Maisha ya machimbo ya dhahabu ni zaidi ya jeshi, nilikimbia

Maisha ya machimbo ya dhahabu ni zaidi ya jeshi, nilikimbia

Yaani sijawahi pata ushuhuda WA mchimbaji mdogo mdogo katoboa...woote ni misoto

Technically hawa sio wachimbaji ni wabangaizaji hawapo hata level ya mchimbaji mdogo. Hawana leseni, mtaji wala basic tools. Mtu ana sululu, jembe na nyundo huyo nae anajiita mchimbaji kweli? Hawa wana tofauti gani na mtu anyejiuzia kiatu pair moja pale Kkoo afu asema biashara ngumu, utamchukulia serious?

Sisemi uchimbanji ni rahisi ila unahitaji uwekezaji, elimu na utaalam. Chunya inatoa 300-400Kg za gold kwa mwezi yani over 35 Billion TSH monthly, wanapataje kama uchimbaji haulipi kabisa?

Wengi wanaingia na matumaini hewa wanaishia kulia tu. Uchimbaji is not a get rich quick scheme kama wengi wanavyodhani hamna rangi utaacha ona ila unalipa.
 
hongera mkuu mdingi wako nampa pongezi kubwa sana,kwani alikupeleka kwenye chuo cha maisha ujue pesa inatafutwaje,mpaka kufikia hapo sizani kama utakuwa na matumizi mabaya yapesa au kuwadharau wengine hawajui kutafuta.mi baada ya kumaliza form six nilitimuliwa hom .maisha yangu ya kawa ya kimtaa kwetu wakishua lakini ilifikia hatua nikajiunga na wachonga kalai nashindia maji na chikichi nikaugua madonda ya tumbo lakini nika kaza.kwa siku nilikuwa napata 1000,nikadunduliza ikafika 30000 nika acha kazi hiyo.nikahamia kuchinga vyombo nanunua besen 30 napata faida 3000, nashukuru mungu nilipanda mpaka mtaji ukafika milion,..baba akawa anaulizia tu niko wapi ila taimu namimi hana.sasaiv na maisha yangu biashara kubwa,na baba anajivunia mimi, aliniita akasema sio kwamba sikupendi,niliambiwa na mchaga ili mtoto awe na akili mtimue ujifanye humpendi..baadae akaita ndugu akasema naona mwanangu shule ime mkaa sasa.namuongezea mil 2.je asingenitimua nika sota mtaani ninge kuwa na nidhamu yapesa? maisha ni chuo ndugu.

So illogical. Mtoto inabidi aendelee mzazi alipoishia na mzazi ana wajibu wa kufanya maisha ya mwanae marahisi sio kumrudisha nyuma makusudi kwa kigezo cha kujifunza, hakuna tuzo ya kupitia maisha magumu zaidi ya kukuharibu tu. I hope wewe hautakua na mawazo ya kijima ya kumfukuza mwanao.
 
Technically hawa sio wachimbaji ni wabangaizaji hawapo hata level ya mchimbaji mdogo. Hawana leseni, mtaji wala basic tools. Mtu ana sululu, jembe na nyundo huyo nae anajiita mchimbaji kweli? Hawa wana tofauti gani na mtu anyejiuzia kiatu pair moja pale Kkoo afu asema biashara ngumu, utamchukulia serious?

Sisemi uchimbanji ni rahisi ila unahitaji uwekezaji, elimu na utaalam. Chunya inatoa 300-400Kg za gold kwa mwezi yani over 35 Billion TSH monthly, wanapataje kama uchimbaji haulipi kabisa?

Wengi wanaingia na matumaini hewa wanaishia kulia tu. Uchimbaji is not a get rich quick scheme kama wengi wanavyodhani hamna rangi utaacha ona ila unalipa.
Sawa nakubali ila shuhuda za KUTISHA NI NYINGI
Hata kwa hao wenye mitaji mikubwa
 
Sawa nakubali ila shuhuda za KUTISHA NI NYINGI
Hata kwa hao wenye mitaji mikubwa

Wachimbaji wakubwa know when to quit akiona mzani wa hasara unazidi faida anaacha Kama biashara zingine tu ila hadi hapo lazima kuna mara ilimlipa maradufu. Huwezi kupata kila siku.

Hapo hapo Chunya wapo Apex the biggest tax payer wilaya ya Chunya, Achimwene wenye mabasi ya Achimwene, Kyando, Mdimi (Huyu alivuta umeme mgodini kwake kwa 800M TSH) na anachimba toka miaka ya 80, Sauli mwenye mabasi ya Sauli. Hawa ni wachache ambao wanafahamika wamekua mbele ya macho yetu, wanalalamika changamoto za kibiashara tu kama biashara zingine sio kwamba uchimbaji haulipi. Hapo sijazungumzia makampuni ya wachina na wachimbaji wengine wakubwa.

