Maisha halisi nchini Marekani

Maisha halisi nchini Marekani

maisha yapo africa na kama tanzania achana na dar es salaam jikiteni mikoani kama una mtaji ambao uwezi kushindana na mji wa dar.
Je maisha ni nini? Kwenda hospitali isiyo na uwezo wa kujua tatizo lako, kwenda shule au chuo usiwe na uhakika wa kuelimika, kulima kwa njia ngumu bila vifaa, na kukosa soko au kupigwa marufuku na serikali ya kuuza unapotaka, achilia mbali, kodi, tozo zisizoeleweka, polisi kukubambikia watakalo, rushwa, wizi kila sekta?
Maisha ni zaidi ya kipato.
 
Habari JF

leo Katika mada yangu kichwa tajwa hapo juu, Ningependa nishare nanyi Uzoefu wangu wa maisha ya marekani, maana nimeona watu wengi sana wakijadili namna watu wanavyoishi nje, ajabu kati ya mia, tano tu ndo wanaelewa maisha halisi ya marekani.

Licha mimi huwa sipendi kuishi Marekani, lakini fursa zilizopo ndo zinatufanya tuelendelee kunganagia haya maisha, ndomana maisha yangu ya uwekezaji Yapo africa lakini utafutaji ni marekani kwa vile tu sijafikia malengo yangu ya maisha.

Miaka 6 ndani ya nchi ya marekani, ninaishi kwa Green card, nina ruhusiwa sasa kuomba uraia lakini mimi kwangu huwa si kipaumbele, maana nina uwezo wa kutoa na kuingia na kukaa nje ya marekani muda wa miezi sita.

Nimeishi majimbo na kufanya kazi kampuni tofauti tofauti, Mara nyingi nafanya hivyo tu ili kujifunza maisha halisi ya marekani. Mwaka jana nimefanya kampani saba na kuishi majimbo matatu. kufanya kazi marekani huwa nafanya tu kukaa bila kazi. nilichokifanya miaka minne ya marekani niliweka nguvu kuwekeza nyumbani jambo ambalo nilifanikiwa na kunipa huakika wa kuishi hapa bila kuwa na kazi.

Katika Harakati zangu za kucompare africa na marekani sehemu nzuri ya kuishi, niligundua africa kinachotufelisha ni uchumi ila ukiwa na pesa napendekeza kuishi afrca badala ya marekani. Marekani ni sehemu tu ya utafutaji ikiwa africa huna cha kupoteza(maono yangu)

MAZURI YA MAREKANI.
naipenda nchi ya marekani ni nchi ambayo inamuwesha kila mtu bila kujali nchi uliotokea kufanya lolote na ukafanikiwa, tofauti na nchi kama vile urusi, china. marekani ni nchi ya kila mtu kufanya anachoweza yaani nchi ya fursa. ukitaka kuwa doctoe, nurse nk.. hata kama umefeli elimu katika nchi yako marekani kuna njia nyingi za kukuwezesha ukarudi shule na ukatimiza ndoto zako.

Ikiwa ndo mara ya kwanza unaingia marekani, Kitu cha kwanza jifunze sana kingereza, kitu cha pili somea fani yeyote, cha tatu kuchuka Credit card. ukiwa na hayo matatu nchi ya marekani umemaliza mambo mengine yanakuja, na hayo yote inawezekana kufanyika kwa mtu yeyote anaishi marekani kihalali.

kazi na makazi, siwezi kushauri kuishi kwenye miji kama Chicago, New york, washington nk.. mara nyingi miji hii kazi zake ni professional. tena ina gharama kubwa ya rent. badala yake nenda kwenye majimbo kama dakota, kenctuky , mara nyingi ni kazi za viwanda au Entry job alafu rent iko chini.

Watu wengi kutoka nje ya marekani wanafanya ENRTY JOBS kutokana na lugha kuwa ngumu alafu pesa zinawachanganya hawataki kusoma.

Marekani kuna uraisi wa kumiliki nyumba gari na kufanya biashara unayotaka(biashara ya import chakula na kuuza kwenye maduka ya africa inalipa). hata kama huna huwezo huo. unaweza kutumia CREDIT yako na kupata nyumba, gari, au pesa baadae utalipa taratibu. kikubwa deal na Scores zako kuwa HIGH, na Credit ni kitu muhimu sana marekani.

