Majiji 5 kwa Uzuri Tanzania

Majiji 5 kwa Uzuri Tanzania

Acha urongo mleta mada mbeya ina uzuri gani sasa labda uniambie ule uzuri wa asili wa kijiografia kama milima,ukijani, na vinginevyo lakini sio kiujenzi
 
Nje ya nchi mbali, hajawahi kuvuka nje ya wilaya yake huyo

Ni kweli Tanzani hakuna jiji zuri hata moja bali kuna baadhi ya sehemu/mitaa nzuri/mizuri.

Kigenzo cha kuwa na jiji zuri inatakiwa jiji lote lipimwe ,wajenge miundombinu ya sehemu zote,kusiwe na slums wala mapori,huduma zote za kijamii zipatikane,jiji zuri foleni kama zote,hakuna subway hata moja!
 
Acha urongo mleta mada mbeya ina uzuri gani sasa labda uniambie ule uzuri wa asili wa kijiografia kama milima,ukijani, na vinginevyo lakini sio kiujenzi
Kwa iyo wakazi wake wanakaa kwenye mashimo Kama panya au kwenye vichuguu?
 
Kama Mbeya ni pazuri basi TAnzania hakuna miji mizuri. Mbeya! Pyuuuuuu!
Mbeya ni nzuri kuliko hivyo Vimiji vyenu uchwara,ukipewa picha ya ziwa ngozi au mlima loleza au miteremko ya barabara ya mlima kawetele unaweza Shani uko uswisi au Himalaya nk

Shida yenu hata hamjawahi tembea Tzn hii.

Kwanza Mwanza na Dom kuna uzuri gani hapo
 
Kwa hiyo kumbe kwenye majiji tu ndiyo pazuri?Nikieleza kwamba fedha/uchumi wa mikoa mingine unatumika vibaya/ambezlement ili kuyaremba tu hayo majiji mtabisha?Mimi kama mkulima wa mihogo nasikitika sana.
Lima tu mihogo hakuna namna ndo ushambiwa kuzuri uko
 
Hii hapa ni orodha ya Miji mizuri Tanzania.
1-Dar es Salaam (Mzizima)
Eneo la mkoa ni jiji la Dar es Salaam ambalo ndilo kitovu cha shughuli za biashara (na za utawala, kwa kiasi fulani) nchini Tanzania, na ni kati ya majiji yanayokua haraka zaidi duniani.

Ni km² 1,800 pamoja na visiwa vidogo 8 na eneo la bahari kati ya pwani na visiwa hivi. Eneo la nchi kavu pekee ni km² 1,393.

Kuna wilaya tano: Kinondoni (wakazi 1,775,049), Ilala (wakazi 1,220,611) na Temeke (wakazi 1,368,881) ambazo zimeongezewa Kigamboni na Ubungo. Kila moja inaangaliwa kama mji. Takwimu hizi ni za mwaka 2012, kwa ujumla idadi ya wakazi ilikuwa 4,364,541.

Wakazi asili wa eneo la mkoa walikuwa Wazaramo pamoja na makabila madogo kama vile Wandengereko na Wakwere. Kutokana na kukua na kupanuka kwa jiji kuna makabila yote ya Tanzania.

2-Mwanza (Rocky city)
Jiji la Mwanza ni mji nchini Tanzania ambao ni makao makuu ya Mkoa wa Mwanza. Mji upo kando la ziwa Viktoria Nyanza Kulingana na sensa ya mwaka 2002 idadi ya wakazi wake ilihesabiwa kuwa 378,327 (ukijumlisha wakazi wa Wilaya ya Nyamagana na sehemu za Wilaya ya Ilemela).

3-Arusha (A city)
Arusha ni jiji la kaskazini mwa Tanzania na makao makuu ya Mkoa wa Arusha. Kiutawala eneo la jiji la Arusha ni sawa na eneo la Wilaya ya Arusha Mjini. Katika sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 416,442

4-Dodoma (Idodomya)
Ilitangazwa kuwa mji mkuu wa Tanzania mwaka 1973, lakini mnamo tarehe 26 Aprili 2018 katika maadhimisho ya miaka 54 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya tano John Magufuli aliupandisha hadhi na kutangaza rasmi kuwa Dodoma ni Jiji. Serikali ya awamu ya tano ilihamia rasmi jijini Dodoma mwaka 2016.

