Majibu ya Kikwete na BBC: Tumevuna tulichokipanda

Majibu ya Kikwete na BBC: Tumevuna tulichokipanda

Kiongozi anatakiwa kutatua matatizo, sio kutoa visingizio.

Kusema "matatizo nimeyakuta" ni kukimbia wajibu wa kuyatatua. Kama hawezi kuyatatua kwa nini alitaka uongozi?


Msimzingizie JK bure kwa mengine.
Umeme haujapata kuwekezwa tangu Baba wa Taifa aondoke
Viwanda tukajidai kuviuza-hata TIPER, kiwanda cha kudistil petroluem kikauzwa(tena na Mh Mwinyi), leo tunalila lia na freight ya mafuta
Matajiri wakakribishwa kwenye CCM toka awamu ya tatu-matokeo yake tunayaona sasa
Master Plan za miji zikachakachuliwa toka muda mrefu sana-leo mafoleni kibao na hakuna jiji endelevu
Rada tokea awamu ya Tatu
EPA mwishoni mwa awamu ya tatu
Meremeta awamu ya ....

Jamani msimtwishe msukuma mzigo mzito!!!
 
Jibu halihitaji kuundiwa tume: ni kiongozi legelege kuliko kiongozi yyeto aliymtangulia! Anaongozwa na matukio, haoni mbele na hakufaa kukabidhiwa cheo kikubwa kiasi hicho kwa uwezo wake ni kuongoza kata {Diwani}
Hata udiwani katika zama hizi hauwezi
 
Mr presidar kiwete wa fikira. Jamani mtasema mengi sana humu. Wenyemakosa ni cc wenyewe. 2015 iwe kweli.
 
Msimzingizie JK bure kwa mengine.Umeme haujapata kuwekezwa tangu Baba wa Taifa aondokeViwanda tukajidai kuviuza-hata TIPER, kiwanda cha kudistil petroluem kikauzwa(tena na Mh Mwinyi), leo tunalila lia na freight ya mafutaMatajiri wakakribishwa kwenye CCM toka awamu ya tatu-matokeo yake tunayaona sasaMaster Plan za miji zikachakachuliwa toka muda mrefu sana-leo mafoleni kibao na hakuna jiji endelevuRada tokea awamu ya TatuEPA mwishoni mwa awamu ya tatuMeremeta awamu ya ....Jamani msimtwishe msukuma mzigo mzito!!!
Jamani..matatizo yapo-mi sikatai.my problem is what is he doing about it??kwa kweli cjaona hatua yoyote ya kujivunia baada ya miaka hamsini ya uhuru!some tymz naona bora tu mkoloni angekuwepo tungemlaumu yeye!Hivi kweli president anaweza jibu 'ziwezi fanya mvua zinyeshe' tena kwa ujasiri wote??watu kama wewe ndo mnampa hicho kiburi..if someone is perfoming below standards shurti aambiwe!kuleanaleana huku hatutafika ndugu zangu!!
 
Nakumbuka wakati mahojiano hayo yanafanyika, nilikuwa na rafiki yangu raia wa Finland, hajui Kiswahili.
Aliniomba nimtafsiri mahojiano hayo.
Amini usiamini ilibidi baadhi ya majibu ya mkuu niweke uongo ili kuficha aibu ya majibu yake mepesi kwenye maswali mazito.
 
Faizafoxy,
Naona ni wewe peke yako unayeendelea kumuamini Kikwete katika forum hii. Mimi imani yangu kwake ilishapotea tangu alipotudanganya 2007 kwamba kufikia Desemba matatizo ya umeme yatakuwa yameisha. Pia akasema Richmond haijalipwa hata senti huku wakichukua mamilioni kila mwezi. Imani yangu ilipotea pale alipotuambia kuwa atapitia mikataba ya madini ili tuwe na win win situation. Mzungu anaendelea kukomba dhahabu zetu na ndugu zetu wa Nyamongo wanaendelea kusota na dhahma ya uonevu. Atamaliza miaka yake 4 kama alivyosema, atatuachia matatizo ya umeme ambayo kishasema kuwa aliyakuta. Mimi hicho ndicho ninachoamini.
 
Kiranga, ulimaanisha hivyo kweli au umekosea hapo? Manake kumbukumbu zangu zinakinzana kabisa na hicho ulichokiandika hapo. Matatizo ya mgao wa umeme hatukuwa nayo enzi za Mwinyi? Una uhakika?
Hayakuwa makubwa kiasi hiki. Nakumbuka 1987 hatukuwa na umeme mchana pale Mikocheni lakini jioni ukiwaka. Sasa hivi nasikia inaweza kuchukua hata masaa 18 hamna umeme.
 