Kazi ni nyingi na unaruhususiwa kufanya kazi masaa yote unayotaka hata kuwa na zaidi zaidi ya kumi, Mfano mimi nina ENTRY JOBS ndo always huwa nafanya kazi za aina hii, Kazi yangu ya Sasa Ni HMI CLASS tunatengenza class, nafanya kazi masaa 8 kila siku nalipwa $21 kwa saa na overtime $27, awali ilikuwa GE Appliance nilikuwa nalipwa $19, Before GE ilikuwa Fedex nilikuwa nalipwa $19.50, kabla ya Fedex ilikuwa Amazon $20.

Now kazi yangu ya sasa nafanya masaa ninayotaka nikisema kwamba nataka nipate $5000 mwezi huu inapatikana na gharama zangu za maisha ya marekani hazifiki hata $600(bills). So hapo nina kitu cha kufanya tayari africa. Imagine miez 12 ya kazi nikiruid africa huwez kusema tunarudi tumechoka.

Fursa nyingine ambayo kwangu huwa naona ni muhumu sana hapa marekani ni technology, Iphone ilipo marekani sio iliopo africa, chrome inavyofanya kazi marekani ni tofauti kabisa na africa, System za simu na Feature baadhi za Social Media ziko tofauti. kuna software kama vile Stripe huwezi kujiunga ikiwa unaishi africa, so mambo kama hayo ni muhimu sana na ni fursa kubwa.
Hat banl system ni tofauti kabisa zinavyotumika africa.

So kuishi marekani kuna fursa ya kuelimika pia, saivi ukimwabia banker maswala ya wallet pay, wireless pay, finger pay haya ni mambo mageni kwake au anasikiaga tu, ila wewe unaelimika kutoka na fursa ya mazingira unayoishi

ITAENDELEA.......
NO PM
Tunashukuru kwa ushuhuda mkuu. Japo mimi katika kusafir kwangu japo cjakaa kwenye hizo nchi niliona Canada inafursa zaid ya marekan. Kuanzia elimu na kazi kama hiz unazosema. Nimefika hizo nchi mbili ila marekan nilifika hiyo miji mikubwa. Na life lake ni kama Hongkong .singapore nk. Kwa mtu aliyetoka nchi masikin kama zetu ni kweli ni vizur kuish miji midogo.
 
Tunashukuru kwa ushuhuda mkuu. Japo mimi katika kusafir kwangu japo cjakaa kwenye hizo nchi niliona Canada inafursa zaid ya marekan. Kuanzia elimu na kazi kama hiz unazosema. Nimefika hizo nchi mbili ila marekan nilifika hiyo miji mikubwa. Na life lake ni kama Hongkong .singapore nk. Kwa mtu aliyetoka nchi masikin kama zetu ni kweli ni vizur kuish miji midogo.
Singapore ni balaaa marekaani ikasome ..Kule maisha ni ghali mnoo
 
Habari JF

leo Katika mada yangu kichwa tajwa hapo juu, Ningependa nishare nanyi Uzoefu wangu wa maisha ya marekani, maana nimeona watu wengi sana wakijadili namna watu wanavyoishi nje, ajabu kati ya mia, tano tu ndo wanaelewa maisha halisi ya marekani.

Licha mimi huwa sipendi kuishi Marekani, lakini fursa zilizopo ndo zinatufanya tuelendelee kunganagia haya maisha, ndomana maisha yangu ya uwekezaji Yapo africa lakini utafutaji ni marekani kwa vile tu sijafikia malengo yangu ya maisha.

Miaka 6 ndani ya nchi ya marekani, ninaishi kwa Green card, nina ruhusiwa sasa kuomba uraia lakini mimi kwangu huwa si kipaumbele, maana nina uwezo wa kutoa na kuingia na kukaa nje ya marekani muda wa miezi sita.

Nimeishi majimbo na kufanya kazi kampuni tofauti tofauti, Mara nyingi nafanya hivyo tu ili kujifunza maisha halisi ya marekani. Mwaka jana nimefanya kampani saba na kuishi majimbo matatu. kufanya kazi marekani huwa nafanya tu kukaa bila kazi. nilichokifanya miaka minne ya marekani niliweka nguvu kuwekeza nyumbani jambo ambalo nilifanikiwa na kunipa huakika wa kuishi hapa bila kuwa na kazi.

