Maisha bila Mungu yamekuwa ya amani na furaha

Maisha bila Mungu yamekuwa ya amani na furaha

😹😹😹 sina uhakika ila huyo aliyekudesign yeye nani alimdesign??
Dunia haijawahi kubadilika kwahyo mungu ni huyo huyo mmoja tuuuu ulishawahi kwenda nje ya ulimwengu huu ukagundua kua Kuna kitu kimekosekana kwenye huu ulimwengu wetu tunaoishi Mimi na wewe
 
Habari wana-JF!

Najua huu uzi wafia dini watausoma kwa kusonya ila ndiyo hivyo inabidi tuvumiliane tu.

Mimi nimekulia katika Ukristo, sijaukana ila nimeliacha kanisa kimyakimya. Baada ya kuanza kukua na kujitambua nilikuwa na maswali mengi sana juu ya nadharia zote kumuhusu Mungu na maswali yangu yote yalikuwa hayana majibu yaliyonyooka.

Baada ya udadisi wa muda mrefu nikafikia hitimisho kuwa "hakuna Mungu" kwasababu angekuwepo na majibu ya maswali yangu yangekuwepo.

Uwanda wa imani ni mpana ila ukiwa ndani ya imani chini ya tawi la dini ni mwiko kudadisi uwepo wa Mungu, huko ni "ndiyo" tu hakuna kuhoji.

Maisha baada ya kulikimbia kanisa yamekuwa na amani kwasababu:

1. Maisha yangu yapo mikononi mwangu.

2. Sina hofu juu ya kifo wala kuzimu kwasababu siamini hadithi za maisha baada ya kifo.

3. Naishi kwa kufuata katiba na sheria za nchi na si vinginevyo.

4. Siishi maisha kwaajili ya kumpendeza yoyote au kitu chochote.

5. Napata muda mwingi wa kufanya mambo ya msingi, siku ya Jumapili kwangu ni kama siku nyingine ya wiki.

6. Badala ya kuhangaika kutafuta maarifa ya maisha ya mbinguni (kusoma biblia), natafuta zaidi maarifa yatakonisaidia kwenye maisha ya hapa duniani maana ndiyo sehemu pekee ninayothibitisha ni ya kweli.

7. Najiheshimu. Kwangu kulia na kuomba msaada kwa M(i)ungu ni kutojiheshimu kama binadamu.

8. Nikipata matatizo sikai chini kuomba na kusubiri miujiza badala yake natumia maarifa niliyonayo kutafuta ufumbuzi.

9. Siishi kwa matumaini ya kuzawadiwa uzima wa milele.

10. Nimepishana na utapeli. Kama wanavyosema "wajinga ndiyo waliwao".

Siamini kama kweli Mungu yupo, lakini kama yupo hawezi kuwa mjinga kama anavyoelezewa kwenye vitabu vya dini.

Mungu hayupo, lakini kama angekuwepo hastahili utukufu wala unyenyekevu kutoka kwangu.

The sweet, sweet relief of knowing I'm going to hell no matter what I do! 🙃
Katika maarifa unayotafuta pia tafuta iwapo kama dish halijayumba.
 
This is an a priori logical fallacy.

Ume assume Mungu yupo kabla ya ku prove.

Thibitisha Mungu yupo.
Kiranga nikuulize na wewe huu ulimwengu tunaoishi wenye Kila kitu very perfect ulitokea tu Kwa bahat mbaya ????
Hata kama hatujibiwi maswali yetu na viulizi vyetu na mungu alieumba ulimwengu huu , haiwezi ikawa Sababu kwamba eti mungu hayupo
 
Designer yupo awe mkatili awe mwenye upendo but he/she is the designer , ilimradi tumezaliwa na tumekuta ulimwengu ulio na mazingira yaliyo perfect basi designer yupo
 
Binafsi sipendi kubishana kisa dini hapana sipendi kabisa
Sasa uko hapa kufanya nini?

Kwa nini hukubaki hukohuko na hiyo dini yako?

Kilicho kuleta hapa ni nini?
kwa sababu maandiko yapo katika biblia takatifu na Quran tukufu maandiko yanathibitisha kuwepo katika zama mbali mbali hasa watu kukataa kuhusu mungu haupo peke yako wapo maelfu ya watu hawaamini katika mola mlezi.
Zama zipi?

Miaka ipi? Miezi ipi? Tarehe ipi na ipi?

Hizo Hekaya za Quran na Biblia mbona hazija specify muda exactly?
Lakini utambue uwepo wa mola mlezi yupo na anatenda miujiza na mambo ya ajabu katika ulimwengu wake.

