maisha ya watu.
Kesi za mirathi zinaogopwa sana na mahakimu.
Noma sanakesi za mirathi zimesababisha maeneo ya tandale,magomeni,na temeke kuwa na machizi wengi sana
Atapigwa mtu hapa naona yanaandaliwa mazingira
...Dah!...kumbe watu wapo kazini?Kuna nyumbu atapigwa muda sio mrefu
🤣🤣🤣🤣🤣🤣Mahakamani kuna vituko sana.. kuna mambo baadhi niliyayokutana nayo kipindi nafanya field kwenye moja kati ya mahakama maarufu tu hapa nchini.
Kisa cha kwanza ilitokea nimewahi mahakamani kama saa 1 kasoro 10 hivi asubuhi nikaingia kwenye chamber (hapa watu wa hii field watanielewa au niseme ni jengo linakua limegawanyika vyumba kwa shughuli za kimahakama sasa kila hakimu huwa na chumba chake cha kuendeshea kesi) .. nimekaa nasoma documents zangu kupitia simu yangu, ghafla nkasikia kama kuna mtu anafunua karatasi kwenye mafaili.. yani ile sauti ya mtu akiwa anafungua ukurasa wa karatasi.
Ikabidi niinuke kwanza niangalie chini ya meza.. nkarudi kwenye shelf inayokaa mafaili ya kesi.. nkatoka nje kuangalia kama kuna mtu yupo chamber nyingine maana hapo chambers zilikua mbili zinazotazamana napo hamna mtu.. nkarudi ndani kukaa ila ile hali ikaendelea vile vile... nkaona isiwe kesi nimpishe tu aendelee na uchambuzi wake huyo jamaaa.. mi nkatoka nje.
Kisa cha pili bwana kuna faili hilo kila ikikaribia kesi halionekani😅 yani hakimu anatuma kazi ya kutafuta hilo faili siku nzima mpaka tunakoma kwa kushirikiana na karani wa mhe. Yani hiyo kesi ilikua balaa.. baada ya tar. ya kesi kupita ndo linaonekana.. ikipangwa tar. nyingine tena mchezo ni ule ule..
sijui liliishiaje lile faili asee...
MTOA MADA SAMAHANI KWA KUINGILIA UZI WAKO.
kesi ikishafika hukumu unafutaje sasa, ninyi hamjui hata procedure za kesi mahakamani.Babu huwa anatuma joka siku ya hukum kama kesi ni ngumu kwake. Hakimu akikaa tu mezani cobra linamsimamia mbele tayari kumgonga akitaka kutamka neno tu. Mahakimu huwa wanatoka na kuita karani ataje siku nyingine mwisho kesi inafutwa.
Siku moja alikutana na hakimu anatokea usukumani
Kilichotokea ............
Nashindwa kusimulia ila ilikuwa ni Singida.
Babu bado yupo.
Sent from my SM-A022F using JamiiForums mobile app
vichaa wengi ni wezi wa wake za watu na biashara za madawa. hata watu kama huyu anayetamba kwenda kwa waganga huwa wanakosea masharti afu dawa zinawarudi wanakuwa machizi fresh. ndugu ni vigumu sana kukuroga kwasababu ya mirathi,ugomvi mwingi wa mirathi huwa wanaua kabisa hawawezi kukuonea huruma uwe kichaa kwasababu hata ukiwa kichaa bado portion yako ya mirathi itakuwepo, si hujafa. huwa nawashangaa sana hata wanawake wanaongángánia mali baada ya waume zao kufariki, hawajui wazazi wa mume walihangaika namna gani kumsomesha na kumfikisha pale alipo. ukiona wazazi wanasema tugawane, we kubali yaishe, endelea na maisha yako, la sivyo huwa wanakudhuru wewe na hata watoto wako (wajukuu zao) mnaweza kupitia garama kubwa ambayo hamkupaswa kuiipitia.Vichaa wengi mjini ni kesi za mirathi,ndugu wakisema tyuze nyuma we kubali tu,ukikataa unapewa uchizi tu
Nimekuelewa sana mkuuvichaa wengi ni wezi wa wake za watu na biashara za madawa. hata watu kama huyu anayetamba kwenda kwa waganga huwa wanakosea masharti afu dawa zinawarudi wanakuwa machizi fresh. ndugu ni vigumu sana kukuroga kwasababu ya mirathi,ugomvi mwingi wa mirathi huwa wanaua kabisa hawawezi kukuonea huruma uwe kichaa kwasababu hata ukiwa kichaa bado portion yako ya mirathi itakuwepo, si hujafa. huwa nawashangaa sana hata wanawake wanaongángánia mali baada ya waume zao kufariki, hawajui wazazi wa mume walihangaika namna gani kumsomesha na kumfikisha pale alipo. ukiona wazazi wanasema tugawane, we kubali yaishe, endelea na maisha yako, la sivyo huwa wanakudhuru wewe na hata watoto wako (wajukuu zao) mnaweza kupitia garama kubwa ambayo hamkupaswa kuiipitia.