Katika Harakati zangu za kucompare africa na marekani sehemu nzuri ya kuishi, niligundua africa kinachotufelisha ni uchumi ila ukiwa na pesa napendekeza kuishi afrca badala ya marekani. Marekani ni sehemu tu ya utafutaji ikiwa africa huna cha kupoteza(maono yangu)

MAZURI YA MAREKANI.
naipenda nchi ya marekani ni nchi ambayo inamuwesha kila mtu bila kujali nchi uliotokea kufanya lolote na ukafanikiwa, tofauti na nchi kama vile urusi, china. marekani ni nchi ya kila mtu kufanya anachoweza yaani nchi ya fursa. ukitaka kuwa doctoe, nurse nk.. hata kama umefeli elimu katika nchi yako marekani kuna njia nyingi za kukuwezesha ukarudi shule na ukatimiza ndoto zako.

Ikiwa ndo mara ya kwanza unaingia marekani, Kitu cha kwanza jifunze sana kingereza, kitu cha pili somea fani yeyote, cha tatu kuchuka Credit card. ukiwa na hayo matatu nchi ya marekani umemaliza mambo mengine yanakuja, na hayo yote inawezekana kufanyika kwa mtu yeyote anaishi marekani kihalali.

kazi na makazi, siwezi kushauri kuishi kwenye miji kama Chicago, New york, washington nk.. mara nyingi miji hii kazi zake ni professional. tena ina gharama kubwa ya rent. badala yake nenda kwenye majimbo kama dakota, kenctuky , mara nyingi ni kazi za viwanda au Entry job alafu rent iko chini.

Watu wengi kutoka nje ya marekani wanafanya ENRTY JOBS kutokana na lugha kuwa ngumu alafu pesa zinawachanganya hawataki kusoma.

Marekani kuna uraisi wa kumiliki nyumba gari na kufanya biashara unayotaka(biashara ya import chakula na kuuza kwenye maduka ya africa inalipa). hata kama huna huwezo huo. unaweza kutumia CREDIT yako na kupata nyumba, gari, au pesa baadae utalipa taratibu. kikubwa deal na Scores zako kuwa HIGH, na Credit ni kitu muhimu sana marekani.

Kazi ni nyingi na unaruhususiwa kufanya kazi masaa yote unayotaka hata kuwa na zaidi zaidi ya kumi, Mfano mimi nina ENTRY JOBS ndo always huwa nafanya kazi za aina hii, Kazi yangu ya Sasa Ni HMI CLASS tunatengenza class, nafanya kazi masaa 8 kila siku nalipwa $21 kwa saa na overtime $27, awali ilikuwa GE Appliance nilikuwa nalipwa $19, Before GE ilikuwa Fedex nilikuwa nalipwa $19.50, kabla ya Fedex ilikuwa Amazon $20.

Now kazi yangu ya sasa nafanya masaa ninayotaka nikisema kwamba nataka nipate $5000 mwezi huu inapatikana na gharama zangu za maisha ya marekani hazifiki hata $600(bills). So hapo nina kitu cha kufanya tayari africa. Imagine miez 12 ya kazi nikiruid africa huwez kusema tunarudi tumechoka.

Fursa nyingine ambayo kwangu huwa naona ni muhumu sana hapa marekani ni technology, Iphone ilipo marekani sio iliopo africa, chrome inavyofanya kazi marekani ni tofauti kabisa na africa, System za simu na Feature baadhi za Social Media ziko tofauti. kuna software kama vile Stripe huwezi kujiunga ikiwa unaishi africa, so mambo kama hayo ni muhimu sana na ni fursa kubwa.
Hat banl system ni tofauti kabisa zinavyotumika africa.

So kuishi marekani kuna fursa ya kuelimika pia, saivi ukimwabia banker maswala ya wallet pay, wireless pay, finger pay haya ni mambo mageni kwake au anasikiaga tu, ila wewe unaelimika kutoka na fursa ya mazingira unayoishi

ITAENDELEA.......
NO PM
Nina uhakika kwa zaidi ya 90% mleta mada hauishi marekani, ni hadithi zako za kutunga tunga. Nikikusoma between the lines naona wazi kabisa huijui Marekani. Kwa mfano:
1. Unazungumzia suala la Credit card kama kitu cha ajabu wakati ni jambo ambalo karibu kila mtu aliyepo Marekani anamiliki.

2. Unazungumzia issue za kusomea fani kama Udaktari kuwa ni issue rahisi na kawaida kwa mbongo kuweza kusomea akitaka akiwa Marekani wakati sio jambo rahisi kabisa ukiwa marekani.

