Majibu ya CCM Mdahalo wa Odemba: Tunasikitishwa na jinsi alivyoupotosha umma, tumeshangazwa na machozi yake!

Majibu ya CCM Mdahalo wa Odemba: Tunasikitishwa na jinsi alivyoupotosha umma, tumeshangazwa na machozi yake!

Huu ufafanuzi wa CCM na taarifa zilizosambaa umenishtua sana! Kwanza, sijui kama wengine ilikuwa hivi yaani, unamwitaje Katibu Mkuu wa Chama kwa mssage fupi ashiriki mdahalo? Pili, huu mdahalo ulikuwa wa taasisi dhidi ya taasisi yaani StarTv na vyama vya siasa au na mtu (Odemba). Jamaa kashindwa kuonyesha professionalism kabisa.🙏🙏🙏
Taasisi hazifanyia mdahalo, watu ndio hufanya midahalo.
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinapenda kutoa taarifa kwa umma kuhusu kutoshiriki kwa Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kwenye mdahalo ulioandaliwa na Kituo cha Televisheni cha Star Tv, na kuratibiwa na Ndugu Edwin Odemba tarehe 31 Agosti, 2024.

CCM inautaarifu umma kuwa Katibu Mkuu hakukimbia wala hakudharau mdahalo huo. Balozi Nchimbi alifanya kila jitihada za mawasiliano na muaandaji na tunasikitishwa na jinsi alivyoupotosha umma.

Tarehe 10 Agosti 2024 mtangazaji wa Kituo cha Televisheni, Star Tv, Ndugu Edwin Odemba alimtafuta Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu (sms) akimuomba Katibu Mkuu ashiriki mdahalo huo wa viongozi wa vyama vya siasa uliopangwa kufanyika Jumamosi, tarehe 31 Agosti 2024.

Katibu Mkuu alimjulisha kuwa masuala ya vyombo vya habari yanaratibiwa na Katibu wa Halmshauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Amos Gabriel Makalla hivyo awasiliane naye na akampa namba ya simu ya mkononi ya Ndugu Makalla.

Kwa sababu ambazo Odemba anaweza kuzieleza mwenyewe, katika kipindi cha takriban wiki tatu, hakufanya mawasiliano au kumtafuta Ndugu Makalla kama alivyoelekezwa na kushauriwa na Katibu Mkuu Balozi Nchimbi.

Baada ya kuhisi kwamba nafasi ya Katibu Mkuu inaweza kuwa ngumu kupatikana kutokana na majukumu yake ya kazi za chama, Ndugu Odemba alimtafuta tena Balozi Nchimbi akiomba amuandae mwakilishi huku matangazo ya mdahalo huo yakiendelea kumtaja Katibu Mkuu wa CCM kuwa ndiye atakayeshiriki. Badala yake Katibu Mkuu alimwelekeza Ndugu Odemba kutofanya lolote kabla ya kupata mawasiliano na Sekretarieti ya Chama.

Kimsingi Ndugu Odemba alitaka wananchi wadanganywe kuwa CCM kupitia kwa Katibu Mkuu ilikuwa imethibitisha kushiriki katika mdahalo huo jambo ambalo si sahihi.

Katika mazingira ya kustaajabisha tumeshangazwa na machozi ya Ndugu Odemba aliyotoa jana akielekeza lawama kwa CCM na kwa Katibu Mkuu wakati alijua bayana kwamba alikuwa hajapata uthibitisho wowote wa CCM kushiriki ikiwa ni pamoja na ukweli kwamba yeye mwenyewe alishajua kwamba alikuwa akiendelea kutangaza kuhusu mdahalo huo kama "promo" pasipo kupata ridhaa ya CCM.

Katibu Mkuu wa CCM ndiye Mwenyekiti wa Sekretarieti na siku nzima ya jana ambayo ndiyo siku Odemba alipanga kufanyika kwa mdahalo huo, kulikuwa na vikao vya maandalizi ya Kamati Kuu Maalum ambayo inafanyika leo tarehe 01 Septemba 2024, jambo ambalo kwa namna yoyote Katibu Mkuu asingeweza kuwapo katika mdahalo huo hata kama angekuwa amethibitisha awali.

Kushiriki kwenye mdahalo kunahitaji mashauriano na maafikiano kati ya waandaji na waalikwa.