Wewe hapo hebu jiulize mungu amekuepusha na mambo mangapi mabaya na upo salama mpaka Leo hii
 
Tumepewa hiari ya kuchagua (freewill) kaa utafakari zaidi kama bado unaishi
Hii freewill ni illusion tu.

Huchagui kuzaliwa au kutozaliwa.
Wala utazaliwa lini, wala utazaliwa wapi, wala utazaliwa na wazazi gani, wala utazaliwa na vinasaba gani. Hatuchagui bahati za maisha tu kwamba tutakutana na nani lini katika mazingira gani.

Hapo hakuna freewill.

Haya ni mambo muhimu sana katika maisha yako.

Mimi kuna wakati nilikuwa nabishana na rafiki zangu. Nikasema mimi ni mtu niliyejitahidi sana kusoma mambo mengi. Nimefanya kazi ya kusoma kujielimisha katika dunia yenye wavivu wengi, na hivyo hao wavivu wa kusoma wakishindwa kujua mengi, hilo ni kosa lao, na mimi kujua mengi ni matokeo ya kazi yangu.

Nikasema nimesoma library ya nyumbani, ninesoma Tambaza library, nimesoma vitabu vya library ya IST, nimesoma Tanganyika library, nimesoma British council na kwingine kwingi.

Rafiki yangu mmoja akaniambia hizo zote ni privileges tu. Akaniambia wewe umebahatika kuzaliwa na wazazi wenye elimu ambao wameweza kuwa na home library, umekuwa na access ya hizo libraries zote na kupewa muda wa kusema. Hizo zote ni privikeges zilizotokana na ajali ya kuzaliwa.

Ungezaliwa familia ya wakulima masikini huko Malampaka, usingekuwa na privileges zote hizo.

Nikafikiria sana kuhusu kauli ile, nikajikuta siwezi kujataa kuwa nimeweka juhudi binafsi kujielimisha, lakini pia, kama mtoto wa Oysterbay ambaye wazazi wangu walisoma, ambaye famikia yangu ina mabalozi kadhaa na ranking civil servants tangu siku za uhuru, kuna mambo mengi sana ambayo mimi naweza kuona nimefanya kwa utashi wangu lakini ukweli ni kwamba nineweza kufanya kwa sababu nimeshapeea pa kuanzia vizuri.

Yani hii habari ya freewill ni kama mtu anachagua movie ya Netflix kuangalia, akifikiri yeye ana uhuru wa kuchagua movie anayoitaka, lakini, hizo movies zenyewe anazochagua kashachaguliwa na Netflix, kuna movies hazipo Netflix, hata zikizopo Netflix kuna zike zinazoketwa juu na algorithm ya Netflix, nyingine ziko mbali sana hataziona.

Kwa hiyo hata pale anapoona anachagua movie kwa uhuru wake, uhuru wake mwenyewe hauko huru hivyo.
 
Kiranga nikuulize na wewe huu ulimwengu tunaoishi wenye Kila kitu very perfect ulitokea tu Kwa bahat mbaya ????
Hata kama hatujibiwi maswali yetu na viulizi vyetu na mungu alieumba ulimwengu huu , haiwezi ikawa Sababu kwamba eti mungu hayupo
Kwanza kabisa, si kweli kwamba ulimwengu huu una kila kitu very perfect.

Ukisema ulimwengu huu una kila kitu very perfect unamaanisha nini?
 
Sasa uko hapa kufanya nini?

Kwa nini hukubaki hukohuko na hiyo dini yako?

Kilicho kuleta hapa ni nini?

Zama zipi?

Miaka ipi? Miezi ipi? Tarehe ipi na ipi?

Hizo Hekaya za Quran na Biblia mbona hazija specify muda exactly?
kabla sijaendelea mbele zaidi nikukumbushe siku zote mwana wa adamu husahau kabisa kabisa hasa uwepo wa mungu.

Wewe unaonekana kijana mdogo mwenye kujitoa ufahamu na KUAMINI ya kwamba hakuna mungu. Je nahitaji uthibitishe kwanini hakuna mungu.

Mungu mtukufu anakupenda Sana pia anakupa rehema zake kwa maana hasira zake ni kali mno hakuna wa kuzuia.

Kwa mtazamo wangu kupitia maandiko yako basi ni dhahiri hujapitia katika mafundisho ya kimungu kanisani au msikitini.

Ukweli ni kwamba kwa Karne ya miaka 17 wazungu walitumia biblia kama fimbo ya kuingia katika makoloni yake na hatimaye kuitafsirisha dini sehemu ya biashara pia na waarabu ni hivyo hivyo. Kwahiyo mkuu usipende kuongelea jambo ambalo huna uhakika kuwa eti mungu hayupo.
 
Habari wana-JF!

