Hahahaha! After Osama Bin Laden assasination.. you can count on another Obama term... huyo Perry anafanya rehearsal .... mkuu nasubiri kwa hamu US elections 2012... endelea kuwafagilia Repugs wako...
That those before him did not do a good job is not a defense. They say two wrongs do not make a right.
Ukichukua urais kutoka kwa dikteta, ukaendeleza udikteta eti kwa sababu aliyekuwa kabla yako alikuwa dikteta, watu wakikusema kwamba utawala wako ulikuwa wa kidikteta, huwezi kukataa. Ukisema "niliyemkuta alikuwa dikteta pia" utakuwa unakubali kosa, hii si defense.
Ukikamatwa unaiba, kusema "hata huyu mwenzangu anaiba" si defence, ni kukubali kwamba wewe mwizi.
If you take someones office, and you see that that someone has been sluggish and doing things wrong, and you continue the same, you are no different.
Kikwete was elected to increase our power capacity, not to decrease or keep it constant, what took him so long into his administration to even start to take adverse measures ?
Mgao ulianza rasmi August 1992 (kama sikosei). Kwa hiyo mwakani tutakuwa tunatimiza miaka 20 ya mgao wa umeme nchini na wakati huo huo hatujawahi kusikia kama kuliwahi kuwa na mgao kipindi chote cha miaka 23 ambacho Mwalimu alikuwa madarakani, lakini pamoja na rekodi hiyo nzuri sana ya Mwalimu ukilinganisha na wale waliomfuatia bado kuna wale ambao hawakubali kwamba Mwalimu alifanya mengi mazuri kwa Tanzania na Watanzabia likiwemo hili la upatikanaji wa umeme kwa uhakika kwa kipindi chote hicho. RIP Mwalimu.
Labda hukuwepo wakati wa nyerere. hata diesel ilikuwa hamna.
Tazama data, harudii makosa yao, anafanya kikweli. Katika hizo figure, wewe unaona increment au decrease?
Ukisoma utaona, tofauti na wengi wanaolaumu tu, mimi kwakweli nimetoa pongezi.
Swali langu la msingi uliloanzia kulibishia ni "what took him so long?".
Wewe ukaanza kujiumuma kwamba hata waliomtangulia walikuwa na matatizo haya, that is beside the point, two wrongs do not make a right.
Kikwete naye sluggish? Hata baada ya kuwa na advantage ya hindsight, kukaa Wizara ya Nishati miaka kibao, Wizara ya fedha miaka kibao, kuona energyuse projections zetu zinaendaje, kuna budgeting projections zetu zinaendaje, alihitaji miaka kuanza kulifanyia kazi swala hili?
Nilishakwambia acha kutuletea urongo wako hapa. Wakati wa Nyerere hatukuwa na matatizo ya umeme. Mimi nimesoma enzi hizo. Kama kulikuwa na upungufu wa diseli au hamna diseli Tanzania haizalishi diseli. Lakini umeme ulikuwepo. Punguza urongo.Labda hukuwepo wakati wa nyerere. hata diesel ilikuwa hamna.
Kitu ambacho nadhani unashindwa kukikubali ni kuwa, Kikwete kafanya mengi ya maana kwenye suala la umeme.
Alipochukua nchi kakumbana na mambo mengi sana, na kwa kibajeti chetu finyu afanye mangapi kwa pamoja? Katika priorities alizokuwa nazo, hili la umeme lipo na hajalisahau, utakumbuka kwamba, alipochukua urais nchi ilikuwa kizani. Akafanya haraka haraka iletwe mitambo ya emergency, matokeo tunayajua, na kwa bahati nzuri zikanyeesha mvua nzuri sana tukawa hatuna haja hata ya kuiwasha hiyo mitambo.
Ukame ule alioukuta Kikwete uliambatana na njaa kali sana, Kikwete akasema hafi mtu hapa. Akafanya kila njia na kweli hakufa mtu kwa njaa ile. Bahati nzuri sana mvua ile iliyojaza mabwawa ya hifadhi kwa ajili ya umeme, ilitusaidia kwa miaka minne mfululizo, na kina cha maji kilikuwa kizuri tu, sasa fedha inayohitajika sana sehemu zingine, ikaanza kutumika huko, kwenye mashule, mabarabara, ma university na mitambo ya umeme iliyokuwepo Ubungo ilionekana kuwa itatosha kabisa kama kuna tatizo.
