Mahusiano kati ya namba ya NIDA na mfumo wa ajira yakoje? Dogo kazinguliwa ajira mpya, naomba ushauri wenu

Mahusiano kati ya namba ya NIDA na mfumo wa ajira yakoje? Dogo kazinguliwa ajira mpya, naomba ushauri wenu

mkuu embu nisaidie na mimi kimawazo,mimi majina yangu ya vyeti vya taalumu ni “hance prosper paul” cheti cha nida ni “hance prosper massawe” ila majina yote hayo yapo kwenye cheti cha kuzaliwa ni kwamba nida walitumia jina la ukoo badala ya jina la babu,je kunachangamoto yotote itayonikumba hasa kwenye application za kazi?? nini nifanye?,natanguliza shukrani zangu aksante
Hao ni watu wawili tofauti.Hapo itakulazimu uwe na kiapo cha majina ambacho kitaonesha kuwa majina yote ni yako.Na sehemu yoyote utakayoenda (kuomba KAZI etc)utalazimika kuambatanisha viapo vyako vya majina.Inshort ni usumbufu kama utaweza nenda NIDA waombe wakubadilishie majina(kuna fee utalipia)
 
Habarini za humu Wana Jf wote!
Niwape hongera kwa ufafanuzi mzuri wa baadhi ya mambo ambayo yamekuwa na sintofahamu.

Binafsi nina suala kama hilo, japo sijabahatika kupata ajira zilizopita, ila huwa nawaza itakuwaje siku nikipata, Ni hivi...

Vyeti vyangu vyote vina majina matatu pamoja na kitambulisho cha NIDA, na yapo sahihi kabisa(yanaendana) ila shida ni zile namba za mwanzoni kwenye kitambulisho zile 4,ambazo huendana na Mwaka wa kuzaliwa zipo tofauti na zile za kwenye cheti cha kuzaliwa, mfano, 1989XXXX....,katika NIDA, ilihali Mwaka kwenye cheti ni 1987,....
je hii haiwezi kuja kuleta shida pindi niliingia kwenye mfumo wa ajira?
 
Habarini za humu Wana Jf wote!
Niwape hongera kwa ufafanuzi mzuri wa baadhi ya mambo ambayo yamekuwa na sintofahamu.

Binafsi nina suala kama hilo, japo sijabahatika kupata ajira zilizopita, ila huwa nawaza itakuwaje siku nikipata, Ni hivi...

Vyeti vyangu vyote vina majina matatu pamoja na kitambulisho cha NIDA, na yapo sahihi kabisa(yanaendana) ila shida ni zile namba za mwanzoni kwenye kitambulisho zile 4,ambazo huendana na Mwaka wa kuzaliwa zipo tofauti na zile za kwenye cheti cha kuzaliwa, mfano, 1989XXXX....,katika NIDA, ilihali Mwaka kwenye cheti ni 1987,....
je hii haiwezi kuja kuleta shida pindi niliingia kwenye mfumo wa ajira?
Kwenye cheti kipi?kama cha kuzaliwa nenda utengeneze kipya,kama ni vya kitaaluma hapo utapaswa kurudi NIDA wanarekebisha.Gharama zao ni ndogo Tu kuliko usumbufu utakaoupata baadae.
 
ila shida ni zile namba za mwanzoni kwenye kitambulisho zile 4,ambazo huendana na Mwaka wa kuzaliwa zipo tofauti na zile za kwenye cheti cha kuzaliwa, mfano, 1989XXXX....,katika NIDA, ilihali Mwaka kwenye cheti ni 1987,....
je hii haiwezi kuja kuleta shida pindi niliingia kwenye mfumo wa ajira?
Waone NIDA wakubadilishie hizo namba waweke 1987.

NIDA imebeba mwaka, mwezi na terehe ya kuzaliwa, pamoja na namba zingine ambazo ni unique kwa kila mmoja
 
Habarini za humu Wana Jf wote!
Niwape hongera kwa ufafanuzi mzuri wa baadhi ya mambo ambayo yamekuwa na sintofahamu.

Binafsi nina suala kama hilo, japo sijabahatika kupata ajira zilizopita, ila huwa nawaza itakuwaje siku nikipata, Ni hivi...

Vyeti vyangu vyote vina majina matatu pamoja na kitambulisho cha NIDA, na yapo sahihi kabisa(yanaendana) ila shida ni zile namba za mwanzoni kwenye kitambulisho zile 4,ambazo huendana na Mwaka wa kuzaliwa zipo tofauti na zile za kwenye cheti cha kuzaliwa, mfano, 1989XXXX....,katika NIDA, ilihali Mwaka kwenye cheti ni 1987,....
je hii haiwezi kuja kuleta shida pindi niliingia kwenye mfumo wa ajira?

iyo ni shida tena shida kubwa nida inatengenezwa kutokana na cheti chako cha kuzaliwa au avidavit swali kwanini zitofautiane ?
njia sahihi ya kutatua tatizo ni kubadilisha cheti cha kuzaliwa ili ziendane na nida maana kubadilisha details za nida ni mlolongo sana kuliko cheti cha kuzaliwa
 
iyo ni shida tena shida kubwa nida inatengenezwa kutokana na cheti chako cha kuzaliwa au avidavit swali kwanini zitofautiane ?
njia sahihi ya kutatua tatizo ni kubadilisha cheti cha kuzaliwa ili ziendane na nida maana kubadilisha details za nida ni mlolongo sana kuliko cheti cha kuzaliwa
Asante sana kwa ushauri.
 
iyo ni shida tena shida kubwa nida inatengenezwa kutokana na cheti chako cha kuzaliwa au avidavit swali kwanini zitofautiane ?
njia sahihi ya kutatua tatizo ni kubadilisha cheti cha kuzaliwa ili ziendane na nida maana kubadilisha details za nida ni mlolongo sana kuliko cheti cha kuzaliwa
Hilo la kubadili cheti cha kuzaliwa linawezekana, ila pia kwenye nakala ya matokeo yangu(transcript) Mwaka wa Kuzaliwa upo, je haiwezi kuwa na athari ikiwa Nitabadili cheti cha kuzaliwa?
 
