Makabila yatakayoendelea kutegemea elimu iwakomboe kiuchumi(ajira) yatashuka kimaendeleo

Makabila yatakayoendelea kutegemea elimu iwakomboe kiuchumi(ajira) yatashuka kimaendeleo

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Elimu ni muhimu na wala sio ya kubezwa, Lengo kuu la elimu huwa ni kumkomboa mtu kifikra alafu ndio yanafata mengine, Kwa bahati mbaya hapa nchini jamii nyingi hasa makabila wameigeuza elimu iwe kwajili ya kuwatajirosha kupitia ajira. njia nyingine kama biashara wanapuuza.


zamani makabila machache sanasana wahaya na wachaga waliwekea kipaumbele elimu ya kusoma shuleni kwa lengo kuu la ajira na kiukweli waliweza kujazana sana kwenye ajira safi na kujikomboa kiuchumi, Hali hii pengine ilileta tafsiri tofauti ya ule msemo kwamba elimu ni ufunguo wa maisha kwa kudhani maisha ni kuajiriwa na kuanza kubonda mshahara.


makabila mengine nayo yakaanza kuingilia hii keki, makabila kama wasukuma, wanyakyusa, wapare, wakerewe, n.k. nao wakaanza kuona elimu ndio dili, watoto wakaanza kuwekewa mkazo kusoma, shule zilianza kujengwa, n.k. hatimae nao wakaingia kwenye mgao wa ile keki ya wachache hasa katika ajira zilizohitaji elimu za juu.

Kwa sasa keki hii imekuwa kama ya wote vile maana elimu imesambaa sana, kila kata kuna shule, shule binafsi zipo kibao, vyuo vipo vingi, elimu imerahisishwa sana siku hizi kuna vitabu vya mitihani iliyopota, notes zilizorahisishwa, n.k ufaulu umepanda sana kiasi kwamba siku hizi form 4 na 6 shule nyingi mpaka huko pemba na mikoa ya Lindi unakuta shule haina division 4 wala 0, wanafunzi kibao wanafaulu, vijana wengi sana kutoka kila kona ya nchi kwa sasa wana degree zao na huu ni mwanzo tu.


Mgao umesambaa sana kwa sasa aisee, Sehemu ambazo zamani ulikuta makabila machache yamerundikana siku hizi utawakuta karibu kila kabila tofauti na zamani, Ni kawaida pia kukuta sehemu haina watu wa makabila yaliyojazana zamani ila ukakuta kuna watu wengine wengi wa makabila mengine,.

Elimu kuwa sehemu ya kutoboa tundu lake linazidi kuwa dogo.

Kwa sasa Biashara ndio mpango, tena iwe ile ya kuinuana, huku kwenye biashara mkiinuana mtafika mbali sana, hizo elimu leo mhaya anastaafu, nafasi anaichukua mfipa wa sumbawanga,, kwenye biashara baba anastaafu mtoto wake anapewa kiti.

Kuhusu elimu kwenye biashara inayohitajika huwa inahitajika ya kawaida tu, cha muhimu ni kuiheshimu biashara, wakinga elimu zao za kawaida tu lakini ona maajabu wanayafanya, wapemba wao elimu ni janga lakini ona walivyotusua kwenye biashara, tuliobahatika kusoma na waarabu ama wasomali tumeona wengi wanaishia darasa la 7 au form 4 lakini leo hii sio wenzetu kiuchumi,,, hata wachaga nao walijitafakari mapema wakaona waingie kwenye biashara na kiukweli wametoboa si mchezo.
 
Elimu haijawahi kuwa na mbadala, cha msingi ni kuboresha mitaala na vijana wetu wasome elimu ambayo watahitimu wakiwa na ujuzi na siyo makaratasi tu.

Nikikupa leo mtaji wa biashara kama huna kipaji hicho mtaji utafilisika, ila nikikugharamia elimu ukapata ujuzi una option mbili za kuajiliwa au kujiajili, na ukiweza kujiajili indirect hiyo tayari ni biashara yako unakuwa mkubwa hadi unaitwa mkurugenzi na wewe unaajiri watu baadaye.
 
Tatizo letu bado ni lile lile. Bado hatujajua lengo kuu la elimu yetu ni nini. Elimu tumeidogosha na kuipa jukumu ambalo siyo lake - kuwatajirisha waipatayo!

Duniani kote lengo-mama la elimu ni kuwafanya waipatayo kuyaelewa vizuri mazingira yao na kuwafanya waishi huku wakijua mifumo inayoendesha maisha yao na malimwengu. Wenzetu wameshaondokana na hizi ngonjera za kwamba kila msomi ni lazima atajirike. Ndo maana utakuta maprofesa wao wengine hata magari hawana na wanakuja kazini kwa baisikeli. Ila wanajua jukumu lao ni nini. Na jamii inawaheshimu sana.

