Maji ni huduma ambayo Serikali inafeli vibaya mno, uhaba na mgao karibu kila mkoa japo mabilioni yanatumika. Rais Samia anashindwa wapi?

Maji ni huduma ambayo Serikali inafeli vibaya mno, uhaba na mgao karibu kila mkoa japo mabilioni yanatumika. Rais Samia anashindwa wapi?

Nadhani kuna tozo pia ikiwa unavuna maji ya mvua utafikiri yametoka serikalini 🤣🤣🤣🤣
Hawa wangekuwepo kwenye ile vita ya Maji Maji wangewatoza Wazee wetu kwa kutumia jina la Maji tu.😆😂
 
Hawa wangekuwepo kwenye ile vita ya Maji Maji wangewatoza Wazee wetu kwa kutumia jina la Maji tu.😆😂
Aaah, machifu wetu hawakuwa na V-8, kwa hiyo enzi hizo ukiwapa kuku mmoja ni tozo tosha kabisa!
 
Pale wao Idara za Maji zinaposhindwa jukumu lao sisi ndio tufe kwa kiu? au tusioge tuwe kama Wachawi?

Kuna kipindi nilikuwa naishi Mkoa fulani Maji yalikuwa hayatoki kabisa na bili wanakuletea tumenyanyasika sana kwenye Nchi yetu.
 
Nilitegemea kwamba serikali inayosema inapigana na kupambana sana kuhudumia watu wake ingefanikiwa sana katika suala la kutoa maji kwa watu wake. Lakini inasikitisha sana kwamba hadi leo Tanzania inafeli sana katika kutoa huduma hii kwa wananchi. Na kinachosikitisha hata zaidi ni kwamba hii ni huduma muhimu sana hasa kwa wananwake na watoto, na ina athari katika mambo mengi.

Huduma mbovu za maji zina athari nyingi sana, kwa mfano;
  • Wanawake wanapoteze muda mwingi katika kufuata maji
  • Matatizo ya kijamii kama kubaka watoto na wanawake wanapokuwa wakifuata maji
  • Hatari za afya za wananchi kutokana na kutokunywa maji safi na kutokuwa na usafi wa mwili
  • Ugomvi katika familia na jamii kutokana na uhaba wa maji
Matarajio yangu yalikuwa kwamba kuwa na raisi mwanamke kungekuwa ni chachu ya tatizo hili kukomeshwa nchini, lakini hali bado ni mbaya leo kama ilivyokuwa jana. Tunachoona ni matumizi makubwa ya fedha kwenye miradi ya maji bila kuona matukio ya miradi huo. Ufisadi umezidi mno kwenye miradi ya maji na hatusikii watu kuchukuliwa hatua.

Jambo la aibu hata zaidi ni kwamba hata sehemu zenye rasilimali ya maji kubwa sana zinakuwa na matatizo ya maji. Mikoa kama Mbeya, KIlimanjaro, Iringa, Morogoro, nk, yenye mito na vyanzo vya maji tele kwa nini iwe na matatizo ya maji?

Kichekesho kwa mfano, ni mwanzoni mwa mwaka huu nilitembelea mji wa Tukuyu huko Mbeya, na kukuta kuna uhaba mkubwa wa maji, ambapo sehemu za mji huu zina mgawo wa maji wa siku mbili au tatu kwa wiki. Niliuliza viongozi wa mji, chanzo cha maji katika mji huu ni wapi? Nikaambiwa ni pembezoni mwa Mlima Rungwe. Nikasema ikiwa chanzo ni huko mlimani, ina maana mnaweza kugawa maji kwa kutumia gravity tu, na kinachihitajika ni mambomba na matenki makubwa labda matatu tu. Sasa kwa nini mji una shida ya maji muda wote huu ikiwa gharama za kusambaza maji ya gravity ni za nchini kiasi hiki? Hakuna aliyenipa jibu la kitaalamu zaidi ya majibu ya kitoto ya kisiasa.

Nina uhakika mikoa kama KIlimanjaro, Arusha, ziko katika mazingira kama haya ya kupata maji kwa gravity lakini hakuna chochote kinachoendelea.

Mama Samia, watu wako wanashindwa wapi katika hili? Huenda ni jambo linahitaji liangaliwe upya na sio kutumia njia za zamani ambazo zimefeli kwa muda mrefu sana. Tunaweza kuelewa matatizo ya umeme na kuyavumilia, lakini sio maji. Ikibidi dedicate tozo za mwaka mzima ziende kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za maji. Kama raisi wa kwanza Tanzania mwananke, ukimaliza muda wako bila kuhakikisha access ya maji nchini ni 100% nitakushangaa sana. Utakuwa umewaangusha na hata kuwasaliti mno wanawake wenzio.