Kilichotokea baada ya hapo ni wimbi la wawekezaji, wimbi la matumizi ya umeme yasio ya kawaida na umeme ukawa unahitajika na unaongezeka kwa 14% kila mwaka. Kikwete akaagiza mitambo kama mahitaji ya maongezeko, ghafla tumekumbwa na ukame, mitambo ambayo iliagizwa ku cover ongezeko la kawaida la kila mwaka ndio inatumika kujaziliz umeme ambao haufuliwi kwa ajili ya kupungua vina vya maji kwenye mabwawa. Hapo jamani ni nani wa kumlaumu? ingekuwa hajafanya kweli, mimi ningekuwa wa kwanza kumlaumu.
Kumbukeni kuna sababu ambazo zinakuwa nje ya uwezo wa yeyote awaye, lakini kizuri ni kwamba Kikweye hata kwa hilo hajasema hapana hapa ndio mwisho, kawekeza kwenye mkaa wa mawe, kawekeza kwenye upepo na sasa anahuisha umeme wa steigler.
Jee, ni madogo hayo?
Data zinaonesha average yake ya kuwekeza kwenye umeme kwa mwaka ni way above wote waliomtangulia. Wakati wenzake waliwekeza wastani wa 7.5MW kwa mwaka yeye anawekeza 50MW kwa mwaka, hilo nii kubwa sana na kasema itaongezeka kufikia uwiano wa 200MW kwa mwaka kabla ya kumaliza muda wake. Its a big achievement uki compare na wote waliopita. Na vilevile akabadilisha sheria ya monopoly kwenye umeme ili wafuaji binafi waweze kuwekeza na matokeo tunayaona.
Kitu ambacho nadhani unashindwa kukikubali ni kuwa, Kikwete kafanya mengi ya maana kwenye suala la umeme.
Alipochukua nchi kakumbana na mambo mengi sana, na kwa kibajeti chetu finyu afanye mangapi kwa pamoja? Katika priorities alizokuwa nazo, hili la umeme lipo na hajalisahau, utakumbuka kwamba, alipochukua urais nchi ilikuwa kizani. Akafanya haraka haraka iletwe mitambo ya emergency, matokeo tunayajua, na kwa bahati nzuri zikanyeesha mvua nzuri sana tukawa hatuna haja hata ya kuiwasha hiyo mitambo.
Ukame ule alioukuta Kikwete uliambatana na njaa kali sana, Kikwete akasema hafi mtu hapa. Akafanya kila njia na kweli hakufa mtu kwa njaa ile. Bahati nzuri sana mvua ile iliyojaza mabwawa ya hifadhi kwa ajili ya umeme, ilitusaidia kwa miaka minne mfululizo, na kina cha maji kilikuwa kizuri tu, sasa fedha inayohitajika sana sehemu zingine, ikaanza kutumika huko, kwenye mashule, mabarabara, ma university na mitambo ya umeme iliyokuwepo Ubungo ilionekana kuwa itatosha kabisa kama kuna tatizo.
Kilichotokea baada ya hapo ni wimbi la wawekezaji, wimbi la matumizi ya umeme yasio ya kawaida na umeme ukawa unahitajika na unaongezeka kwa 14% kila mwaka. Kikwete akaagiza mitambo kama mahitaji ya maongezeko, ghafla tumekumbwa na ukame, mitambo ambayo iliagizwa ku cover ongezeko la kawaida la kila mwaka ndio inatumika kujaziliz umeme ambao haufuliwi kwa ajili ya kupungua vina vya maji kwenye mabwawa. Hapo jamani ni nani wa kumlaumu? ingekuwa hajafanya kweli, mimi ningekuwa wa kwanza kumlaumu.
Kumbukeni kuna sababu ambazo zinakuwa nje ya uwezo wa yeyote awaye, lakini kizuri ni kwamba Kikweye hata kwa hilo hajasema hapana hapa ndio mwisho, kawekeza kwenye mkaa wa mawe, kawekeza kwenye upepo na sasa anahuisha umeme wa steigler.
Jee, ni madogo hayo?
Data zinaonesha average yake ya kuwekeza kwenye umeme kwa mwaka ni way above wote waliomtangulia. Wakati wenzake waliwekeza wastani wa 7.5MW kwa mwaka yeye anawekeza 50MW kwa mwaka, hilo nii kubwa sana na kasema itaongezeka kufikia uwiano wa 200MW kwa mwaka kabla ya kumaliza muda wake. Its a big achievement uki compare na wote waliopita. Na vilevile akabadilisha sheria ya monopoly kwenye umeme ili wafuaji binafi waweze kuwekeza na matokeo tunayaona.
Kitu ambacho nadhani unashindwa kukikubali ni kuwa, Kikwete kafanya mengi ya maana kwenye suala la umeme.