3. Unasema umeshafanya kazi kwenye zaidi ya makampuni 7 ili kupata exposure tu wakati kiuhalisia huna kazi rasmi na unaishi kama kibarua tu, huku suala la ajira kwa US nalo limekuwa changamoto, na watu wanazisaka na hufanya kazi ili kuweza kuishi tu na sio their choice job.


4. Unasema mtu unatengeneza zaidi ya dola 5000 kwa mwezi lakini unaishi kwa dola 600 tu halafu hizo zote zinazobakia unazileta kuwekeza nyumbani Tz! Hizo ni hadithi za Abunawasi. Wakati kuna utitiri wa Diaspora hawana chochote Tz na hawana chochote US, wapo wapo tu, na siku wakifa huishia kuchomwa moto huko huko marekani.

5. Unazungumzia issue ya Green card kuwa unaimiliki as if ulikwenda marekani na kupewa au kuipata kama njugu, haki yako au uamuzi wako tu kuipata. Wakati kiuhalisia Green card ni mchakato mrefu, na karibu kila mtu anausaka huko Marekani na wachache hubahatika.

6. Unasema ukiwa US ni rahisi kumiliki nyumba! Huu ni uongo wa 100%. Hivi Diaspora wangapi wanamiliki nyumba marekani?
 
Hivi mbona mmoja wenu huko akifariki huko Kusafirisha Mwili tu huwa ni Shughuli Pevu.?
Bakuli La michango linatuhusu mpaka huku Kwa Mtogole.!
Halafu Mkifiwa na Mzazi Utasikia Mtoto Kashindwa Nauli Kuja Kumzika Mzazi Wake..! Hivi Diaspora Tuelezeni shida nini?
Mi mwenyewe nilitaka Kuja kuwa Diaspora ila ninachokishuhudia Kinachowatokea huko nimeghairi..!

Katika Diaspora 20 ni Wawili au Watatu ndo Wanatoboa.
Jaribu kutofautisha kati ya wazamiaji haramu na waishio huku kihalali.
 
Jaribu kutofautisha kati ya wazamiaji haramu na waishio huku kihalali.
Sasa Wewe Ambaye Upo huko Kihalali Huwataki Diaspora Wenzio Waliofika huko Kwa Kuzamia.?
Sisi huku tunawatambua wote mpo Majuu,Kwaiyo ndo Kusema Mkikutana huko wala hamsalimiani na Kupeana Michongo.!
Ndo maana Wengine ni Choka mbaya ..!
 
Nina uhakika kwa zaidi ya 90% mleta mada hauishi marekani, ni hadithi zako za kutunga tunga. Nikikusoma between the lines naona wazi kabisa huijui Marekani. Kwa mfano:
1. Unazungumzia suala la Credit card kama kitu cha ajabu wakati ni jambo ambalo karibu kila mtu aliyepo Marekani anamiliki.

2. Unazungumzia issue za kusomea fani kama Udaktari kuwa ni issue rahisi na kawaida kwa mbongo kuweza kusomea akitaka akiwa Marekani wakati sio jambo rahisi kabisa ukiwa marekani.

3. Unasema umeshafanya kazi kwenye zaidi ya makampuni 7 ili kupata exposure tu wakati kiuhalisia huna kazi rasmi na unaishi kama kibarua tu, huku suala la ajira kwa US nalo limekuwa changamoto, na watu wanazisaka na hufanya kazi ili kuweza kuishi tu na sio their choice job.


4. Unasema mtu unatengeneza zaidi ya dola 5000 kwa mwezi lakini unaishi kwa dola 600 tu halafu hizo zote zinazobakia unazileta kuwekeza nyumbani Tz! Hizo ni hadithi za Abunawasi. Wakati kuna utitiri wa Diaspora hawana chochote Tz na hawana chochote US, wapo wapo tu, na siku wakifa huishia kuchomwa moto huko huko marekani.

5. Unazungumzia issue ya Green card kuwa unaimiliki as if ulikwenda marekani na kupewa au kuipata kama njugu, haki yako au uamuzi wako tu kuipata. Wakati kiuhalisia Green card ni mchakato mrefu, na karibu kila mtu anausaka huko Marekani na wachache hubahatika.

6. Unasema ukiwa US ni rahisi kumiliki nyumba! Huu ni uongo wa 100%. Hivi Diaspora wangapi wanamiliki nyumba marekani?
Kwani wewe unaishi US pia?
 
