Maisha yetu huendeshwa na Nyota?

Maisha yetu huendeshwa na Nyota?

Status
Not open for further replies.
kwahiyo hizo nguvu ndo zinaendesha maisha ya mwanadamu kwa hyo hta mafanikio ya mtu yana tokana na hizo nguvu?

Ndio mafanikio na hata kufeli kwetu nk vina mwingiliano mkubwa sana na hizo nguvu na sub conscious mind zetu
 
Nyota inaanza kama kitu kinaitwa "molecular cloud" ambayo inacontain hydrogen na helium... ikitokea inbalance ya forces zinazo hold hizi clouds in place zinaanza ku-collide against one another na hapo ndipo mwanzo wa nyota unapoanza hadi inakua nyota sawa ilivo jua au nyota nyingine...

Force pekee inayounganisha mtu na nyota ni force of gravitation ambapo kama nyita iko mbali sana basi hii force ni negligible... uchawi uchawi mwingine ni ndoto tu na hauna evidence yoyote, leo asimame mtu aniambie nyota yangu afu aniambie nifanye nini nifanikiwe,

Nitafanya opposite na nitafanikiwa kumprove wrong... ukisema unaamini predictions za maisha kuoingana na nyota basi dini zooote ni uongo, sayansi ni uongo, study ya nyota tu ndio ukweli which is nonsense, maana utakua umeondoa "free will" kama nyota zinaendesha maisha ya mtu..
 
Tatizo lenu wakristo ni kutosoma biblia na kuielewa Yesu alipozaliwa nyota ya kung'aa ilionekana kwa wasafiri na ikawaongoza hadi mji alipozaliwa yesu. Biblia haikuchambua kwa kina juu ya nyota japokuwa wakati wa kuzaliwa yesu mamajusi wa mashariki walikwenda yerusalem Math. 2:1-2. Sasa niwaulize swali wakristo je, ile nyota inauhusiano gani na yesu? Au kabla ya kuzaliwa yesu nyota hazikuwepo? Ukweli ni kwamba nyota zina uhusiano mkubwa na maisha yetu sisi wanadamu. Tatizo letu hatupendi kusoma na kuchunguza juu ya maisha yetu. Mungu aliturahisishia maisha yetu ili tuweze kumuabudu bila vikwazo tumeyafanya maisha yetu kuwa magumu ndo maana hata ibada zetu zimekuwa ngumu kwa sababu tumejipa uvivu wa kufikiri na kujifunza.

Ile nyota ilionyesha direction na haikuendesha maisha ya Yesu, it was simply an indication na hakuna kitu kama nyota kuendesha maisha ya mtu.. Uhusiano pekee ulionao na nyota ni kwanza jua hukupa nguvu, pili nyita nyingine angani pamoja na jua zina force inaitwa "gravitation" ambayo ina keep kila kitu in balance... Hakuna nyota kukuendesha wewe ati uwe secretary, nyota inajua usecretary? hahahaha
 
Nyota inaanza kama kitu kinaitwa "molecular cloud" ambayo inacontain hydrogen na helium... ikitokea inbalance ya forces zinazo hold hizi clouds in place zinaanza ku-collide against one another na hapo ndipo mwanzo wa nyota unapoanza hadi inakua nyota sawa ilivo jua au nyota nyingine... force pekee inayounganisha mtu na nyota ni force of gravitation ambapo kama nyita iko mbali sana basi hii force ni negligible... uchawi uchawi mwingine ni ndoto tu na hauna evidence yoyote, leo asimame mtu aniambie nyota yangu afu aniambie nifanye nini nifanikiwe, nitafanya opposite na nitafanikiwa kumprove wrong... ukisema unaamini predictions za maisha kuoingana na nyota basi dini zooote ni uongo, sayansi ni uongo, study ya nyota tu ndio ukweli which is nonsense, maana utakua umeondoa "free will" kama nyota zinaendesha maisha ya mtu..


Afadhali leo nimepata mwanasayansi mwenzangu.


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Ile nyota ilionyesha direction na haikuendesha maisha ya Yesu, it was simply an indication na hakuna kitu kama nyota kuendesha maisha ya mtu.. Uhusiano pekee ulionao na nyota ni kwanza jua hukupa nguvu,

Pili nyita nyingine angani pamoja na jua zina force inaitwa "gravitation" ambayo ina keep kila kitu in balance... Hakuna nyota kukuendesha wewe ati uwe secretary, nyota inajua usecretary? hahahaha

Your right scientifically although naweza pingana nawe kupingana nawe spiritually. Sayansi ni ishu nyingine na natural force ni ishu ya pili. Vitu hivi huenda pamoja sana ingawa kuna mahali vinapingana na hasa pale sayansi inaposhindwa ku prove jambo ambalo ni la asili.