Ulivyoandika kama wamemkataa ila nina imani wamempa mwongozo wa namna ya kuondoa hiyo dosari nadhani ungemuuliza ili wakati unaandika hapa utupe ABC walizomwambia za kufanya ili wadau wakusaidie kukupa mwongozo maana kuna ambao herufi moja imeleta shida wameambiwa kuna issue za viapo na kutoa tangazo plus warudi NIDA pia kuna issue za kurekebisha mfano mtu anaitwa Jodoki alafu cheti kimeandikwa Jodok.
 
Inabidi uwaambie NIDA watoe Massawe waweke Paul
Nina mdogo wangu yeye alisajili NIDA kwa majina ya ubatizo sio yale ambayo yapo kwenye Vyeti vya kitaaluma,baada ya kumaliza kusoma ndio amegundua hiyo shida,katika kuomba Ajira,Je nida inaweza kuedit majina? na kuweka yale yaliyo kwenye vyeti?
 
Ukisoma comment hapa, lawama zote zinaenda kwa wananchi.

  1. Yaani NIDA wanakosea kuingiza taarifa kwa usahihi wakati wa kukusajili ila sasa inabidi mwananchi ukalipe gharama ili waweze kurekebisha taarifa zako walizoingiza vibaya ilhali wewe ulileta kwa usahihi.
  2. Watanzania tunaona ni bora kurekebisha cheti cha kuzaliwa kwa kuomba kipya bila kufuta kile cha awali ili tu taarifa ziendane kwenye NIDA na cheti cha kuzaliwa, bila kujali kuwa tunazalisha taarifa za uongo kwa msajili (RITA), yaani anaweza sema watanzania 12 wana vyeti vya kuzaliwa kumbe ni watanzania 6 ila wana vyeti viwili viwili.
  3. Maofisa wa halmashauri na sehemu nyingine, wekeni njia ya kurekebisha kasoro ndogo kama hizo zinazojitokeza. Mtu majina yametofautiana mnamwambia NIDA imegoma aondoke, nafasi yake inabaki wazi, huko mtaani mnaona hakuna shida yoyote kama atabaki na majina yaliyokosewa, ila mnaona shida pale tu anapoomba ajira. Nyie mlipaswa kuwa sehemu ya marekebisho ya daftari la NIDA, msimuache mtu aondoke kwenda kupambana huko mitaani, hata hiyo option ya viapo nk, haikufaa kutumika yenyewe bali ilipaswa kiapo kitumike kurekebisha taarifa za mtu (hasa NIDA) kwa kuwa ndio unaonekana kuwa mfumo rasmi unaotumika sehemu nyingi. Kurekebisha taarifa NIDA kunafanya serikali iwe na taarifa sahihi na za uhakika kuhusu raia wake.
 
Wacha uongo wako; kabla ya mfumo wa NIDA kuanzishwa asilimia kubwa wameandikishwa shule kwa majina mawili au majina ya mkato.

Huwezi sema aliyetumia majina mawili shule ni watu wawili tofaut kama NIDA yake ina majina matatu.. hii siyo sababu kwa kuwa NIDA usajili wake unalazimisha majina matatu ila shuleni hulazimishwi majina matatu.

Nafikiri labda kuna tatizo lingine
Uko sahihi mkuu
 
Hilo la kubadili cheti cha kuzaliwa linawezekana, ila pia kwenye nakala ya matokeo yangu(transcript) Mwaka wa Kuzaliwa upo, je haiwezi kuwa na athari ikiwa Nitabadili cheti cha kuzaliwa?
Kibadili cheti cha kuzaliwa kiendane na transcript
 
Nina mdogo wangu yeye alisajili NIDA kwa majina ya ubatizo sio yale ambayo yapo kwenye Vyeti vya kitaaluma,baada ya kumaliza kusoma ndio amegundua hiyo shida,katika kuomba Ajira,Je nida inaweza kuedit majina? na kuweka yale yaliyo kwenye vyeti?
Ndio afuatilie NIDA ili wambadilishie majina yaendane na ya Vyeti
 
Mimi majina yangu yote matatu kwenye vyeti vya taaluma hadi nida yapo sawa ila cheti cha kuzaliwa jina la mwisho ni tofauti ila affidavit ninayo sitasumbuka kweli ?
Wacheki RITA wakubadilishie ili yawe sawa kotekote na uondoe huo usumbufu moja kwa moja
 
Kwanza serikalini hawaangalii transcript ukiwa tayari una academic certificate.
Kwa upande wangu na-prefer matching ya taarifa zote zinazotakiwa kumatch kwenye vyeti vyangu vyote na IDs.

Ingekuwa mimi ningejitahidi nirekebishe ziwe sawa, huwezi jua mbeleni unaweza kuhitaji huduma halafu hicho kitu kikakukwamisha
 
Back
Top Bottom