Jamani naomba kuwauliza waungwana mana hivi karibuni hasa kwenye suala la umeme kumekua na kauli za JK kujitetea na pia wafuasi wake kumtetea kwamba "matatizo ya umeme ameyakuta".
Hivi kweli kauli hii ina tija na ni ya kutolewa na kiongozi makini?maana wakati anagombea urais hayo matatizo yalikuepo na aliyaona ina maana angekua mtu makini angekua na strategy kbs ya kutuondolea hayo matatizo! Sasa suala la kusema matatizo nimeyakuta tumueleweje?kwamba kma kayakuta sio jukumu lake kuyaondoa au kwamba alikua anataka kua rais tu ila hakua na nia ya kutuondolea hayo matatizo aliyoyaona kabla hajawa rais?
Mungu ibariki tanzania ili tupate viongozi wanaotaka kututatulia matatizo yetu na sio watawala wanaotaka kutuongoza tu ila matatizo wanasema sio yao
Hiyo kauli si sawa kwasababu aliomba urais ili ayatatue so kitendo cha kuanza kulaumu waliopita ni usaliti kwa watanzania kwani alitulaghai tumchague kwamba angetusaidia

HE IS JUST RUNNING AWAY FROM HIS OWN SHADOW

NA HII LAANA YA USALITI ATAKAA NAYO HADI ANAINGIA KABURINI
 
Hayakuwa makubwa kiasi hiki. Nakumbuka 1987 hatukuwa na umeme mchana pale Mikocheni lakini jioni ukiwaka. Sasa hivi nasikia inaweza kuchukua hata masaa 18 hamna umeme.

Kwa hiyo unakubaliana na mimi kuwa yalikuwepo. Kilichotofauti na sasa ni severity tu. Manake mimi nakumbuka miaka ya mwanzoni mwa 90 mgao ulikuwepo.
 
Haviwezi kunisuta wakati miradi iko kwenye paper and not completed projects. Kwani katika hizo mw 2000, mbona nyingine zimefanyiwa study tangu nyakati za Nyerere, Mwinyi na Mkapa?

Lets talk of what has been done and not a project that is still on paper! Ndio maana nikakuuliza, nitajie major projects 5 tu ambazo kazikamilisha Kikwete ambazo by the way, alizianzisha yeye (UDOM ilianza na Mkapa na Kikwete akamalizia)!

Unaongelea studies, sisi tunaongelea projects in hand, ni vitu viwili tofauti, katika hizo megawati 2000, hakuna hata moja iliyokuwepo wakati wa nyerere, Nyerere ni steigler aliikataa na Kikwete kaianzisha tena study yake, hiyo haipo kwenye hizo 2,000MW zilizokwisha anza kufanyiwa kazi.
 
yaani kama vile wakati wa kugombea urais ilikuwa nchi ya asali na maziwa na sasa ghafla ndo kagundua kuwa ilikuwa haina nyuki wala ng'ombe!

Alivokuwa ana ahidi maisha bora alikuwa hajui anarithi matatizo ya waliomtangulia?
 
Faizafoxy,
Naona ni wewe peke yako unayeendelea kumuamini Kikwete katika forum hii. Mimi imani yangu kwake ilishapotea tangu alipotudanganya 2007 kwamba kufikia Desemba matatizo ya umeme yatakuwa yameisha. Pia akasema Richmond haijalipwa hata senti huku wakichukua mamilioni kila mwezi. Imani yangu ilipotea pale alipotuambia kuwa atapitia mikataba ya madini ili tuwe na win win situation. Mzungu anaendelea kukomba dhahabu zetu na ndugu zetu wa Nyamongo wanaendelea kusota na dhahma ya uonevu. Atamaliza miaka yake 4 kama alivyosema, atatuachia matatizo ya umeme ambayo kishasema kuwa aliyakuta. Mimi hicho ndicho ninachoamini.

Sio naendelea kumuamini blindly, naona kazi anayoifanya na na appreciate. Richmond alilipwa na nani? hakuna kitu kama hiyo, data ulizonazo ni za kupikwa. Richmond walikuwa wapewe letter of credit ndio vumbi lilianzia hapo.

Dhahabu si aliiweka tume ya kupitia mikataba ya madini na Zitto ndani au umesahau? walishaauri nini? Miaka minne atamaliza na aliyoyafanya mema tutayakumbuka. Hakuna malaika aliyewahi kutawala hii nchi , hata Saint to be nae alitutia mkenge.
 
