Maji nayo yakatika mkoani Texas, Marekani, wananchi Wachota barafu kwa matumizi

Maji nayo yakatika mkoani Texas, Marekani, wananchi Wachota barafu kwa matumizi

Jamaa hapo anafikiri ni sababu kama za akina DAWASCO.

Mito yetu inapokauka kutokana na ukame kukithiri umeme hukatika.

Na huko Texas pia hali ya hewa imesababisha kukatika kwa maji na umeme.

Yote haya ni mabadiliko ya tabia nchi.

Lakini huwa kuna uzembe pia, iwe hapa kwetu au huko mkoani Texas, Marekani.

Bwana Bill Gates, mwanaharakati wa kimazingira wa mabadiliko ya tabia, nchi amepinga vikali visingizio vya hali mbaya ya hewa mkoani Texas akidai kwamba mikoa kama Iowa mbapo kuna baridi zaidi na kwa muda mrefu umeme wala maji havikatiki.

Bwana Gates alihoji ni kwa nini miundombinu ya huduma hizo, kama vile mapangaboi ya kufua imeme, haigandi theluji mkoani Iowa.
 
Kwameh,

Texas kwa kawaida huwa hawapati barafu nyingi, kwa hiyo hawana uzoefu wa ku-deal na barafu kama majimbo ya Iowa, New York, etc ambayo hupata barafu nyingi kila mwaka.

Huenda barafu waliyopata Texas ingeanguka New York au Iowa, usingesikia majimbo hayo yakishindwa ku-deal na hali hiyo kama ilivyotokea Texas.

Kwa uchunguzi wangu nimebaini kwamba majimbo ya Marekani yanatofautiana kwa changamoto za hali ya hewa. Yako majimbo yanayopata barafu mara kwa mara. Majimbo hayo huwa na uzoefu wa ku-deal na barafu. Yako majimbo yenye kupata mvua zinazoambatana na upepo mkali. Majimbo hayo yana uzoefu wa ku-deal na hali hiyo.

Sokomoko na maafa hutokea pale ambapo jimbo fulani limekabiliwa na hali ya hewa ambayo hawana uzoefu nayo, kwa mfano Texas walivyopata barafu nyingi kupita kiasi. Vilevile usije ukashangaa kusikia kwamba Texas hawana vifaa vya kutosha vya kusafisha barafu kwenye mabarabara. Lakini ukienda jimbo kama New York wao huwa wana vifaa vya ku-deal na barafu kwasababu wana kawaida ya kupata barafu nyingi kila mwaka.
 
Kuna habari nyingi kuhusu ulaya na america haziripotiwi hasa zinazohusu umaskini na hali mbaya kimaisha.
Hata ingekuwa haziripotiwi watu wa USA ni mara 100 % Kwa maisha Bora zaidi yetu hivo ndio ilivyo
 
Niliambiwa kuna tofauti kati ya barafu(ice) na theluji(snow)
 
Hata ingekuwa haziripotiwi watu wa USA ni mara 100 % Kwa maisha Bora zaidi yetu hivo ndio ilivyo
U.S. waliopata uhuru wao miaka 245 iliyopita wana tofauti kubwa na Tanzania ya miaka 60. Halafu Kwenye ubora na udhaifu upo, kuusema sio dhambi
 
Niliambiwa kuna tofauti kati ya barafu(ice) na theluji(snow)

..Ice huwa inaganda, na ina utelezi mkali sana.

..Snow iko kama barafu iliyopondwa-pondwa, ni laini ukiishika, na haina utelezi ukiikanyaga.

..barafu / ice ndiyo husababisha ajali nyingi kwa mfano watu kuteleza, au magari kuserereka na kupinduka.

..Tatizo lingine huko Texas unaweza kukuta madereva wake hawawezi kuendesha kwenye snow.

..Wakati huohuo dereva wa New York au Iowa hali ya hewa iliyotokea Texas inaweza isimpe shida barabarani.
 
