Maisha Yako ya sasa ni Matokeo ya family background yako

Maisha Yako ya sasa ni Matokeo ya family background yako

Utandawazi umewaharibu vijana, msijisahau bila hao wazazi usingekuwepo duniani leo.
Hapa tukiwaweka pembeni wale wazazi waliotelekeza watoto wao wakiwa wadogo....

Inasikitisha kijana miaka 25+ bado unalalamika mzazi hajakutengenezea njia, amka pambana maana wao walifanya kadri ya uwezo wao.
Kuna watu wametokea familia za kimasikini sana Ila hiyo iliwapa motisha wakakaza saivi wanaenjoy mema ya nchi na wazazi wao.
 
Hapa Duniani ukizaliwa pambania maisha yako tu, wazazi wetu wanaturudisha nyuma sana wanakuwa ombaomba, mara wanataka kujengewa nyumba ilihali wao hawakujenga mm nawezaje kuwajengea

Mwaka 2024 sitatoa hata mia yangu Kwa mtu yoyote yule na Sina mke Wala mtoto
Kwamba kama ni rahisi kujenga nyumba mbna wao wamekaa miaka mingi duniani na hawajajenga 😂😂😂😂
 
Kuzaa hata Panya [emoji242] anazaa.

Kuzaa sio excuse ya mzazi kukwepa uhalisia wa kwamba yeye ni maskini.

Umaskini ni tishio kubwa sana, Kama umaskini sio tishio huyo mzazi Alishindwaje kuwa tajiri?

Halafu ana tarajia wewe mtoto uje upambane umsaidie yeye.

Mzazi anaye zaa watoto kwa matarajio aje asaidiwe nao, mzazi huyo ni mjinga na mpumbavu.
Umeandika nini hapa sasa.
 
Utandawazi umewaharibu vijana, msijisahau bila hao wazazi usingekuwepo duniani leo.
Hapa tukiwaweka pembeni wale wazazi waliotelekeza watoto wao wakiwa wadogo....

Inasikitisha kijana miaka 25+ bado unalalamika mzazi hajakutengenezea njia, amka pambana maana wao walifanya kadri ya uwezo wao.
Kuna watu wametokea familia za kimasikini sana Ila hiyo iliwapa motisha wakakaza saivi wanaenjoy mema ya nchi na wazazi wao.
Sio utandawazi kama unavyodhani na kuna scenario nyingi sana huwa zinatukuta sisi Vijana na mshukuru sana Mungu hujakutana na changamoto na ukikutana na changamoto msaada au kimbilio la kwanza ni kwa Wazazi lakini huyo huyo mzazi uliyekuwa una msaidia kipindi hauna matatizo anaanza kukufanyia visa, ubaguzi na maneno ya kuumiza akili,moyo na hisia huyo unamuonaje? Wazazi wa Kiafrika wengi ni Wajinga sana na huwa wanadhani kwamba Sisi Watoto huwa tunataka kupata matatizo.

Kuna uzi humu niliuandika ukielezea ngoja nione kama nitaupata nikuwekee hata link
 
Wazazi wanaimpact kubwaa sana katika future ya watoto ukizaliwa katika family isio jali future ya watoto automatically upo kwenye risky ya kuongia kwenye chain ya umaskin.

Once ukishaingia kwenye cycle ya umaskin kuchomoka ni ngumuh Sana.
Wazaz wengi WA kiafrika WAnazaa watoto kutafuta sifa watoto hawapat elimu Bora ,no ushauri wowote WA future life n.k

Nenda maeneo mengi ya kijijin utagundua wazazi ni kiwanda Cha kutengeneza poor generations.

Mtoto since day one mzazi hampi mtoto ushauri wowote hâta WA future carrier.

Wewe kama baba mtoto akiwa 7yrs Kaa nae chini mwambie fact about life ,mkazie
asome,mtengenezee hobby ya carrier ya kueleweka kwa Faida ya maisha yake .

Sio baba na mama wote kupost mtoto Mitandaon. Ndo wanaona furaha





.
Haijalishi una watoto wangapi kama unajiweza wote watasoma.

Mila za kiasili za Kitanganyika ni kuwa na wake wengi na watoto wengi ili wewe mzee kazi yako inakuwa kula, kugida, kuwalala wake zako, kujikuna mbupu na kitambi.


Yanini tabu na raha ipo?
 
Utandawazi umewaharibu vijana, msijisahau bila hao wazazi usingekuwepo duniani leo.
Kuna ulazima gani wa kwamba ungezaliwa na hao wazazi?