Reference: Mgawo wa maji watikisa mijini, vijijini
Tena Bora na Rais Samia kafanya uwekezaji mkubwa kiasi kwenye hii sekta maana waliopita walipuuza kabisa sekta ya Maji na kilimo..

Mwaka ukiopita mvua ilikuwa kidogo ni automatically maji itakuwa tatizo maana hata visima vyetu vya majumbani maji yamekauka au kupungua Sana..

Mwisho tatizo la maji haliwezi kutatuliwa overnight bali kwa uwekezaji ambao utachukua mda fulani..

Kwa sasa Nina matumaini maana naona serikali inajaribu kuchukua hatua za kuwa na suluhisho la kudumu na kusema ukweli miradi ya maji Kwa sasa ni countless si Vijijini si mjini..

Kwa ishu ya Maji nadhani Rais Samia ataimaliza kwa sababu ni moja ya kipaombele chake na anatakiwa asifanye mchezo maana huko ndiko kuna wanawake wenzie ambao wanaweza mhakikishia Kura kama akiwatua ndio kichwani..
 
Nilitegemea kwamba serikali inayosema inapigana na kupambana sana kuhudumia watu wake ingefanikiwa sana katika suala la kutoa maji kwa watu wake. Lakini inasikitisha sana kwamba hadi leo Tanzania inafeli sana katika kutoa huduma hii kwa wananchi. Na kinachosikitisha hata zaidi ni kwamba hii ni huduma muhimu sana hasa kwa wananwake na watoto, na ina athari katika mambo mengi.

Huduma mbovu za maji zina athari nyingi sana, kwa mfano;
  • Wanawake wanapoteze muda mwingi katika kufuata maji
  • Matatizo ya kijamii kama kubaka watoto na wanawake wanapokuwa wakifuata maji
  • Hatari za afya za wananchi kutokana na kutokunywa maji safi na kutokuwa na usafi wa mwili
  • Ugomvi katika familia na jamii kutokana na uhaba wa maji
Matarajio yangu yalikuwa kwamba kuwa na raisi mwanamke kungekuwa ni chachu ya tatizo hili kukomeshwa nchini, lakini hali bado ni mbaya leo kama ilivyokuwa jana. Tunachoona ni matumizi makubwa ya fedha kwenye miradi ya maji bila kuona matukio ya miradi huo. Ufisadi umezidi mno kwenye miradi ya maji na hatusikii watu kuchukuliwa hatua.

Jambo la aibu hata zaidi ni kwamba hata sehemu zenye rasilimali ya maji kubwa sana zinakuwa na matatizo ya maji. Mikoa kama Mbeya, KIlimanjaro, Iringa, Morogoro, nk, yenye mito na vyanzo vya maji tele kwa nini iwe na matatizo ya maji?

Kichekesho kwa mfano, ni mwanzoni mwa mwaka huu nilitembelea mji wa Tukuyu huko Mbeya, na kukuta kuna uhaba mkubwa wa maji, ambapo sehemu za mji huu zina mgawo wa maji wa siku mbili au tatu kwa wiki. Niliuliza viongozi wa mji, chanzo cha maji katika mji huu ni wapi? Nikaambiwa ni pembezoni mwa Mlima Rungwe. Nikasema ikiwa chanzo ni huko mlimani, ina maana mnaweza kugawa maji kwa kutumia gravity tu, na kinachihitajika ni mambomba na matenki makubwa labda matatu tu. Sasa kwa nini mji una shida ya maji muda wote huu ikiwa gharama za kusambaza maji ya gravity ni za nchini kiasi hiki? Hakuna aliyenipa jibu la kitaalamu zaidi ya majibu ya kitoto ya kisiasa.

Nina uhakika mikoa kama KIlimanjaro, Arusha, ziko katika mazingira kama haya ya kupata maji kwa gravity lakini hakuna chochote kinachoendelea.