Let me give you an example, kuna imani imeenea kwa jamii ya wtz kuwa kitovu cha mtoto kikiangukia kwenye uume wa mtoto atakuwa -------. If you ask any doctor atakwambia hakuna kitu kama hicho because there is no scientific relation between or not proved scientifically. Ngoja niendelee kufuatilia nitakupa data zaidi
 
Your right scientifically although naweza pingana nawe kupingana nawe spiritually. Sayansi ni ishu nyingine na natural force ni ishu ya pili. Vitu hivi huenda pamoja sana ingawa kuna mahali vinapingana na hasa pale sayansi inaposhindwa ku prove jambo ambalo ni la asili. Let me give you an example, kuna imani imeenea kwa jamii ya wtz kuwa kitovu cha mtoto kikiangukia kwenye uume wa mtoto atakuwa -------. If you ask any doctor atakwambia hakuna kitu kama hicho because there is no scientific relation between or not proved scientifically. Ngoja niendelee kufuatilia nitakupa data zaidi

Hapo kwenye red -"you are right"

Sasa wewe hilo la kitovu ushawahi shuhudia na ukaona effect yake? sayansi inajaribu kuprove vitu vingi tu kwenye dini, biblia inavosema dunia ni round, sayansi nayo ikaprove hilo, biblia ilivosema binadamu aliumbwa wa mwisho hata evolution inasema vilianza vingine oceans, miti afu binadamu complete ni wa juzijuzi tu kwenye life tree ya evolution...

Ila imani za ajabu ajabu zisizo na proof siwezi kuzisikiliza kabisa... I trust ndio kuna vitu spiritual ambavo scince haiwezi kuprove ila sio swala la nyota, swala la nyota is just a hoax watu wanapiga hela
 
Angalia video hapo!


 
Last edited by a moderator:
Kwa wakristo BIBLIA TAKATITU imekataza kufuata utabiri wa nyota na mengine yafafananayo na hayo sijui kwa jirani zetu wa kibla

huku kibra aya inasema......hakika kamali,ulevi na kupiga ramli ni amali za shetani, jiepusheni nazo
uliza jingine, uislamu ni hoja bana hahaaaaa
 
huku kibra aya inasema......hakika kamali,ulevi na kupiga ramli ni amali za shetani, jiepusheni nazo
uliza jingine, uislamu ni hoja bana hahaaaaa

Well said!
Ila nna maswali ya kukuuliza!

Jee unatambua kuna wanaotabiri kwa ushirikina (kwa kutumia mashetani) na kunawanaotabiri kupitia sayansi ya anga = astrologers (bila ya kutumia mashetani)???

Kwanini kunaukweli juu ya hao wanaotabiri?
 
Wale akina mamajusi walifuata nyota mpaka wakafika alipozaliwa mtoto yesu.

Elimu ya nyota ipo sahihi kabisa katika kutabiri ila biblia imekataza.

Labda niongeze tu hapo. Mbona mesiya aliyabiriwa? Utabiri nini? Mimi naamini kuna nguvu ambazo hatuzifaham. N hz nguvu zimetoka kwakwe Mwenyezi Mungu,ambaye ndie aliyeumba kila kitu kwa pumzi yake na mikono yake.




The king.
 
Kwa wakristo BIBLIA TAKATITU imekataza kufuata utabiri wa nyota na mengine yafafananayo na hayo sijui kwa jirani zetu wa kibla

"Mshike elimu usimuache aende zake" huu ni moja ya mistari iliyopo kwenye bibla ndugu na mambo ya nyota nadhani ni elimu pia sema itategemea na matumizi yake na kuna ushaidi tosha kwamba elimu hii ilikuwa inatumika toka enzi hizo kwa mfano wale wachungaji walipoiona nyota na kuifwata ikawaongoza mpaka zizini alipokuwa amezaliwa yesu ...

Je nani aliwaambia waifwate ile nyota? walijuaje wakiifwata ile nyota itawapeleka ilipowapeleka na kadhalika... sasa maamuzi ni yako kufanya mambo ya nyota kama elimu na kufwata muongozo wake kutokana na maelekezo ya biblia ama kuacha kabisa na kubaki vivyoivyo pasipo kujua ili hali sidhani kama kutakuwa na manufaa
 
Mtoa hoja hayo uliyoyasikia yanaukweli ndani yake ila si kwamba yanakuzuia usiende kinyume au tofauti na nyota husika hapana sema tatizo linakuwa unakuta kama ulistaili kupata kumi kwa kufwata nyota bac unapata pungufu kwa kuto kuifwata ila zaidi na zaidi kama alivyosema mchangiaji mwingine kuna other factors nazo ambazo zinalandana na habari ya nyota kama vile Will Powers, Omens na mengineyo ambapo wigo wake ni mkubwa sana inategemea ww ni wa mlengo upi
 
Well said!
Ila nna maswali ya kukuuliza!

