Majibu ya Kikwete na BBC: Tumevuna tulichokipanda

Majibu ya Kikwete na BBC: Tumevuna tulichokipanda

Rais wetu anajigamba na anafanya kosa kubwa sana kujisifia alichokifanya tofauti na wenzake waliomtangulia. Ni dalili ya kutokujiamini na kujitilia mashaka uwezo wake na inaelekea kana kwamba anataka apewe tukuzo na sifa wakati bado yupo madarakani kwa kazi ambayo matunda yake hayaonekani.

Nikirudi kwenye hizi megawati zake 300, sehemu kubwa ni kuwa tumejenga viwanda vya kufua umeme, lakini mitambo ya kuzalisha umeme si yetu. Pale Ubungo panapozalishwa mw 104, kuna IPTL (sina uhakika kama wanachangia sehemu), Symbion na sasa Jacobsen ambao mradi wao wa Dola milioni 125 za Kimarekani, sisi tumetoa asilimia 15 (15%) tuu kwa mradi mzima, na sehemu iliyobakia ni mikopo na ni Jacobsen na si Tanesco ndio inawezekana wakawa wamiliki wa mitambo.

Kuna hili jambo la umeme wa thermal na hiki kipande ni very interesting ukizingatia kuwa ni habari ya miaka miwili iliyopita na Tanesco hawajabadilisha walichoandika kwenye webusaiti yao. KIpande hiki, kinaonyesha mapungufu kwa vituo vinavyozalisha umeme kwa kutumia mafuta, na hovyo tukirudi kwemye majibu ya kudai mvuoa ndio chanzo, je hizi megawati nyingine zisizozalishwa kutokana na uchakavu wa mitambo ni nani alaumiwe?



Ama jedwali hili



na hili




na hii ambayo bado haijakamilika na iko chini ya wafadhili




So there goes mahesabu ya awamu yetu imefanya haya, in comparison to yaliyofanywa na awamu ya kwanza na ya pili.

Habari uliyoiweka pamoja na takwimu za Tanesco zinakusuta. Au kusoma takwimu zinakupiga chenga? Mikataba ya umeme wakati wa Kikwete ni over 2,000MW. kama ulivyoonyesha katika jedwali la Tanesco ni nani aliyefanya zaidi yake katika awamu zote zilizopita? Hakuna hata uchanganye na mkoloni.
 
Hakuna kauli ya rais mkwele inayoniudhi na kunichefua siku nzima inayosema "serikali haina uwezo wa kufanya mvua inyeshe". Kwa maoni yangu binafsi kauli hiyo ndiyo inayopambanua waziwazi uwezo mdogo wa kikwete. Siju kama kuna chizi anayeweza kutamka maneno ya ajabu kama hayo.


Anasema govt haiwezi kuleta mvua! Si amwulize yule mshikaji wake Edwadi aliyepata ajali ya kisiasa...c kuna kipindi alienda kutafuta mvua huko sijui wapi vile!....Hahahaha...Mtani wangu mkwe..re ni zero.........
 
Jamani mtukufu Rais kajibu kwa hoja na nimemwelewa na yuko sahihi sana. Nasi waandishi tuulize kwa hoja. Mfano pia kutambua jitihada na kumshukuru Mheshimiwa Rais na jopo lake na sio kuuliza maswali ya kishenzi. Ikiwa sisi wenyewe katika ngazi zetu za kaya hatumudu hata kununua jenereta au kuweka solar panels sasa tunamlaumu Mheshimiwa wetu. Acheni Usenge bwana tutumie akili, hii nchi ni ya kwetu sote na siyo ya Mheshimiwa Kikwete wala nani peke yake bali yetu sote. Akili na jitihada zetu ni kulaumu. Mi kesho nahamasisha jamii yangu kununua generator na hivy kuangalia uwezo wa kuchaji kama TANESCO na bili kidiuchu kwa mwezi pamoja na kununua solar panels na solar rechargeable lights. Tufikirie Jitihada binafsi kabla ya kumlaumu mzee. Yeye kishafanya jitihada.

Jitihada binafsi tunazifanya kwa mambo binafsi kama nyumba ya kuishi, kununua nguo, kununua chakula, kulipia bill zingine. Kama wewe utataka tufanye jitihada binafsi kwa mambo makubwa kama hayo na kipato chetu cha kima cha chini kuna siku utatuambia kila mtu awe na mwalimu kwa ajili ya wanae, awe na daktari wake, ajenge barabara yake mwenyewe, kila mtu achimbe kisima chake mwenyewe. Mkuu fikirisha ubongo wako utambue kuna mambo makubwa lazima serikali ifanye ndo maana inakusanya kodi karibia kwa kila mtu ili itumie hiyo hela kwa ajili ya mambo makubwa kama kutuletea umeme, kujenga barabara na kuboresha huduma zote za jamii na sio kutuletea habari za kufanya jitihada hapa.
 
Anasema govt haiwezi kuleta mvua! Si amwulize yule mshikaji wake Edwadi aliyepata ajali ya kisiasa...c kuna kipindi alienda kutafuta mvua huko sijui wapi vile!....Hahahaha...Mtani wangu mkwe..re ni zero.........

Ilikuwa kitu cha Vietnam hicho, ungefanywa mradi na tungekuwa tunalipia service charge, sijui na capacity charge na mvua ikinyesha ile ya kawaida itabidi muendelee kulipia tu na ile mvua ya wavietnam, nadhan ule ndo ungekuwa ufisadi babu kubwa.
 
Nadhani jibu sahihi ila kwa sasa walikuwa wapi zamani inaeleweka kuwa mvua zina pungua daily, walifanya nini kujikinga na hili walilolijua kale?we need to pumzisha them
 
Mie naomba niulize swali. Kama kila kitu tutakua tunamlaumu JK tutafika kweli?

Urais ni kazi kubwa sana, sababu mawaziri anachagua miongoni mwa wabunge; wabunge ambao wengine wala hawajui. Pia inalazimika kuteua ili kuleta uwiano wa mikoa. Ana Challenges nyingi sana.

Mpira ukiuangalia kwa nje unaona kabisa pale angepiga hivi ingekua goli, ila ukiaingia uwanjani mambo ni tofauti. Mie naona tuanze na viongozi wenye dhamana ya kwanza, PRIMARY RESPONSIBILITY, Kisha twende kwake mwenye secondary responsibility.

Majibu yake siyaungi mkono lakini pia inategemea swali liliulizwaje. Kukosoa always ni rahisi kuliko kutenda.
Ninaomba tunapojibu hoja tujibu kkwa HOJA na sio VIHOJA.

Asanteni

Ndimi Devil's Advocate
 
Hakuna kauli ya rais mkwele inayoniudhi na kunichefua siku nzima inayosema "serikali haina uwezo wa kufanya mvua inyeshe". Kwa maoni yangu binafsi kauli hiyo ndiyo inayopambanua waziwazi uwezo mdogo wa kikwete. Siju kama kuna chizi anayeweza kutamka maneno ya ajabu kama hayo.
usimlaumu yeye walaumu marafiki ambao hawawezi kumwambia kuwa mzee kauli si nzuri hii!
 
personally nimemuelewa Mr. President sasa kama chadema wana alternatives hebu wauweke hapa tupime.
Mbona Mbowe alishasema iundwe kamati ya wataaalamu kutatua tatizo na PINDA alipinga! chadema wanashauri watalaamu washilikiswe!
 
Mhhhh!! yaani nasoma mpaka naona aibu mwenyewe kwa majibu ya mkuu wetu!!! Mhhhh!!!! kweli kazi tunayo...mpaka miaka 4 iishe!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nchi inazidi kukumbwa na GIZA mtu anaendelea kusema JITIHADA KUBWA JITIHADA KUBWA!

"Sasa ufikirie kwamba toka Uhuru tumeweza kuzalisha umeme wa MW600, lakini toka 2009 mpaka Disemba mwaka huu tutakuwa tumeongeza MW300! Ni jitihada kubwa.


Hiyo ndio sentensi kamili, mbona unaweka unayoyapenda wewe tu?
 
