Majibu ya Kikwete na BBC: Tumevuna tulichokipanda

Majibu ya Kikwete na BBC: Tumevuna tulichokipanda


"Sasa ufikirie kwamba toka Uhuru tumeweza kuzalisha umeme wa MW600, lakini toka 2009 mpaka Disemba mwaka huu tutakuwa tumeongeza MW300! Ni jitihada kubwa.


Hiyo ndio sentensi kamili, mbona unaweka unayoyapenda wewe tu?
Umeshaamini kuwa "ikifika Disemba, 2011 watakuwa wameongeza MW300"?. Umeasahau ahadi zilizokuwa zikitolewa kwenye hotuba za mwisho wa mwezi mwaka 2006?
 
Ee bana tujaribu kumtetea prezdaa wetu kwa nguvu zote kwa kuficha upumbavu. Asiruhusiwe mwandishi yeyote kumuuliza maswali ya moja kwa moja. Tuweke mda wa angalau siku moja kabla ya majibu.
Au watanzania wenzangu mnasema je?

.
 
Hakuna kauli ya rais mkwele inayoniudhi na kunichefua siku nzima inayosema "serikali haina uwezo wa kufanya mvua inyeshe". Kwa maoni yangu binafsi kauli hiyo ndiyo inayopambanua waziwazi uwezo mdogo wa kikwete. Siju kama kuna chizi anayeweza kutamka maneno ya ajabu kama hayo.
hata mimi mkuu inanikera visivyo kawaida inaonyesha ni jinsi gani alivyooba uongozi pasipokujua majukumu yake
 
Mbona Mbowe alishasema iundwe kamati ya wataaalamu kutatua tatizo na PINDA alipinga! chadema wanashauri watalaamu washilikiswe!
si kwavile upinzani wanasubiria hoja itolewe na ccm ndo ikubalike mamba na yeye hashikishi ubongo aweke uccm pembeni atafute utatuzi
 
Du pole jk na uccm wanu mpaka kwenye masuala yanayogarimu uchumi wa nchi nadhan pindi mtakapoweka uccm pembeni nakuamua kutatua matatizo ya nchi tutasonga mbele sana
 
kwa nilivyosoma haya mahojiano, kwanza, ni hakika Mheshimiwa hana kauli nzuri, ana majibu makali and he answered rudely, hili jambo ni serious na lina frustrate most of the citizens the least he could have done was to answer calmly, pili, nimepata uhakika kua hili tatizo haliishi leo wala kesho.
 
Umeshaamini kuwa "ikifika Disemba, 2011 watakuwa wameongeza MW300"?. Umeasahau ahadi zilizokuwa zikitolewa kwenye hotuba za mwisho wa mwezi mwaka 2006?

Nikuulize wewe, mnayeona hajafanya kitu. Unanshangaza kuniuliza mimi!

Rais gani aliofanya hivyo katika awamu nzima aliokaa kitini? pamoja na Mkoloni changanya. 300 in 3 Years, 600 in 5 Years, over 2000 by the end of his tenure.
 
Nikuulize wewe, mnayeona hajafanya kitu. Unanshangaza kuniuliza mimi!

Rais gani aliofanya hivyo katika awamu nzima aliokaa kitini? pamoja na Mkoloni changanya. 300 in 3 Years, 600 in 5 Years, over 2000 by the end of his tenure.
We've been generating less than 500mw for the past 15yrs......the promises are not bankable.
Can you tell me when and where did we invest those 300mw?
 
haikuwa vietnam jamani, ilikuwa Thailand, baada ya ile ziara yule Waziri Mkuu akaondolewa kwa nguvu za umma, huyu wa kwetu naye hakukaa sana akajiuzulu kwa kashfa ya richmond

Asante kwa Masahihisho mkuu.
 
Nikuulize wewe, mnayeona hajafanya kitu. Unanshangaza kuniuliza mimi!

Rais gani aliofanya hivyo katika awamu nzima aliokaa kitini? pamoja na Mkoloni changanya. 300 in 3 Years, 600 in 5 Years, over 2000 by the end of his tenure.
Mkuu FF, sasa kama kafanya yote hayo na wengine hawakufanya kama alivyofanya yeye, Mbona kipindi chake pamoja na kufanya makubwa kama unavyotaka tuamini mgawo wa umeme haukomi na unaendelea kila siku tena kiasi cha masaa ya kutokuwa na umeme yanaongezeka?
 
Jamani naomba kuwauliza waungwana mana hivi karibuni hasa kwenye suala la umeme kumekua na kauli za JK kujitetea na pia wafuasi wake kumtetea kwamba "matatizo ya umeme ameyakuta".
Hivi kweli kauli hii ina tija na ni ya kutolewa na kiongozi makini?maana wakati anagombea urais hayo matatizo yalikuepo na aliyaona ina maana angekua mtu makini angekua na strategy kbs ya kutuondolea hayo matatizo! Sasa suala la kusema matatizo nimeyakuta tumueleweje?kwamba kma kayakuta sio jukumu lake kuyaondoa au kwamba alikua anataka kua rais tu ila hakua na nia ya kutuondolea hayo matatizo aliyoyaona kabla hajawa rais?
Mungu ibariki tanzania ili tupate viongozi wanaotaka kututatulia matatizo yetu na sio watawala wanaotaka kutuongoza tu ila matatizo wanasema sio yao
 
.