Wewe ni mvivu na hauna uwezo mkubwa wa kushindana na kupambana kiakili.
Mimi nimekaa Marekani mji wa Washington. Ubaya wa Marekani hakuna undugu kila mtu kivyake kiutafutaji. Maisha ya Marekani ni magumu sana kwa kiingereza tunaita hand to mouth. Kwa gharama ya $600 kwa mwezi naona mtu huyo anapata mateso makubwa. Kama alivyosema kuwa anaweka akiba ya $4500 kwa mwezi. Kwa Afrika ukiwa unajishughulisha hicho kiasi ni kidogo kwa mfanyabiashara wa Afrika. Kinachotuharibu hapa Afrika hatuna utaratibu mzuri wa maisha. Familia tegemezi za afrika huwezi linganisha na familia ya America ya mtu mmoja, mkewe na mtoto. Nawashauri hapa kwetu Afrika kuna fursa nyingi sana kuliko America ambapo hata usingizi hupati kwa kudandia kazi za kuhama hama kwa siku.
 
Kwani mtu akienda kuishi Marekani lazima atoboe? Change your Stupid and Idiotic Mindset.
Kwahiyo unaenda kufanya nini kama hakuna mafanikio?.........unapoteza 20yrs ughaibuni, unarudi kuanza maisha upya hapa bongo that's life failure, na wengi wamefeli maisha kwa kufuata mawazo ya motivational speaker kama mtoa uzi,

anapotosha vijana kwa kuweka mindset yao kuwaza Marikani, US isn't as simple kama alivo andika, hayo yote kasimliwa na watu walio feli maisha ya ughaibuni, maratino wengi kutoka Mexico na latini America ni machokora hawana chochote na hawana nyuma au mbele wanaanza kua drug addicts tena ni majirani na Us ndo uanze kudaganya Msabaa wa bongo aende kupoteza mda na pesa zake, after 20yrs arudi vile vile,na kuonyesha picha za barafu tu.

Kwa wanao ende ughaibuni ni 10% ndo wanafanikisha tena their cases are special 90% wanabakiza stori na picha za barafu huo ndo ukweli, naongea hili out of experience en peacticle examples kwa ndg jamaa marafiki na mimi mwenyewe.
 
Wabongo tunapaswa kufahamu kuwa, tupate exposure yakuja kuwekeza bongo ila tusijidanganye kuwa mifumo ya nchi za magharibi zinaweza kusaidia kuvimba ugenini.
Ukiamua kupata na kutoboa kwanini usivimbe?

Raia wa nchi nyingine wanatoboa?

Angalia wachezaji wa africa kwenye ligi za ulaya. Hawavimbi?

Huu ushamba wa lazima kurudi home mnautoa wapi?
 
Ukiamua kupata na kutoboa kwanini usivimbe?

Raia wa nchi nyingine wanatoboa?

Angalia wachezaji wa africa kwenye ligi za ulaya. Hawavimbi?

Huu ushamba wa lazima kurudi home mnautoa wapi?
Kutoboa kupo popote ila nu asilimia ngapi wanao fanikisha kwa huyo njia
 
Ndio maana nasema wanakuja kuchuma na kuondoka.

Mitaji mikubwa ipo concentrated in Dar. Nyie ndo mnakuwa mawakala wa kuwaibia wanyonge wenzenu.

Nimetembea mikoa yote kasoro Mara na Zanzibar. Hizo fursa hazipo na hazitakaa ziwepo.

Miundombinu bora ipo mijini, huduma bora za afya na elimu zipo mijini.

Mpaka leo wakazi wa Ifakara huko hawana barabara, unakaza kichwa uende ukalime mpunga kisa fursa ipo.

Utaishia kuuza mashineni tajiri atoke Dar akauze mara 2. Unadhani nani amefaidika hapo.?
Duuuh umetaja kwetu kabisa, alafu ifakara kilimo cha kubahatisha nililima nusu nife kuulizia km mvua inenyesha au laah sintasahau
 
Shida ni kuwa hata Lemutuz mwenye konekshen amekaa marekani miaka 30 lakin leo hii karudi anaishi kwa baba na anamiaka 60+
Kama marekan panalipa endelea kuish mkuu ila ukiona hali ni mbaya usione aibu kurud maana usije ukarud mzee na huna hata familia na wenzako uliowaacha wamepiga hatua zaid
 
Back
Top Bottom