all in all, uchawi dawa yake ni moja tu. Okoka, kimbilia kwa Yesu. ila nakuhakikishia ukijidanganya sijui unasali maria sijui lozari, utakungútwa na utakufa. Nimethibitisha katika maisha yangu kwamba Uchawi hauwezi kwa watu walio ndani ya Yesu Kristo, hauwezi kabisa na wengi wakiendelea kukufuatilia huwa yanawarudi. Mungu akiwa upande wetu ni nani aliye juu yetu. sasa utakuta kuna viwatu havina Mungu na vinategemea uchawi, uchawi na waganga wote wanamfuata shetani aliye baba wa uongo na mitego. unaweza kupigwa chale kwa mganga huyu mwenzako akaenda kwa mganga mkubwa zaidi ukafyatulia. shetani haaminiki, ila Yesu is the only one to be rusted. huu ni ushauri wa bure.
kesi za mirathi zimesababisha maeneo ya tandale,magomeni,na temeke kuwa na machizi wengi sana
Sheria za utumishi zinawapendelea wenye uzoefu kazini, elimu kubwa, na wenye vyeo.Katika Mahakama naona Mahakimu ndio wana kazi ngumu sana kuliko Majaji.
Mahakimu ndio wanao fanya kazi kwenye mazingira magumu zaidi kuliko Majaji, lkn cha kushangaza eti Majaji ndio wanalipwa vizuri zaidi kuliko Mahkimu.
hivyo ni vyema Serikli ikwajali sana Mahakimu ktk masilahi yao kuliko Majaji.
Kutoa haki sio kazi ndogo.
Unachoongea ni kweli kabisa mkuu, mimea ina maajabu makubwa sana kuna vitu haviitaji kabisa kwenda kwa mganga.Hizi mambo sometimes huhitaji hata kwenda kwa hao Waganga,ukiijua miti/mizizi vizuri tu kwisha habari yao.
Naomba unielekeze tofauti ya hakimu na jaji.Katika Mahakama naona Mahakimu ndio wana kazi ngumu sana kuliko Majaji.
Mahakimu ndio wanao fanya kazi kwenye mazingira magumu zaidi kuliko Majaji, lkn cha kushangaza eti Majaji ndio wanalipwa vizuri zaidi kuliko Mahkimu.
hivyo ni vyema Serikli ikwajali sana Mahakimu ktk masilahi yao kuliko Majaji.
Kutoa haki sio kazi ndogo.
Maandalizi ya mtu kutapeliwa. Watu wataingia In box na watapigwa pesa kwa hiari yao.Wanabodi,
Nayaandika haya sio kwa kufurahisha bali ni mambo yaliyonikuta na sitaki kuyakumbuka kabisa lakini kwa yaliyomtokea shahidi namba 13 wa upande wa jamuhuri Kamanda Swilla kwa kuugua ghafla kizimbani na muda mwingi kuomba ruhusa kwenda washroom au maliwato siyo mambo ya kucheka huwa yanatokea.
Mwaka 2005 Katika purukushani za uchaguzi na kikiri kakala za hapa na pale nilishtakiwa mahakamani kwa kosa ya matumizi mabaya ya pesa yaani rushwa na kuharibu kumbukumbu za ushahidi.
Kwa kuwa Mimi Gussie ni Mkinga automatic Rafiki zangu wengi ni wakinga hivyo kwa kuwa kuna mambo mengi tunasimuliana nikaona isiwe shida kuomba msaada wa ushauri kwa wakinga wenzangu kuhusu kesi inayonikabili Mahakamani.