Mama Samia, watu wako wanashindwa wapi katika hili? Huenda ni jambo linahitaji liangaliwe upya na sio kutumia njia za zamani ambazo zimefeli kwa muda mrefu sana. Tunaweza kuelewa matatizo ya umeme na kuyavumilia, lakini sio maji. Ikibidi dedicate tozo za mwaka mzima ziende kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za maji. Kama raisi wa kwanza Tanzania mwananke, ukimaliza muda wako bila kuhakikisha access ya maji nchini ni 100% nitakushangaa sana. Utakuwa umewaangusha na hata kuwasaliti mno wanawake wenzio.

Reference: Mgawo wa maji watikisa mijini, vijijini
Samia hajawahi kuweza sababu anarembua rembua tu badala ya kuwajibisha watu...
 
Sisi upinzani tunasema.
UKIONA ADUI YAKO ANAFANYA MAKOSA YA KIJINGA.
USIMSTUE
 
Nilitegemea kwamba serikali inayosema inapigana na kupambana sana kuhudumia watu wake ingefanikiwa sana katika suala la kutoa maji kwa watu wake. Lakini inasikitisha sana kwamba hadi leo Tanzania inafeli sana katika kutoa huduma hii kwa wananchi. Na kinachosikitisha hata zaidi ni kwamba hii ni huduma muhimu sana hasa kwa wananwake na watoto, na ina athari katika mambo mengi.

Huduma mbovu za maji zina athari nyingi sana, kwa mfano;
  • Wanawake wanapoteze muda mwingi katika kufuata maji
  • Matatizo ya kijamii kama kubaka watoto na wanawake wanapokuwa wakifuata maji
  • Hatari za afya za wananchi kutokana na kutokunywa maji safi na kutokuwa na usafi wa mwili
  • Ugomvi katika familia na jamii kutokana na uhaba wa maji
Matarajio yangu yalikuwa kwamba kuwa na raisi mwanamke kungekuwa ni chachu ya tatizo hili kukomeshwa nchini, lakini hali bado ni mbaya leo kama ilivyokuwa jana. Tunachoona ni matumizi makubwa ya fedha kwenye miradi ya maji bila kuona matukio ya miradi huo. Ufisadi umezidi mno kwenye miradi ya maji na hatusikii watu kuchukuliwa hatua.

Jambo la aibu hata zaidi ni kwamba hata sehemu zenye rasilimali ya maji kubwa sana zinakuwa na matatizo ya maji. Mikoa kama Mbeya, KIlimanjaro, Iringa, Morogoro, nk, yenye mito na vyanzo vya maji tele kwa nini iwe na matatizo ya maji?

Kichekesho kwa mfano, ni mwanzoni mwa mwaka huu nilitembelea mji wa Tukuyu huko Mbeya, na kukuta kuna uhaba mkubwa wa maji, ambapo sehemu za mji huu zina mgawo wa maji wa siku mbili au tatu kwa wiki. Niliuliza viongozi wa mji, chanzo cha maji katika mji huu ni wapi? Nikaambiwa ni pembezoni mwa Mlima Rungwe. Nikasema ikiwa chanzo ni huko mlimani, ina maana mnaweza kugawa maji kwa kutumia gravity tu, na kinachihitajika ni mambomba na matenki makubwa labda matatu tu. Sasa kwa nini mji una shida ya maji muda wote huu ikiwa gharama za kusambaza maji ya gravity ni za nchini kiasi hiki? Hakuna aliyenipa jibu la kitaalamu zaidi ya majibu ya kitoto ya kisiasa.

Nina uhakika mikoa kama KIlimanjaro, Arusha, ziko katika mazingira kama haya ya kupata maji kwa gravity lakini hakuna chochote kinachoendelea.

Mama Samia, watu wako wanashindwa wapi katika hili? Huenda ni jambo linahitaji liangaliwe upya na sio kutumia njia za zamani ambazo zimefeli kwa muda mrefu sana. Tunaweza kuelewa matatizo ya umeme na kuyavumilia, lakini sio maji. Ikibidi dedicate tozo za mwaka mzima ziende kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za maji. Kama raisi wa kwanza Tanzania mwananke, ukimaliza muda wako bila kuhakikisha access ya maji nchini ni 100% nitakushangaa sana. Utakuwa umewaangusha na hata kuwasaliti mno wanawake wenzio.

Reference: Mgawo wa maji watikisa mijini, vijijini
KWANI RIPOTI YA KIKOSI KAZI HAIJATOA MAPENDEKEZO JUU YA MAJI?
 
Oyaaa, tupeni maji, hatujaoga wiki mbili sasa na tunafanya kazi maji machafu! Kula urefu wa kamba yako sio kwa watu wa maji machafu.
 
Back
Top Bottom