Maisha ya machimbo ya dhahabu ni zaidi ya jeshi, nilikimbia

Maisha ya machimbo ya dhahabu ni zaidi ya jeshi, nilikimbia

hongera mkuu mdingi wako nampa pongezi kubwa sana,kwani alikupeleka kwenye chuo cha maisha ujue pesa inatafutwaje,mpaka kufikia hapo sizani kama utakuwa na matumizi mabaya yapesa au kuwadharau wengine hawajui kutafuta.mi baada ya kumaliza form six nilitimuliwa hom .maisha yangu ya kawa ya kimtaa kwetu wakishua lakini ilifikia hatua nikajiunga na wachonga kalai nashindia maji na chikichi nikaugua madonda ya tumbo lakini nika kaza.kwa siku nilikuwa napata 1000,nikadunduliza ikafika 30000 nika acha kazi hiyo.nikahamia kuchinga vyombo nanunua besen 30 napata faida 3000, nashukuru mungu nilipanda mpaka mtaji ukafika milion,..baba akawa anaulizia tu niko wapi ila taimu namimi hana.sasaiv na maisha yangu biashara kubwa,na baba anajivunia mimi, aliniita akasema sio kwamba sikupendi,niliambiwa na mchaga ili mtoto awe na akili mtimue ujifanye humpendi..baadae akaita ndugu akasema naona mwanangu shule ime mkaa sasa.namuongezea mil 2.je asingenitimua nika sota mtaani ninge kuwa na nidhamu yapesa? maisha ni chuo ndugu.
 
Mkuu hapa turudi kwenye hoja ya msingi achana na ushuani v/s uswazi.
Kwakifupi uchimbaji wa kienyeji unao usema wewe ulisha pitwa na wakati kwasababu ni kazi ya kubahatisha/haina uhakika. Zaidi watu wengi wanaufanya uchimbaji wa kienyeji kutokana kutokua na mtaji wa kutosha, kukosa elimu na umasikini.
Lakini bado nasisitiza kwamba kazi ya uchimbaji wa kienyeji ni high risk because of the nature and unsafe conditions
Ni sahihi. Ni Kweli kazi ngumu.
Mazingira ya uchimbaji wa madini (uchimbaji mdogo) Kwa nchi za kiafrika ni magumu sana. Angalia DR Congo watu wengi wameangamia Kwa sababu ya kufukiwa na vifusi Vya udongo.
Nakumbuka machimbo ya dhahabu ya kitunda-Sikonge Tabora Kuna watu wengi walifunikwa na gema kisa wanagombania mchirizi wa dhahabu.
 
Nljichanganya nkaenda mwakitolyo bila mtaj nkasema ntakomaa asee[emoji119] kwanza jua n kal sana kulko sehem yoyote tanzania dhahabu kupatikana nikwa mbinde sana yan unachakaa mpaka unajisahau siku ukitaka kwenda mjin inabid upumzke hata siku mbil kwanza unyoe uoge mara mbil mbil il kesho hata ukienda mjin uonekane n mtu. Machimbon maisha ni ghal sana na hela ni ngum sana kupatikana
Nmecheka sana et nilivoona mwaktolyo ni mwaka Gani? Ilikuwa
 
Bwana Yesu Asifiwe. Tusifike mbali maisha ya machimbo ya dhahabu yasikie tu kwa jirani kama unampenda mtoto wako huwezi ruhusu akatafute maisha machimbo sisemi kwamba watu wasiende ila naandika hapa siwezi rudi tena machimbo kwangu mimi ni heri saidia fundi lakini sio maisha ya solovea maporini.

Ilikuwa ni mwaka 2007 nilipelekwa na mdingi wangu Kwenda kuchimba machimbo ya dhahabu CHUNYA Mbeya kufupisha stori ile nimefika tu kijiji napokelewa na watu walio choka balaa wamekunywa pombe na wengine sigala yani mtu ukimuangalia nguo alizo vaa zilivyo chakaa duh nilivyo ona tu hivyo pale kijijini mbona nilianza kudata na Nguvu zilianza niishia kidogo.

Sikueleza jina la kijiji hapo nyuma kijiji nilichofikishwa kilikuwa Kinaitwa Igundu Ila kazi tulikuwa tunafanyia mapori fulani mbali kidogo yani kuna kijiji kingine unakipita Kinaitwa mwankonyonto ndio unafika sasa kwenye Eneo tuliko kuwa tunachimba haya tuendelee.

Basi Baada ya kukutani na zile sura ngumu of course Nguvu ziliniisha Nikaanza muona dingi kama vile kaja kunileta matesoni maana story nilizo kuwa nasikia vijiweni ni kwamba watu wa machimbo wanapesa lakini nilivyo Kutana ni tofauti na mategemeo yangu nilitegemea nitawakuta wapo kawaida na sio kwa kuchakaa waponcha kiukweli walikuwa wamechoka balaa nasikia tu harufu Za sigala basi bwana

Kutokana Na mda nilio kuwa nimefika ulikuwa ni jioni jioni kama saa 11 Au kumi na mbili jioni hivi nikaomba wanipeleke nikampumzike maghetoni mwao basi jamaa mmoja hivi jina nimpe Kibakuli akanipeleka mpaka wanapolala maana ilikuwa ni hapo hapo kijijini Igundu ila pembeni kidogo porini ndio walikuwa wanalala hapo lakini mimi hapo akilini mwangu wakati Kibakuli akanipeleka gheto nikapumzike nikajua ni gheto chumba KIZURI cha kawaida tu kama nilivyo zoea tu Vya mjini.

Basi bwana nikiwa njiani na Kibakuli kuelekea ghetoni sasa Nikakuta huyu mshikaji mbona kama tunatembea mpaka tunaanza kukiacha kijiji cha Igundu na tunaanza ingia porini nikajiuliza gheto gani hili lipo porini hivi basi bwana baada ya kukiacha kijiji cha Igundu kama km moja ndio Nikakuta washikaji kumbe wametengengeza kambi la turubai porini duh hapo ndipo nilipo choka Zaidi maana baada ya kufika hapo kambini yani pale palikuwa hakuna godolo wala branketi nilikuta Chini wametandika mabox na yenyewe yamechakaa balaa na vipisi Vya sigala Vya Kutosha.

Nilivyoyaona Hayo kiukweli nikachoka sana nikasema Hapa ni pa moto aise na hapo ndio mwanzo tu malazi Yapo hivi je hiyo kazi ya kuchimba itakuwaje kiukweli nilichoka na kukata tamaa basi baada ya Kibakuli kuniambia ndio Hapa mwanangu gheto akaniacha Akaniambia dagaa hizo mwanangu na ugali Huo kiberiti hicho kuni utaingia porini humu humu zipo nyingi tu aise kimoyo moyo nikasema Hapa nimefika ni pamoto nikamjibu tu fresh mwanangu mimi kamanda nitaungurumisha.

Lakini kiukweli Nguvu Za kupika nilikuwa sina maana nilikuwa nawaza sijui nirudi nyumbani Au nikiamka kesho Niseme naumwa ili nirudi home maana haya maisha kwa mwanzo tu huu yamenishinda anyway nikawaza waza giza likaingia nikaona nilale tu na wakati Huo mimi Nipo peke yangu hapo porini washikaji wapo kijijini wanakunywa pombe hofu ikaanza niingia Kutokana ndio mara yangu ya kwanza kukaa peke yangu vile Afu porini nasikia kelele Za vyura tu.

Lakini nikajipa moyo kwamba washkaji watakuja hata saa tatu usiku lakini ikafika saa tatu usiku hola kimya saa NNE hola pia saa tano hola mpaka saa 6 NA nusu ndio nikawa nasikia kama watu wanaoongea Afu wanakuja upande wangu kwanza wenge likanishika nikawa na mashaka lakini kwa kadili walivyo kuwa wanasogea na Maongezi yao nikawasoma tu kwamba Ni Kama watu waliolewa pombe na kweli baada ya sekunde kadhaa watu hawa Hapa "dogo vepe umelala mimi sikuwajibu Kitu ila mwisho Kutokana Na kelele zao nikawajibu kama mtu alie kwenye usingizi ndio nimelala"

Basi Baada ya kuwajibu wakaanza story zao yani kesho tunapiga hela na mgeni amekuja pale lazima tuwashe mkanda "maana ya Kuwasha mkanda ni dhahabu Kutoka nyingi" Basi wakapiga story sana mimi zile story zao zikanipa Nguvu nikasema moyoni yesi kesho siondoki kumbe tunaenda Kuwasha mkanda Lakini mimi siku hiyo sikulala maana usingizi haukuja Kutokana Na sehemu ile panavyo minya aise.

Basi kulivyo kucha asubuhi mapema masela walikuwa wameamka walikuwa watatu jumla na huyo Nilie mpa jina Kibakuli basi tukasalimiana maana hapo wote walikuwa na akili zao na sio Za pombe basi wakasema tufanye fasta ili tukachukue kipimo kijijini Igundu na sululu na makoleo sehemu wanapoachaga vyombo basi tukabeba unga wa ugali kwenye vile vibegi vyeusi wanaita vibobu na dagaa kidogo mimi sasa nikaawambia mbona mnabeba unga mwingi sana hivyo na mimi sili sana chakula basi wakacheka wa kaniambia we wa Town tu.

Basi tulivyo Fika kijijini Igundu tukachukua kipimo na sululu na makoleo na kipimo fulani kidogo Kinaitwa Fisher gold Bug 2 kina kasahani kadogo sana Basi bwana baada ya kuchukua hivyo vifaa tukanunua na mafuta ya kupikia ya mia tano safari ya kuelekea kazini ikaanza aise tulitembea sana kama km 3 hivi maana ni Mbele ya kijiji fulani Kinaitwa mwankonyonto ukivuka hicho kijiji kwa Mbele ndio Unakuwa umefika na hapo ni umebaba sululu na koleo kila mmoja

Basi Baada ya kutembea sana tukafika Eneo la kuchimba tukawakuta na baadhi ya watu wanachimba basi Yule mjomba mwingine tumpe jina sekesa Akaniambia Wewe dogo utachimba Hapa nikasema poa tena kwa Nguvu yote basi bwana nikaanga kuchimba aise ile kazi ni Ngumu Kuliko kazi zote maana nilichimba mpaka Nikaanza kuona kizungu zungu na hewa nakosa basi nikauliza kwa sauti Kubwa jamani maji Yapo Hapa mmoja wa wale Jamaa tulio wakuta Akaniambia yale pale kwenye mti aise nikaenda fasta nikanywa yale ndio kujisikia Nafuu.

Basi sasa ikawa nikichimba kidogo naenda kupozea na maji kidogo maana nilikuwa nikipiga ile sululu ndefu iliyofulishwa (chongwa) kifua kilikuwa kina pata moto mpaka wale Jamaa wengine tulio wakuta wakasema huyu atamaliza kweli hii kazi basi nikaenda na mwendo Huo lakini kazi haisogei Jua linapiga balaa aise kazi ya kuchimba ni ngumu sana nikaenda nayo wee mpaka saa tisa kazi imesogea kidogo udongo nilio chimba ili kipimo kije kinipimie ulikuwa mdogo sana na nimechoka balaa basi akaja Jamaa wa kipimo akazungushia ule udongo wangu wanaita kibongo Bongo hola hakuna cha dhahabu wala nini Akaniambia nianze kusambaza ili wapime kwa kusambaza aise nilisambaza udongo ule lakini hola hakuna cha dhahabu wala nini Mpaka namaliza kusambaza hakuna cha dhahabu wala nini nikapolola (kukosa) dhahabu.

Kufupisha stori nikakomaa machimbo na hali ya kupolola ilikuwa Kubwa Japo siku Zingine tunapata point tatu Au tano na kipindi hicho point moja ni ilikuwa Elfu 8 kwa Kifupi hali ya machimbo ni ngumu maana unga mda mwingine ulikuwa unakata na mpo polini chawa zikaanza kunitesa maana mda wa kuoga ukaanza kuwa hadithi kwangu Kutokana Na mda ninao rudi mbovu na hela sina mfukoni nimepolola chakula mda mwingine hamna labda ukaombe kambi lingine maisha ya kushindia matunda ya porini matoo na michongoma ndio yakawa kawaida yetu Nikaanza Kushinda vilabuni na wale masela kwa Kifupi kipindi KILE nawaona wale masela wamechoka hawachani nywele wamevaa nguo zimechanika chanika yani mimi Na wao tukawa sawa tu.

Maisha yakawa ni Kushinda VILABUNI Lakini asubuhi mapema unajikaza uende kazini ukipata point moja mbili sawa Japo kukosa ilikuwa ni mara nyingi sana ukifika kijiji ni kushindia pombe Au na viazi Vya kugongea ili baki kidogo tu nianze kuvuta sigara na bangi kwa Kifupi nilichakaa kuzidi wale Jamaa nilio wakuta KUMBU KUMBU YA MWISHO WALITUMWA NDUGU TU KUJA KUNICHUKUA MAANA.

Katika Wale Jamaa Watatu Wawili Nilikuja Kusikia Walipata Ukimwi Na Yule Mmoja kibakuli sijui aliishia Wapi.

MIMI KWA SASA NASHUKULU NI MZIMA NA POMBE NILIACHA NAENDELEA NA MISHE ZANGU TU HAPA MBEYA TOWN ILA NIMALIZE TU KWA KUSEMA MACHIMBO YA DHAHABU NI ZAIDI YA JESHI LA TALIBANI SIJI KURUDI.

Ulidhani kupasua kimaisha ni rahisi tu ? Pole sana. Lazima uteseke kwanza kabla ya kutusua
 
Huko ndio anapotea mazima mwisho wa siku apate msongo wa mawazo kisha ajimalize kabisa
Uchimbaji wa dhahabu ni mgumu sana kuna jamaa mwaka jana kaacha kazi Benki kaingia kwenye hizi mishe kule Kilindi Handeni kapoteza zaidi ya milion 25 na aliambulia 7grms tu. Kazi kapoteza, hela imeisha na familia yake imemdhrau na kumtenga yaani sasa hivi kachanganyikiwa kwa kifupi dishi limeyumba na kapoteza dira kabisa na sasa hivi kaingia kwenye kubet [emoji28]
 
Machimboni sio kabisa aisee bora ukae town uwe dalali.

Imagine sehemu ya kutafutia riziki ambayo 80% ya wajuba wanaamini ramani za waganga, 80% ya raia hawana connection na dunia civilized maana yake hamna mwenye address wala ID yoyote, 80% wanajisaidia porini na ni hadi ale ugolo vinginevyo ngoma haitoki na hii husababishwa na kuishi kwa mandazi ya azam na energy drink za mo.

Watu hawaendi kwao hata miaka 10 ni mwendo wa kuhama mgodi hadi mgodi. Unaenda na mamilioni ya hela kwa namna biashara isivoeleweka unarudi na begi chakavu lenye nguo chakavu.

Kuna dingi aliingizwa king na madalali akaingia mgodini mazima bila kushirikisha kichwa katika tani 540 ya material aliondoka na gram 49, aisee almanusura ampige nyundo meneja wa Elution plant.

Hii biashara tuwaachie wazungu kiukweli haieleweki kwa asilimia 90.
 
Daa hii stori imenikumbusha tulivomaliza skuli ile praimari bado tukiwa wadogo kuna wenzetu walienda uko machimboni kutafuta maisha. Walivorudi tulikuwa tunawaskia wanalalamikia mazingira ya uko. badae wakazoea mazingira wakawa wanaenda na kurudi. badae wengine waliumwa matumbo walisema maji ya yalikuwa machafu sana. Mmoja hakurudi alifia ukouko.
 
Dahhh maisha haya.Ila umenikumbusha kisa fulan hivi.Jamaa alienda kuchimba na yeye alitokea town alikuja vizuri yaan kifedha.alichimba kama wiki mbili hivi bila kupata akijitahid anapata 8000 ahhh akaamua kuacha.Na kutangazia umma kuwa ile kazi haifai.jamaa mmoja akamwomba lile shimo aendelee kuchimba mwenye shimo kakubali,ehhh bwana haikupita siku jamaa kangusha mzigo milion mia mbili.sasa ule ugomvi uliwa sio wa inchi hii. na yule jamaa aliye achia shimo.Maisha kaka ni kujifunza si mpaka upate
 
Daa hii stori imenikumbusha tulivomaliza skuli ile praimari bado tukiwa wadogo kuna wenzetu walienda uko machimboni kutafuta maisha. Walivorudi tulikuwa tunawaskia wanalalamikia mazingira ya uko. badae wakazoea mazingira wakawa wanaenda na kurudi. badae wengine waliumwa matumbo walisema maji ya yalikuwa machafu sana. Mmoja hakurudi alifia ukouko.
Mkuu niazime I'd yako
 
Kimsingi huo wako haukua uchimbaji hata level ya mchimbaji mdogo ulikua hujafika bali ulikua mbangaizaji tu. Watu mnachafua sana sifa za uchimbaji wakati mnaofanya sio uchimbaji.

Ni sawa na mtu awe anauza pair moja ya kiatu Kariakoo akose mteja aseme kkoo pagumu. Huyu hana duka, hata level ya umachinga hajafikia, hajui anything kuhusu ins and outs za Kkoo afu aseme kkoo pagumu, utamchukulia seriously kweli?

Chunya inatoa 300-400Kg of gold yani over 35 Billion TSH monthly. Mnadhani hizi dhahabu zinatoka mbinguni?

Uchimbaji kama biashara zingine unahitaji uwekezaji tena uwekezaji wa maana na maarifa na uchimbaji sio a get rich quick scheme kama wengi mnavyojazana. Wengine tukitoa story zetu hapa mtashangaa. Hizo kona zote nazifahamu na nitakua huko soon.
 
Uchimbaji wa dhahabu ni mgumu sana kuna jamaa mwaka jana kaacha kazi Benki kaingia kwenye hizi mishe kule Kilindi Handeni kapoteza zaidi ya milion 25 na aliambulia 7grms tu. Kazi kapoteza, hela imeisha na familia yake imemdhrau na kumtenga yaani sasa hivi kachanganyikiwa kwa kifupi dishi limeyumba na kapoteza dira kabisa na sasa hivi kaingia kwenye kubet 😅

Kwa 25M alidhani atapata nini? 25M kwenye madini is nothing Bora angefuga kuku tu. Tatizo wengi wanadhani uchimbaji is a get rich quick scheme it's absolutely not.
 
Itumbi naoasikia sikia tu sikuwahi kufika, ukanda wa kusini maeneo ya matundasi, makongorosi na mkwanuni sijawahi kufika.

Ishu ya kufhulumiwa ipo sana ngoja nikupe kisa kimoja.

Kuna siku tulienda kuchimba Chunya mjini eneo moja linaitwa swiswi maeneo fulani hivi ya porini milimani kule karibia na minara ya simu.

Kufika kule nikakutana na wazee wengi waheshima nikawa najua hapa busara zipo.

Wakati naendelea kuchimba upande wa pili kuna mwana alikuwa tayari ameufikia mwala, so akaita kipimo kike kupima.

Kipimo kilivyokuja, kuna bro mmoja akatoka kwenye shimo lake akaenda kuangalia huyo mwana anavyopimiwa.

Katika kupima, kipimo kikatoa mlio ishara ya kuonesha kuna dhahabu au metal objects

Sasa ule wakati wa kuchota mchanga kugawa kwenye viganja kujua ni dhahabu au kibati, alikuja yule bro ambaye sio shimo lake, akachota mchanga kwenye viganja viwili akawa anagusisha kwenye sahani ya kipimo.

Kipimo kilivyopitishwa kwenye mkono mmoja alioshika mchanga hakikukia, akautupa ule mchanga.

Mkono wa pili kilivyopita kipimo kikatoa mlio, yule bro akasema "aaah kumbe ni kibati" halafu akaurusha ule mchanga mbali kabisa.

So jamaa wakaendelea kuoima kwenye mwala, ikaonekana jamaa amepolola akarudi home.

Yule bro alisubiria watu wote wameondoka akaruri kwenye ule mchanga alioutupa kumbe kulikuwa na dhahabu sio kibati kama alivyosema, jamaa akachukua dhahabu akasepa zake.

Apex the biggest tax payer wilaya ya Chunya wanachimba Itumbi. Achimwene wenye Mabasi ya achimwene wanachimba Itumbi. Mdimi ana shafts Itumbi. Hawa wamefanya uwekezaji wa nguvu.

Watu wengi including mleta Uzi hawajafanya uchimbaji bali ubangaizaji tu kama machinga hawapo hata level ya mchimbaji mdogo. Tatizo watu wanajazana ujinga kwamba wataenda migodini na sululu na jembe watoboe, that will never happen. Watarudi kwao wamechakaa ndugu zao wawasahau.
 
Mkuu hapa turudi kwenye hoja ya msingi achana na ushuani v/s uswazi.
Kwakifupi uchimbaji wa kienyeji unao usema wewe ulisha pitwa na wakati kwasababu ni kazi ya kubahatisha/haina uhakika. Zaidi watu wengi wanaufanya uchimbaji wa kienyeji kutokana kutokua na mtaji wa kutosha, kukosa elimu na umasikini.
Lakini bado nasisitiza kwamba kazi ya uchimbaji wa kienyeji ni high risk because of the nature and unsafe conditions

Word. Nawaambia waende pale pale Chunya Itumbi kwa Achimwene mwenye mabasi ya Achimwene, Apex, Kyando, Mdimi na Sauli mwenye Mabasi ya Sauli waulize wanavuna kiasi gani kwa mwezi na uwekezaji wao wajionee tofauti.

Uchimbaji kama biashara zingine zote inahitaji uwekezaji wa nguvu, maarifa na utaalam sio kubahatisha kienyeji enyeji tu.
 
Back
Top Bottom