Jee unatambua kuna wanaotabiri kwa ushirikina (kwa kutumia mashetani) na kunawanaotabiri kupitia sayansi ya anga = astrologers (bila ya kutumia mashetani)???

Kwanini kunaukweli juu ya hao wanaotabiri?


watoa mada wenzangu kwa mtazamo wangu mimi naona wote mpo sawa ila kwa uwakika zaidi na uelewa wa kina jaribuni kufanya tafiti kwenye kitu kinachoitwa Shiriki mtapata mwanga zaidi na kujua tofauti iko wapi na kipi ni lipi na lipi ni kipi
wasallam
 
watoa mada wenzangu kwa mtazamo wangu mimi naona wote mpo sawa ila kwa uwakika zaidi na uelewa wa kina jaribuni kufanya tafiti kwenye kitu kinachoitwa Shiriki mtapata mwanga zaidi na kujua tofauti iko wapi na kipi ni lipi na lipi ni kipi
wasallam

Mkuu shirki kutokana na imani yangu, imegawika sehemu 4!
Nikihusisha shirki na hayo mambo ya nyota, ni wazi kuwa nyota ni moja kati ya shirki!

Nimeona hapo juu umemjibu mdau amtafute elimu, nikaona tena umesema hata wachungaji waliifata nyota ya Yesu hadi walimfikia!

Upande wa pili huku, temeambiwa tutafute elimu hata china! Elimu yeyote inaruhusika kusomwa na kutumika! Ispokuwa itumike kwa mambo mema, either kwa kusaidia watu!

Tupaache hapo!
Na kunakitu ningependa nijue:

Kama nyota zinaukweli ndani yake, kwanini imekatazwa kufatilia?
Natambua wenzetu (wazungu na wachina) hutumia nyota kuangalia vipaji vyao na kudetermine nini wafanye ili wapate maendeleo!
Na kunabaadhi ya watu (wanandoa) hutegea hata miezi ya kupeana mimba ili mtoto wao azaliwe ktk nyota wanayoitaka wao na kwa kuamini mtoto atakuwa vile wapendavyo!

Jee unaliongeleaje hilo?
...
Na pia niliskia na watu wazima kwamba kunasiku (tarehe/mwezi na mwezi/mfunguo) fulani ndani ya mzunguko wa mwaka, ukioa ndani ya siku hizo, ndoa yako haitadumu! Wakati kuna baadhi ya siku ukioa ndoa inakuwa imara!

Jee ulishawahi kuskia hilo?
Kama umewahi, kwanini iko hivyo?

Binafsi haya mambo yananichanganya sana, ningependa nitambue kuna nini nyuma ya pazia! Kwa nini iwe hivyo?

Cc: MziziMkavu!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu shirki kutokana na imani yangu, imegawika sehemu 4!
Nikihusisha shirki na hayo mambo ya nyota, ni wazi kuwa nyota ni moja kati ya shirki!

Nimeona hapo juu umemjibu mdau amtafute elimu, nikaona tena umesema hata wachungaji waliifata nyota ya Yesu hadi walimfikia!

Upande wa pili huku, temeambiwa tutafute elimu hata china! Elimu yeyote inaruhusika kusomwa na kutumika! Ispokuwa itumike kwa mambo mema, either kwa kusaidia watu!

Tupaache hapo!
Na kunakitu ningependa nijue:

Kama nyota zinaukweli ndani yake, kwanini imekatazwa kufatilia?
Natambua wenzetu (wazungu na wachina) hutumia nyota kuangalia vipaji vyao na kudetermine nini wafanye ili wapate maendeleo!
Na kunabaadhi ya watu (wanandoa) hutegea hata miezi ya kupeana mimba ili mtoto wao azaliwe ktk nyota wanayoitaka wao na kwa kuamini mtoto atakuwa vile wapendavyo!

Jee unaliongeleaje hilo?
...
Na pia niliskia na watu wazima kwamba kunasiku (tarehe/mwezi na mwezi/mfunguo) fulani ndani ya mzunguko wa mwaka, ukioa ndani ya siku hizo, ndoa yako haitadumu! Wakati kuna baadhi ya siku ukioa ndoa inakuwa imara!