Najua huu uzi wafia dini watausoma kwa kusonya ila ndiyo hivyo inabidi tuvumiliane tu.

Mimi nimekulia katika Ukristo, sijaukana ila nimeliacha kanisa kimyakimya. Baada ya kuanza kukua na kujitambua nilikuwa na maswali mengi sana juu ya nadharia zote kumuhusu Mungu na maswali yangu yote yalikuwa hayana majibu yaliyonyooka.

Baada ya udadisi wa muda mrefu nikafikia hitimisho kuwa "hakuna Mungu" kwasababu angekuwepo na majibu ya maswali yangu yangekuwepo.

Uwanda wa imani ni mpana ila ukiwa ndani ya imani chini ya tawi la dini ni mwiko kudadisi uwepo wa Mungu, huko ni "ndiyo" tu hakuna kuhoji.

Maisha baada ya kulikimbia kanisa yamekuwa na amani kwasababu:

1. Maisha yangu yapo mikononi mwangu.

2. Sina hofu juu ya kifo wala kuzimu kwasababu siamini hadithi za maisha baada ya kifo.

3. Naishi kwa kufuata katiba na sheria za nchi na si vinginevyo.

4. Siishi maisha kwaajili ya kumpendeza yoyote au kitu chochote.

5. Napata muda mwingi wa kufanya mambo ya msingi, siku ya Jumapili kwangu ni kama siku nyingine ya wiki.

6. Badala ya kuhangaika kutafuta maarifa ya maisha ya mbinguni (kusoma biblia), natafuta zaidi maarifa yatakonisaidia kwenye maisha ya hapa duniani maana ndiyo sehemu pekee ninayothibitisha ni ya kweli.

7. Najiheshimu. Kwangu kulia na kuomba msaada kwa M(i)ungu ni kutojiheshimu kama binadamu.

8. Nikipata matatizo sikai chini kuomba na kusubiri miujiza badala yake natumia maarifa niliyonayo kutafuta ufumbuzi.

9. Siishi kwa matumaini ya kuzawadiwa uzima wa milele.

10. Nimepishana na utapeli. Kama wanavyosema "wajinga ndiyo waliwao".

Siamini kama kweli Mungu yupo, lakini kama yupo hawezi kuwa mjinga kama anavyoelezewa kwenye vitabu vya dini.

Mungu hayupo, lakini kama angekuwepo hastahili utukufu wala unyenyekevu kutoka kwangu.

The sweet, sweet relief of knowing I'm going to hell no matter what I do! 🙃
Nimei pronpt Meta AI hapa.

Me: What are the problems of an overly religious society?

Meta AI: An overly religious society can face several problems, including:

1. Intolerance and discrimination: Against those who hold different beliefs or no beliefs.
2. Restriction of individual freedoms: Limiting personal choices and autonomy.
3. Science and progress hindrance: Rejecting scientific advancements and critical thinking.
4. Social divisions and conflicts: Creating tensions between different religious groups.
5. Lack of critical thinking and education: Prioritizing dogma over knowledge and inquiry.
6. Oppression of minorities and women: Justifying discrimination through religious texts.
7. Mental health issues: Guilt, shame, and anxiety from strict religious expectations.
8. Economic stagnation: Prioritizing religious institutions over economic development.
9. Political manipulation: Using religion to control and manipulate citizens.
10. Human rights violations: Justifying harmful practices through religious beliefs.
11. Lack of artistic and cultural expression: Restricting creative freedom.
12. Fear and mistrust: Encouraging fear of hell, damnation, or divine retribution.
13. Resistance to social progress: Opposing social reforms and equality.
14. Educational limitations: Restricting access to comprehensive education.
15. Healthcare limitations: Restricting access to medical care and family planning.

It's essential to strike a balance between religious freedom and individual rights, promoting tolerance, inclusivity, and critical thinking.

(Note: These problems can arise in societies where religion dominates all aspects of life, but not necessarily in societies with a healthy balance of religion and secularism.)
 
Na
Kwanza kabisa, si kweli kwamba ulimwengu huu una kila kitu very perfect.

Ukisema ulimwengu huu una kila kitu very perfect unamaanisha nini?
Na wewe nipe sababu ya kusema hii Dunia haiko perfect, nini kimekosekana kwenye hii Dunia au nini kimekosekana
 
Wengi wanazaa Kwa uchungu...kuwepo Kwa wanaozaa Kwa oparesheni kutokana na changamoto zao haizuii kuona ukubwa wa muumba wetu ,na tumnamshukuru sana Kwa uwezo aliotupa binadamu kusaidia ambao wanachangamoto ya kuzaa Kwa kawaida..mpe Maua yake mungu asee
Wewe hujaelewa nilicho kiandika kabisa ,hapo mwazo church lilizuia mwanamke kufanyiwa surgery, walitaka mwanamke azae Kwa uchungu Kwa bible ilivyo andikwa.