Wakinga wenzangu Walinipa machaguo mawili
1. Kuifuta kesi kwa njia ya giza yaani mafaili na kumbukumbu zote kwenye Kompyuta na Polisi zipotee kabisa na hata jina langu lisionekane kabisa
2. Watu walionishtaki wakiniona wanikimbie sehemu yeyote ili au washindwe kuzungumza kitu mbele yangu na mahakamani
Mimi nilichagua chaguo namba mbili kwani hawa watu walionishtaki Nilitaka hata Ikifika uchaguzi mwingine waniogope na kunikimbia kila wakiona sura yangu au Uwepo wangu au washindwe kuongea mbele yangu
Nilisafiri toka Dar es Salaam mpaka Mbeya kuelekea Malawi huko kwa Mganga wa Kienyeji, Mganga alinipatia chupa ndogo ukubwa wa chupa ya glycerine yenye mafuta ndani yake na yenye vipande vidogo dogo vya miti ndani yake pamoja na unyoya sijui unyoya wa ndege gani sikumuuliza Mganga, huu unyoya ulikuwa ndani ya hicho chupa unaelea elea tu.
Mganga huyu wa Malawi pia alinikabidhi leso ndogo ambayo kona moja ameifunga ndani ya sehemu aliyofunga sikujua aliweka dawa gani, na Mimi sikuuliza
Kazi ya mafuta ilikuwa pale ninapoenda polisi najipaka kidogo tu usoni au kwenye paji la uso na kuongea maneno ninayotaka mimi mwenyewe, Siku niliporudi tu nikaelekea polisi kwa confidence kabisa kwani walikuwa wananitafuta sijaonekana Mahakamani na wala sijaripoti kwao Polisi, Mimi kabla ya kufika Nilitamka kuwa polisi wa Uchunguzi wanisahau kabisa.
Kweli nilipofika tu polisi, kila polisi pale kituoni alikuwa ananiuliza umekuja kufanya nini hapa, Moyoni nikawa nawaza ni hawa hawa au Wengine. Mwisho wa siku niliamua kuaaga mwenyewe na kurudi zangu nyumbani kwani hakuna polisi aliyenikumbuka au kushughulika na Mimi.
Niliamua kurudi tena pale polisi siku ya pili kwa kutumia ile leso niliyopewa ambayo niliambiwa kazi ya ile leso ni kufukuza nuksi na lolote baya juu yangu, Nilitakiwa kuweka ile leso mfukoni mahala popote kama nikihisi kutakuwa na tatizo au naenda kuonana na mpinzani au adui yangu au mtu yeyote aliye kinyume na malengo yangu, Kumbuka hii ni leso ya kawaida isipokuwa kwenye kona moja tu ndio imefungwa dawa kwa ndani ambayo sijui, Kwa kutumia hii leso pia natakiwa "kunuia" kwa lugha ya kiganga au natakiwa kusema lile ninalotaka lifanyike kwa wakati wowote ule kwa kuigusa leso mfukoni mwangu.
Nikiwa karibu na kituo cha polisi niliigusa leso yangu na kutamka wale wote polisi wanoko walionikamata na kunichunguza naomba wahamishwe kazi pale kituoni kwani wao ndio walikuwa vimbelembele kunisumbua, Nikaingia kituoni counter na kuwaulizia kama wapo nikawakuta, Nikaanza kuwaulizia kuhusu kesi yangu nikaona kila mmoja anamtupia Mwenzake mpira kuwa tuyamalize yaishe huku wakitaka mimi niondoke pale kituoni nirudi nyumbani, Wakanisihi wale polisi basi niwatafuta jioni tuyaongee kwani Mimi wakati huo nilikuwa nafahamika baadhi ya Pub nikila bata, Nikawaambia niwatafuta kesho.
Mambo yalibadilika badala ya polisi kuendelea kunitafuta Mimi, Ikawa mimi ndio nawafuatilia wao ili kujua mwisho wa kesi, Siku iliyofuata wale polisi walinipigia simu wamehamishwa kabisa Mkoa na kutupwa mikoa tofauti.
Baada ya hawa polisi kuhamishwa na hali kupoa kidogo, Nikasafiri tena kuelekea huko Malawi kwenda kutoa report na hatua iliyofikiwa, Kumbuka hizi connections zote za huko ni Mwanamke ndie aliyeniunganishia mpaka Malawi huko hivyo akawa sio rafiki tu ila zaidi ya Rafiki maana hakuna siri ambayo nilikuwa namficha hivyo alinijua ndani nje huyo Mwanamke, Na yeye alifika huko Malawi na kukufahamu huko huyo Dada baada ya watu kumroga akawa ana bleed kila siku karibu miezi mitano bila nafuu mpaka anaongezewa damu mwilini hivyo alidhoofu sana ni kutokana na yeye kuwa na mahusiano na Mume wa Mtu, Aliponea huko Malawi.