Jee ulishawahi kuskia hilo?
Kama umewahi, kwanini iko hivyo?

Binafsi haya mambo yananichanganya sana, ningependa nitambue kuna nini nyuma ya pazia! Kwa nini iwe hivyo?

Cc: MziziMkavu!
Ki-Dini Haswa Dini ya Kiislam kuangalia mambo ya nyota imekatazwa

hairuhusiwi kabisa. Ila kidunia yetu Ki-Sayansi inaruhusiwa kwa Sayansi haiamini mambo ya Dini.

Kuangalia siku tarehe mwezi na mwaka kwa ajili ya kufunguwa duka au kuowa mke au kusafiri au kuafanya jambo lolote lile zuri ipo na ni kweli ni elimu yake Mungu ndio maana tumekatazwa

katika dini ya Kiislam kutaka kujuwa siri zake Mwenyeezi Mungu. Lakini hapa hatupo kwenye

jukwaa la Mambo ya Dini tupo sehemu nyingine ya jukwaa la la ( Jamii Intelligence) tupo huru

kuzungumzia kila kitu kwa uwazi.
 
Mengi nimesikia kuhusiana na nyota binafsi bado nko njia panda juu ya hili kutokana na maelezo yake kua watu hutofautiana nyota kulingana na mwezi na tarehe ya mtu kuzaliwa pia tabia ya mtu inatokana na nyota yake ilivyo hata kazi pia hutegemeana na nyota swali langu linakuja kwann iwe ivo inamaana ikitokea mtu nyota yake inamtaka afanye kazi ya aina fulan inabidi afanye hata kma haipend ilimrad tu nyota yake inasema ivo au hata kwenye masuala mazima ya mapenzi mtu itabidi achague yule anaye endana kwa kuangalia nyota ili aweze kudumu nae mbona kuna mambo unaweza ukafanya na ukaenza kudumu katika mapenzi.naomben mchango wenu juu ya hili
1.jpg
Maalim Hassan Yahya Hussein (kushoto) akihojiwa na mwandishi wa habari.


MAALIM HASSAN YAHYA ATOA UTABIRI WA MWAKA 2014



LEO mnajimu maarufu, Maalim Hassan Yahya Hussein amefanya mkutano na waandishi wa habari. Ametabiri mambo zaidi ya kumi, yasome mwenyewe.
Ndugu Wanahabari
UTANGULIZI:

Mwaka huu tulionao hivi sasa wa 2014 umeanzia siku ya Jumatano, siku hii inatawaliwa Na Sayari ya Mercury, Sayari hii iko Mbingu ya 2, na nyota zake ni mbili nazo ni Mapacha (Gemini) ambayo asili yake ni upepo na Mashuke au (Virgo) ambayo asili yake ni Udongo


Hii sayari ya Mercury inahusika na mambo yanayohusiana na Adabu, Malezi mema, Mantiki, Kupata kitu, Fasihi ya lugha, Ufahamu, Uelewa, Elimu, Urafiki, Hila na kudanganya, Hesabu, Vitabu, Sanaa za aina zote, Ukatibu au Ukarani, Shule au Kumpeleka mtoto shule.
Vile vile inahusiana na mambo ya Nakshi, sanaa masuala ya Urembo, kuandaa Majeshi, nidhamu na mapato.


Mwaka 2014 Mwezi utapatwa mara mbili tarehe 15 Aprili ambayo itakuwa siku ya Jumanne na Oktoba 8 ambayo ni siku ya Jumatano na Jua nalo litapatwa mara mbili tarehe 29 Aprili ambayo ni siku ya Jumapili na Oktoba 23 ambayo itakuwa siku ya Alkhamisi

Nimeyaeleza haya kwa sababu katika Elimu ya Unajimu na Utabiri kupatwa kwa Jua na Mwezi kuna athari za moja kwa moja na matukio yanayotokea hapa Duniani.


Mwaka ukianzia siku ya Jumatano, unaashiria shida kubwa na nyingi sana. Unaashiria kuibuka kwa maradhi mengi, uadui kuwa mwingi kati ya watu au nchi, vimbunga na majanga asilia yanayotokana na upepo, vifo vingi hasa wanaume vijana na Viongozi wa kidini na kisiasa. Aidha, wajawazito kupata shida katika uzazi, Jua kuwa kali sana, Njaa kuwa nyingi na ukame.