If anything nitasema story za uchimbaji are overhyped watu wanaingina with the wrong mindset.
 
Wachimbaji wakubwa know when to quit akiona mzani wa hasara unazidi faida anaacha Kama biashara zingine tu ila hadi hapo lazima kuna mara ilimlipa maradufu. Huwezi kupata kila siku.

Hapo hapo Chunya wapo Apex the biggest tax payer wilaya ya Chunya, Achimwene wenye mabasi ya Achimwene, Kyando, Mdimi (Huyu alivuta umeme mgodini kwake kwa 800M TSH) na anachimba toka miaka ya 80, Sauli mwenye mabasi ya Sauli. Hawa ni wachache ambao wanafahamika wamekua mbele ya macho yetu, wanalalamika changamoto za kibiashara tu kama biashara zingine sio kwamba uchimbaji haulipi. Hapo sijazungumzia makampuni ya wachina na wachimbaji wengine wakubwa.

If anything nitasema story za uchimbaji are overhyped watu wanaingina na a wrong mindset.
Kwa kifupi mkuu kule ukienda na sururu unajipeleka kwa nyapala bila kujua,
Naona investment inatakiwa ya maana.,,,Hatareee
 
Kwa kifupi mkuu kule ukienda na sururu unajipeleka kwa nyapala bila kujua,
Naona investment inatakiwa ya maana.,,,Hatareee

Exactly. Tena I'll add to that Kuna wengine wanajazana kwamba ukinunua Karasha (crusher) tu umemaliza kazi utasagia mawe wengine utapata hela. That's a big fat lie. Hata Uwe na Karasha na jaw crusher bado kabisa. Inabidi uwekeze kwenye vifaa na maarifa yani vinaenda sambamba.

Kadhalika asikujaze mtu kwamba utaenda Leo upate hela next month ni uongo mkavu. Utasota ila inalipa na inalipa big time sio hela za mbuzi sijui 20M au 50M. Ukiingia vizuri huwezi acha Wengine tunaona kazi zingine ni kupoteza muda tu sijui kilimo unalima mwaka mzima ili upate 20M tena kama huo mwaka mzuri na serikali haijawaingilia sokoni. Dhahabu Bei inatoka soko la Dunia.
 
Wachimbaji wakubwa know when to quit akiona mzani wa hasara unazidi faida anaacha Kama biashara zingine tu ila hadi hapo lazima kuna mara ilimlipa maradufu. Huwezi kupata kila siku.

Hapo hapo Chunya wapo Apex the biggest tax payer wilaya ya Chunya, Achimwene wenye mabasi ya Achimwene, Kyando, Mdimi (Huyu alivuta umeme mgodini kwake kwa 800M TSH) na anachimba toka miaka ya 80, Sauli mwenye mabasi ya Sauli. Hawa ni wachache ambao wanafahamika wamekua mbele ya macho yetu, wanalalamika changamoto za kibiashara tu kama biashara zingine sio kwamba uchimbaji haulipi. Hapo sijazungumzia makampuni ya wachina na wachimbaji wengine wakubwa.

If anything nitasema story za uchimbaji are overhyped watu wanaingina na a wrong mindset.
Hivi mkuu unataka kuniambia Apex Resources ndiye analipa tax kubwa kuliko Shanta wa kule Saza Mkwajuni?
 
Hivi mkuu unataka kuniambia Apex Resources ndiye analipa tax kubwa kuliko Shanta wa kule Saza Mkwajuni?

Mkuu, Mkwajuni sasa ipo Songwe. Angalia maelezo yao wenyewe:

Screenshot_20230628_221605_Instagram.jpg
 
Exactly. Tena I'll add to that Kuna wengine wanajazana kwamba ukinunua Karasha (crusher) tu umemaliza kazi utasagia mawe wengine utapata hela. That's a big fat lie. Hata Uwe na Karasha na jaw crusher bado kabisa. Inabidi uwekeze kwenye vifaa na maarifa yani vinaenda sambamba.

Kadhalika asikujaze mtu kwamba utaenda Leo upate hela next month ni uongo mkavu. Utasota ila inalipa na inalipa big time sio hela za mbuzi sijui 20M au 50M ni hela hasa. Ukiingia vizuri huwezi acha Wengine tunaona kazi zingine ni kupoteza muda tu sijui kilimo unalima mwaka mzima ili upate 20M tena kama huo mwaka mzuri na serikali haijawaingilia sokoni. Dhahabu Bei inatoka soko la Dunia.
Sasa mkuu kumbuka hawa kina Achimwene na wadogo zao kina Mbwiga walimilikishwa haya maeneo kitambo na wazazi wao. Hapo mwanzo nao walikuwa wakichimba na kununua dhahabu kama madigala kwenye klem zao na kukuza mitaji. Na pia walipata pesa baada ya kuingia ubia kwenye klem zao na makampuni makubwa. Kwa mfano pale anapochimba Apex Itumbi ni klem ya kina Achimwene. All in all uchimbaji mdogo mdogo wanaouongelea hawa watoa ushuhuda wengi humu ni ule wakizamani wakitegemea "IPO SIKU" ndio wanaofia kwenye maduala kwa kupigwa na magema au kuishia kupata gram mbili tatu, ukisikia duala limetoa grams kuanzia tano wanaita MLIPUKO na hapo wachimbaji wote watajaa😂
Pia wengi wanajidanganya kununua makalasha (crushers) moja au mbili na kusaga mawe ilimradi akuze rudio apeleke kuozesha plant bila kuwa na uwakika wa mawe yenyewe yatasomaje kwenye PP.
Gold Extraction tuwaachie hao uliowataja kwa Chunya maana Inahitaji A BIG INVESTMENT kuanzia lasilimali watu, vifaa na teknolojia ili upate makilo ya kueleweka.
Hivi wale wachina waliokuwa wakichimba Saza na kuleta udongo wao plant Matundas B bado wapo au walishafirisika na kuondoka?
 
Mkuu, Mkwajuni sasa ipo Songwe. Angalia maelezo yao wenyewe:

View attachment 2672498
Sawasawa Shanta wapo Songwe kimkoa( Nilipitiwa kidogo). Ila Apex wanapitia msoto sasa hivi, huu ni mwezi wa 3 Sasa wafanyakazi hawajalipwa mishahara mkuu. Unakumbuka stori ya yule tajiri wa kisafwa anayechimba Mlima Njiwa (Jina limenitoka) ana mbwa wengii wazungu walipomfuata ili wanunue eneo lake kuna dhahabu ya kutosha kwenye ardhi yake kumbe ameifungia ndani store?
 
Sasa mkuu kumbuka hawa kina Achimwene na wadogo zao kina Mbwiga walimilikishwa haya maeneo kitambo na wazazi wao. Hapo mwanzo nao walikuwa wakichimba na kununua dhahabu kama madigala kwenye klem zao na kukuza mitaji. Na pia walipata pesa baada ya kuingia ubia kwenye klem zao na makampuni makubwa. Kwa mfano pale anapochimba Apex Itumbi ni klem ya kina Achimwene. All in all uchimbaji mdogo mdogo wanaouongelea hawa watoa ushuhuda wengi humu ni ule wakizamani wakitegemea "IPO SIKU" ndio wanaofia kwenye maduala kwa kupigwa na magema au kuishia kupata gram mbili tatu, ukisikia duala limetoa grams kuanzia tano wanaita MLIPUKO na hapo wachimbaji wote watajaa😂
Pia wengi wanajidanganya kununua makalasha (crushers) moja au mbili na kusaga mawe ilimradi akuze rudio apeleke kuozesha plant bila kuwa na uwakika wa mawe yenyewe yatasomaje kwenye PP.
Gold Extraction tuwaachie hao uliowataja kwa Chunya maana Inahitaji A BIG INVESTMENT kuanzia lasilimali watu, vifaa na teknolojia ili upate makilo ya kueleweka.
Hivi wale wachina waliokuwa wakichimba Saza na kuleta udongo wao plant Matundas B bado wapo au walishafirisika na kuondoka?

Mkuu, I agree. Ndo maana nasema uchimbaji unahitaji investment ya nguvu sio ubangaizaji ambao wengi wamekua wakiongelea hapa jukwani. Kina Achimwene wamepata pesa na wamejua kuiendeleza huko huko migodini that speaks volume. Mabasi yao wamenunua mwaka huu huu baada ya mdogi kutema. Mbona hawajakimbia machimbo kama hakulipi?

Wale wachina wa Saza nilisikia wameondoka ila sina uhakika, kuna wachina wengine Mdimi alinunua claim yao na kavuta umeme kwa 800M TSH. Wachina wajinga wajinga tu.
 
Sawasawa Shanta wapo Songwe kimkoa( Nilipitiwa kidogo). Ila Apex wanapitia msoto sasa hivi, huu ni mwezi wa 3 Sasa wafanyakazi hawajalipwa mishahara mkuu. Unakumbuka stori ya yule tajiri wa kisafwa anayechimba Mlima Njiwa (Jina limenitoka) ana mbwa wengii wazungu walipomfuata ili wanunue eneo lake kuna dhahabu ya kutosha kwenye ardhi yake kumbe ameifungia ndani store?

