Majirani wamemripoti jamaa kituo cha polisi kisa kazi yake haijulikani! Sasa anadai Milioni 500 kwa kuletewa usumbufu

Majirani wamemripoti jamaa kituo cha polisi kisa kazi yake haijulikani! Sasa anadai Milioni 500 kwa kuletewa usumbufu

Na si kila mtu afagie kwake na kukondeshwa na yake,sasa pain ni ya nini mtu akiwa na maisha mazuri na kazi yake hujui,kwani lazima majirani wajue kazi yako?
Itabidi wamemlipa fidia yes,mjini kila mtu aishi kivyake,kwani yeye balozi, mtendaji au mbunge ndio wajue kazi yake?

Hiyo time ya kuchunguza maisha mtu wanatoa wapi?
 
me sijaliona tatizo la majirani ujue.
Majirani ndiyo wana makosa,maana wao ndiyo walitakiwa watowe ushahidi kua jamaa ni muhalifu,tena siyo ushahidi wa maneno matupu! Ukimshutumu mtu toa na ushahidi wa shutuma zako, kuishi maisha mazuri siyo dalili za kua muhalifu!!
 
Majirani ndiyo wana makosa,maana wao ndiyo walitakiwa watowe ushahidi kua jamaa ni muhalifu,tena siyo ushahidi wa maneno matupu! Ukimshutumu mtu toa na ushahidi wa shutuma zako, kuishi maisha mazuri siyo dalili za kua muhalifu!!
Aisee nimejifunza vitu vingine sio vya kukurupuka
 
Wakuu Kuna jamaa hapa mtaani alikua anahisiwa anafanya shuguli haramu sababu anamaisha mazuri ila kazi yake haijulikani

Sasa Kuna majirani wawili wamemripoti polisi akaja kukamatwa. Sasa akiwa huko polisi akasema yeye kazi yake ni kubeti na analipa Kodi Kwa serikali kupitia mikeka yake anayoshinda na kweli kaonyesha mikeka anakula mamilioni ya pesa ni aina ya watu wanaoweka pesa nyingi sana kwenye mechi.

Sasa kingine kaenda mahakamani anawashitaki majirani zake hao wawili Kwa kosa la kumdhalilisha na kumpotezea mda wa kufanya mambo yake ya msingi na anadai fidia million 500 na ana mawakili wake kabisa wa 3

Hivi hii kesi anaweza kushinda huyu jamaa ishu ipo serious sana
Hizi ni tabia za kizamani za Kikomunisti.

Kwa tuliojisumbua kusomasoma vitabu mbalimbaki vya muhimu tumezisoma tabia hizi kama sehemu ya police state katika maandiko ya mshindi wa nishani ya Nobel ya Literature ya mwaka 1970, Mrusi Aleksandr Solzhenitsyn "The Gulag Archipelago".

Mimi ninapoishi ningekuwa na majirani wajinga hivi, ningesumbuliwa sana, kwa sababu kuna kipindi nakaa miaka hata mitano nafanya kazi zangu kutika nyumbani tu. Naongoza project ya kutuma watu South America, North America, Europe, Asia, Africa, Australia, kutoka nyumbani.
 
D

Duuh hatari mkuu
serously best,ilikuwa 2022,,,,waliona nina gari,nina nyumba na shamba hapohapo home [PUGU],,nafuga nguruwe,kuku na mabata kibao,nauza maji na ninalima mihogo,,,huku nikitoka asubui kwenda job nakurudi usiku,watoto wanasoma boarding,,nalamba MAJI YA MENDE dailly......da!! nikaitwa serikali za mtaa kujieleza,,,mimi niliwaambia sina cha kujieleza,nyie nichunguzeni,mkinikuta nina hatia nipelekeni mahakamani,,,,,kwa sasa majirani wananiogopa balaa!!!
 
kwa hiyo jirani kutoa ripoti polisi ni vibaya?haya incase ikiwa jamaa alikuwa drugs dealer?

mahakama haitatenda haki,kwani hiyo ni kawaida kuhisi.
hisia sio sababu za kumripot mtu , bali ushaidi pia .

kila mashitaka ujue ukishindwa kuna fidia pia za usumbuf zipo
 
Kwa kupata mamilioni Kwa mbinu anayotumia Kwa masikini ni ngumu sababu jamaa anabeti mechi Moja anaweka hata million 10
Tuanze kwanza na mtaji wa kubeti alipata wapi!? Maana usijisifie una nyumba nyingi za kupangisha,kumbe umetakatisha pesa kupitia hizo nyumba!!
 
Tuanze kwanza na mtaji wa kubeti alipata wapi!? Maana usijisifie una nyumba nyingi za kupangisha,kumbe umetakatisha pesa kupitia hizo nyumba!!
Hayo Sasa maisha binafsi ndio hayo mwisho wa siku unashitakiwa sababu ya vitu kama hivi unaulizaje mtu mtaji wa kubet amepata wapi maswali haya ndio yamewaponza majirani wenzangu maana ukimuuliza akikutajia halafu ikawa kapata kihalali je utafidia mda aliopoteza kukaa na wewe Ili akuelezee
 
Kumdhalilisha kwa kutoa taarifa polisi ? Ametoa taarifa polisi au ameandika kwenye magazeti au kuwatangazia watu ? (angetangazia jamii hio ndio ingekuwa slander) ila kama ametoa taarifa kwamba jamaa simuelewi ni kwamba amewapa kazi polisi wafanye uchunguzi (sio wamshike) bali wachunguze sasa kama walimshika bila uchunguzi wa kina huo ni uzembe wa polisi sio mtoa taarifa..., vilevile polisi wana haki ya kuja kuchunguza kuna nini kinaendelea kama wana vibali maalumu ni kama ukisimamishwa kwenye gari na kuombwa leseni yako haimaanishi wamekwambia hauna leseni ?
unahisi jamaa mpuuz kwenda mahakamba bila kuwepo vitendo au lugha mbofu kwake ? watz tunapenda kuishia shallow in thinking

mtu ashitaki kisa kuhojiwa tu ? kwamba hajui kuwa ni wajibu wa polisi kujuwa chanzo cha mapato cha mkazi wao

NB ; Majiran kuna namna walifanya kabla na hata walipomfikisha polisi
 
Hayo Sasa maisha binafsi ndio hayo mwisho wa siku unashitakiwa sababu ya vitu kama hivi unaulizaje mtu mtaji wa kubet amepata wapi maswali haya ndio yamewaponza majirani wenzangu maana ukimuuliza akikutajia halafu ikawa kapata kihalali je utafidia mda aliopoteza kukaa na wewe Ili akuelezee
Yaani umuulize za kubetia kapata wapi,nae atauliza Wewe kama nani?!
 
Naile

d. Labda hao majirani zake amewakadiria na kuona wepesi. Lkn nje na hapo ajipange hiyo hela ya kubeti kulipa gharama za kesi baadae, kama hawana wakili waweke tu mlipaji yupo huyo huyo
kwamba jiran anaejiweza angeaza fuatilia maisha ya jiran ? hesabu nyepesi kbs
 
Hao majirani wanamiliki hizo nyumba wanazoishi hapo mtaani au ni wapangaji tu? Maana naskia harufu ya Mali zisizohamishika, mwamba anaenda kuwa landlord wa mtaa.
 
Hizi ni tabia za kizamani za Kikomunisti.

Kwa tuliojisumbua kusomasoma vitabu mbalimbaki vya muhimu tumezisoma tabia hizi kama sehemu ya police state katika maandiko ya mshindi wa nishani ya Nobel ya Literature ya mwaka 1970, Mrusi Aleksandr Solzhenitsyn "The Gulag Archipelago".

Mimi ninapoishi ningekuwa na majirani wajinga hivi, ningesumbuliwa sana, kwa sababu kuna kipindi nakaa miaka hata mitano nafanya kazi zangu kutika nyumbani tu. Naongoza project ya kutuma watu South America, North America, Europe, Asia, Africa, Australia, kutoka nyumbani.
Mi nazani wewe wangekuzushia la kukwepa kodi na kuhujumu uchumu au kutakatisha pesa, yaani wewe ndio ungeenda kutoa hela ndeeeeefu ili kutoka lupango.
 
Hao majirani wanamiliki hizo nyumba wanazoishi hapo mtaani au ni wapangaji tu? Maana naskia harufu ya Mali zisizohamishika, mwamba anaenda kuwa landlord wa mtaa.
Ni za kwao wanamiliki mkuu
 
serously best,ilikuwa 2022,,,,waliona nina gari,nina nyumba na shamba hapohapo home [PUGU],,nafuga nguruwe,kuku na mabata kibao,nauza maji na ninalima mihogo,,,huku nikitoka asubui kwenda job nakurudi usiku,watoto wanasoma boarding,,nalamba MAJI YA MENDE dailly......da!! nikaitwa serikali za mtaa kujieleza,,,mimi niliwaambia sina cha kujieleza,nyie nichunguzeni,mkinikuta nina hatia nipelekeni mahakamani,,,,,kwa sasa majirani wananiogopa balaa!!!
Actually shughuli nyingine zina trade secrets na mtu kukutajia shughuli yake unaweza kumgeza na kumharibia nafasi yake ya kupata kipato.

Kwa msingi huo, habari nzima ya kumtaka mtu ajieleze shughuli yake ni uonevu.

Kama unamshuku mtu, mchunguze mpaka upate makosa, halafu mshitaki kwa makosa hayo.

Kuna watu wana uwezo wa kuishi kwa kuwekeza pesa kwenye masoko ya mitaji na hisa tu, pesa zinawafanyia kazi wao hawahitaji kufanya kazi.

Kuna watu wanafanya kazi kwenye mitandao, unaweza kuona mtu hatoki nje, kumbe anafanya kazi mitandaoni, analipwa mishahara ya kimataifa. Mimi kuna rafiki yangu anafanya kazi remotely online huku Marekani, kuna wakati anaona hana haja ya kuwa Marekani anarudi Tanzania anafanya kazi mtandaoni mapaka miezi 6.

Sasa mtu kama huyo ukimshangaa kwamba hatoki nje kwenda kazini, utamshangaa kwa ushamba na ujima tu.
 
Back
Top Bottom