Pia wanyama kupata magonjwa, watu kulalamikia mifumo ya kiutawala, watu kurukwa na akili, Ajali kuwa nyingi zitakazosababisha vifo vya watu wengi kwa wakati mmoja, safari kutotimia. Pamoja na hayo, uongo na propaganda kutawala waimbaji, wasanii kufa au kupatwa na kashfa.
Jumatano haioneshi kuwako kwa vita, bali mazao yatakuwa kidogo.
Katika hali hii,


1. Natabiri Mwaka huu kinyota unaashiria shida na maafa makubwa. Maradhi kama vile Malaria, Kuhara, Kuhara Damu, Kichocho vitakuwa vingi iwapo watu au jamii haitajihadhari.


2. Natabiri Uadui wa Taasisi au Chama na Chama utakuwa mkubwa na kuna dalili za kupigana kwa wafuasi wa Vyama Pinzani.


3. Natabiri: Nyota pia zinaonesha kuwa Tanzania itakuwa katika mzozo mkubwa na majirani zake lakini uwezekano wa kupiganwa kwa vita kati sisi na wao hauko.


4. Natabiri: Tahadhari ya hali ya juu inatakiwa iwepo kwani Tanzania inaonekana kuwindwa na mataifa ya mbali ili iingie kwenye vita isipokuwa kwa haiba ya Siku ya Jumatano, vita hivyo vitadhibitiwa kitaifa na kimataifa.


5. Natabiri:- Vifo vya Vijana vikiongozana na mauaji ya kupanga vitakuwa jambo la kawaida kwenye Mwaka huu na wahusika zaidi ni Wasanii wa fani zote wakiwemo Waandishi wa Habari.


6. Natabiri:- Wanasiasa wataendelea kuwa walengwa kwa mambo ya kijamii hasa kashfa za ngono na biashara haramu. Nyota zinaonesha kuwa mmoja wa watu mashuhuri sana hapa nchini atatumbukia kwenye kashfa hiyo na itamuangusha kijamii pale atakaposhughulikiwa kwa kufilisiwa mali na kufungwa kitaifa na kimataifa.


7. Natabiri;- Kwa vile siku ya Jumatano ni siku mbaya katika mwaka, kuna dalili za watu kuswekwa kizuizini kwa kashfa za ukiukwaji wa utiii kwa Serikali na vyombo vyake vya dola.


8. Natabiri;- Kuna kiongozi mmoja wa Kisiasa na kijamii mwenye hadhi kubwa hapa nchini atarukwa na akili kuelekea mwisho wa Mwaka huu na itakuwa anguko lake na wafuasi wake kwenye harakati za kuimarisha Ustawi wa Watanzania na dola yake.


9. Natabiri:- Nyota zinaonesha kuwa kinamama wajawazito watakufa kwa uzazi kutokana na tabia ya kutozingatia mafunzo ya uzazi na taratibu zake. Wengi watashindwa kujifungua na kusababisha wao pamoja wa watoto watarajiwa kufa.


10. Natabiri;- Ukame utaigubika nchi kwa kiasi kikubwa na wananchi watakuwa na wakati mgumu katika mwaka huu kulingana na nyota hasa mwaka unapoanza na siku ya Jumatano. Vimbunga na pepo kali zitatawala mwaka huu.


11. Natabiri;- Kutokana na ukame huo wanyama watakuwa katika wakati mgumu na Tanzania itapoteza asilimia kubwa ya wanyama wake mwaka huu na hivyo kusababisha wafugaji na wakulima kuwa kwenye wakati mgumu kimaisha.


12. Natabiri;- Kelele za kudai haki za kibinadamu zitajitokeza kwenye mwaka huu na kusababisha hali ya mpito ya dharura kutangazwa na wakuu wa nchi. Hatua hiyo itampa Rais ushujaa na utasababisha aendelee kuwa kiongozi mwenye mvuto mkubwa duniani kama alivyokuwa kwa mwaka uliopita.


13. Natabiri:- Pamoja na kwamba muda Bado lakini Nyota bado hazioneshi Tanzania kuongozwa na Rais mwanamke ingawa kuna harakati nyingi zinazotaka iwe hivyo. Hata hivyo natabiri Kupatikana kwa viongozi wengi wanawake au wanawake kushika nafasi kubwa katika siasa.


14. Natabiri:- Katiba mpya ya nchi yetu itapita kwa mbinde, kwani kutakuwa na malumbano na utata mkubwa hasa kuhusu agenda ya serikali tatu. Nyota zinaonesha kuwa Rais Kikwete atatumika zaidi kuweka mambo sawa baada ya jamaii nzima kuweweseka katika hili.


