Majina ya Kinyakyusa na maana zake, twenzetu hapa

Majina ya Kinyakyusa na maana zake, twenzetu hapa

Mwakibinga,Mwakasege na Mwabulambo

Kiasili majina ya pili ya wanyakyusya ni tofauti sana na taratibu za kizungu.

Wanyakyusya hawarithi majina ya baba zao, wanaume wanarithi majina ya mashangazi, wana wanawake wanarithi majina wa mabibi zao upande wa baba. Tofauti tu ni kwamba wanaume wanawekewa "mwa" mbele ya hilo jina. Kwahiyo kama wewe ni mwanaume na dada yako anaitwa Ms Jane Kalinga, watoto zako wa kiume wataitwa Mr John Mwakalinga. Na kama mama yao alikuwa anaitwa Ms Anna Bulambo, basi watoto zako wa kike wataitwa Ms Amina Bulambo(bibi).

Na kwasababu wewe kama baba ulipata jina kwa shangazi yako sio ajabu kukuta baba surname anaitwa MwaAbc, mtoto wa kiume anaitwa surname MwaXyz na binti yako anaitwa surname anaitwa egh. Sema siku hizi watu hawafuati hizi taratibu, ndio unakuta Baba, Kijana wake wa kiume na wa kike wana surname zinafanana.

Kwanini waliweka utaratibu huo, nimewahi ambiwa kuwa hawakutaka majina ya watoto wao wa kike yapotee. Na ukiangalia, ni majina ya kiume ndio yanapotea, ya wa kike kwenye familia yanabebwa either ya watoto wa kiume(shangazi) au wa kike (bibi).
Si kweli uliyoandika,kurithi majina ya sijui kwa shangazi au kwa baba au kwa mama ni hiari ya mtu mwenyewe,wale wanaotumia sana majina ya upande wa mama ni wale ambao wengi wao wamezaliwa kwenye mitala yaani kwa mfano machifu walikuwa na wake wengi kwa hiyo kutofautisha kuwa huyu anatoka kwa mama fulani wengi wao pamoja na kutumia jina la baba yao lakini mwishowe waliongoza majina ya upande wa mama zao badala ya kuongoza majina ya upande wa ukoo wa baba yao,kwa mfano utakuta kwa machifu wa zamani kama chifu Koroso,Mwakyembe watoto wao mbali na kutumia majina ya Korosso tu na ukoo wa Korosso pia walitumia majina ya koo za mama zao
 
Si kweli uliyoandika,kurithi majina ya sijui kwa shangazi au kwa baba au kwa mama ni hiari ya mtu mwenyewe,wale wanaotumia sana majina ya upande wa mama ni wale ambao wengi wao wamezaliwa kwenye mitala yaani kwa mfano machifu walikuwa na wake wengi kwa hiyo kutofautisha kuwa huyu anatoka kwa mama fulani wengi wao pamoja na kutumia jina la baba yao lakini mwishowe waliongoza majina ya upande wa mama zao badala ya kuongoza majina ya upande wa ukoo wa baba yao,kwa mfano utakuta kwa machifu wa zamani kama chifu Koroso,Mwakyembe watoto wao mbali na kutumia majina ya Korosso tu na ukoo wa Korosso pia walitumia majina ya koo za mama zao
Sijui kuhusu hili la majina kuwa la machifu peke yao. Lakini nimeona utaratibu huu wa majina mpaka kwenye familia za kawaida, maybe am wrong, lakini hata familia za kawaida ninazozijua nimeona hii
 
Back
Top Bottom