"Sasa ufikirie kwamba toka Uhuru tumeweza kuzalisha umeme wa MW600, lakini toka 2009 mpaka Disemba mwaka huu tutakuwa tumeongeza MW300! Ni jitihada kubwa. Hiyo ndio sentensi kamili, mbona unaweka unayoyapenda wewe tu?
watu hawa wanaishi Tanzania ipi?
 
Waandishi wanapowahoji viongozi wetu huwa wanashangaa sana kwa majibu ya ajabuajabu!!!!
 
Mbavu zangu mimi, du hahahahahahahhahahaaaa yyeyeyeyeyeyyeeyeyee uwiiiiiiii. As easy as simple
 
Habari uliyoiweka pamoja na takwimu za Tanesco zinakusuta. Au kusoma takwimu zinakupiga chenga? Mikataba ya umeme wakati wa Kikwete ni over 2,000MW. kama ulivyoonyesha katika jedwali la Tanesco ni nani aliyefanya zaidi yake katika awamu zote zilizopita? Hakuna hata uchanganye na mkoloni.

Haviwezi kunisuta wakati miradi iko kwenye paper and not completed projects. Kwani katika hizo mw 2000, mbona nyingine zimefanyiwa study tangu nyakati za Nyerere, Mwinyi na Mkapa?

Lets talk of what has been done and not a project that is still on paper! Ndio maana nikakuuliza, nitajie major projects 5 tu ambazo kazikamilisha Kikwete ambazo by the way, alizianzisha yeye (UDOM ilianza na Mkapa na Kikwete akamalizia)!
 
Mie naomba niulize swali. Kama kila kitu tutakua tunamlaumu JK tutafika kweli?

Urais ni kazi kubwa sana, sababu mawaziri anachagua miongoni mwa wabunge; wabunge ambao wengine wala hawajui. Pia inalazimika kuteua ili kuleta uwiano wa mikoa. Ana Challenges nyingi sana.

Mpira ukiuangalia kwa nje unaona kabisa pale angepiga hivi ingekua goli, ila ukiaingia uwanjani mambo ni tofauti. Mie naona tuanze na viongozi wenye dhamana ya kwanza, PRIMARY RESPONSIBILITY, Kisha twende kwake mwenye secondary responsibility.

Majibu yake siyaungi mkono lakini pia inategemea swali liliulizwaje. Kukosoa always ni rahisi kuliko kutenda.
Ninaomba tunapojibu hoja tujibu kkwa HOJA na sio VIHOJA.

Asanteni

Ndimi Devil's Advocate

FP,

KUna vitu mtu unaweza endelea ku-delegate na vingine lazima uweke full stop na kuanza kuviangalia kwa makini na hata kuvifanyia kazi ya ziada mwenyewe.

Tatizo ni kuwa bado watu (Serikali) ama kwa makusudi au ufupi wa upeo, hawaoni kushabihiana kwa tatizo la umeme na nchi kuendelea kuwa masikini kutokana na ukosefu wa mapato kunakotokana na upungufu wa uzalishaji mali. Mawazo na majibu kuhusiana na hili suala ni kana vile umeme ni anasa.

Ni January, Mnyika na Kafulila (I think Zitto too perhaps) ambao wako katika safu ya timu inaitwa SERIKALI ambao wanajaribu kuoanisha hivi viwili na ndio maana wamekuwa mstari wa mbele kuliongelea bila kumumunya meno.

HIvyo kwa sasa jinsi uchumi wa nchi unavyoyumba na mambo yanavyoharibika, Rais hawezi kuendelea ku-delegate au kuwa laid back akijisemea "Ngeleja will sort things out". Ni sawa na leo hii Marekani na suala la Bajeti na Deni la Taifa, ni Rais yuko mstari wa mbele kuongea na nchi na chama cha upinzani kujadiliana cha kufanya na si Waziri wa fedha!
 
Ilikuwa kitu cha Vietnam hicho, ungefanywa mradi na tungekuwa tunalipia service charge, sijui na capacity charge na mvua ikinyesha ile ya kawaida itabidi muendelee kulipia tu na ile mvua ya wavietnam, nadhan ule ndo ungekuwa ufisadi babu kubwa.






haikuwa vietnam jamani, ilikuwa Thailand, baada ya ile ziara yule Waziri Mkuu akaondolewa kwa nguvu za umma, huyu wa kwetu naye hakukaa sana akajiuzulu kwa kashfa ya richmond
 
BBC: Kuna njia kama umeme wa jua, umeme wa kutokea ardhini wa mvuke, kwanini serikali haitafuti njia mbadala kuzalisha umeme kwa njia hizo?

