Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Habari wakuu.
Kama mnakumbuka niliwahi kuandika uzi juu ya ndoto yangu ya kuanzisha Lodge na nikaumba ushauri juu ya biashara hiyo ambayo Kwa mapenzi ya Mungu mwakani nitakua tayari kuifanya InshaAllah🙏🏼.
Sasa ktk harakati zangu za kufanya research juu ya biashara hii kuna mtu akanishauri nipite pite ktk Lodge kadhaa nione wenzangu wanavyofanya na akanishauri ktk Lodge nitakazopitia nisiache kufika ktk Lodge inayoitwa ALAFAYA iliyoko VIKINDU.
Nikamwambia why niende mbali kote huko?Akasema wewe nenda amini utajifunza mengi.Siku ya siku nikaenda hapo ALAFAYA nikajifanya mteja.Nilipofika hapo nikaelewa kwanini jamaa yangu alisisitiza niende hapo.
Ni ka Lodge fulani hivi kadogo dogo kenye mazingira tulivu na yenye kuvutia sana ndani na nje.Naweza kusema kwa wilaya nzima ya mkuranga hakuna Lodge Classic kama ile.Vipo vingi nimeiga na kuvifanya vizuri zaidi yao😀😀
Tuachane na hayo.Kilichonishangaza hadi kuandika huu uzi ni majina ya vyumba vya ile Lodge.Nimezoea kuona watu wakiandika room numbers au majina ya mikoa au wanyama ila huyu mwenye hii Lodge sijui aliwaza nini hadi akaweka haya majina.
Hili la haya majina sina uhakika kama ni la kuiga bado linanifikirisha😀😀😀
Jioneeni wenyewe kwenye picha wakuu🙃⬇️⬇️View attachment 3153877View attachment 3153878View attachment 3153879View attachment 3153880View attachment 3153882View attachment 3153889View attachment 3153890
Kaniibia bandiko langu aisee .View attachment 3155057
Huyu amekuibia au huyu ni ww kule X?
Uungwana angekupa credit zako au ht acknowledge basi JF km source!...
Nasisitiza,"BABU UPEWE" Wajukuu lazima wakutunze babu bado jamii inahitaji busara zakoNinavyotengwa, yaani hata kupewa kwa kuonjeshwa sipewi Mjukuu 🙌
Hapa baridi litaniua Babu yenu
Mjukuu hebu chukua ile wine yako uipendayo pamoja na mdudu kilo Kwa bill yanguNasisitiza,"BABU UPEWE" Wajukuu lazima wakutunze babu bado jamii inahitaji busara zako
😀😀😀Mwanaume unapewa chumba, unaambiwa nenda kalale chumba Cha Zuchu.....😂😂😂..... Very interesting... Na usikute kuna chumba Huwa kinagombaniwa.... 😂😂😂Eidha Zari au Zuchu.....😂😂😂