Maisha yanakuhitaji umiliki vitu vitatu tu

Maisha yanakuhitaji umiliki vitu vitatu tu

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Maisha yanahitaji umiliki vitu vitatu tu:-​
  • Makazi -nyumba ya kuishi​
  • Usafiri- wa kukutoa sehemu moja kwenda kwingine​
  • Biashara- kitu cha kukuingizia kipato, iwe majengo, usafirishaji n.k​
Na wengi wanapambana kuajiriwa, kutafuta nafasi n.k ili tu kuweza kufanikisha hayo mambo makuu matatu.

Ukiyatafuta mengine zaidi ya hayo, ni kuuchosha mwili kwa vitu visivyokuwa na msingi; kwa sababu hata upambane vipi, hutokuja kumiliki 'private jet' wala 'train' kwa mazingira uliyopo.

Wengi mtatofautiana kwa ukubwa katika hayo maeneo matatu, lakini haitaathiri hivyo vitu vitatu.

Kwa hiyo kama umeshakamilisha hivyo vitu vitatu, unatakiwa utembee kifua mbele na usiangaike na mengineyo yatakayokuletea presha na kufa mapema.

Njooni kwa mjadala.​
 
Maisha yanahitaji umiliki vitu vitatu tu:-​
  • Makazi -nyumba ya kuishi​
  • Usafiri- wa kukutoa sehemu moja kwenda kwingine​
  • Biashara- kitu cha kukuingizia kipato, iwe majengo, usafirishaji n.k​
Na wengi wanapambana kuajiriwa, kutafuta nafasi n.k ili tu kuweza kufanikisha hayo mambo makuu matatu.

Ukiyatafuta mengine zaidi ya hayo, ni kuuchosha mwili kwa vitu visivyokuwa na msingi; kwa sababu hata upambane vipi, hutokuja kumiliki 'private jet' wala 'train' kwa mazingira uliyopo.

Wengi mtatofautiana kwa ukubwa katika hayo maeneo matatu, lakini haitaathiri hivyo vitu vitatu.

Kwa hiyo kama umeshakamilisha hivyo vitu vitatu, unatakiwa utembee kifua mbele na usiangaike na mengineyo yatakayokuletea presha na kufa mapema.

Njooni kwa mjadala.​
Hayo yote hayawezekani bila hela
 
kaa vizuri na matajiri hii kitu mara nyingi huwa inawakumba......kuna kitu kinaitwa amani ya moyo, na ndilo tatizo linalomsumbua kwa sasa rafiki yangu doctor hamis kigwa
Kuna hatua fulani inabidi kukubali haya ndio maisha yangu, muhimu napata mahitaji ya msingi; ila ukizidi kutafuta zaidi, utulivu wa nafsi unakuwa haupo.
 
Back
Top Bottom