BBC: Kuna njia kama umeme wa jua, umeme wa kutokea ardhini wa mvuke, kwanini serikali haitafuti njia mbadala kuzalisha umeme kwa njia hizo?

Rais Kikwete: Nasema hivi, hata umeme wa jua lazima ujenge, umeme wa mvuke lazima ujenge, si kitu cha mwezi mmoja. Nasema huo ndio ukweli wenyewe na wakati mwingine na nyinyi mjifunze hayo mambo ya kitaalamu kulikoni kuuliza tu hivi hivi. Unajua ungekuwa na wewe unauliza kwa hoja - "unajua kwamba hiki kitu hiki ingekuwa umeme wa jua miezi miwili tu upo" - tungeweza kufanya hivyo.Sisi sasa hivi kwa mfano tunajiandaa kuzalisha umeme wa kutumia Upepo, pale Singida. Tuna mwaka wa tatu sasa tuna mipango na Wakorea wa Kusini, umeme haujakuwepo. Kwa hiyo nasema hayo ni maelezo rahisi. Wanasema "mbona jua lipo?" katengeneze umeme wa jua kama jua lipo! (kicheko).

Hivi Mheshimiwa wetu nani anampa maelekezo ya kitaalamu kama haya, ni mhandisi gani huyo aliyempa maelekezo kama haya kuhusu umeme wa jua? kusanifu na kusimika mifumo ya kuzalisha umeme jua kweli ina hitaji miezi miwili? Tafadhali nifafanulie hapo.
 
Hivi Mheshimiwa wetu nani anampa maelekezo ya kitaalamu kama haya, ni mhandisi gani huyo aliyempa maelekezo kama haya kuhusu umeme wa jua? kusanifu na kusimika mifumo ya kuzalisha umeme jua kweli ina hitaji miezi miwili? Tafadhali nifafanulie hapo.

Ama kweli katika watu niliyowaona JF ambao wameleta pumba, wewe unaweza kuwaongoza kwa pumba zako, hivi unafikiri umeme wa jua wa kiwango kikubwa ni kama wakuwashia vitaa vya nyumbani pekee?

Tafadhali tumia google kidogo uone 100MW za solar zimekaaje na nini inabidi kifanyike. Usituletee pumba hapa.
 
Jibu halihitaji kuundiwa tume: ni kiongozi legelege kuliko kiongozi yyeto aliymtangulia! Anaongozwa na matukio, haoni mbele na hakufaa kukabidhiwa cheo kikubwa kiasi hicho kwa uwezo wake ni kuongoza kata {Diwani}
 
Kiongozi anatakiwa kutatua matatizo, sio kutoa visingizio.

Kusema "matatizo nimeyakuta" ni kukimbia wajibu wa kuyatatua. Kama hawezi kuyatatua kwa nini alitaka uongozi?
 
Mkuu FF, sasa kama kafanya yote hayo na wengine hawakufanya kama alivyofanya yeye, Mbona kipindi chake pamoja na kufanya makubwa kama unavyotaka tuamini mgawo wa umeme haukomi na unaendelea kila siku tena kiasi cha masaa ya kutokuwa na umeme yanaongezeka?

Kumbuka kipindi cha Kikwete umeme unatumika sana kuliko awamu yoyote ile, makampuni yamezidi, watu wengi sana ambao walikuwa hatumii umeme (wako shamba) wameingia mijini na inabidi watumie umeme, viwanda vimezidi, usambazaji wa umeme hadi vijijini umezidi sana wakati huu. Impact ya kukosa umeme miaka 6 iliyopita sio kama ya sasa hivi. Matumizi ya umeme yamezidi kuliko tunavyowekeza kwenye umeme.

Hii Kikwete anaibadilisha, tueona jinsi alivyowekeza kwenye umeme kwa muda mfupi sana, lakini mitambo ya umeme unayonunua leo sio kama itafika leo hii hii, inabidi ukimbizane na wakati na bahati mbaya sana umeme wetu tuliokuwa tunautegemea ni wa maji na maji ndio ukame.
 
Kiongozi anatakiwa kutatua matatizo, sio kutoa visingizio.

Kusema "matatizo nimeyakuta" ni kukimbia wajibu wa kuyatatua. Kama hawezi kuyatatua kwa nini alitaka uongozi?

Mkumbushe hayo na Obama wenu basi....aache kumlaumu Bush kila apatapo fursa!
 
Hivi Obama angewaambia Wamarekani kuwa matatizo ya deficit ameyakuta (which is true) halafu asifanye juhudi zozote kupambana nayo hivi kweli angepata term ya pili? Mimi nadhani angekuwa one term president. Lakini anajitahidi na anaendelea kujitahidi kuapmbana na matatizo ya unemployment, deficit, na deni la nchi. Hajasingizia mtangulizi wake licha kwamba ana haki kabisa ya kufanya hivyo. Huo ndio mfano bora wa uongozi. Kikwete angetuambia kuwa ameyakuta na amefanya hiki na hiki kupambana nayo ingekubalika. Lakini hivi visingizio visivyo na tija vinapelekea mtu kuuliza aliutaka urais wa nini, na anafanya nini pale Magogoni?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom