Makalla atua Katavi na kusema Watasikiliza kero za Wananchi lakini siyo zile zilizopo Mahakamani

Makalla atua Katavi na kusema Watasikiliza kero za Wananchi lakini siyo zile zilizopo Mahakamani

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mwenezi wa CCM Komredi Amos Makala amesema katika Ziara yao Katavi na maeneo mengine watasikiliza kero za wananchi lakini siyo zile zilizoko mahakamani

Makala amesema wanajua Wananchi Wana changamoto mbalimbali na kimbilio lao ni CCM

Source Jambo TV


====== ======

KAULI YA MAKALLA
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa, Amosi Makalla amesema lazima Watu wajue kuwa mambo yaliyo Mahakamani yanamalizwa Mahakamani na hakuna Kiongozi wa Serikali au Chama anayeweza kuingilia Mhimili wa Mahakama.

Akiongea Mkoani Katavi leo wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Emmanuel Nchimbi na Viongozi wengine, Makalla amesema:

“Ninaposikiliza kero Mimi nimetoka kwenye Ukuu wa Mkoa, la kwanza tutasikiliza kero ambazo hazipo Mahakamani, siku moja nipo Mbeya kuna Mtu alikuja na makabrasha akasema Mahakama ya kwanza nilishindwa, Mahakama ya Wilaya nillishindwa, Mahakama Kuu nilishindwa, Mahakama ya Rufaa nilishindwa, wewe umeteuliwa na Rais tengua hizo hukumu zote, itawezekana wapi!?”

“Lazima Watu wetu wajue mambo yaliyo Mahakamani yanamalizwa Mahakamani, tutakachokupa ushauri basi kata rufaa, tunachowasaidia Wananchi yale mashauri ambayo yanahitaji mambo ya utawala, kwahiyo ukija mkutano wa hadhara tunawakaribisha lakini usilete mambo ambayo yapo Mahakamani, ukweli lazima usemwe itakuwa tunawadanganya tu Watu kwamba hili unajua lipo Mahakamani tutakusaidia, sio kweli lazima wakati mwingine tuwe Wakweli”

Katika hatua nyingine Makalla amesema katika jitihada za kuufanya Mkoa wa Katavi uwe na umeme wa uhakika, mradi kuunganisha Mkoa huo na gridi ya Taifa unaendelea kwa kasi na sasa umefikia 56%.

“Nilikuwa natembelea mara kwa mara kwenye jenereta zetu, umeme hautoshi unakatikakatika na huku mvua za radi zikianza kila saa umeme unakatika na wakati huo unaangalia Simba na Yanga halafu umeme unakatika, ninayo heshima na furaha kusema tayari Serikali inaendele kutekeleza wa kuunganisha Katavi na gridi ya Taifa, mradi umefikia 56% na kasi ya mradi huo mtaiona ikiendelea lazima tuwe na umeme wa uhakika.”


=====

KAULI YA NCHIMBI
Upande wa Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi naye amesema:

Katika mambo tutakayoshughuliki kama kero hatutagusa ambayo yapo Mahakamani, ndio utaratibu wa Utawala Bora.

Katika kutekeleza sera za CCM, moja ya jambo muhimu ni kusimamia suala la Utawala wa Sheria, wakati wote tutakuwa tunahamasisha na kuziwezesha Mahakama kutenda haki wakati wote bila kuingilia katika maamuzi yake.

Nchi inayotaka kufanikiwa lazima isimamie Utawala wa Sheria, ukijenga utaratibu wa kuingilia Mahakama katika mfumo wa Sheria siku moja zitawaumiza wote.

====

Pia soma:

- Makonda kusikiliza kero zenye kesi Mahakamani Arusha, asema yupo tayari kupoteza chochote mradi mtu apate haki yake

- Makalla: CCM tunaheshimu Mahakama kama chombo cha kutoa haki, hatuingilii kesi zinazosikilizwa huko

- Katibu Mkuu CCM kumpinga RC Arusha kimafumbo anataka kumfurahisha nani?
 
Ushauri hawa wazee wangepumzika wakalea wajukuu na kuwa washauri wa vijana, ifike hatua tuone aibu, vyuo vikuu kila mwaka vinatoa zaidi ya wahitimu elf 60, kweli hizi nafasi tunashindwa kuwapa vijana waonyeshe ubunifu?
Aanze kupumzika Mbowe 🤣
 
Mwenezi wa CCM Komredi Amos Makala amesema katika Ziara yao Katavi na maeneo mengine watasikiliza kero za wananchi lakini siyo zile zilizoko mahakamani

Makala amesema wanajua Wananchi Wana changamoto mbalimbali na kimbilio lao ni CCM

Source Jambo TV
muhimu kazi iendelee.