15. Natabiri:- Mwelekeo wa nyota za mwaka huu pia zinaonesha kuwa kutakuwako na majaribio ya kiuhalifu katika uongozi ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo vitasababisha tafrani lakini vitadhibitiwa na mambo kwenda sawa-bin-sawia.


16. Natabiri;- Warembo, Wana-filamu, Wanamuziki, Wanasoka, Wanahabari na Wanasiasa wako katika hatari ya kuanguka kihali na mali na kutokana na hilo yakawapo mabadiliko ya mwelekeo wa kimaisha kwao katika mwaka huu kuelekea Uchaguzi Mkuu was Rais, Wabunge na Madiwani mwakani. Hatua hiyo itasababisha pia vifo vya kawaida na vya ghafla kwao.


Mwaka 2014 si mzuri kwao hata hivyo muelekeo wa mafanikio makubwa kwa makundi hayo ni mzuri. Wako baadhi kutoka katika katika makundi hayo niliyoyataja wataula kisiasa na kimataifa.


17. Natabiri: Kiongozi mmoja wa Chama cha Siasa hapa nchini atangolewa kwenye uongozi na kitendo hicho kinaweza kumsababishia anguko kubwa la kisiasa kwake au hata kifo.

18. Natabiri:-Baadhi ya chaguzi za awali za Serikali za Mitaa mwaka huu zitakumbwa na na kizungumkuti kiasi cha kuiingiza nchi yetu kwenye mizozo yenye muelekeo wa mapigano ya kijamii.


19. Natabiri: msiba wenye sura ya kitaifa


20. Natabiri :- Kuna Baadhi ya Wabunge watapata dhoruba kubwa majimboni itakayosababisha kupoteza nyadhifa zao siku za usoni


21. Natabiri :-Mwaka 2014 si mzuri kwa viongozi wa Kidini, wako watakaokufa ghafla, huku baadhi yao wakingolewa madarakani au kwenye mamlaka kwa haiba yenye aibu na kashfa.


22. Natabiri;- Rais atafanya Tukio Kubwa la kutikisa nchi lakini tukio hilo litaleta Neema baadae kama vile heshima kwa Taifa, amani uzalendo, uwajibikaji na staha katika Jamii


Alhajj Maalim Hassan Yahya Hussein

Mrithi wa kazi za Sheikh Yahya Hussein, Bingwa wa utabiri nchini na mtaalamu wa nyota
Jumapili tarehe 5/1/2014. Chanzo.
http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/maalim-hassan-yahya-atoa-utabiri-wa-mwaka-2014?xg_source=activity
 
Namna Ya Kuelewa Nyota Za Mbinguni

Astronomia ni utaalamu wa nyota, sayari na nyendo zake. Watu wengi huvutiwa na maelezo na mazungumzo yanayohusu mambo ya nyota. Wakibahatika kuona tukio fulani la ajabu mbinguni pia wanavutiwa sana. Lakini papo hapo, wengi wao hushindwa kuelewa mambo hayo kwa undani.

Ni muhimu kujifunza kuhusu nyota kwa sababu tunaweza kuelewa umbo na mwenendo wa Dunia yetu na kuelewa namna tabia ya hali ya hewa Dunia yetu ilivyobadilika katika mamilioni ya miaka iliyopita. Tunaweza kujifuza kuhusu chimbuko la mfumo wa Juan na sayari zake na hata wa ulimwengu (universe) wenyewe, na kufikiria kuhusu namna nyingine za maisha zinazoweza kuwepo ulimwenguni.


Tunaweza kujifunza kuhusu vitu vingi vya ajabu vilivyopo ulimwenguni, kama vile nyota za mbali sana zinazotoa mawimbi ya redio yenye nguvu kali mno na nyota za nutroni. Pia kuna sehemu za anga ambazo zinauwezo wakuvuta hata mwanga ndani yake (BLACK HOLES). Pengine kwa kuelewa elimu ya Astronomia tutaweza kuthamini na kuelewa ukubwa wa ulimwengu wetu kuipana na kiumri.


Duniani tunaweza kuelewa mvuto wa Jua na Mwezi juu ya Dunia yetu ambao huleta kujaa na kupwa kwa maji baharini. Tutaweza kuelewa kwamba kupatwa kwa Jua na Mwezi si mazingaombwe ya waganga au wanajimu lakini ni matukio yaliyo na sababu maalum inayoeleweka - yaani hutokea kwa sababu Mwezi na Dunia zinaizunguka Jua.


Je Tutaanzaje?