Hata ivyo huo ujuzi wa upasuaji ni binadamu mwenyewe kajifunza through try and errors mpaka wakafanikiwa kufanya surgery kwa mafanikio makubwa , Mungu hakuwasaidia Kwa lolote kufanikisha upasuaji huo .Kwa mama mjauzito.

Ina maana wewe Historia ya kanisa, Islam bado huzijui ?
 
Na
Na wewe nipe sababu ya kusema hii Dunia haiko perfect, nini kimekosekana kwenye hii Dunia au nini kimekosekana
Kwanza kabisa, ujinga ni imperfection.

Dunia hii ina ujinga mwingi.

Mjadala huu unaonesha kuna ujinga sehemu fulani katika uelewa wetu wa habari za Mungu, ndiyo maana hatuelewani.

Wote tungekuwa na uelewa nzuri, kungekuwa hakuna mjadala. Wote tyngeelewana vizuri.

Huu mjadala tu unaonesha ulimwengu hauko perfect. Una ujinga. Ujinga ni ukosefu wa maarifa, ni imperfection.

Kwenye ulimwengu perfect hakuna ujinga wowote.
 
Kuna sehemu nimekushikia fimbo kukulazimisha au kumlazimisha mtu Mungu hayupo?

Na wewe kama unajua huyo Mungu yupo kaa kimya, umwache huyo Mungu ajiongelee mwenyewe kama yupo.

Kwa nini unahangaika kumuongelea huyo Mungu?

Kwa nini unahangaika kuelezea wengine juu ya uwepo wa huyo Mungu?

Kwa nini Hukai kimya, Huyo Mungu ajiongelee mwenyewe kama yupo?
😹😹😹
 
Habari wana-JF!

Najua huu uzi wafia dini watausoma kwa kusonya ila ndiyo hivyo inabidi tuvumiliane tu.

Mimi nimekulia katika Ukristo, sijaukana ila nimeliacha kanisa kimyakimya. Baada ya kuanza kukua na kujitambua nilikuwa na maswali mengi sana juu ya nadharia zote kumuhusu Mungu na maswali yangu yote yalikuwa hayana majibu yaliyonyooka.

Baada ya udadisi wa muda mrefu nikafikia hitimisho kuwa "hakuna Mungu" kwasababu angekuwepo na majibu ya maswali yangu yangekuwepo.

Uwanda wa imani ni mpana ila ukiwa ndani ya imani chini ya tawi la dini ni mwiko kudadisi uwepo wa Mungu, huko ni "ndiyo" tu hakuna kuhoji.

Maisha baada ya kulikimbia kanisa yamekuwa na amani kwasababu:

1. Maisha yangu yapo mikononi mwangu.

2. Sina hofu juu ya kifo wala kuzimu kwasababu siamini hadithi za maisha baada ya kifo.

3. Naishi kwa kufuata katiba na sheria za nchi na si vinginevyo.

4. Siishi maisha kwaajili ya kumpendeza yoyote au kitu chochote.

5. Napata muda mwingi wa kufanya mambo ya msingi, siku ya Jumapili kwangu ni kama siku nyingine ya wiki.

6. Badala ya kuhangaika kutafuta maarifa ya maisha ya mbinguni (kusoma biblia), natafuta zaidi maarifa yatakonisaidia kwenye maisha ya hapa duniani maana ndiyo sehemu pekee ninayothibitisha ni ya kweli.

7. Najiheshimu. Kwangu kulia na kuomba msaada kwa M(i)ungu ni kutojiheshimu kama binadamu.

8. Nikipata matatizo sikai chini kuomba na kusubiri miujiza badala yake natumia maarifa niliyonayo kutafuta ufumbuzi.

9. Siishi kwa matumaini ya kuzawadiwa uzima wa milele.

10. Nimepishana na utapeli. Kama wanavyosema "wajinga ndiyo waliwao".

Siamini kama kweli Mungu yupo, lakini kama yupo hawezi kuwa mjinga kama anavyoelezewa kwenye vitabu vya dini.

Mungu hayupo, lakini kama angekuwepo hastahili utukufu wala unyenyekevu kutoka kwangu.

The sweet, sweet relief of knowing I'm going to hell no matter what I do! 🙃
Unajitekenya, halafu unacheka mwenyewe, eti? Utaishije bila Mungu, wakati Mungu huyo unayemkana ndiye anayekutunza na unaishi kwa amani kwa vile amekupa afya na ulinzi?
 
Back
Top Bottom