U.S. waliopata uhuru wao miaka 245 iliyopita wana tofauti kubwa na Tanzania ya miaka 60. Halafu Kwenye ubora na udhaifu upo, kuusema sio dhambi
Nafikiri kupata Uhuru mapema zaidi sio tatizo kuna nchi hazijawahi kutawaliwa na uchumi wao sio mzuri. Pia kuna nchi zilizopata Uhuru miaka ya kulingana na za kwetu wapo mbali kiuchumi kitu kukibwa ni uongozi uliopo Madaraka nchi nchi kama za china , India , Malaysia , Singapore etc uchumi wake umekuwa Kwa kasi ya hatari
 
U.S. waliopata uhuru wao miaka 245 iliyopita wana tofauti kubwa na Tanzania ya miaka 60. Halafu Kwenye ubora na udhaifu upo, kuusema sio dhambi

Malaysia walipata uhuru 1963.

Singapore walipata uhuru 1965 baada ya kujitenga na Malaysia.

Nchi hizo zimepata maendeleo makubwa kuliko Tanganyika iliyopata uhuru 1961.
 
Nafikiri kupata Uhuru mapema zaidi sio tatizo kuna nchi hazijawahi kutawaliwa na uchumi wao sio mzuri. Pia kuna nchi zilizopata Uhuru miaka ya kulingana na za kwetu wapo mbali kiuchumi kitu kukibwa ni uongozi uliopo Madaraka nchi nchi kama za china , India , Malaysia , Singapore etc uchumi wake umekuwa Kwa kasi ya hatari

Umri wa taifa haukwepeki tunapoangalia maendeleo yake japo kuna vigezo vingine vinavyoweza kurudisha nyuma au kuspeedup maendeleo pia.

Tunapolinganisha tunatakiwa kulinganisha vitu vinavyofanana katika nyanja mbalimbali
 
Hata bila mito yenu kukauka umeme huwa unakatika tu, labda kama wewe ni mgeni bongo.
Mito yetu inapokauka kutokana na ukame kukithiri umeme hukatika...
 
Umri wa taifa haukwepeki tunapoangalia maendeleo yake japo kuna vigezo vingine vinavyoweza kurudisha nyuma au kuspeedup maendeleo pia
Vietnam iliyochakazwa na USA Kwa miaka 20 je ikaachwa imesambaratishwa mwaka 1975 ndio Vita vilikwisha. Na je South Africa iliyopata Uhuru 1994. Na je Ethiopia, Nepal ambazo hazijawahi kutawaliwa je. Nafikiri maendeleo ni kitu complicated Sana
 
Kwanini hukuandika"Katika HALMASHAURI kubwa mkoani humo kama HOUSTON,badala yake umeandika(katika majiji makubwa)ukilitolea mfano Houston wakati hilo jiji lipo MKOANI?
 
Mwaka 1960 Korea ya kusini, Vietnam na nchi nyingine za Asia ya Kusini Mashariki zilikuwa hazina tofauti kimaendeleo na Tanzania na nchi nyingine nyingi za barani Africa.
Umri wa taifa haukwepeki tunapoangalia maendeleo yake japo kuna vigezo vingine vinavyoweza kurudisha nyuma au kuspeedup maendeleo pia
 
Vietnam iliyochakazwa na USA Kwa miaka 20 je ikaachwa imesambaratishwa mwaka 1975 ndio Vita vilikwisha. Na je South Africa iliyopata Uhuru 1994. Na je Ethiopia, Nepal ambazo hazijawahi kutawaliwa je. Nafikiri maendeleo ni kitu complicated Sana
Tunapolinganisha tunatakiwa kulinganisha vitu vinavyofanana katika nyanja mbalimbali na umri wa taifa ni mojawapo
Ukifanya utafiti utapata majibu ya ulichoandika
 
Tunapolinganisha tunatakiwa kulinganisha vitu vinavyofanana katika nyanja mbalimbali na umri wa taifa ni mojawapo
Nadhani Tanzania tuna hali nzuri kuliko Haiti iliyopata uhuru 1804 hivyo tunapaswa kutembea kifua mbele.
 
Mwaka 1960 Korea ya kusini, Vietnam na nchi nyingine za Asia ya Kusini Mashariki zilikuwa hazina tofauti kimaendeleo na Tanzania na nchi nyingine nyingi za barani Africa.
Uwoga wetu ndio umetuweka hapo, hivi tungeshikilia msimamo kama wa Korea kusini na China si tungekua sawa eee
 
Kwenye kuchambua hatua za maendeleo ya nchi uwoga sio factor.

Umefanikiwa hata kumaliza kidato cha nne?
Uwoga wetu ndio umetuweka hapo, hivi tungeshikilia msimamo kama wa Korea kusini na China si tungekua sawa eee
 
Back
Top Bottom