Mkuu
Mashaxizo kama kitu hujui ni bora ukauliza kwanza umenukuu hiyo Wamakabayo, halafu hata ulichonukuu hujui kinazungumzia kitu gani nitakiweka hapa chini ili twende vizuri, hata mistari yenyewe uliyoipangilia umeipangilia ndivyo sivyo, hivi unafanya hivyo kwa lengo gani!? ngojea tuiangalie hiyo Wamakabayo uliyonukuu 1 Wamakabayo 1:53-58
1 Wamakabayo 1:53-59
53 na kuwafanya watu waaminifu wa Israeli watoroke na kujificha popote walipoweza.
54 Siku ya kumi na tano ya mwezi wa Kislevu, mwaka 145, mfalme Antioko aliisimamisha lile Chukizo Haribifu juu ya madhabahu kuu ya sadaka za kuteketezwa hekaluni, na vimadhabahu vya miungu vikajengwa katika miji yote ya Yudea,
55 wakawa wanafukiza ubani milangoni mwa kila nyumba na mitaani.
56 Vitabu vyovyote vya sheria walivyoviona walivichanachana na kuvichoma moto.
57 Yeyote aliyeshikwa ana kitabu cha agano au anaifuata sheria, aliuawa kwa amri ya mfalme.
58 Mwezi hata mwezi, watu hao waovu walitumia mabavu dhidi ya Waisraeli waliokamatwa katika miji mbalimbali.
59 Siku ya ishirini na tano ya mwezi huo huo, watu hao walitoa tambiko katika kimadhabahu kilichosimamishwa juu ya madhabahu kuu ya sadaka za kuteketezwa hekaluni.
Haya hiyo hapo juu Wamakabayo uliyoileta, Wewe si ni mtaalamu wa kuchambua scripture, haya niambie Antioko ni nani!? ukishindwa google Antiochus Epiphanes uweze kumtambua, huyo ndio mfalme wanayemzungumzia hapo...
chukizo la uharibifu ni kitu gani!? nijibu maana wewe ndio unatufundisha kwamba unajua japokuwa nimeona hujui ulichokileta
Unafahamu hao Wamakabayo ni kina nani!?
Halafu kitu kingine hapa mmepewa ushauri ila nashindwa kuelewa sijui huwa hausomi
Quran 29:46
Wala msijadiliane na Watu wa Kitabu ila kwa njia iliyo nzuri kabisa, isipo kuwa wale walio dhulumu miongoni mwao. Na semeni: Tumeyaamini yaliyo teremshwa kwetu na yaliyo teremshwa kwenu. Na Mungu wetu na Mungu wenu ni Mmoja. Na sisi ni wenye kusilimu kwake
Quran 29:47 Na namna hivi tumekuteremshia Kitabu (cha Qur'ani). Basi wale tulio wapa Kitabu (cha Biblia) wataiamini (Qur'ani), na miongoni mwa hawa (washirikina) wapo watakao iamini. Na hawazikatai Ishara zetu isipo kuwa makafiri.
Wewe Mashaxizo, unasema Biblia imechakachuliwa halafu ukatolea mfano ilianza kuchakachuliwa kipindi cha Wamakabayo ndio maana umeleta andiko kutoka kwa Wamakabayo, kipindi hicho cha Wamakabayo ilikuwa hata kabla ya Yesu hajaja, Uislamu haupo kwa maana Muhammad wala Quran havipo, hapa chini nitakuwekea aya zinazowataka nyie mtuulize sisi wenye kitabu, Je inamaana Mungu wenu alikuwa hajielewi wakati akiwaagiza hivyo!? wakati anajua tayari imeshachakachuliwa kipindi hicho
Quran 10:94
Na ikiwa unayo shaka katika tuliyo kuteremshia, basi waulize wasomao Kitabu kabla yako. Kwa yakini imekwisha kujia Haki kutoka kwa Mola wako Mlezi. Basi usiwe miongoni mwa wenye shaka.
Quran 21:7 Na kabla yako hatukuwatuma ila watu wanaume tulio wapa wahyi (ufunuo). Basi waulizeni wenye ilimu ikiwa nyinyi hamjui.
Quran 16:43 Nasi hatukuwatuma kabla yako ila watu wanaume tulio wapa Wahyi (Ufunuo). Basi waulizeni wenye ukumbusho kama nyinyi hamjui
Hizo aya zote zinaelezea mmeagizwa mtuulize sisi kama nyie hamjui, Sasa kama Mungu wako alijua yamechakachuliwa kitambo, kwanini awaambie hivyo!?
Hapo juu mnaambiwa muwaulize watu wa kitabu, halafu mnaelekezwa pia hapa chini namna hii
Quran 10:64
Wao wana bishara njema katika maisha ya dunia na katika Akhera. Hapana mabadiliko katika maneno ya Mwenyezi Mungu. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
Quran 6:115 Na yametimia maneno ya Mola Mlezi wako kwa kweli na uadilifu. Hapana awezaye kuyabadilisha maneno yake. Na Yeye ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua.
Nijibu tuendelee...