NB: Kwa heshima na nia njema, naomba upitie wasifu wangu na unisaidia ktk hitaji langu la ajira.
Mimi ni kijana mchapakazi na mwaminifu, miaka 32, makazi yangu Dar es Salaam. Nina shahada ya utawala, na uzoefu wa miaka 8 katika usimamizi wa miradi, utafiti, data entry, na usimamizi wa mitandao ya kijamii, pia nina ujuzi na uzoefu kwenye customer care, masoko, na mauzo. Naweza kusaidia katika kuandika maandiko mbalimbali ya kiofisi, miradi, tafsiri, na kubuni nakutengeneza tovuti kwa ubora.
Ninaomba fursa ya ajira na nipo tayari kufanya kazi mara moja mahali popote nchini.
Nipigie/text kwa 0769 055050. Asante!
 
Ushauri hawa wazee wangepumzika wakalea wajukuu na kuwa washauri wa vijana, ifike hatua tuone aibu, vyuo vikuu kila mwaka vinatoa zaidi ya wahitimu elf 60, kweli hizi nafasi tunashindwa kuwapa vijana waonyeshe ubunifu?
Ni sahihi chama na serikali kinahitaji vijana na ndiio walio wengi kwa mujibu wa sensa

Hawa wazee no please wanaendesha mambo kizamani sana Hata hilo la kusikikiliza wananchi kijana makonda ndio kalianzisha .Viongozi vizee vikongwe vilivyoko CCM wala havikuwa na huo ubunifu akiwemo Kikongwe Makalla mwenyewe
 
Kuna zeto brain alikuwa anatukana hadj mihimili mingine.....yeye ndio awe hakimu police na DPP na wakili utetezi
 
Makonda alizunguka mikoa ishirini akitangaza kutatua kero, ripoti yake ilipofika kenye chama ikawekwa kapuni.

Leo karibu mkuu ameeleza umma kwamba awapo tayari kuingilia mahakama. Je, wale wananchi walioshangilia ahadi za Makonda ikiwemo zile za kupingana mahakama watasaidikaje?

Kwanini CCM imewachanganya wananchi? Viongoz kila mmoja ana msimamo wake?
---
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa, Amosi Makalla amesema lazima Watu wajue kuwa mambo yaliyo Mahakamani yanamalizwa Mahakamani na hakuna Kiongozi wa Serikali au Chama anayeweza kuingilia Mhimili wa Mahakama.

Akiongea Mkoani Katavi leo wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa CCm, Emmanuel Nchimbi na Viongozi wengine, Makalla amesema
“Ninaposikiliza kero Mimi nimetoka kwenye Ukuu wa Mkoa, la kwanza tutasikiliza kero ambazo hazipo Mahakamani, siku moja nipo Mbeya kuna Mtu alikuja na makabrasha akasema Mahakama ya kwanza nilishindwa, Mahakama ya Wilaya nillishindwa, Mahakama Kuu nilishindwa, Mahakama ya Rufaa nilishindwa, wewe umeteuliwa na Rais tengua hizo hukumu zote, itawezekana wapi!?”

“Lazima Watu wetu wajue mambo yaliyo Mahakamani yanamalizwa Mahakamani, tutakachokupa ushauri basi kata rufaa, tunachowasaidia Wananchi yale mashauri ambayo yanahitaji mambo ya utawala, kwahiyo ukija mkutano wa hadhara tunawakaribisha lakini usilete mambo ambayo yapo Mahakamani, ukweli lazima usemwe itakuwa tunawadanganya tu Watu kwamba hili unajua lipo Mahakamani tutakusaidia, sio kweli lazima wakati mwingine tuwe Wakweli”

Katika hatua nyingine Makalla amesema katika jitihada za kuufanya Mkoa wa Katavi uwe na umeme wa uhakika, mradi kuunganisha Mkoa huo na gridi ya Taifa unaendelea kwa kasi na sasa umefikia 56%.

