Mahojiano ya Diamond katika kipindi cha leo tena, amkubali mtoto wa Hamisa kuwa wake

Hakusoma alama za nyakati
 
Kwa nini alimkana sasa?hv do u know hamisa ametukanwa Mara ngapi na mashabiki mpk na zari mwenyewe?angepaswa akubali toka mwanzo
Hakumkana ilikuwa ndani ya makubaliano yao....sasa Hamisa na uswahili wake akajua anamkomoa Zari....

Mtu amelea mimba mpka kujifungua hadi gharama na vifaa vya Mtoto unataka nini tena kama sio kuuza gazeti.?
 
Atasema alichokitaka kimetokea amekubali mtoto

😀😀 anachokitaka sio icho,yeye anasubilia asikie tu Domo na Zari chaliiii ili afanye sherehe....halafu Domo ndo kwaaanza anapigilia msumari kwamba hawawezi kuachana....Siku Zari akipost tu kuwa anamsupport Domo kwa kila kilichotokea naamini kuna watu watafuta acount zao kwa insta kwa hasira
 
Hamisa hajielewi yaani kwa maelezo ya diamond kama ni kweli hamisa angemsikiliza akakaa kimya angepata mambo mengi mazuri na pengine angepewa hata mtaji wa biashara kwa ajili ya mtoto sasa kwa ujinga wake na uswahili kaharibu
 
Maana yake ya nini
 
Kwa akili hizi ndio maana tuna watoto wa mitaani wengi! Mwanamke mwenye akili anafikiria future ya watoto wake no matter what na hapa ndipo Zari anapowafunika dada zangu wa kibongo!
Kabisa,wajinga wamemshauri apate umaarufu kuliko matunzo ya mtoto,angekaa kimya Dai angeendelea kwenda kisirisiri na kucheza na mtoto wake na kumpatia mahitaji muhimu,ukute hadi mjengo angemshushia ili asipate shida kwenye Nyumba za kupanga.

Hakika wanawake sijui tumelogwa na nani
 
Mmmmhhh hii vita haitamuacha mtu salama
 
Reactions: R.B
Samahani kwani ndoa walishafunga nahoji tu??
 
Kwa akili hizi ndio maana tuba watoto wa mitaani wengi! Mwanamke mwenye akili anafikiria future ya watoto wake no matter what na hapa ndipo Zari anapowafunika dada zangu wa kibongo!
What is future ya mtoto ambae anakataliwa hadharani? Hivi unamjenga vipi huyo mtoto kisaikolojia katika jamii inayomfahamu kua amekataliwa hadharani? Tena huku mamake akiitwa Bitch !! Kisa tu watembelee Rav 4 na wale chakula kizuri etc.
Kupenda pesa kutawauwa future yoyote ya mtoto huanza kujengwa kwa kujiamini kwa mtoto mwenyewe, nitakupa mfanyo mmoja wakati tupo shule kuna kijana alikua akiitwa Ongala ni mtoto wa damu wa Remmy Ongala alikua akiishi maisha ya kimasikini sana maana Remmy alikua hamtunzi yule mtoto ila mtoto alikua akijisia fahari sana kua mtoto wa Remmy Ongala,pamoja na umasikini wake maisha duni anayoishi yeye na bibi yake (maana mamake aliolewa kwingine) lakini alikua haachi kujitambukisha kua yeye ni mtoto wa Remmy Ongala
Siku moja Remmy alikuja shuleni kwetu na Bendi yake ya Matimila katika kampeni za kuhamashisha mapambano dhidi ya ukimwi, na kipindi kile kilikua kuna ule wimbo wake ulikua unaitwa "mambo yote kwa soksi"
Huwezi amini Ongala alikua mtu wa kwanza kwenda kumkumbatia Remmy na kuita jina "baba" na kwa namna walivyokua wakifanana Remmy nae akamkumbatia na tangu hapo alianza kufatilia maisha ya mtoto wake mpaka kifo kilipomchukua.
 
Bi dada hii umenena ukweli! Namhurumia Daimond maana kiboko cha Hamisa hasa kutoka kwa influence ya mama yake haitamuacha salama. Tuna uzoefu na hii kitu, ukizaa na mwanamke asiye na aibu na staha ni kunadi maisha yako. Aidha Hamisa alifanya kosa la kuonyesha picha za kitandani kwa Diamond maana Zari hatamsamehe na zahama zitakwenda kwa mtoto maskini. Naona wanawake wengi kwa ubinafsi wao huwa hawafikirii watoto wao. Mimi ...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…