Elimu ina umuhimu wake na ina jukumu kubwa sana katika kuleta maendeleo ya jumla kwa waipatayo. Lakini kwa vile lengo ni kutaka kila msomi atajirike, hapo ndipo elimu yetu inakosa maana kabisa na dhana hii potofu ndiyo inachochea rushwa, ufisadi na maovu ya kila aina katika jamii wasomi wetu wakichacharika ili watajirike wasije wakachekwa kuwa elimu yao haijawaendeleza.

Kama lengo la elimu ni utajiri elimu ya fomu foo inatosha. Baada ya hapo mtu apatiwe mtaji aingie mtaani. Madaktari, walimu, wauguzi, wahandisi, wanasheria...na kada zinginezo-hawa tutawapata kutoka katika jamii ambazo hazipendi maendeleo (isomeke utajiri). Sad!
 
Ni kama zamani ukiwa na gari lako utaendesha kwa uhuru mkubwa sana, ila siku hizi wenye magari ni wengi sana, haupo peke yako na kuna foleni.

Hapo zamani makabila machache sana yalikuwa yana access ama / na uwezo mkubwa wa kusoma shuleni na hatimae kutumia elimu zao kurundikana katika ajira zilizohitaji elimu hasa za vyuoni,

Waliozifaidi sana hizi ajira walikuwa ni wahaya na wachaga.

Kadri miaka inavyozidi kwenda makabila mengine nayo yakaanza kuingilia hii keki, makabila kama wasukuma, wanyakyusa, wapare, wakerewe, n.k. nao wakaanza kuona elimu ndio dili, watoto wakaanza kuwekewa mkazo kusoma, shule zilianza kujengwa, n.k. hatimae nao wakaingia kwenye mgao wa ile keki ya wachache hasa katika ajira zilizohitaji elimu za juu.

Mwamko wa elimu ukazidi kuwa mkubwa kwa makabila mengi zaidi na kusambaa zaidi mpaka vijijini huko ndani ndani, ile keki iliyokuwa ya wachache ikaanza kumegwa na watu wengi zaidi,

Na mpaka sasa tulipo, Eimu imerahisishwa sana kiasi kwamba siku hizi hata matokeo ya form 4 na 6 ni kawaida sana kukuta shule nyingi hazina division 4 wala 0, hii ni mpaka huko Pemba na mikoa ya Lindi ambayo licha ya kuburuza mikia unakuta siku hizi kuna wanafunzi wanafaulu.

Mgao uesambaa sana kwa sasa aisee, Sehemu ambazo zamani ulikuta makabila machache yamerundikana siku hizi utawakuta karibu kila kabila tofauti na zamani, Ni kawaida pia kukuta sehemu haina watu wa makabila yaliyojazana zamani ila ukakuta kuna watu wengine wengi wa makabila mengine,.

Elimu kuwa sehemu ya kutoboa tundu lake linazidi kuwa dogo.

Kwa sasa Biashara ndio mpango, tena iwe ile ya kuinuana kama wachaga, wapemba na wakinga, wachaga nadhani tangu zamani walishaona mbali wakaamua kuruka na kwenye biashara tofauti na makabila mengine, Kimbembe kipo kwa waliokuwa wanategemea elimu pekee, mzee anastaafu na ajira hairithishwi na ndipo penye shida hapo.
Elimu ni muhimu kwa mkulima, mfanyabiashara, na yeyote anayeitwa binadamu anayeishi katika nyanja yoyote ya kimaisha.
Elimu ni haki ya binadamu!
 
Tatizo letu bado ni lile lile. Bado hatujajua lengo kuu la elimu yetu ni nini. Elimu tumeidogosha na kuipa jukumu ambalo siyo lake - kuwatajirisha waipatayo!

Duniani kote lengo-mama la elimu ni kuwafanya waipatayo kuyaelewa vizuri mazingira yao na kuwafanya waishi huku wakijua mifumo inayoendesha maisha yao na malimwengu. Wenzetu wameshaondokana na hizi ngonjera za kwamba kila msomi ni lazima atajirike. Ndo maana utakuta maprofesa wao wengine hata magari hawana na wanakuja kazini kwa baisikeli. Ila wanajua jukumu lao ni nini. Na jamii inawaheshimu sana.

Elimu ina umuhimu wake na ina jukumu kubwa sana katika kuleta maendeleo ya jumla kwa waipatayo. Lakini kwa vile lengo ni kutaka kila msomi atajirike, hapo ndipo elimu yetu inakosa maana kabisa na dhana hii potofu ndiyo inachochea rushwa, ufisadi na maovu ya kila aina katika jamii wasomi wetu wakichacharika ili watajirike wasije wakachekwa kuwa elimu yao haijawaendeleza.

Kama lengo la elimu ni utajiri elimu ya fomu foo inatosha. Baada ya hapo mtu apatiwe mtaji aingie mtaani. Madaktari, walimu, wauguzi, wahandisi, wanasheria...na kada zinginezo-hawa tutawapata katika jamii ambazo hazipendi maendeleo (isomeke utajiri). Sad!
Swadakta!
 
Tatizo letu bado ni lile lile. Bado hatujajua lengo kuu la elimu yetu ni nini. Elimu tumeidogosha na kuipa jukumu ambalo siyo lake - kuwatajirisha waipatayo!

Duniani kote lengo-mama la elimu ni kuwafanya waipatayo kuyaelewa vizuri mazingira yao na kuwafanya waishi huku wakijua mifumo inayoendesha maisha yao na malimwengu. Wenzetu wameshaondokana na hizi ngonjera za kwamba kila msomi ni lazima atajirike. Ndo maana utakuta maprofesa wao wengine hata magari hawana na wanakuja kazini kwa baisikeli. Ila wanajua jukumu lao ni nini. Na jamii inawaheshimu sana.

Elimu ina umuhimu wake na ina jukumu kubwa sana katika kuleta maendeleo ya jumla kwa waipatayo. Lakini kwa vile lengo ni kutaka kila msomi atajirike, hapo ndipo elimu yetu inakosa maana kabisa na dhana hii potofu ndiyo inachochea rushwa, ufisadi na maovu ya kila aina katika jamii wasomi wetu wakichacharika ili watajirike wasije wakachekwa kuwa elimu yao haijawaendeleza.

Kama lengo la elimu ni utajiri elimu ya fomu foo inatosha. Baada ya hapo mtu apatiwe mtaji aingie mtaani. Madaktari, walimu, wauguzi, wahandisi, wanasheria...na kada zinginezo-hawa tutawapata katika jamii ambazo hazipendi maendeleo (isomeke utajiri). Sad!
Tatzo n aina ya elimu tuliyonayo yan leo mwaka 2022 bado tunafuata mitaala ya mwaka 70 wakati dunia inabadilika kila kukicha ndo mana n kawaida kukuta graduate wa computer science hajui hata kupga window
 
Wasambaa mzee hawategemei elimu kabisa tangu kuumbwa kwao watu wa biashara tu. Hata wasome biashara ni damuni
 
Elimu haijawahi kuwa na mbadala, cha msingi ni kuboresha mitaala na vijana wetu wasome elimu ambayo watahitimu wakiwa na ujuzi na siyo makaratasi tu.
Vijana wamelenga sana magamba kiasi kwamba wengine wana magamba feki hasa jeshini
 
Elimu haiwezi kuepukika that's y Kuna vitu vya maana msomi anavifanya hata akiwa Hana pesa tofauti na tajiri mwenye pesa

Kifupi, msomi anaweza kuish mazngira tofauti tofaut
Kwa hapa bongo janga la wasomi kupigika na maisha linazidi kuwa kubwa sana, degrees zimekuwa nyingi sana mitaani lakini wasomi wengi wamekariri njia ya kutoboa ni mona tu kuajiriwa.
 
Tatizo letu bado ni lile lile. Bado hatujajua lengo kuu la elimu yetu ni nini. Elimu tumeidogosha na kuipa jukumu ambalo siyo lake - kuwatajirisha waipatayo!

Duniani kote lengo-mama la elimu ni kuwafanya waipatayo kuyaelewa vizuri mazingira yao na kuwafanya waishi huku wakijua mifumo inayoendesha maisha yao na malimwengu. Wenzetu wameshaondokana na hizi ngonjera za kwamba kila msomi ni lazima atajirike. Ndo maana utakuta maprofesa wao wengine hata magari hawana na wanakuja kazini kwa baisikeli. Ila wanajua jukumu lao ni nini. Na jamii inawaheshimu sana.

Elimu ina umuhimu wake na ina jukumu kubwa sana katika kuleta maendeleo ya jumla kwa waipatayo. Lakini kwa vile lengo ni kutaka kila msomi atajirike, hapo ndipo elimu yetu inakosa maana kabisa na dhana hii potofu ndiyo inachochea rushwa, ufisadi na maovu ya kila aina katika jamii wasomi wetu wakichacharika ili watajirike wasije wakachekwa kuwa elimu yao haijawaendeleza.

Kama lengo la elimu ni utajiri elimu ya fomu foo inatosha. Baada ya hapo mtu apatiwe mtaji aingie mtaani. Madaktari, walimu, wauguzi, wahandisi, wanasheria...na kada zinginezo-hawa tutawapata katika jamii ambazo hazipendi maendeleo (isomeke utajiri). Sad!
Ushindani katika elimu unaenda kuwa mzito sana, Leo hii kuna wahaya, wanyakyusa, wasukuma kibao wana degree zao na ajira hawana, nafasi zao wapo watu wa makabila mengine kabisa ambayo hata hatukudhania yatakuja kuelimika... Wachaga wajann
ja waliamua kuingia kwenye biashara wawe wanapiga kote kote.
 
Kumpa mtoto elimu ni muhimu sana ili aweze kuyamudu mazingira yake hata kama ajaajiliwa, ndugu tambua kuwa kuna utofauti mkubwa sana kiutendaji kati ya aliyesoma na mjinga.
 
vipi makabila yanayotegemea ndoa /ushirikina /akili / ibada / etc ili viwatoe kimaisha ni yapi hayo?
 
Kumpa mtoto elimu ni muhimu sana ili aweze kuyamudu mazingira yake hata kama ajaajiliwa, ndugu tambua kuwa kuna utofauti mkubwa sana kiutendaji kati ya aliyesoma na mjinga.
Ndio maana nimeweka wazi hilo mwanzoni kabisa, Vijana wengi siku hizi wakiwa hata na miaka 18 tayari wanakuwa na elimu ya form 4 kuweza kuyamudu mazingira, baada ya hapo wengi huenda form 6 na vyuoni kuanza kujikita kusomea taaluma
 
Hii ni pumba!!

Africans wengi tunashindwa kuendelea kwasababu ya mawazo kama haya, tunahitaji Elimu kujikomboa kifikra kuna watu kama nyiny mnataka elimu kwaajili ya kuajiliwa na hii ni kutokana na uvivu wa vijana wa kiafrika na ndo inapelekea mkalili mpate grades nzuri mkaajiliwe na sio kuelewa mnachofundishwa.
kama kina maxwell, Einstein,Newtons, Tesla e.t.c wangekuwaa na mawazo kama yenu pengine tusingekuwa hata na umeme wala magari dunia hii ya sasa, tungeendelea kuishi kama karne za nyuma.

Elimu sio chombo cha kukufanya uajiriwe ila elimu itumike kuturahisishia maisha
 
Alafu unaongea vitu ambavyo hauna uhakika navyo, eti wameona elimu ina blah blah blah blah wakaamua waende kwa biashara, maelezo haya umeyatoa wapi????
umezungumza maswala ya ukabila ambayo binafsi sioni msingi wake hata kidogo hizo ni statistics za vijiwe vya kahawa zunguka ufanye research uje na takwimu za kueleweka usizungumze akili yako..

Nachukia sana kuona vijana wenzangu wa Taifa langu wanakuwa na mawazo kama haya! Wewe kijana ndo tunakutegemea ujenge Taifa la kesho alafu unakuja na kaulimbiu eti elimu sio muhimu.. "Nonsense"!
 
Alafu unaongea vitu ambavyo hauna uhakika navyo, eti wameona elimu ina blah blah blah blah wakaamua waende kwa biashara, maelezo haya umeyatoa wapi????
umezungumza maswala ya ukabila ambayo binafsi sioni msingi wake hata kidogo hizo ni statistics za vijiwe vya kahawa zunguka ufanye research uje na takwimu za kueleweka usizungumze akili yako..

Nachukia sana kuona vijana wenzangu wa Taifa langu wanakuwa na mawazo kama haya! Wewe kijana ndo tunakutegemea ujenge Taifa la kesho alafu unakuja na kaulimbiu eti elimu sio muhimu.. "Nonsense"!
Umesoma post nzima au umesoma kichwa tu umekimbilia kukocomemt, hakuna sehemu nimeandika elimu sio muhimu, elimu ni muhimu ila isipewe uzito wote wa kummkomboa mtu kiuchumi kupitia ajira ambazo sasa ni kama kubeti
 
Wasambaa mzee hawategemei elimu kabisa tangu kuumbwa kwao watu wa biashara tu. Hata wasome biashara ni damuni
Wasambaa wa wapi acha utani mzee.

Wasambaa ni manamba tangu enzi enzi

Wao kazi za ni za kutumia nguvu lkwa walio mjini wa kijijini ni kilimo.

Ukikuta msambaa kipanga basi ni kipanga kweli kweli.
 
Back
Top Bottom