Jamani naomba kuwauliza waungwana mana hivi karibuni hasa kwenye suala la umeme kumekua na kauli za JK kujitetea na pia wafuasi wake kumtetea kwamba "matatizo ya umeme ameyakuta".
Hivi kweli kauli hii ina tija na ni ya kutolewa na kiongozi makini?maana wakati anagombea urais hayo matatizo yalikuepo na aliyaona ina maana angekua mtu makini angekua na strategy kbs ya kutuondolea hayo matatizo! Sasa suala la kusema matatizo nimeyakuta tumueleweje?kwamba kma kayakuta sio jukumu lake kuyaondoa au kwamba alikua anataka kua rais tu ila hakua na nia ya kutuondolea hayo matatizo aliyoyaona kabla hajawa rais?
Mungu ibariki tanzania ili tupate viongozi wanaotaka kututatulia matatizo yetu na sio watawala wanaotaka kutuongoza tu ila matatizo wanasema sio yao
huyu jamaa m.s.e.nge sana ! tunajua matatizo aliyakuta ila si alisema mwenyewe wakati anatafuta kura kwamba atahakikisha umeme unapatikana vizuri na gharama yake itakuwa nafuu? lakini alipopata kura gharama za umeme zikapanda na akasema mwenyewe kwenye vi hotuba vyake fake vya mwisho wa mwezi kwamba mgao wa umeme hauepukiki! sijui tumfanyeje huyu nguruwe!
 
Ukiangalia mradi wa Nyakato wa MW60 ambao ni wa Mafuta mazito, na mradi wa IPTL ambao ni kuibadilisha mitambo badala ya mafuta mazito itumie gas, hapo unashindwa kuelewa kama hawa watu akili zao zinafanya kazi vizuri au ni mambo ya 10%, IPTL iko Tegeta ambapo ni kama 20km kutoka bandarini mmeshindwa kwa sababu ya gharama, leo mnataka mjenge Mwanza ambapo ni zaidi ya 1000km kutoka bandarini kuna nini hapo?

Mradi wa Shinyanga-Buzwagi na mradi wa Musoma-Nyamongo ni miradi ambayo inaenda mgodini lakini Migodi inachangia asilimia ngapi kwenye pato la Taifa, na kama kusingekuwa na hiyo migodi huwezi ona mradi huo unajengwa, na afadhali basi wangekuwa wanajenga substation katikati ya miradi ili kuwapatia wananchi wanaopitiwa na hiyo miradi umeme.

Kuna kipindi nilienda mgodi wa Buhemba umeme umefika Buhemba lakini wanavijiji wa njiani wanaangalia nyaya tu zinapita juu, hata miradi ya maji watu wanashuhudia mitaro inachimbwa kwa ajili ya kuweka mabomba tu, wanavijiji hawafaidiki na chochote, kwa hali kama hiyo hata kama kuna hujuma zitafanyika kwenye hiyo miradi wananchi hawezi kuwa walinzi kwa hakika.

Miradi mingi uliyotaja inaongelea kutumia gas, kuna jamaa yangu anafanya PAE anasema gas ya kutosha kwenye reservoir ipo ila namna ya kuisafirisha na itosheleze mitambo yote inayojengwa ndo hamna, hakuna bomba lililojengwa zaidi ya lililopo ambalo tayari limekuwa saturated, mambo ni magumu kuliko unavyofikiria ndugu FF.

Kingine naomba ufafanuzi kwa nini mitambo ya Aggreko ilizimwa?

Hayo ya juu sikujibu kwani ni pumba tuu, au hujui kuwa huwezi tuu kuushusha umeme mkubwa kila kijiji? lazima uwe na substations?

Hilo la mwisho ni very simple, gas inaweza kusafirishwa na mabomba yakaongezwa na au kutumia transport ya gas trucks mpaka bomba kubwa litapokuwa tayari.

Jamani hebu kuweni, kidooogo mna appreciate yafanywayo, hivi miaka 80 (80 Years) 600MW na miaka 3 (3 Years) 300MW na tayari zaidi ya 2,000 signed and projects have started. Hivi kuna nini ambacho mnashindwa kuelewa? Au ndio majina tu yanawatatiza?
 
Nakumbuka wakati mahojiano hayo yanafanyika, nilikuwa na rafiki yangu raia wa Finland, hajui Kiswahili.
Aliniomba nimtafsiri mahojiano hayo.
Amini usiamini ilibidi baadhi ya majibu ya mkuu niweke uongo ili kuficha aibu ya majibu yake mepesi kwenye maswali mazito.

Ina maana wewe ni muongo.
 
Mr presidar kiwete wa fikira. Jamani mtasema mengi sana humu. Wenyemakosa ni cc wenyewe. 2015 iwe kweli.

2005 Kikwete, aah kisha maliza muda wake. Mchagueni Slaa ambae anashindwa hata kutatua mgogoro wa madiwani watatu na Mbunge mmoja.
 
Kwa majibu hayo ya mkuu wa nchi, basi tatizo la mgao wa umeme kumbe halina ufumbuzi.ufumbuz ninao uona mm ni kuing'oa Ccm madarakan

Rais anataka kutuambia kuwa nchi zote zilizokumbwa na ukame africa/dunian Mwaka huu wana mgao wa umeme???hii thinking sijui katoka nayo wap mungu wangu!!!!
 
Back
Top Bottom