Majina ya Kiafrika mbioni kutoweka

Majina ya Kiafrika mbioni kutoweka

Mnyakyusa unakataa kumuita mwanao Gwamaka au Lusajo. Unaona ni la mizimu ili tu umuite Sean Roberts?

Unakataa kumuita mtoto Mwamba ila unamuita Peter, ambayo kimsingi ina maana ileile.
 
Ndugu wanaJF,
Kufikia mwisho wa karne ya 21, majina kama Masawe, Otieno, Gwamaka, Kamugisha, Masanja n.k yatafutika nchini kwetu.

Imekuwa nadra mno kukuta mtanzania mwenye majina matatu, yote yenye asili ya kabila lake, au hata ya makabila ya hapa Tanzania au Afrika kwa ujumla.

Ubantu unaisha. Unailoti unaisha.

Watu wa pwani walishapotezwa kitambo. Wao wengi wao wana majina ya kiarabu tupu.
Wakina Mohammed Said. Hata Surname za kiafrika walishaacha.

Watu wa bara ndiyo walikuwa badobado, lakini nao sasa watoto wao ni wakina Brian McDonald, Humphrey Jr. Scott au Natasha-Rose Leonard.

Hata wazungu, wachina, wahindi na waarabu wanatushangaa sana.

Wao hawana huu ujinga.

Hakuna mzungu anaitwa Manka, hakuna muarabu anaitwa Mabula wala mchina anayeitwa Mahenge.

Ngugi wa Thiong'o huyaita haya majina colonial tags.
Yeye aliachana na colonial tag yake 'James' akabaki na Ngugi wa Thiong'o.

Je, waafrika tumeshindwa kuthamini majina ya tamaduni zetu na kuachana na majina ya kigeni?
Mfano Mimi Charles Joachim Elias manoni

Hapo ni kupambana surname origin isipotee
Mtoto wangu nimemwita Brian Charles manoni instead of Brian Charles Joachim Elias manoni.

Surname yetu ya manoni haito potea..

Majina ni ya kubuni 😅
 
Ndugu wanaJF,
Kufikia mwisho wa karne ya 21, majina kama Masawe, Otieno, Gwamaka, Kamugisha, Masanja n.k yatafutika nchini kwetu.

Imekuwa nadra mno kukuta mtanzania mwenye majina matatu, yote yenye asili ya kabila lake, au hata ya makabila ya hapa Tanzania au Afrika kwa ujumla.

Ubantu unaisha. Unailoti unaisha.

Watu wa pwani walishapotezwa kitambo. Wao wengi wao wana majina ya kiarabu tupu.
Wakina Mohammed Said. Hata Surname za kiafrika walishaacha.

Watu wa bara ndiyo walikuwa badobado, lakini nao sasa watoto wao ni wakina Brian McDonald, Humphrey Jr. Scott au Natasha-Rose Leonard.

Hata wazungu, wachina, wahindi na waarabu wanatushangaa sana.

Wao hawana huu ujinga.

Hakuna mzungu anaitwa Manka, hakuna muarabu anaitwa Mabula wala mchina anayeitwa Mahenge.

Ngugi wa Thiong'o huyaita haya majina colonial tags.
Yeye aliachana na colonial tag yake 'James' akabaki na Ngugi wa Thiong'o.

Je, waafrika tumeshindwa kuthamini majina ya tamaduni zetu na kuachana na majina ya kigeni?
Utumwa wa kifikra mbaya sana aseee.
 
Pale Makumbusho ya vita ya Majimaji Songea, mashujaa walionyongwa na wajerumani tarehe 27. 02. 1906 ni kama vile:

1. Mfuta Mkuzo Gama
2. Njoroza Mbamba Mbano
3. Mgendera Gama
4. Mahengo na wengine wengi sana.

Lakini leo hii, mjukuu wa Mbano au Gama anaona Mkuzo au Mbamba ni jina baya la mizimu.
Bora aitwe Peter au John, majina kama ya wale walionyonga babu zake kwa halaiki, ambao pia washakufa na ni mizimu vilevile.

Upumbavu ni kipaji.
 
Urithi wa kwanza uliobora kwa mtoto ni jina...

Wewe mwite Mashaka, Masumbuko, Gwandumi, Mayala au Anyosise, Kamala au Rugaba au Manka hakuna Shida.

Mwingine atamwita Happy au Joy,Marry, Joshua sawa tu...

Ila kumbuka Urithi ulio bora wa kwanza ni jina.
 
Urithi wa kwanza uliobora kwa mtoto ni jina...

Wewe mwite Mashaka, Masumbuko, Gwandumi, Mayala au Anyosise, Kamala au Rugaba au Manka hakuna Shida.

Mwingine atamwita Happy au Joy,Marry, Joshua sawa tu...

Ila kumbuka Urithi ulio bora wa kwanza ni jina.
Mkuu, unadhani kwanini jamii zingine hazitumii majina yetu ya kiafrika, ila sisi tunatumia yao?
 
Mkuu, unadhani kwanini jamii zingine hazitumii majina yetu ya kiafrika, ila sisi tunatumia yao?
Hata Lugha zetu hawazijui

Siku wakianza kutumia Lugha itakuwa rahisi kutumia majina.

Unawezaje kumrithisha mtoto wako kipenzi zawqdi yake ya kwanza kwa kitu usichojua maana yake?
 
Hata Lugha zetu hawazijui

Siku wakianza kutumia Lugha itakuwa rahisi kutumia majina.

Unawezaje kumrithisha mtoto wako kipenzi zawqdi yake ya kwanza kwa kitu usichojua maana yake?
Sasa maana yake si unamuambia tu.

Hata ukimuita Mary, hawezi kujua maana ya Mary ni nini mpaka umueleze.
Kwanini usimpe jina la asili yake Kisha umwambie maana yake?
 
Back
Top Bottom