Tunaweza kutamka bayana na kwa uhakika kwamba Katibu Mkuu hakuwa ametoa uthibitisho wa kuhudhuria mdahalo huo. Hakukuwa na makubaliano yoyote rasmi ya yeye au mwakilishi wake kuhudhuria katika shughuli hiyo. Mwisho, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Nchimbi yupo tayari kwa midahalo, majadiliano na makongamano yanayolenga kujenga umoja wa kitaifa na maridhiano ya kisiasa kadiri ya taratibu zilizopo na ratiba yake ya kazi inavyoruhusu.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

View attachment 3084263

View attachment 3084264

Pia soma
- Kuelekea 2025 - Mdahalo wa Makatibu Wakuu wa Vyama vya Siasa: Nchimbi kaingia mitini, wengine wagoma kushiriki!
Karibu mkuu wa nini?

Tunamtaka Mwenyekiti wenu taifa Bi Samia Suluhu Hassan aache kujificha na badala yeye ndiye aje kwenye midahalo...

CCM mlivyo dhaifu na waoga kwa sababu ya tabia na mienendo yenu mibaya, haitashangaza akakataa na kukiambia kuzungumza na wananchi kwa dhana ileile ya "ana majukumu mengi...."

Lakini ukweli ni kuwa CCM kwenye midahalo huru na ya wazi hawawezi kujitokeza na sababu ni ukweli kuwa maswali magumu ya kujibu mengi na hawana majibu sahihi ya kuwapa wananchi...!!
 
Karibu mkuu wa nini?

Tunamtaka Mwenyekiti wenu taifa Bi Samia Suluhu Hassan aache kujificha na badala yeye ndiye aje kwenye midahalo...

CCM mlivyo dhaifu na waoga kwa sababu ya tabia na mienendo yenu mibaya, haitashangaza akakataa na kukiambia kuzungumza na wananchi kwa dhana ileile ya "ana majukumu mengi...."

Lakini ukweli ni kuwa CCM kwenye midahalo huru na ya wazi hawawezi kujitokeza na sababu ni ukweli kuwa maswali magumu ya kujibu mengi na hawana majibu sahihi ya kuwapa wananchi...!!
Juzi Faustin Ndugulile kashinda na kuwa Mkurugenzi wa WHO Afrika. Huenda wewe unatatizo kichwani mwako.
Vile vile Tulia ni Rais wa Mabunge yote duniani. Ina maana wabunge wote duniani wanazidiwa akili na bwana The Palm Beach 🤣 🤣 🤣 🤣
 
Huyo Nchimbi na sisiem hata wakipewa wao nafasi ya kupanga ratiba ya mdahalo bado wataukimbia tu.

Hivi unaenda kwenye mdahalo kuwakilisha kambi ya mashetani yenye kila aina ya uovu, unategemea uongee nini zaidi ya kujiaibisha? Wasitufanye sie maboya, Nchimbi kafanya calculations kaona anaenda kujivua nguo mwenyewe akala kona, over.
Hakika...

Hata mimi ningeshangaa kama CCM wangehudhuria.

By the way:
Mimi nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa Odemba na StarTV kwa ujumla ni unprofessional, wajinga na wapumbavu kiasi hicho warushe hewani kupitia vyombo vya habari mbalimbali tangazo ambalo linaitaja CCM au mtu fulani kuwa atashiriki kwenye tukio fulani bila wao kuruhusu na kuthibitisha ushiriki wao...!
!

Huu ni uongo na ulaghai uleule wa siku zote wa CCM ambao tunaujua.....

CCM mambo ya wazi na ya haki hawayawezi. CCM imezoea maisha ya uongo, wizi, udanganyifu, utekaji, kutesa na kumwaga damu za watu wasio na hatia iwe ni serikalini ama ndani ya chama chao wenyewe...!

Kuwaamini CCM kwa chochote wasemalo, lazima uwe na akili nusu kisoda...!
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinapenda kutoa taarifa kwa umma kuhusu kutoshiriki kwa Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kwenye mdahalo ulioandaliwa na Kituo cha Televisheni cha Star Tv, na kuratibiwa na Ndugu Edwin Odemba tarehe 31 Agosti, 2024.

CCM inautaarifu umma kuwa Katibu Mkuu hakukimbia wala hakudharau mdahalo huo. Balozi Nchimbi alifanya kila jitihada za mawasiliano na muaandaji na tunasikitishwa na jinsi alivyoupotosha umma.

Tarehe 10 Agosti 2024 mtangazaji wa Kituo cha Televisheni, Star Tv, Ndugu Edwin Odemba alimtafuta Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu (sms) akimuomba Katibu Mkuu ashiriki mdahalo huo wa viongozi wa vyama vya siasa uliopangwa kufanyika Jumamosi, tarehe 31 Agosti 2024.

Katibu Mkuu alimjulisha kuwa masuala ya vyombo vya habari yanaratibiwa na Katibu wa Halmshauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Amos Gabriel Makalla hivyo awasiliane naye na akampa namba ya simu ya mkononi ya Ndugu Makalla.

