Maisha ya Biashara Bongo ni magumu kumaintain, Yapo Overrated kwa kuangalia wachache waliopiga mshindo, nasisitiza ajira serikalini ndio mpango

Biashala za wabongo

"Nunua bajaji moja, milioni 7, mpe dreva, kila siku atakuletea elfu 30, kwa wiki laki 2, kwa mwezi kwa mwaka utakua umetusua kimaisha.."
Bajaji kwasasa bei ni kati ya 10M -12M kwa ya mafuta na petroli.

Moto bado mkali masta
 
Sijasoma yote nimeishia hapo kwa Mo,Bahresa na GSM.
Wewe muongo na muoga na mvivu sana. Sijui jinsia gani?
Yaani wewe huku kwenye underground ndio uanze kwa kujifananisha au hata uwe sawa na akina Bahresa?. Unajua Bahresa alianzia wapi?.

Mawazo yako yameganda. Wewe unahisi kuna watu walipiga hela mshindo kama ulivyosema. Endelea kuota. Hivi unavyoendelea kuota kuna mtu anaanza biashara leo. Ukiwa bado usingizini,kuja kuamka atakuajiri..

Hakuna biashara inayoanzia juu. Biashara zote lazima upambane huku chini.
 
Ndio maana kina hata Fenandes wa Nala kahamishia biashara yake Kenya, kapata udhamini wa dola za kimarekani milioni 40 (shilingi za kitanzania bilioni 105)

Hakuna correlation ya Nala kuwa Kenya na 40M fund aliyopata. Nala Ipo Kenya from its inception. Hata ingekua bongo au nchi yeyote ile so long as ingekua inafanya vizuri na kuonyesha promising signs angepata hiyo fund.

In the meantime Mobius Kampuni ya kuunda magari ya Kenya imefilisika na kutangaza kufunga Kampuni.

Kuna kiwanda cha cement Kenya kinanunuliwa na wawekezaji kutoka Tanzania for over 100M USD. Kwahiyo usikariri biashara ngumu nchi zote.
 
Tupe idadi ya wafanyabiashara tuone uchache wao pia idadi ya watumishi tulinganishe
 
Kuna Point za Msingi kama Nne:

Moja Bongo tuna wachuuzi na madalali (from government to mtu wa chini) ofcourse hao bado ni wafanyabiashara pia ila ni mwendo wa kubangaiza na kucheza pata potea.... The real wealth creators, the corporations au niseme the conglomerates hata duniani ni wachache let alone Bongo (na ukishafika at that level wewe ndio unatunga sheria na kuongoza serikali hence you can not lose)

Mbili SECURITY, mwajiriwa ana Security ya kupata hata kama ni kidogo na siku akizeeka ana retirement pension hence ana minimum amount which is guaranteed

Tatu sababu umeongelea maisha basi inabidi mtu mwenyewe ajitazame, biashara pia ni hobbie na lifestyle ya mtu mwingine anapenda deal making na accumulating of wealth, ingawa inahitaji discipline kubwa ambayo wachache wanayo

Hitimisho sababu umeongelea maisha inabidi mtu binafsi kujiuliza kwanini UNAISHI...
 
Tuulizane Kwanini watanzania wenye asili ya wahindi, waarabu hawaombi ajira serikalini?? Je tukilinganisha maisha yao na ya wafanyakazi yapi bora?

Hata mishahara mnayolipwa ni pesa za kodi 😂No biashara =No kodi =No ajira, biashara ndiyo boss.

Jiulize kwanini wastaafu hujitahidi kuanzisha biashara?? 😃😃Usiseme hukuambiwa.
 
Biashara sio ngumu shida ni sisi Watanzania kufanya biasbara za kizamani za kuigana Biashara za Frame economy,Biashara za kichuuzi tu, Wewe hapo ukipewa mtaji leo hii utataja biashara moja kati ya zifuatazo;
1. Saloon ya kiume au kike
2.Stationaries
3.Car wash
4.Pub
5.Duka la vipodozi
6.Duka la nguzo za kike na kume
7.Dalaladala
8.Min supermarket
9.Duka la jumla na reja reja
10. Mpesa agents

Hizo ndio biashara za kibongo, lazima kutoboa iwe ngumu, tunapenda biashara sizizo umiza akili, biasjara za kuigana then tunakuja humu kujatisha tamaa.
 
Wabongo tunajua biashara? au unazungumzia biashara za kuigana za kichuuzi
 
Swala sio mtaji swala ni kwamba Watanzania Biashara tunaso zijuia ni za uchuuzi za kuwa na Frame katikati ya mji
 
Mkuu shida inayo yufanya tusitoboe Tanzania ni biashara za kuigana, asilimia 80 ya biashara zetu ni za kuigana hapo lazima tulogane
 
Nimepitia huu uzi nina mawili ya kusema

1. Wengi wa wana jf ni wasomi ambao either wameajiriwa au wanasubiri ajira huku wakifanya shughuli mbalimbali ambazo wanaziita biashara

2. Ili tupate data kamili kati ya wafanyabiashara walio wengi at the ground na waajiriwa walio wengi wenye mishahara duni ni nani ana maisha yenye afadhali ni lazima tuulizane kuanzia humu tujue unafanya kitu gani na una maisha gani kwa mmoja mmoja bila kudanganya ili tuone nani ana afadhali

NB, Tukianza na mtoa mada unafanya nini(umeajiriwa au mfanyabiashara) na unamiliki nini na nini ili wengine watoe za kwao tulinganishe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…