“Nilikuwa natembelea mara kwa mara kwenye jenereta zetu, umeme hautoshi unakatikakatika na huku mvua za radi zikianza kila saa umeme unakatika na wakati huo unaangalia Simba na Yanga halafu umeme unakatika, ninayo heshima na furaha kusema tayari Serikali inaendele kutekeleza wa kuunganisha Katavi na gridi ya Taifa, mradi umefikia 56% na kasi ya mradi huo mtaiona ikiendelea lazima tuwe na umeme wa uhakika”
 
Awapo ndio nini mleta mada?
Makonda alizunguka mikoa ishirini akitangaza kutatua kero, ripoti yake ilipofika kenye chama ikawekwa kapuni.

Leo karibu mkuu ameeleza umma kwamba awapo tayari kuingilia mahakama. Je, wale wananchi walioshangilia ahadi za Makonda ikiwemo zile za kupingana mahakama watasaidikaje?

Kwanini CCM imewachanganya wananchi? Viongoz kila mmoja ana msimamo wake?
 
Makonda alizunguka mikoa ishirini akitangaza kutatua kero, ripoti yake ilipofika kenye chama ikawekwa kapuni.

Leo karibu mkuu ameeleza umma kwamba awapo tayari kuingilia mahakama. Je, wale wananchi walioshangilia ahadi za Makonda ikiwemo zile za kupingana mahakama watasaidikaje?

Kwanini CCM imewachanganya wananchi? Viongoz kila mmoja ana msimamo wake?
---
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa, Amosi Makalla amesema lazima Watu wajue kuwa mambo yaliyo Mahakamani yanamalizwa Mahakamani na hakuna Kiongozi wa Serikali au Chama anayeweza kuingilia Mhimili wa Mahakama.

Akiongea Mkoani Katavi leo wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa CCm, Emmanuel Nchimbi na Viongozi wengine, Makalla amesema
“Ninaposikiliza kero Mimi nimetoka kwenye Ukuu wa Mkoa, la kwanza tutasikiliza kero ambazo hazipo Mahakamani, siku moja nipo Mbeya kuna Mtu alikuja na makabrasha akasema Mahakama ya kwanza nilishindwa, Mahakama ya Wilaya nillishindwa, Mahakama Kuu nilishindwa, Mahakama ya Rufaa nilishindwa, wewe umeteuliwa na Rais tengua hizo hukumu zote, itawezekana wapi!?”

“Lazima Watu wetu wajue mambo yaliyo Mahakamani yanamalizwa Mahakamani, tutakachokupa ushauri basi kata rufaa, tunachowasaidia Wananchi yale mashauri ambayo yanahitaji mambo ya utawala, kwahiyo ukija mkutano wa hadhara tunawakaribisha lakini usilete mambo ambayo yapo Mahakamani, ukweli lazima usemwe itakuwa tunawadanganya tu Watu kwamba hili unajua lipo Mahakamani tutakusaidia, sio kweli lazima wakati mwingine tuwe Wakweli”

Katika hatua nyingine Makalla amesema katika jitihada za kuufanya Mkoa wa Katavi uwe na umeme wa uhakika, mradi kuunganisha Mkoa huo na gridi ya Taifa unaendelea kwa kasi na sasa umefikia 56%.

“Nilikuwa natembelea mara kwa mara kwenye jenereta zetu, umeme hautoshi unakatikakatika na huku mvua za radi zikianza kila saa umeme unakatika na wakati huo unaangalia Simba na Yanga halafu umeme unakatika, ninayo heshima na furaha kusema tayari Serikali inaendele kutekeleza wa kuunganisha Katavi na gridi ya Taifa, mradi umefikia 56% na kasi ya mradi huo mtaiona ikiendelea lazima tuwe na umeme wa uhakika”
Naona mama kawekwa mtu kati. Wateule wake wa Chama wanapingana na Makonda, Makonda kipenzi cha mama. Sijui anasimamia wapi maana kuwa na serikali ambapo watu wanapingana nayo kisanga
 
Naona mama kawekwa mtu kati. Wateule wake wa Chama wanapingana na Makonda, Makonda kipenzi cha mama. Sijui anasimamia wapi maana kuwa na serikali ambapo watu wanapingana nayo kisanga
Huyu makonda atakuja kuwa kama job, maana atakosa upande. Amejichanganya sana. Mara anatetea wanyonge mara anasimama na mama yake hataki asemwe kwa mabaya. Atajikuta anaishia kujiuzulu
 
Back
Top Bottom