Nyota ni ngumu kuzielewa kwa sababu ziko mbali mno na sisi na hatuwezi kuzifikia kwa njia yoyote. Mojawapo ya njia rahisi ya kukielewa kitu ni kwa kukiangalia kwa makini. Kwa bahati mbaya ukianza kuangalia nyota za angani, utakuta zinaleta picha ya min'garo na mimeremeto zilizokaa shaghalabaghala bila mpangilio wowote. Ukiongezea matatizo utakayopata kutokana

mawingu kufunika nyota mara kwa mara, hutalaumiwa ukikata tamaa kabla hata hujaanza! Lakini amini usiamini, kuna utaratibu maalum wa kimsingi unaoweza kuutumia kuelewa mpangilio wa nyota. Na kama utakuwa makini na mvumilivu, utaweza kujifunza namna ya kutambua nyota nyingi pamoja na kutofautisha maumbo mbali mbali yanayoonekana angani. Ukielewa namna ya kutambua nyota, basi utakuwa umejipanulia uwezo wako wa kuelewa elimu nzima ya Astronomia na hatimaye ya ulimwengu wetu.


Je, ni lazima kutumia darubini za hali ya juu kutazamia mbinguni? Hapana. Macho yetu yanatosha kuanza kuelewa na kufurahia mbingu zetu za usiku. Iwapo kuna darubini, zinaweza kutumiwa kuchunguzia milima na mabonde yaliyopo mwezini. Iwapo utapenda kuona mambo mengi na kwa undani zaidi kwenye sayari, utahitaji darubini kali (telescope).


Kutambua nyota na Makundi ya Nyota


Angani, nyota zote zimejipanga kwa mfumo ambao haubadiliki. Lakini kuna vitu vingine kwa mfano Mwezi, sayari mbali mbali, vimondo (comets) na vinginevyo vinavyobadilisha nafasi zake angani siku hadi siku. Ni muhimu sana kwanza kutambua na kuuelewa mandhari ya mfumo wa nyota ambayo haibadiliki. Lakini kwa kutazama tu mara moja moja angani utashindwa kutambua mfumo wowote.

Kuna tatizo gani? Kwanza, mawingu yanaelekea kuziba nyota nyingi mara kwa mara. Hata hivyo sababu ya msingi ni kwamba mfumo wa mpangilio wa nyota husogea magharibi kila saa kutokana na mzunguko wa Dunia kwenye mhimili wake (zingatia kuwa mzunguko huu ni kama ule unaosababisha Jua kusogea angani asubuhi hadi jioni). Sababu ya tatu ya kubadilika kwa mandhari ya nyota ni kwamba nyota zote husogea mgharibi pole pole siku hadi siku, kufuatana na mzunguko wa Dunia kuizunguka Jua mara moja kwa mwaka.


Kwa hiyo ukitaka kutambua maumbo ya nyota katika mandhari ya anga za usiku, hakikisha unaangalia vizuri sehemu moja ya anga saa ile ile kwa siku chache mfululizo. Huna budi kuchagua sehemu nzuri ambapo sehemu hiyo ya anga haizuiliwi mno na miti au vizuizi vingine. Si wote tuliyo na muda wa kuangalia anga kwa makini kila siku. Na pamoja hiyo, hali ya hewa inaweza

kutuzuia kuangalia nyota vizuri. Kwa hiyo hatuna budi kuzingatia mwendo ule wa pole wa kusogea magharibi kwa umbo la mbingu baada ya siku kadhaa. Inabidi kuiangalia sehemu hiyo hiyo ya anga saa moja kabla kila baada ya majuma mawili.

Kama utafauta kanuni hizi za msingi (ingawa zinatumia muda sana!), utaweza kutambua maumbo machache ya muhimu. Upande mzuri wa kuangalia mbingu hapa kwetu Tanzania ni upande wa kusini ambako kuna nyota nyingi na maumbo mengi yanayoweza kutambulika kwa urahisi.

Jambo la msingi ni kutambua maumbo sanifu yanayojulikana kuwa ni Makundi Ya Nyota (constellations). Kwenye anga la mbingu ya kusini utaweza kupata umbo kama tiara au kishada la nyota nne zijulikanazo kama ni "Msalaba wa Kusini". Iwapo utaangalia kwa muda wa saa chache usiku huo huo, utatambua kwamba upande mrefu wa msalaba daima unaelekea kusini. Umbo jingine l

