Maisha yako ya Ndoa yamekuwaje baada ya kutofanikiwa kuoa/kuolewa na 'your dream man/woman?

Maisha yako ya Ndoa yamekuwaje baada ya kutofanikiwa kuoa/kuolewa na 'your dream man/woman?

Carleen

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2018
Posts
7,982
Reaction score
27,272
Hi guys,

Hope mmekuwa na mapumziko poa,

Nilikuwa najiuliza hili swali, hasa kwa walioko kwenye Ndoa tayari.

Je, kwako imekuwa baraka ama tofauti pale ambapo mume/mke unayeishi naye siye yule hasa ulikuwa unamuota every now and then?

This is serious, natamani kweli kujifunza, kuna majuto yoyote? Kuna utofauti mkubwa sana? Mko na furaha? Matarajio yako yamefikiwa? Are you thanking God for that? And why?

Please, Mr. Liverpool VPN and the Co, this ain't your cup of tea.

Niko nimekaa pale nasubiri miujiza na shuhuda zenu mbalimbali.
 
Hivyo umejifunza kupenda na you're enjoying.?
Ama umesemea wengine.?

Nimeandika kulingana na research niliyowahi kuifanya.

Kuna wakati nilikuwa na shauku ya kutaka kufahamu maswali kama haya uliyoyauliza, nikatenga muda kuchunguza baadhi ya ndoa za watu wa karibu.

Katika hizo ndoa kuna ambazo zimevunjika tena kwa ugomvi au kurogana, kuna ambazo wanandoa wamefariki kwa kuleteana ngoma na wapo ambao wameamua kujifunza kupendana (conclusion yangu imetokea hapa)
 
Ndoa zinafungiwa mbinguni, hapa duniani tunakamlisha tu.

Unaweza ukapambana sana kumpata flan lakin ukaja kuangukia kwingine, trust me that happens for a good reasons (divine purpose).

Tunayoyapenda vijana mengi ni illusion, siyo vitu halisia, lakini tunakuwa kama tumefungwa macho (mind) kwenye vitu flan ambavyo ikipita miaka kadhaa tu unakuja kuona ungepoteza pakubwa/kujisababishia shida.

Back to your questions: utachagua wewe kufurahia au kuhuzunika, wapo waliofurahi wapo waliohuzinika Tofauti yao ni jinsi walivyolikubali na kulipokea hilo. Kama unaingia hujakubali manake unakuwa huna upendo ndani, vurugu kila kukicha automatically unamfanya the other party naye anakuwa inferior mwishowe mnaharibu.

Lakini ukakubali ukapokea zawadi uliyoipata kwa mikono miwili ukaipenda na kuiheshimu, ukaiongoza/focusing on building better future together, unamfanya na mwenzako akuheshimu sana, akukubali sana, AND YOU WILL LIVE HAPPILY FOREVER!
 
Hii comment inafaa kupigwa lamination
Yap nimeongea kwa experience yangu sijawahi kupendwa nilipopenda... na hata mke wangu ninaeishi nae huwezi amini sikuwa namkubali kivile ila aliponizalia... nikaona ipo haja ya mimi na yeye kuishi pamoja...

Tulianza kuishi pamoja na ni almost miaka 5 sasa tunaishi... kugombana kupo ni hali ya kawaida... but ni familia yangu na nimeizoea... kile kipindi cha likizo huwa chumba nakiona kikubwa sana kwakweli.​
 
Back
Top Bottom