Baada ya kukamilisha shukrani huko Malawi, Nikauliza nini mwisho wa yale mafuta na ile lesso, Niliambiwa yale mafuta yakipungua niwe naongeza mafuta ya kawaida tu ya kupikia nayatikisa na kutumia kupaka pale nitakapohitaji kuyatumia
Ishu ya polisi ikawa imeisha sasa ikabaki ishu ya Mahakamani kujua mambo yamekaa vipi huko kwani tayari wambea wameshahamishwa vituo vya kazi hawapo tena
Ishu ya Mahakama Nikaamua kuelekea huko kwetu Ukingani, Nikaelezea hatua niliyofikia na nini kimebaki, Huko kwetu ndio nilikutana na funga kazi ya mwaka, Nilipewa dawa kamzizi kana urefu kama njiti ya kiberiti lakini kanene kidogo, Hiyo dawa kimatumizi haitofautiani sana na zile za Malawi kwani nayo lazima unuie yaani utamke maneno utakavyo nini kifanyike. Wazo langu hapa likanijia kichwani niwafanye watu wa mahakama kuanzia hakimu na Wengine wawe Mabubu yaani washindwe kuongea
Kujaribu uwezo wa huo mzizi kwanza kabla ya kufika kwa pilato yaani Mahakamani Nilitamka nipande gari bure toka Makete huko mpaka Dar bila kulipa nauli njiani, Wakati huo kulikuwa hakuna gari ya moja kwa moja toka Makete mpaka Dar es Salaam, Nilipanda gari toka Makete mpaka Njombe bure kabisa,
Nilifika kwa konda Nikamwambia sina nauli naomba msaada akajifanya kama anataka kuchomoa hivi mara paap akalainika kama bigijii na kwenda mwenyewe kunichukulia ticket kwa Wadada wanaokatisha sijui aliwaambia kitu gani, Nilifika Njombe usiku Nikaamua kutafuna tena kale kamzizi ili nilale guest pale bure kabisa pale Njombe nikisubiri ifike asubuhi nielekee Dar, Baada ya kufika Guest nikamkuta Dada kaunta Nikamwambia Nahitaji chumba lakini sina pesa ya kulipa, Dada akajibu hakuna chumba vimejaa, Nikamwambia sasa tunafanyaje mara paap akalainika kama bigijii akapiga simu guest inayofuata akaongea nao nikalala guest hiyo nyingine bure kabisa bila kulipa kitu
Nitaendelea tena baadae kuelezea
Wale wapambanaji hawawezi kushangaa ninachokisema hapa, Hakuna maisha ya mteremko hapa duniani you have to fight
Nyie wote kundi moja. Mmerusha ndoano mtawaliwa wajingaMahakamani kuna vituko sana.. kuna mambo baadhi niliyayokutana nayo kipindi nafanya field kwenye moja kati ya mahakama maarufu tu hapa nchini.
Kisa cha kwanza ilitokea nimewahi mahakamani kama saa 1 kasoro 10 hivi asubuhi nikaingia kwenye chamber (hapa watu wa hii field watanielewa au niseme ni jengo linakua limegawanyika vyumba kwa shughuli za kimahakama sasa kila hakimu huwa na chumba chake cha kuendeshea kesi) .. nimekaa nasoma documents zangu kupitia simu yangu, ghafla nkasikia kama kuna mtu anafunua karatasi kwenye mafaili.. yani ile sauti ya mtu akiwa anafungua ukurasa wa karatasi.
Ikabidi niinuke kwanza niangalie chini ya meza.. nkarudi kwenye shelf inayokaa mafaili ya kesi.. nkatoka nje kuangalia kama kuna mtu yupo chamber nyingine maana hapo chambers zilikua mbili zinazotazamana napo hamna mtu.. nkarudi ndani kukaa ila ile hali ikaendelea vile vile... nkaona isiwe kesi nimpishe tu aendelee na uchambuzi wake huyo jamaaa.. mi nkatoka nje.
Kisa cha pili bwana kuna faili hilo kila ikikaribia kesi halionekani[emoji28] yani hakimu anatuma kazi ya kutafuta hilo faili siku nzima mpaka tunakoma kwa kushirikiana na karani wa mhe. Yani hiyo kesi ilikua balaa.. baada ya tar. ya kesi kupita ndo linaonekana.. ikipangwa tar. nyingine tena mchezo ni ule ule..
sijui liliishiaje lile faili asee...
MTOA MADA SAMAHANI KWA KUINGILIA UZI WAKO.
Nyie wote kundi moja. Mmerusha ndoano mtawaliwa wajinga