la kuvutia unaloweza kulitambua upande wa mashariki kwa sehemu ya tosini. Hili ni kundi la nyota lijulikanalo kuwa ni NG'E, kundi la nyota lenye umbo la ng'e ambalo limeundwa na nyota tatu au nne zinazo unda "kichwa" chake na nyota yenye mwanga mkali mwekundu ijulikanayo kama ANATARES kwenye "shingo" yake. Na mfuatano wa nyota nyingi huunda "mkia" wake na kumalizia na nyota mbili zilizokaribiana zinazounda "mwiba". Linganisha unachokiona mbinguni na ramani rahisi ya nyota

iliyoonyeshwa hapa. Ili uweze kuitumia ramani hii iishike wima na kuizungusha ili upande unaoelekea unasomeka chini. Mara baada ya kutambua umbo au kundi moja, ramani kama hizi zinaweza kukuongoza kutafuta maumbo mengine angani na hatimaye kutambua nyota zote angani. Jaribu kutambua angalau umbo moja la nyota kila wakati unapoweza kuona mbingu kwa urahisi, na hatimaye utaelekea kupenda elimu ya nyota kwa ukamilifu.


Maelezo Machache Ya Jinsi Ya Kutumia Ramani Ya Nyota


Iwapo ramani iliyochapwa ni ndogo, ikuze nakala kivuli asilimia 200, na tumia nakala hiyo kwa kuainisha nyota na Makundi ya nyota. Tafuta eneo unaloweza kuona vizuri sehemu kubwa ya mbingu kuanzia kwenye upeo wa macho hadi utosini. Tafuta mwelekeo wako wa wastani kwa kutumia Jua wakati wa mchana na zoea eneo lako. Ifikapo kiasi cha saa 2 usiku, uelekee

upande uliochagua na iishike wima ramani ya mbingu na igeuze hadi upande unaoelekea unasomeka chini katika ramani.

Yazoeze macho yako kwa dakika tano au kumi na kinga macho yako kutokana na mwanga wowote mkali unaoweza kuwa upande unaoangalia. Tumia tochi yenye mwanga hafifu kumulika ramani. Nyota zilizoko karibu na ukingo wa mzingo katika ramani zitaonekana angani karibu na upeo wa macho wa upande unaoelekea. Nyota zilizopo katikati katika ramani ni zile

zitakazoonekana utosini. Zingatia kwamba katika ramani zimeonyeshwa nyota zile zile tu zenye mwanga mkali, lakini uhakika wa kuonekana nyota angani utategemea hali ya mwanga katika eneo lako. Watazamaji walioko katika miji mikubwa kama Dar es Salaam wataona nyota chache zaidi kwa vile mwanga mkali wa mji utang'arisha anga na kufunika mwanga wa nyota hafifu.

Lakini watu wanoishi mbali na mji wanaweza wakaona nyota nyingi zaidi kuliko zile zilizoonyeshwa katika ramani kwa vile anga huwa nyeusi kabisa sehemu hizo.

Kumbuka kwamba ukibadilisha mwelekeo, zungusha ramani pia huku ukiwa umeishika wima na hakikisha kwamba upande unaoelekea upo chini katika ramani.
Nakutakia utazamaji mwema wa nyota.

Kwa wale wanaotaka kujuwa nyota yao na bahati zao na pete gani wakivaa ili waweze kufanikiwa kimasiha na kimapenzi unaweza kunitumia Baruwa ya Pepep email Address yangu hii hapa fewgoodman@hotmail.com au waweza pia kunitembelea Blog yangu bonyeza hapa.
Mawasiliano
 
Ki-Dini Haswa Dini ya Kiislam kuangalia mambo ya nyota imekatazwa

hairuhusiwi kabisa. Ila kidunia yetu Ki-Sayansi inaruhusiwa kwa Sayansi haiamini mambo ya Dini.

Kuangalia siku tarehe mwezi na mwaka kwa ajili ya kufunguwa duka au kuowa mke au kusafiri au kuafanya jambo lolote lile zuri ipo na ni kweli ni elimu yake Mungu ndio maana tumekatazwa

katika dini ya Kiislam kutaka kujuwa siri zake Mwenyeezi Mungu. Lakini hapa hatupo kwenye

jukwaa la Mambo ya Dini tupo sehemu nyingine ya jukwaa la la ( Jamii Intelligence) tupo huru

kuzungumzia kila kitu kwa uwazi.

Well said MziziMkavu!
Kwa vile hapa tupo Jamii intelligence watuache tupumue!

Mimi napenda kufaham kuna nini nyuma ya pazia. Hasa apo kwenye kutiming tarehe ili kufanya tukio!
Kwanini hizo siku nyengine ziwe mzuri na hizo nyengine ziwe mbaya kwa kufanya tukio? Ni nini kinasababisha hilo?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom