Makadirio mbao kupaua nyumba vyumba 5 na sebule?

Makadirio mbao kupaua nyumba vyumba 5 na sebule?

Kweli mkuu bati za siku hizi kimeo mkuu mpaka basi, Uganda bado wanatengeneza bati standard kwa wale wanaoishi kanda ya ziwa wameona utofauti wa bati za Uganda na za kwetu hata kama zipo gauge moja. Kikubwa ni kununua bati kwa mtu ambae unaamini anauza bati genuine maana kuna mzigo kibao umechakachuliwa upo sokoni tena hata hizi za South nazo ndio balaa kuna zingine ukipiga bati leo baada ya miezi 6 zinakuwa zimepauka zinakuwa na rangi ya kijivu kwa mbali. (angalau walionunua miaka ya 2009 kushuka chini haya mabati yalikuwa hayajachakachuliwa hivyo ukinunua bati mkuu kuwa makini ikiwezekana nenda kiwandani kabisa kama upo Dar kwani ukiwapa ramani wanakutolea bati refu kuanzia mwanzo mpaka kwenye kofia na kukupa mabati ya size ya kawaida kutokana na ramani ya nyumba yako)

Vipi za Uganda kwa Kanda ya Ziwa unajua dealer anazo au ndio inabidi kuagiza (ambapo mambo ya ushuru tena na usafiri huenda ikawa issue).

Ila kama hata mtu haupo Dar naona bora ni kuongea kiwandani wakupe bati za moja kwa moja kama kuna uwezekano wa kuzifold na kuzisafirisha
 
Vipi mtu ukiamua kuezeka kwa Slab(zege), yaani badala ya kutumia Bati/vigae na ceiling board wewe unatumia Zege(cement+nondo+mchango) kitu chenye kudumu maisha! Tunawezaje kulinganisha gharama kati ya Zege na bati/vigae.
 
Vipi mtu ukiamua kuezeka kwa Slab(zege), yaani badala ya kutumia Bati/vigae na ceiling board wewe unatumia Zege(cement+nondo+mchango) kitu chenye kudumu maisha! Tunawezaje kulinganisha gharama kati ya Zege na bati/vigae.

Zege itakuwa juu kuliko hivyo vyote ukizingatia bei ya nondo, kokoto, nyavu, cement ni kubwa kuliko ya mbao na mabati au vigae..

Na my experience ni kwamba nadhani nyumba yenye zege ina joto kuliko yenye mabati/vigae hence ceiling board
 
inategemea na mkoa ulipo

Jamaa hapo juu ame-suggest kupeleka roof plan ili kiwanda kikate mabati full kulingana na nyumba inayojengwa kwa uzoefu wako naweza kukunja hilo bati na kulisafirisha kwa urahisi ?
 
Jamaa hapo juu ame-suggest kupeleka roof plan ili kiwanda kikate mabati full kulingana na nyumba inayojengwa kwa uzoefu wako naweza kukunja hilo bati na kulisafirisha kwa urahisi ?

Hilo linasafirishwa bila kukunjwa kwani siku hizi kuna magari kibao yanatoka Dar kwenda mikoani na vice versa, sema tatizo tu ni kuhakikisha guarantee ya mzigo kufika salama hasa ukizingatia mzigo ukitumwa under local arrangement maana yake lolote litakalotokea njiani let say gari imeanguka au gari limetekwa mzigo ukashushwa inakuwa imekula kwako though ni matukio machache kutokea maana watu kibao wanasafirisha pia mikoani kama Mwanza kuna makampun yamefungua matawi yao hivyo mabati yanazalishwa huko huko. Mabati ya Uganda sijaona dealer ila kimjini mjini yanakuwepo kwa baadhi ya maduka
Vipi za Uganda kwa Kanda ya Ziwa unajua dealer anazo au ndio inabidi kuagiza (ambapo mambo ya ushuru tena na usafiri huenda ikawa issue).

Ila kama hata mtu haupo Dar naona bora ni kuongea kiwandani wakupe bati za moja kwa moja kama kuna uwezekano wa kuzifold na kuzisafirisha
 
Wakuu huu uzi useful kwa wadau ujenz nimejifunza mengi sana hasa kutoka kwa mapolomoko, pendael, kalimilo na wadau mengine sasa himetoka kununua bati simba dume 75 kwa tshs=15500/ kwa kila bati moja kwa ajili ya maadalizi ya kupaua. Shukurani sana wajf. Tueendelee kuulizana, kufahamishana, kushauriana na kuelimishana ndani ya uzi huu.
 
Wakuu huu uzi useful kwa wadau ujenz nimejifunza mengi sana hasa kutoka kwa mapolomoko, pendael, kalimilo na wadau mengine sasa himetoka kununua bati simba dume 75 kwa tshs=15500/ kwa kila bati moja kwa ajili ya maadalizi ya kupaua. Shukurani sana wajf. Tueendelee kuulizana, kufahamishana, kushauriana na kuelimishana ndani ya uzi huu.
Vipi upo Dar ungekuwa haujanunua labda ungefata ushauri wa mdau hapo juu kupeleka ramani ya paa kiwandani ili uchukue bati la moja kwa moja mpaka kwenye kofia na sio kuunganisha unganisha (napenda sana kujua cost ya hii)
 
Wakuu huu uzi useful kwa wadau ujenz nimejifunza mengi sana hasa kutoka kwa mapolomoko, pendael, kalimilo na wadau mengine sasa himetoka kununua bati simba dume 75 kwa tshs=15500/ kwa kila bati moja kwa ajili ya maadalizi ya kupaua. Shukurani sana wajf. Tueendelee kuulizana, kufahamishana, kushauriana na kuelimishana ndani ya uzi huu.

Mkuu hizo ni za gauge ngapi umepata
 
Jodoki Kalimilo na Mapolomoko

Kama nikitumia hizo bati direct kutoka kiwandani za kukatwa kulingana na Paa langu..., Je nitapunguza matumizi ya mbao sababu ya ukubwa wa bati na hakuna kuunganisha ?
 
Last edited by a moderator:
Jodoki Kalimilo na Mapolomoko tunahitaji ujuzi wenu juu ya bati gauge 32 zinaweza kuwa imara?? Na ktk utalaam wa kupaua kunauwezekano wa kupaua vizuri ile kuyafanya kuwa imara zaidi?
 
Vipi za Uganda kwa Kanda ya Ziwa unajua dealer anazo au ndio inabidi kuagiza (ambapo mambo ya ushuru tena na usafiri huenda ikawa issue).

Ila kama hata mtu haupo Dar naona bora ni kuongea kiwandani wakupe bati za moja kwa moja kama kuna uwezekano wa kuzifold na kuzisafirisha

si usafiri tu,hata ushuru bidhaa ya bati kuingiza hapa nchini kodi ni nusu ya bei uliyo nunulia nchi nyingine
 
Jodoki Kalimilo na Mapolomoko tunahitaji ujuzi wenu juu ya bati gauge 32 zinaweza kuwa imara?? Na ktk utalaam wa kupaua kunauwezekano wa kupaua vizuri ile kuyafanya kuwa imara zaidi?

32g. ni zahali ya chini, ila zinadumu. fundi atakae kuezekea ahakikishe ana weka vipimo vya papi hadi papi (sm90) yaani papi nne kwa bati, na wakati wa kupiga bati akipiga bati la chini apige na lajuu ili kuepuka kuyakanyaga. na kwavipimo ulivyotoa KING POST iwe ( sm.281 ) mwinuko wa kisasa,hapo nitakuwa nimemsaidia fundi wako. kazi ni kwake kujua nimeipataje, 281
 
Jodoki Kalimilo na Mapolomoko

Kama nikitumia hizo bati direct kutoka kiwandani za kukatwa kulingana na Paa langu..., Je nitapunguza matumizi ya mbao sababu ya ukubwa wa bati na hakuna kuunganisha ?
Mie sio fundi ila kwa uzoefu tu ni kwamba idadi ya mbao ni zilezile tu mkuu kwani mwisho wa siku ili bati liwe imara lazima kila baada ya umbali flani wapige misumari hivyo hata ukinunua bati refu kutokana kiwandani arrangement ya kenchi na papi zake ni ile ile tu (kwa maana nyingine roof plan ni ile ile haibadiliki) ila utakacho-save ni bati kwa kuwa itapunguza idadi ya mabati ambayo yanakatwakatwa hasa kwa hizi bati tunazoita za south ambazo zikikatwa unakuta vipande vyake vingi havitumiki tena tofauti na bati zetu za kizalendo hata kama utakata bati kuna sehemu lazima kita-fit tu
 
Jodoki Kalimilo na Mapolomoko tunahitaji ujuzi wenu juu ya bati gauge 32 zinaweza kuwa imara?? Na ktk utalaam wa kupaua kunauwezekano wa kupaua vizuri ile kuyafanya kuwa imara zaidi?
Angalau tumia gauge 30 kama gauge 28 unakuwa huiwezi, gauge 32 ni ya kijasiamari zaidi kama una-investment yako unatumia ili mwisho wa siku upige hela yako mapema maana kadri gauge inavyoongezeka ndipo na idadi ya mabati kwenye bundle moja inakuwa kubwa
 
(1) Mbao 4*2- 100pcs, 2*2- 60pcs, 1*8- 12pcs,
(2) Misumali nch, 4" 50kg, 3" 15kg, 2" 2kg, baning waya 5kg,
(3) Bati 3mt, shit 60,
Nitafute nikupaulie kwa bei poa no. 0683447725
 
Wanajf tuendelee kufahamishana na kuelimishana juu ya kupaua na finishing ya nyumba! Na amin jf ni sehemu nzuri ya kujifunza. Karibun sana wadau wa ujenzi na mafundi
 
Back
Top Bottom