Hao wazazi walikuwa kwenye starehe zao ndio ukazaliwa. Wala hawakujua kwamba mtoto anaye zaliwa ni wewe au mimi.

Si lazima kwamba ndio ungezaliwa na wazazi wako, ungeweza kuzaliwa na mtu mwingine yeyote yule.

Hakuna anaye taka kuzaliwa na Maskini. Kwanza kama ungejua unazaliwa na mzazi maskini unge ghairi kuzaliwa.
Hapa tukiwaweka pembeni wale wazazi waliotelekeza watoto wao wakiwa wadogo....

Inasikitisha kijana miaka 25+ bado unalalamika mzazi hajakutengenezea njia, amka pambana maana wao walifanya kadri ya uwezo wao.
Kuna watu wametokea familia za kimasikini sana Ila hiyo iliwapa motisha wakakaza saivi wanaenjoy mema ya nchi na wazazi wao.
Mzazi akishindwa kumtengenezea mwanaye njia, Mwanae akipambana na akapata njia yake.

Mzazi huyo hana mamlaka tena ya kumtaka mwanaye amsaidie.

Maana yeye kama kama mzazi alishindwa kumsaidia mtoto.

Hivyo asitake misaada ya mtoto kwa kigezo eti yeye ni mzazi.
 
Kuna ulazima gani wa kwamba ungezaliwa na hao wazazi?

Hao wazazi walikuwa kwenye starehe zao ndio ukazaliwa. Wala hawakujua kwamba mtoto anaye zaliwa ni wewe au mimi.

Si lazima kwamba ndio ungezaliwa na wazazi wako, ungeweza kuzaliwa na mtu mwingine yeyote yule.

Hakuna anaye taka kuzaliwa na Maskini. Kwanza kama ungejua unazaliwa na mzazi maskini unge ghairi kuzaliwa.

Mzazi akishindwa kumtengenezea mwanaye njia, Mwanae akipambana na akapata njia yake.

Mzazi huyo hana mamlaka tena ya kumtaka mwanaye amsaidie.

Maana yeye kama kama mzazi alishindwa kumsaidia mtoto.

Hivyo asitake misaada ya mtoto kwa kigezo eti yeye ni mzazi.
Upo sahihi
 
Nakwambia hivi Hata panya, kuku, wanazaa.Tena wana wajibika ipasavyo kulea watoto wao.

Binadamu mwenye akili timamu anaye tumia "Kuzaa" kama excuse ya kukwepa uhalisia wa kwamba yeye ni maskini huyo mzazi ni mjinga na mpumbavu.


Maana hata wapumbavu huzaa watoto.
Unaongelea panya while we talking about human. Sasa panya anaweza kuwa mfano hai kwenye hili dada yangu?
Hamna mtu anazaa mtoto tu ili mradi hakuna labda kama naongea na kijana, ukikua utaelewa.
 
Wazazi wanaimpact kubwaa sana katika future ya watoto ukizaliwa katika family isio jali future ya watoto automatically upo kwenye risky ya kuongia kwenye chain ya umaskin.

Once ukishaingia kwenye cycle ya umaskin kuchomoka ni ngumuh Sana.
Wazaz wengi WA kiafrika WAnazaa watoto kutafuta sifa watoto hawapat elimu Bora ,no ushauri wowote WA future life n.k

Nenda maeneo mengi ya kijijin utagundua wazazi ni kiwanda Cha kutengeneza poor generations.

Mtoto since day one mzazi hampi mtoto ushauri wowote hâta WA future carrier.

Wewe kama baba mtoto akiwa 7yrs Kaa nae chini mwambie fact about life ,mkazie
asome,mtengenezee hobby ya carrier ya kueleweka kwa Faida ya maisha yake .

Sio baba na mama wote kupost mtoto Mitandaon. Ndo wanaona furaha





.
Mafanikio ni tabia,na tabia inajengwa tokea utotoni.

Pale kuanzia mtoto ana miaka mi3 lazima kuna tabia umtengenezee tabia hizo zitamsaidia kukua nazo na baadae kutoboa.

Uweledi katika mawasiliano.
Pia matumiizi sahihi ya pesa.
Uwezo wa kuzungumza kwa ufasaha.
Uaminifu
Nidhamu binafsi.
Kuwajibika.

Hayo yote unamfundisha mtoto kuanzia pale miaka mi3 mpaka miaka 7 mpaka 10 na unamfundsiah kwa njia ya michezo ya kitoto na vitu fulani vya kufanya.

Mfsno tu unaweza kumjengra mtoto tabia ya kwamba kila jioni saa 10 aende kujichotea maji bombani kwenye kidumu cha lita 3 kwa ajili ya kukoga yeye mwenyewe,hiyo haina maana kwamba maji hakuna ndani ila unamtengenezea nidhamu binafsi na uwajibikaji,na kuna mifano kingi sana.

Akikua na tabia hizo itamjengea wepesi katika safari yake.
 
Wazazi wanaimpact kubwaa sana katika future ya watoto ukizaliwa katika family isio jali future ya watoto automatically upo kwenye risky ya kuongia kwenye chain ya umaskin.

Once ukishaingia kwenye cycle ya umaskin kuchomoka ni ngumuh Sana.
Wazaz wengi WA kiafrika WAnazaa watoto kutafuta sifa watoto hawapat elimu Bora ,no ushauri wowote WA future life n.k

Nenda maeneo mengi ya kijijin utagundua wazazi ni kiwanda Cha kutengeneza poor generations.

Mtoto since day one mzazi hampi mtoto ushauri wowote hâta WA future carrier.

Wewe kama baba mtoto akiwa 7yrs Kaa nae chini mwambie fact about life ,mkazie
asome,mtengenezee hobby ya carrier ya kueleweka kwa Faida ya maisha yake .

Sio baba na mama wote kupost mtoto Mitandaon. Ndo wanaona furaha





.
Kazi hipo tajiri na mali zake masikini na watoto na mikokoteni inauma sana
 
Don't blame anybody in this life.

Kuzaliwa masikini sio laana wala tatizo Ila kuishi kimasikini na kufa ukiwa masikini that is ur problems.

Doesn't matter umesoma au haujasoma u can get success and become rich au financial enough.


If you need to stuck and getting brain freezing all you need is to blame people.
Wewe mzungu mswahili unafahamu maana ya neno masikini?
 
Unaongelea panya while we talking about human. Sasa panya anaweza kuwa mfano hai kwenye hili dada yangu?
Hamna mtu anazaa mtoto tu ili mradi hakuna labda kama naongea na kijana, ukikua utaelewa.
Vibinti vinavyo pata mimba vikiwa sekondari si wana ongeza maskini duniani?

Mtu anajua hana uwezo ila bado anazaa zaa hovyo hovyo tu bila mpangilio, Huyo si ana ongeza maskini wengine duniani?

Chunguza matajiri wengi wana mtoto mmoja, wawili, watatu wakizidi sana sita.

Sasa nenda huko vijijini unasikia mzee mmoja ana watoto 12, wajukuu 4, vitukuu 2.

Yani hata kabla mtoto wake wa kumi na mbili hajakuwa mkubwa, tayari mtoto wake wa kwanza kampatia mjukuu.

Hapo ni kuendeleza generation ya Maskini.
 
Hapa Duniani ukizaliwa pambania maisha yako tu, wazazi wetu wanaturudisha nyuma sana wanakuwa ombaomba, mara wanataka kujengewa nyumba ilihali wao hawakujenga mm nawezaje kuwajengea

Mwaka 2024 sitatoa hata mia yangu Kwa mtu yoyote yule na Sina mke Wala mtoto
Umeongea kwa uchungu sana, wazazi wa kiafrika mentality zao za hovyo sana anafanya kazi miaka 30+ hajengi wala nn anapata pensheni pesa haeleweki amezifanyia nini watoto wakipata kazi wazazi Hao wanataka kujengewa, kuhidumiwa wanasahau watoto nao wana future zao walete watoto wao duniani wawahudumie circle goes on unmasking hautaisha Africa!!
 
Utandawazi umewaharibu vijana, msijisahau bila hao wazazi usingekuwepo duniani leo.
Hapa tukiwaweka pembeni wale wazazi waliotelekeza watoto wao wakiwa wadogo....