Kwa sababu ambazo Odemba anaweza kuzieleza mwenyewe, katika kipindi cha takriban wiki tatu, hakufanya mawasiliano au kumtafuta Ndugu Makalla kama alivyoelekezwa na kushauriwa na Katibu Mkuu Balozi Nchimbi.

Baada ya kuhisi kwamba nafasi ya Katibu Mkuu inaweza kuwa ngumu kupatikana kutokana na majukumu yake ya kazi za chama, Ndugu Odemba alimtafuta tena Balozi Nchimbi akiomba amuandae mwakilishi huku matangazo ya mdahalo huo yakiendelea kumtaja Katibu Mkuu wa CCM kuwa ndiye atakayeshiriki. Badala yake Katibu Mkuu alimwelekeza Ndugu Odemba kutofanya lolote kabla ya kupata mawasiliano na Sekretarieti ya Chama.

Kimsingi Ndugu Odemba alitaka wananchi wadanganywe kuwa CCM kupitia kwa Katibu Mkuu ilikuwa imethibitisha kushiriki katika mdahalo huo jambo ambalo si sahihi.

Katika mazingira ya kustaajabisha tumeshangazwa na machozi ya Ndugu Odemba aliyotoa jana akielekeza lawama kwa CCM na kwa Katibu Mkuu wakati alijua bayana kwamba alikuwa hajapata uthibitisho wowote wa CCM kushiriki ikiwa ni pamoja na ukweli kwamba yeye mwenyewe alishajua kwamba alikuwa akiendelea kutangaza kuhusu mdahalo huo kama "promo" pasipo kupata ridhaa ya CCM.

Katibu Mkuu wa CCM ndiye Mwenyekiti wa Sekretarieti na siku nzima ya jana ambayo ndiyo siku Odemba alipanga kufanyika kwa mdahalo huo, kulikuwa na vikao vya maandalizi ya Kamati Kuu Maalum ambayo inafanyika leo tarehe 01 Septemba 2024, jambo ambalo kwa namna yoyote Katibu Mkuu asingeweza kuwapo katika mdahalo huo hata kama angekuwa amethibitisha awali.

Kushiriki kwenye mdahalo kunahitaji mashauriano na maafikiano kati ya waandaji na waalikwa.

Tunaweza kutamka bayana na kwa uhakika kwamba Katibu Mkuu hakuwa ametoa uthibitisho wa kuhudhuria mdahalo huo. Hakukuwa na makubaliano yoyote rasmi ya yeye au mwakilishi wake kuhudhuria katika shughuli hiyo. Mwisho, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Nchimbi yupo tayari kwa midahalo, majadiliano na makongamano yanayolenga kujenga umoja wa kitaifa na maridhiano ya kisiasa kadiri ya taratibu zilizopo na ratiba yake ya kazi inavyoruhusu.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

View attachment 3084263

View attachment 3084264

Pia soma
- Kuelekea 2025 - Mdahalo wa Makatibu Wakuu wa Vyama vya Siasa: Nchimbi kaingia mitini, wengine wagoma kushiriki!
Chama cha hila, chama chenye dharau, chama kisicho na aibu kimesha tiona wote ni wajinga. Wame amua kucheza na lugha.
Asubuhi walisema Katibu wao mkuu hawezi kuongea na watu wasio na PhD. Sasa new story. Its fine, kuna siku Mungu wa mbinguni ata weka kila kitu wazi..
 
msacky ana mikono michafu anakuwaje msaidizi wa katibu mkuu??? au ndege wafananao huruka pamoja??
Je, unaweza kuthibitisha hilo? Au ni hisia zako chafu?
 
Chama cha hila, chama chenye dharau, chama kisicho na aibu kimesha tiona wote ni wajinga. Wame amua kucheza na lugha.
Asubuhi walisema Katibu wao mkuu hawezi kuongea na watu wasio na PhD. Sasa new story. Its fine, kuna siku Mungu wa mbinguni ata weka kila kitu wazi..
Hao waliosema hivyo asubuhi ni akina nani?
 
Hakijaharibika kitu, ngoma ipangwe upya tena mapema iwezekanavyo kabla haijapoa.
Schedule ya SG iko very tight hadi Novemba, 2025 baada ya uzinduzi wa Bunge jipya. Waandaji wawasiliane na Idara ya Itikadi, Habari, na Uenezi kuangalia uwezekano wa SG kushiriki mdahalo baada ya kipindi hiko.
 
Makonda angeenda!!

Hivi ccm chama changu hao wanachama tunaowalipa mapesa ya mshahara kama hawana uwezo wa kukitetea chama kwenye midahalo tunawalipa wa nini!!?

Hadi hasira aiseh!!
 
Back
Top Bottom