Maisha ya machimbo ya dhahabu ni zaidi ya jeshi, nilikimbia

Bonge la stori
 
We unazungumzia saineti ambalo linaitwa rudio.

Hicho kipindi ambacho yeye alikuja shughuli za uchimbaji madini zilizokuwa zinafanyika miaka hiyo ilikuwa ni uchimbaji wa kusambaza.

Maeneo machache sana yalikuwa yanafanya extraction ya madini kutoka kwenye mawe.

Nakupa mfano mmoja Chunya Mjini kulikuwa kuna wazungu eneo fulani karibia na Kanisa la Mashahidi wa Yehova.

Hao wazungu walikuwa na mitambo ya kusaga mawe ndio waliokuwa wanatoa dhahabu za kwenye mawe.

Miaka ilivyosogea sogea ndio watu wakaanza kushtuka nao wakaja na makarasha wakawa wanasaga na profit kwa mwenye mashine alikuwa anategemea kwenye cash ya mteja anayo mchaji kwa ajili ya kumsagia mawe yake.

Lakini ilivyokuja hiyo tech ya kukamua tena ile rudio naskia wameshusha gharama huku wengine wakifanya free kusaga, kwasababu wanajua at the end watakuja kunufaika kwenye rudio.
 
Kwa simulizi ya huyu mwamba maana yake alipelekwa kwenye small mining scale/uchimbaji mdogo/uchimbaji wa kienyeji.
Ukweli ni kwamba kwenye mining industries, hakuna mzazi wa mtoto anae weza akakubali kumpeleka mwanae akachimbe kwa sururu pasipo kujua kama anauhakika wa kupata hata 1 point, ukiacha 1 gram
 
Kwenye shughuli ya machimbo unabeba zana ya jembe?

Basi hiyo ardhi ni soft sana

Nenda Chunya utaoneshwa sululu zilizopinda baada ya kukutana na hardcore rocks na vijana hawataki kukubali kuwa imeshindikana.
 
Itumbi napasikia sikia tu sikuwahi kufika, ukanda wa kusini maeneo ya matundasi, makongorosi na mkwanuni sijawahi kufika.

Ishu ya kudhulumiwa ipo sana ngoja nikupe kisa kimoja.

Kuna siku tulienda kuchimba Chunya mjini eneo moja linaitwa swiswi maeneo fulani hivi ya porini milimani kule karibia na minara ya simu.

Kufika kule nikakutana na wazee wengi waheshima nikawa najua hapa busara zipo.

Wakati naendelea kuchimba upande wa pili kuna mwana alikuwa tayari ameufikia mwala, so akaita kipimo kije kupima.

Kipimo kilivyokuja, kuna bro mmoja akatoka kwenye shimo lake akaenda kuangalia huyo mwana anavyopimiwa.

Katika kupima, kipimo kikatoa mlio ishara ya kuonesha kuna dhahabu au metal objects

Sasa ule wakati wa kuchota mchanga kugawa kwenye viganja kujua ni dhahabu au kibati, alikuja yule bro ambaye sio shimo lake, akachota mchanga kwenye viganja viwili akawa anagusisha kwenye sahani ya kipimo.

Kipimo kilivyopitishwa kwenye mkono mmoja alioshika mchanga hakikulia, akautupa ule mchanga.

Mkono wa pili kilivyopita kipimo kikatoa mlio, yule bro akasema "aaah kumbe ni kibati" halafu akaurusha ule mchanga mbali kabisa.

So jamaa wakaendelea kupima kwenye mwala, ikaonekana jamaa amepolola akarudi home.

Yule bro alisubiria watu wote wameondoka akaruri kwenye ule mchanga alioutupa kumbe kulikuwa na dhahabu sio kibati kama alivyosema, jamaa akachukua dhahabu akasepa zake.
 
Ilifika time watu wakawa wanapishana.

Yani watu wanatoka mikoa ya mbali kuja Chunya kuchimba madini, na wazawa wa Chunya wanapakimbia kwao wanaenda Zambia na Msumbiji kwenda kuchimba

Yale maisha asikuambie mtu ni msoto sana.

Huko Msumbiji walikoenda zilikuwa zinakuja story za kila aina aisee.
 
Wachimbaji wadogo wengi sana walifia Zambia na Msumbiji kwa kisingizio cha uhamiaji haramu, uhalifu na kugologosha.
Na wengi waliofanikiwa kukutana na vikole (pure gold) ndio walikutana na majanga ya aina hii...
 
Wachimbaji wadogo wengi sana walifia Zambia na Msumbiji kwa kisingizio cha uhamiaji haramu, uhalifu na kugologosha.
Na wengi waliofanikiwa kukutana na vikole (pure gold) ndio walikutana na majanga ya aina hii...
Kule kulikuwa kuna sheria ngumu kwasababu mostly hawakuwa na passport

Na bado ilikuwa hairuhusiwi kuondoka na dhahabu kule.

Wachimbaji wa huku hawakuwa tayari kuuza dhahabu Msumbiji kutokana na kwamba soko lao ni dogo, wananunua kwa bei ndogo ambayo haiwafaidishi.

Kuna jamaa alikuja home akiwa na kidonda kikubwa, akatuambia hiki kidonda ni cha kujitakia maana bila hivi nisingeweza kuficha dhahabu.

Watu tukabaki hoi midomo wazi, maswali ya mshangao tukamuuliza ina maana mchizi ulijitoboa ili ufiche tu dhahabu. Akasema ndio kwa maana kule hata kipimo tu wakikukamata nacho wanapora.
 
Uchimbaji wa dhahabu ni mgumu sana kuna jamaa mwaka jana kaacha kazi Benki kaingia kwenye hizi mishe kule Kilindi Handeni kapoteza zaidi ya milion 25 na aliambulia 7grms tu. Kazi kapoteza, hela imeisha na familia yake imemdhrau na kumtenga yaani sasa hivi kachanganyikiwa kwa kifupi dishi limeyumba na kapoteza dira kabisa na sasa hivi kaingia kwenye kubet 😅
 
Ushaelewa nazungumzia labda hata hujazaliwa, 90 huko
Unaweza ukawa mkubwa kwangu hilo naliheshimu.

Ila unachoshindwa kuelewa ni matumizi ya maneno kulingana na eneo.

Ukiwa Chunya ukimuambia mtu ulikuwa unachekecha, hautoeleweka hata umuambie mzee wa 1930.

Ukimuambia ulikuwa unasekesa au kuosha hapo atajua unazungumzia aina gani ya uchimbaji

Kuna kusekesa, kuosha, kupiga makarai, kusaga mawe na kubinuka (kusambaza)

Hizo ndio slang za machimboni kwa Chunya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…