Inasikitisha kijana miaka 25+ bado unalalamika mzazi hajakutengenezea njia, amka pambana maana wao walifanya kadri ya uwezo wao.
Kuna watu wametokea familia za kimasikini sana Ila hiyo iliwapa motisha wakakaza saivi wanaenjoy mema ya nchi na wazazi wao.
Kwenye huu uzi nilishawahi kuku tag sijui kama uliusoma? Kama majanga hayajakukuta shukuru Mungu na uwe tayari kwa lolote kukutokea katika haya maisha. Yakikutokea majambo usiyoyatarajia kimbilio la kwanza ni kwa Wazazi lakini Wazazi nao wanakuletea mapichapicha yaani hii dunia iache tu kama ilivyo.

https://www.jamiiforums.com/
[IMG alt="Manyanza"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/30/30724.jpg?1699110413[/IMG]

Manyanza

Wakuu maisha ni safari ndefu yenye kila aina ya changamoto, Mimi mwenyewe nina mkasa mzito sana yaani kwa kifupi nilizaliwa kwenye familia iliyokuwa inajiweza kwa kila kitu lakini tatizo lilikuwa kwa Mzee alikuwa hataki Mama afanye kitu chochote na Mzee alikuwa ni mwanajeshi na kipindi hicho miaka ya 1995 fursa za ajira zilikuwa nyingi sana Ualimu na Uaskari lakini baba alikuwa akimwambia Mama yaani Mwanamke ufanye kazi ili uje uanze kuleta dharau?

Baba alikuwa anafanya na michakato mingine akawa anafanya anasa tu akishauriwa jambo hataki kusikiliza na alikuwa sio mlevi lakini ni kiburi tu kuna siku mwaka 1998 nikiwa na miaka 11 alimjibu Mama yaani wewe Mwanamke utanishauri nini?

Na maneno mengi ya kejeli ilipofika mwaka 1999 akanunua gari na Mama akamwambia yaani 6 Milioni unanunua gari? Kwanini usinunue hata Mashamba bado mzee alikuwa ni jeuri tu na kuna siku alinunua pikipiki bovu BMW yale mapikipiki yaliyotumiwa na Wajerumani vita ya pili kwa 2 M mama alimwambia lakini hakujali na hakutaka kushauliwa kitu, gharama za matengenezo sometimes zinafika mpaka laki 4 na kipindi kile hiyo pesa ilikuwa ni nyingi sana na mwaka huo huo 1999 gari ikapata ajali akaisafirisha kuja Dar kwa ajili ya matengenezo na hapo balaa ndio lilikoanzia.

Kule kazini akawa na absent mgogoro ukazuka mkubwa mpaka akawekwa mahubusu ya jeshi aliporudi kutoka Dar baada ya siku 42 lakini mahitaji yote muhimu tulikuwa tunapata.mimi na wadogo zangu, akawa na kesi kazini ilimsumbua sana na Mama ndio akawa anahangaika sana na.ishu zake zikzwa hazipo tena tukawa tunaishi kwa nusu Mshahara hali ilikuwa tough sana lakini kwa upande wangu nilipata rafiki ambaye familia yake ilikuwa inajiweza sana na Mzee wa ile familia alikuwa na Afsa wa idara ya serikali.

Baada ya Mzee kutoka mahabusu akapigiwa simu gari yake imepata kesi ilikamatwa katika tukio la Ujambazi alipagawa akaifuata gari yake na akaitelekeza familia mkoani yaani ni kwa neema ya Mungu tulikuwa tunaishi mkoani na Mimi sasa nilikuwa na rafiki wa kishua ambapo nilikubalika kwa Wazazi wa rafiki yangu kama mtoto wao nikawa napewa Mchele, Unga, Maharage na mimi nikawa napeleka home wanatumia maana Mimi nilihamia kwa rafiki yangu na nikiwa form 2 nilikuwa na kamera ya mzee YASHICA nikawa napiga picha wanafunzi na raia mtaani hapo nikawa napata pesa ya kuisaidia familia maana mama hakuwa na kazi hali ilizidi kuwa mbaya akaja mtoto wa Shangazi ambaye ni dereva wa magari akaibeba familia yote gharama zake.

Kumbe mzee alikuwa amesitafishwa kwa sababu alikuwa ameenda kinyume na kanuni za ajira za jeshi. Niliachwa kwa rafiki yangu niliishi pale vizuri na wadogo zangu wakagawanywa anayenifuata alienda kwa Shangazi na wengine walienda kwa Baba zangu wadogo mkoa.

