Majambazi wapora kwenye benki ya Barclays tawi la Kinondoni TX

Majambazi wapora kwenye benki ya Barclays tawi la Kinondoni TX

mrangi

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2014
Posts
88,759
Reaction score
123,368
baclays kinondoni branch wazee wa kazi au wazee wa ngwasuma au majambazi.inasemekana wamechukua hela mule bank....nilipigiwa sm nkaambiwa sahvv napita naona watu kibao wa jf...naona huu ni msimu wa majambazi kutafuta hela ya pasaka sjui

-------------------------

Watu wasiojulikana wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wamevamia benki ya Barclays tawi la Kinondoni na kupora kiasi kikubwa cha fedha ambazo idadi yake haijajulikana mara moja.

Tukio hilo limetokea muda huu saa nne , katika tawi la benki hiyo iliyopo Kinondoni eneo la Bakwata likihusisha watu watatu waliokuwa na pikipiki mmoja wao akiwa na bastola.
PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Siku hizi kuiba bank ni rahisi kuliko kukwapua mkoba au kuku wa mtu mtaani
 
Benki za tz zinaibiwa mchana kweupe, wateja wameponea kweli? Hii lazima utasikia pikipiki zimehusika.
 
Asubuhi hii Majambazi watatu waliokua na pikipiki moja yamempora mama mmoja aliekua anaweka hela bank ya barclays maeneo Kinondoni TX, akiwa amebeba kwenye mfuko bila tabu waliomba "mzigo" wao, hakuna aliejeruhiwa na hawakutumia bastola
Boxer hizi hatari....
 
baclays kinondoni branch wazee wa kazi au wazee wa ngwasuma au majambazi.inasemekana wamechukua hela mule bank....nilipigiwa sm nkaambiwa sahvv napita naona watu kibao wa jf...naona huu ni msimu wa majambazi kutafuta hela ya pasaka sjui


Pasaka!!!!!? si kweli ni uchaguzi 2015
 
Hapo, lazima boxer bm 150 imehusika.......
 
Watu wanaosadikiwa kuwa majambazi wamevamia bank ya backlays tawi la kinondoni na kupora kiasi kikubwa cha fedha.
 
Kama hawajauwa au kujeruhi watu basi Pasaka kwa hao majambazi wataila vizuri sana
 
Back
Top Bottom