Du miezi 3 mingi sana kwa mgodi kama Apex ila najua huwa kuna muda nao wanafukuzia mwamba labda ndo wapo hapo sasa. Wanafanya survey kufungua eneo lingine pia labda hiyo nayo inawamaliza pesa.

Hiyo ya msafwa na wazungu siipati mkuu 🤣

 
Mkuu, I agree. Ndo maana nasema uchimbaji unahitaji investment ya nguvu sio ubangaizaji ambao wengi wamekua wakiongelea hapa jukwani. Kina Achimwene wamepata pesa na wamejua kuiendeleza huko huko migodini that speaks volume. Mabasi yao wamenunua mwaka huu huu baada ya mdogi kutema. Mbona hawajakimbia machimbo kama hakulipi?

Wale wachina wa Saza nilisikia wameondoka ila sina uhakika, kuna wachina wengine Mdimi alinunua claim yao na kavuta umeme kwa 800M TSH. Wachina wajinga wajinga tu.
Kwa miaka ya mbele na kuendelea Chunya itaendelea kushikwa na akina Achimwene, Kyando, Mdimi hawa ni watanzania wachache ambao tunaweza kusema hakika hii biashara wameipatia. Wa size ya Kati wapo kina Mabula, Musa, Omary, Shedrack na wengineo Wana klem na makalasha meengi at least nao wanaambulia kiasi na kusogeza maisha.
Ila huu uchimbaji mwengine wa kukusanya mafelo, kusambaza, kusekesa na kuchimba maduala kuutafuta mwamba wataishia kunyauka tu maana ni wakubahatisha.
 
Du miezi 3 mingi sana kwa mgodi kama Apex ila najua huwa kuna muda nao wanafukuzia mwamba labda ndo wapo hapo sasa. Wanafanya survey kufungua eneo lingine pia labda hiyo nayo inawamaliza pesa.

Hiyo ya msafwa na wazungu siipati mkuu 🤣


Nahisi huyo msafwa anaitwa Mwambe kama sijakosea, ndiye mchimbaji wa kwanza kabisa kusambaza vipimo Chunya nzima. Na Hilo swala la vipimo lina habari yake wakati Mboma (Msafwa mwenzake na rafiki yake) akiwa mkuu wa majeshi( Hapa sitagusia😀🙌)
 
Kwa miaka ya mbele na kuendelea Chunya itaendelea kushikwa na akina Achimwene, Kyando, Mdimi hawa ni watanzania wachache ambao tunaweza kusema hakika hii biashara wameipatia. Wa size ya Kati wapo kina Mabula, Musa, Omary, Shedrack na wengineo Wana klem na makalasha meengi at least nao wanaambulia kiasi na kusogeza maisha.
Ila huu uchimbaji mwengine wa kukusanya mafelo, kusambaza, kusekesa na kuchimba maduala kukutafuta mwamba wenye dhahabu wataishia kunyauka tu maana Ni wakubahatisha.

I couldn't agree more Mkuu. Umemaliza kila kitu.
 
Nahisi huyo msafwa anaitwa Mwambe kama sijakosea, ndiye mchimbaji wa kwanza kabisa kusambaza vipimo Chunya nzima. Na Hilo swala la vipimo lina habari yake wakati Mboma (Msafwa mwenzake na rafiki yake) akiwa mkuu wa majeshi( Hapa sitagusia😀🙌)

Mwambe nishamsikia 🤣 ujanja ujanja ulikua mwingi kipindi kile hadi sasa upo ila kama unajua unachokifanya na una mtaji hii biashara inalipa.
 
Nashukuru kwa wote mliochangia huu uzi, nimepata muda mzuri wa kusoma na kufahamu mengi kuhusiana na uchimbaji. Nilishampoteza Kaka yangu alitoroka nyumbani kwenda machimboni alikaa huko miaka zaidi ya mitano hatuwahi kupata taarifa zake hadi mwili wake uporudishwa kwa ajili ya kupumzishwa kwani alifariki akiwa njiani akipelekwa Hospital ya Rufaa Mbeya, mwingine alirudishwa akiwa amechoka mbaya na hana kitu ( yeye alitumwa amfuate Kaka mkubwa huyo aliyefariki naye kazamia huko) kumbe wachimbaji wadogo wanaotumia Sululu na koleo wanapitia mazingira magumu kiasi hicho! Mungu awasaidie.

OMBI: Kwa mlioko au mliowahi kufika Itumbi kuna fursa gani za kibiashara( halali) ambazo mtu mwenye mtaji mdogo anaweza kuzifanya angalau apate riziki, naomba nisaidiwe mawazo ya nini naweza kufanya au nini kinahitajika kwa maeneo hayo. Mimi niko Mbeya
 
Back
Top Bottom