Lakini, kama haya maelezo ni kweli you gotta hand it to him, and ask him "what took you so long?"
Ndugu zangu,
Kuna mengine yamenipita hapa kati. Leo nimesikiliza mahojiano ya mwandishi wa BBC na Rais Jakaya Kikwete kuhusu tatizo la upatikanaji wa umeme Tanzania.
Nimefuatilia pia maoni ya Watanzania mtandaoni juu ya majibu ya Kikwete. Tafsiri yangu; uongozi wa nchi ni kitu kigumu sana. Wengi wamemshambulia Kikwete kwa majibu yake kiasi wengine wamediriki kuandika; kuwa hatuna Rais.
Tunafanya makosa sana kutoa hukumu zenye kusukumwa na hisia hasi. Nimesikiliza mara mbili majibu ya Rais. Sikuona mahala pa kumshutumu Rais isipokuwa nimesikitishwa na maswali ya mwandishi wa BBC ambayo kwa Kikwete ilikuwa kama penalti alizokuwa akipigiwa mikononi na yeye kuzidaka huku akitabasamu.
Tusisahau, kuwa Kikwete ni mwanasiasa mahiri. Mwandishi anayekutana na Kikwete ni vema akajiandaa vilivyo juu ya namna ya kumbana Kikwete ndani ya majibu yake. Afanye hivyo ili kupata maswali mapya na hivyo basi habari mpya kutokana na majibu ya Rais.
Niseme tu, mahojiano yale ya Kikwete na BBC hayakutoa maswali mapya wala kuja na habari mpya. Na huo si udhaifu wa Kikwete bali mwandishi wa BBC aliyemhoji Kikwete.
Si tumemwona? Kikwete aliweza kucheza anavyotaka kwenye mahojiano yale. Na umahiri wake ulijidhihirisha pale alipogeuza sura ya mahojiano yale na Kikwete kuchukua nafasi ya mwandishi kwa kumbana mwandishi na husuan juu ya maarifa ya mwandishi katika eneo husika;
" Wakati mwingine na nyinyi mjifunze hayo mambo ya kitaalamu kulikoni kuuliza tu hivi hivi. Unajua ungekuwa na wewe unauliza kwa hoja - "unajua kwamba hiki kitu hiki ingekuwa umeme wa jua miezi miwili tu upo" - tungeweza kufanya hivyo." Kikwete anamwambia mwandishi wa BBC.
Katika mahojiano yale Kikwete alikwenda na takwimu zake mfukoni. Kama moja ya mbinu katika sanaa ya mawasiliano ili kufikisha ujumbe, mara tatu ndani ya mahojiano yale Kikwete alizungumzia MW 600 zilizozalishwa tangu uhuru na MW 145 zilizozalishwa tangu 2009, na MW 160 zitakazozalishwa ifikapo Desemba mwaka huu. Jumla zitakuwa MW 305 tangu 2009. Na hapo ndipo kwenye hoja ya msingi ya Kikwete. Ana haki kuwashangaa wasioona jitihada zake.
Na Kikwete hakosi majibu ukimwuliza juu ya umeme wa jua, upepo na mvuke. Ana hoja anaposema kuwa umeme huo pia unahitaji mipango na kuwa huwezi kupata umeme wa jua kesho kwa vile jua linawaka.
Kama msikilizaji ningependa mwandishi ambane Kikwete kwenye maeneo ya ufisadi kwenye mikataba ikiwamo yenye kuhusiana na nishati ya umeme. Hakika, kama tungedhibiti ufisadi kwenye mikataba, basi, ni imani ya wengi kuwa tungejenga uwezo wa kuzalisha MW nyingi zaidi za umeme na kwa kasi kabisa, kulifanya tatizo la umeme kuwa ni historia. Tungeweza pia kupunguza gharama za mtumiaji wa umeme.
Tuna tatizo pia la baadhi ya wanasiasa kujiingiza katika kuwekeza kwenye eneo la nishati ya umeme. Wachague kati ya uongozi na uwekezaji. Kiongozi huwezi kuwa na hisa kwenye kampuni binafsi ya kuzalisha umeme na wakati huo huo ukalinda maslahi ya umma badala ya kampuni yako.
Vinginevyo, kwa waliokuwa na utayari wa kuelewa, mahojiano yale ya BBC na Kikwete yamempa nafasi Kikwete ya kujenga hoja ya msingi juu ya nini alichofanikiwa kufanya tangu aingie madarakani katika jitihada za kutatua tatizo la umeme nchini.
Nawasilisha.