Jiji hili pia ni makao makuu ya Mkoa wa Dodoma na eneo lake linahesabiwa kama Wilaya ya Dodoma .

Eneo la mji liko mita 1135 juu ya usawa wa bahari UB. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, mji wa Dodoma ulikuwa na wakazi wapatao 410,956 waishio humo.

5-Mbeya (Green city)
Mbeya ni mji wa nne kwa ukubwa nchini Tanzania. Idadi ya wakazi imehesabiwa kuwa 385,279 katika sensa ya mwaka 2012. Wengine 300,000 hivi wanaishi katika mazingira karibu na Mbeya mjini.

Kiasili Mbeya ilikuwa eneo la Wasafwa. Siku hizi sehemu kubwa ya wakazi wanaweza kuwa mchanganyiko wa Wasafwa pamoja na makabila ya Wanyakyusa kutoka wilaya za Rungwe na Kyela, Wanyiha kutoka Mbozi, Wandali kutoka Ileje na Wakinga kutoka Makete.

Tazama zaidi video ya mandhari ya majiji hayo.


Mwanza iwe Na 3. Arusha ipande Na. 2, tenda haki!!
 
Mbeya ni nzuri kuliko hivyo Vimiji vyenu uchwara,ukipewa picha ya ziwa ngozi au mlima loleza au miteremko ya barabara ya mlima kawetele unaweza Shani uko uswisi au Himalaya nk

Shida yenu hata hamjawahi tembea Tzn hii.

Kwanza Mwanza na Dom kuna uzuri gani hapo
Sure, kwa uzuri wa kimandhari hakuna hapo mji wa kuufikia mji wetu wa Mbeya.
 
Tanzania Hakuna jiji zuri hata moja.

Tembeeni hata hapo Harare Zimbabwe uone Kama hutakuja kuufuta huu Uzi.

Eti mbeya ni Jiji, Dodoma ni jiji.[emoji3]
Ukisema ivo
Atakuja mtu kukutajia mji zaidi ya huo Harare
 
Shida inakuja pale wanapoweka mahaba na kusifia mikoa wanayotoka

Ni kuwaacha tu
Hilo ndio tatizo mkuu..

Shida kubwa ya Tanzania Ni mipango miji , nchi nzima ni takataka. Tuko zero. Nilikuwa naisikia Mwanza na sifa kila siku.

Siku nimefika niliingiwa na simanzi kuwa hi nchi haina watu wa City Plan? ... Mji uko hovyo. Kwenye makazi ya watu ni slams tupu. Milimani kwenye Good View kumejengwa vijumba jumba.

TANZANIA miji haitofautian Hakuna mji wa kumcheka mwingine yote ni sawa. Na tatizo kubwa Ni mipango miji. Haijulikani wapi Ni makazi ya watu na wapi Ni sehemu za biashara . Kwenye makazi watu pengine hakuna hata Barabara za mitaani na Kama zipo ni nyembamba hata Gari 2 hazipishani.

Kwenye makazi ya watu watu wameweka mafrem kila nyumba. Jamani tutembeeni hata hapo Malabo tuone majiji yanavyokuwa. Mji umepangwa Hadi unatamani ingemuwa bongo.


Tanzania kwakweli raia wake Wana hela na wanajenga ile mbaya ila wanaangushwa na serikali yao haipangi miji. Ndio maana unakuta mtu ana mjemgo wa maana katikati ya slam. Au ana jengo la maana sehemu haina hata mfumo wa majitaka.
 
Uzuri?Katika yepi?Majengo mazuri,watu wazuri,maisha maziri,hali ya hewa nzuri,uchumi mzuri "unaoshikika" ,rasilimali nzuri au kipi hasa unajikita?Au ndiyo Wanyaturu wanavyosema ..."the beauty is in the eyes"...?
Hata mimi nilitaka kumuuliza swali kama hili.
Anaposema uzuri anamaanisha nini? Mimi binafsi nimefika kwenye miji yote hiyo aliyoitaja na sijaona "uzuri" wowote wa hii miji.
Miji yote hii imepangwa vibaya, nyumba zimejengwa kiholela, uchafu umetapakaa kila mahali, miundo mbinu mibovu yaani kwa kifupi tu hakuna mji unovutia hapa Tanzania.
 
Back
Top Bottom