Na mama ikabidi amfuate Mzee Dar hivyo hivyo. Naikatisha baada ya kufanya mtihani wa form two nikahamishiwa Dar es Salaam kwa juhudi za Baba Mkubwa ambaye alikuwa Afsa kwenye project za USAID nilihitimu kidato cha nne mwaka 2005 naada ya hapo nikaumwa sana miguu ilivimna kama nina matende na huu ilikuwa ni ushirikina na hii ilitokana na kumtukana sana Mjomba ambaye alikuwa akiishi na mdogo wangu maana walikuwa wanamnyanyasa na kumtumikisha kama Punda na shule alikuwa haendi vizuri na hii ilitokea baada ya kumfuata Mkoani Njombe nilipofika na kuikuta ile hali nilichukia na kuamua kutukana sana.

Tulivyoondoka pale kurudi Dar nikiwa mzima kuna siku mchana nimelala nikaota nipo kwenye mteremko kama pale Mkwajuni kwa wale wa Dar es Salaam mjomba akanigonga na baiskeli miguuni ndio hapo tatizo lilipoanza la.miguu niliteseka nalo sana. Nilivyopona sina haja ya.kuelezea.. ni.mengi nilipitia kuna siku nipo kanisani kuna Mama alikuwa ni Mwenyekiti wa NGO fulani akaniita akaniambia kuna kazi unaweza kuzingumza kiingereza nikamwambia nikaaa nafanya.kazi pale kwenye ile NGO kwa ujira wa euro 200 na nyumba ya kuishi pamoja na vijana wa kijerumani.

Hali ya familia ilikuwa ni mbaya mno Mzee alikuwa anafuatilia hela yake tuliomba na kufunga ili afanikiwe na.Mimi hapo nilikuwa nimeshapata kazi kwa Wajerumani ikabidi nijiendeleze kielimu na huku natoa support pale ilipobidi kufanya. Nilijiendeleza.mpaka nikapata diploma ya IT na Mzee akapata.pesa yake akaamua kuitelekeza familia hapa mjini na.

Mimi mkataba na Wajerumani ukaisha nikaingia tena kitaa nikawa nafanya kazi stationary pale posta kulikuwa.kuna dada akawa ananiuliza umesomea nini nikamwambia IT lakini sina uzoefu sana akaniambia hata mume wake kasomea IT kuna.siku mume wake akaja pale stationary akanikuta yule Dada akanitambulisha basi kwa neema ya Mwenyezi Mungu jamaa akawa ananichukua tunaenda kupiga kazi sehemu mbalimbali mpaka jamaa akaniambia dogo umeiva kuna kazi Zanzibar utaenda?

Nikamwambia nipo tayari nikaenda Zanzibar nikaanza kazi ilikuwa sio haba maisha.yalikuwa mazuri niliweza kumsomesha mdogo wangu ninayefuatana nae, hata yule wa tatu wa kiume nae nilimpa support kubwa sana kwenye mavazi na hela ndogo ndogo na mdogo wangu wa kike nae alikuwa shule ya.seminary nae nilimpatia pocket.money kama.kawaida...

Tatizo lilikuja pale nilipopata ajali ya gari nilipata.fracture yaani nilipasuka fuvu la kichwa na neva zinazopeleka taarifa kutoka kwenye jicho kupeleka kwenye ubongo zilitikisika. Nikapoteza kazi kutokana na kuwa napoteza fahamu nikarudi Dar es Salaam sasa hapo mpaka leo bado cha moto nakiona. Baba alishatelekeza familia, mdogo wangu niliyemsomesha kwa kupambana kila namna mpaka tulikuwa tunamwibia Mhindi ili nipate pesa asome,

Mama naye akapata mtaji wa biashara na wadogo zangu wale wengine kuvaa na mahitaji mengine wakaamua kunitelekeza kisa yule dogo alipata kazi ni mengi napitia lakini Maisha yetu yana siri kubwa sana na mamno yanapoenda hovyo inakuwa ni kwa sababu maalum. Kama Mungu amekuandikia kupata utapata tu maisha yanavyokuwa hovyo piga moyo konde. Siku zote nikupambana tu haina haja ya kulalamika hali niliyokuwa nayo Mimi ni mbaya sana nimejikubali na ninapambana.

Nimefanya kazi za hovyo nyingi sana pamoja na elimu kidogo niliyo nayo... Mkuu Maxence Melo ananijua vizuri sana na kipindi hicho nipo na kazi tulikuwa tunakutana hapa mjini tunapanga mikakati mingi tu ila kuna siku kama miezi mitatu alinikuta sehemu namfungulia geti atoke hakuamini ikabidi nimwambie mkasa wote maana hata ile ajali aliona picha zangu...

Maisha sio kulalamika ni kupambana tu.
 
Back
Top Bottom