Rais Kikwete: Nasema hivi, hata umeme wa jua lazima ujenge, umeme wa mvuke lazima ujenge, si kitu cha mwezi mmoja. Nasema huo ndio ukweli wenyewe na wakati mwingine na nyinyi mjifunze hayo mambo ya kitaalamu kulikoni kuuliza tu hivi hivi. Unajua ungekuwa na wewe unauliza kwa hoja - “unajua kwamba hiki kitu hiki ingekuwa umeme wa jua miezi miwili tu upo”

KAMA KWELI RAIS WETU JK ALIJIBU HIVYO BASI KUNA TATIZO KUBWA LA MSINGI. KWENYE UKAME WA 2006 SERIKALI YA JK HAIKUTAKA KUWEKEZA KWENYE VYANZO MBADALA KWA SABABU VINACHUKUA MUDA MREFU KUZALISHA UMEME KWA HIYO AKAKIMBILIA KWENYE RICHMOND. LEO HII SERIKALI YA JK BADO INA MAWAZO YALEYALE YA SHORT TERM PLANS. INA MAANA KWAMBA UKAME WA MIAKA IJAYO UTASHUGHULIKIWA KWA MIPANGO HIYOHIYO YA DHARURA MAANA JK HATAKI KUSHUGHURIKIA MATATIZO YA KESHO, AMEELEMEWA NA YA LEO. HIVI HII MIPANGO YA DHARURA ITAISHA LINI?
 
Pengine nitakuwa ninazungumza kwa jazba. Siwezi kuzuwia hasira zangu. Mniwie radhi!
Nafikiri umefika wakati wa kuwacha kabisa kulalamika na kumlalamikia Jk na magamba wenzake.
Kulalamika zaidi hakutotufikisha popote. Imefika wakati tuwe na dhamiri ya makusudi ya kusema "INATOSHA".

JK na watu wake wapo pale kwa sababu sisi tunawaruhusu kuwepo. Kama kweli hatuwataki, tuwaondoshe, "For hook or crook".
Kama tutaendelea kulalamika tu, Disemba itafika na tatizo la umeme litaendelea kuwepo, tena kwa kasi zaidi kwa sababu Disemba ni wakati wa kiangazi. Kama tutaendelea kulalamika, 2015 itafika na CCM wataendelea kuwepo pale kwa sababu ni wachakachuaji na tunaruhusu uchakachuaji.
Wataendelea kuwepo pale kwa sababu Watanzania "tuna amani". Amani ya woga. Amani ndani ya giza. Amani na mlo mmoja kwa siku. Amani na kipato cha chini ya dola moja kwa siku. Amani huku tunakufa tukijiona kwa kukosa matibu. AMANI GANI?

Watanzania tunasifika kwa bla bla bla na maamuzi ya zimamoto, nguvu ya soda.
Nani leo anazungumzia tena Katiba?
Nani leo anazungumzia tena malipo kwa Dowans?
Nani leo anazungumzia tena posho za wabunge? Ni mengi tu!
Tulifokafoka, yamepita, yatakuja mengine tutafokafoka na yatapita. Siku zinakwenda, tuliopo hoi bin taabani, vizazi vyetu sijui vitakuja kuishi vipi.
Watanzania, kwa imani kabisa CCM imekosa radhi ya wananchi kuiongoza nchi. Imekosa uhalalai wa kuwatawala Watanzania. Tufanye jambo, watatumaliza hawa. Hatuna cha kupoteza zaidi ya tulivyokwishapoteza. Hatuwezi kunyanyua bango angalu kuonesha hasira zetu. Hatuwezi kujikusanya tukalalamika wanayotutendea.
Watanzania, hatuna AMANI, hatuna UHURU. Tumebakiwa na dhamira. Tuitumie.
 
Back
Top Bottom