Mahubiri ya Baba Askofu Mtetemela pale KKKT Mbezi Beach yamenishawishi kuachana na siasa za "Kishabiki"

Redundancy zinaendelea hapo Lumumba?
 
Utumwa haukukomeshwa kwasababu ya William Wilberforce au kanisa.Utumwa ulikomeshwa kwa kuwa mapinduzi ya viwanda yalishabadilisha mifumo ya kiuchumi ,kisiasa na kiuchumi.Utumwa ulidumu zaidi ya miaka 300 na wahubiri ,kanisa na wapigania haki walikuwepo lakini utumwa ulishika hatamu.
 
Ili uachane na siasa za kishabiki inabidi ukiri kwanza je, uchaguzi ulikuwa huru au haukuwa huru?
 
Kila siku nakukumbushia hili.

Zaburi 1: 1 - 6
1.Heri mtu yule asiyekwenda
Katika shauri la wasio haki;
Wala hakusimama katika njia ya wakosaji;
Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

2.Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo,
Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.

3.Naye atakuwa kama mti uliopandwa
Kandokando ya vijito vya maji,
Uzaao matunda yake kwa majira yake,
Wala jani lake halinyauki;
Na kila alitendalo litafanikiwa.

4.Sivyo walivyo wasio haki;
Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.

5.Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni,
Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.

6.Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki,
Bali njia ya wasio haki itapotea.
 
Naona ingekuwa vizuri zaidi uondoke kabisa CCM, kuacha siasa za kishabiki maana yake utaacha kushangilia uharamia kama ushindi wa kura feki, badala yake utakaa kimya hayo yakitendwa na chama chako, hapo sioni lolote la maana ulilofanya.
 
Nilmsikia Askofu. hasa pale alipotoa mfano kuwa maaskofu wawilili waliokuwa wakisafiri walivunja sheria ya barabarani kupita round about isivyopasa kwa kuwa tu ilikuwa usiku a mara paap trafik huyoooooo. inatupasa kutenda mema/haki bila kujali usiku au mchana, watu wanakuona au uko gizani.
Kama Mungu akiongoza maisha yako unakuwa chumvi ya dunia, kazi ya chumvi ni kuzuia uharibifu.

Johnthebaptist yafikishe mahubiri hayo huko kwenye chama chenu, nyie wacheche mkiwa chumvi mkasababishe kusiwepo tena uharibifu na maonevu dhini ya wasio na nguvu hasa kwenye siasa za uchaguzi.

Usisahahu kumfikishia Slowslow!
 

Nadhani wewe ndio Polepole mwenyewe, umelamba uteuzi sasa unasepaa
 
Hii peleka Fb Lumumba mnakwama
 
Kutangaza kuacha siasa za ushabiki huku unasema unabaki kuwa mwana-CCM, hauna tofauti na mlevi anayejipongeza kwa pombe kwa kuacha pombe
 
Umeandika vizuri,lkn ulipokuja kuharibu ni hapo ulipoitaja ccm ,nimekupuuza wewe lkn sio Ujumbe mzuri wa Mtumishi wa Mungu Askofu mstaafu Donald Mtetemela.

Sent from my TECNO WX3 using JamiiForums mobile app
 
Amina mpendwa!
 
Ndugu yangu katika KRISTU-Kama KRISTU ndiye aliyekuongoza kwenye kweli kwa mapenzi yake makubwa na upendo wa ajabu,basi na ukawe nuru ya haki kwa wote manake MUNGU ni haki.Askofu Bagonza alikuwa mwana CCM mtiifu lakini linapokuja swala la mtu anayeonewa husimamia HAKI bila kujali gharama.Mtakatifu PAULO nadhan ni mfano bora kwetu wakati wa safari ya maisha yake hapa duniani.
 
Amina.

Kuna tofauti kati ya mwaminifu na mtiifu, ahsante!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…