Maggid,
Sweden, Jumanne, Julai 26,2011
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo
Ndugu zangu,
Kuna mengine yamenipita hapa kati. Leo nimesikiliza mahojiano ya mwandishi wa BBC na Rais Jakaya Kikwete kuhusu tatizo la upatikanaji wa umeme Tanzania.
Nimefuatilia pia maoni ya Watanzania mtandaoni juu ya majibu ya Kikwete. Tafsiri yangu; uongozi wa nchi ni kitu kigumu sana. Wengi wamemshambulia Kikwete kwa majibu yake kiasi wengine wamediriki kuandika; kuwa hatuna Rais.
Tunafanya makosa sana kutoa hukumu zenye kusukumwa na hisia hasi. Nimesikiliza mara mbili majibu ya Rais. Sikuona mahala pa kumshutumu Rais isipokuwa nimesikitishwa na maswali ya mwandishi wa BBC ambayo kwa Kikwete ilikuwa kama penalti alizokuwa akipigiwa mikononi na yeye kuzidaka huku akitabasamu.
Tusisahau, kuwa Kikwete ni mwanasiasa mahiri. Mwandishi anayekutana na Kikwete ni vema akajiandaa vilivyo juu ya namna ya kumbana Kikwete ndani ya majibu yake. Afanye hivyo ili kupata maswali mapya na hivyo basi habari mpya kutokana na majibu ya Rais.
Niseme tu, mahojiano yale ya Kikwete na BBC hayakutoa maswali mapya wala kuja na habari mpya. Na huo si udhaifu wa Kikwete bali mwandishi wa BBC aliyemhoji Kikwete.
Si tumemwona? Kikwete aliweza kucheza anavyotaka kwenye mahojiano yale. Na umahiri wake ulijidhihirisha pale alipogeuza sura ya mahojiano yale na Kikwete kuchukua nafasi ya mwandishi kwa kumbana mwandishi na husuan juu ya maarifa ya mwandishi katika eneo husika;
" Wakati mwingine na nyinyi mjifunze hayo mambo ya kitaalamu kulikoni kuuliza tu hivi hivi. Unajua ungekuwa na wewe unauliza kwa hoja - "unajua kwamba hiki kitu hiki ingekuwa umeme wa jua miezi miwili tu upo" - tungeweza kufanya hivyo." Kikwete anamwambia mwandishi wa BBC.
Katika mahojiano yale Kikwete alikwenda na takwimu zake mfukoni. Kama moja ya mbinu katika sanaa ya mawasiliano ili kufikisha ujumbe, mara tatu ndani ya mahojiano yale Kikwete alizungumzia MW 600 zilizozalishwa tangu uhuru na MW 145 zilizozalishwa tangu 2009, na MW 160 zitakazozalishwa ifikapo Desemba mwaka huu. Jumla zitakuwa MW 305 tangu 2009. Na hapo ndipo kwenye hoja ya msingi ya Kikwete. Ana haki kuwashangaa wasioona jitihada zake.
Na Kikwete hakosi majibu ukimwuliza juu ya umeme wa jua, upepo na mvuke. Ana hoja anaposema kuwa umeme huo pia unahitaji mipango na kuwa huwezi kupata umeme wa jua kesho kwa vile jua linawaka.
Kama msikilizaji ningependa mwandishi ambane Kikwete kwenye maeneo ya ufisadi kwenye mikataba ikiwamo yenye kuhusiana na nishati ya umeme. Hakika, kama tungedhibiti ufisadi kwenye mikataba, basi, ni imani ya wengi kuwa tungejenga uwezo wa kuzalisha MW nyingi zaidi za umeme na kwa kasi kabisa, kulifanya tatizo la umeme kuwa ni historia. Tungeweza pia kupunguza gharama za mtumiaji wa umeme.
Tuna tatizo pia la baadhi ya wanasiasa kujiingiza katika kuwekeza kwenye eneo la nishati ya umeme. Wachague kati ya uongozi na uwekezaji. Kiongozi huwezi kuwa na hisa kwenye kampuni binafsi ya kuzalisha umeme na wakati huo huo ukalinda maslahi ya umma badala ya kampuni yako.
Vinginevyo, kwa waliokuwa na utayari wa kuelewa, mahojiano yale ya BBC na Kikwete yamempa nafasi Kikwete ya kujenga hoja ya msingi juu ya nini alichofanikiwa kufanya tangu aingie madarakani katika jitihada za kutatua tatizo la umeme nchini.
Nawasilisha.
Maggid,
Sweden, Jumanne, Julai 26,2011
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo