Makamanda walioigharimia CHADEMA kwa machozi, jasho na damu, leo ni wakuitwa wasaliti? Karma Haitawaacha salama, itawatandika tu

Duni Haji alisema Chadema wapo kama Kambale ndio haya tunayaona ila kama kweli wana baraka ya mwenyekiti bila katibu kujua wala cc ya chadema haijakaa ni vema waadhibiwe wote mwenyekiti na wasaliti lakini kama walijiamria wachukuliwe hatua za kinidhamu na pia chadema ifungue kesi ya kuwashitaki wote walihousika na mchakato batili hata kama watabebwa na mahakama lakini hila zao zitawekwa wazi , ikiwa mwenyekiti kahusika na hataki wachukuliwe hatua ni bora Mnyika ajiuzulu ili ampe nafasi mwenyekiti kuendelea na mipango yake
 
Huyu ndio Paskal💪
 
Jitahidi ku-summarise bro. Unaongea Sana. But mbona hukuhoji Chama Kumvua uanachama Membe?? Au unadhani Membe hakukitumikia Chama?

Unachoelezea ni kuwa baadhi wa wanachama wapewe immunity na provision ya kuvunja Katiba tu kwa vile wao ni wakongwe.

Kama ikiruhisiwa hivyo, wewe mwenyewe Pakal Njaa utakuja kuandika mambo meeeeengi hapa kuhoji na kuponda.
 
Mnyika ni radical kama Dr Slaa , hii issue inaweza kuishia kwa yeye kuamua kujiuzulu ...kama haitakuwa well handled ....ccm wamewaweza chadema this time ..sijui kama chadema wanajua hilo ...... wakiwafukuza KOSA wakiwaacha KOSA ....
Dawa waishughulikie baada ya hali ya hewa kupoa ..kuna pressure nje ya kuona amajibu
 
P. Asante sanaaaa kwa ufafanuzi
 
Mayala endelea kusherehesha watu. Kama karma ipo, basi itaanza na wewe kwa kuisailiti nafsi na utu wako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiona unaonewa huruma/ unasifiwa na adui yako jiulize saaaaana mswali kichwani mwako
 
The fact kwamba leo Pascal kawa mtetezi mkuu wa kina Mdee inatia shaka sana. Imekuwaje na iweje leo Mayalla awe ndio mtetezi wao? Sijui huu ni uzi wa ngapi umeanzisha kuhusu hili, Kunani nyuma ya hili?
 
Mwishowe ni muhimu sana hao wanawake wafukuzwe kwa chadema ya baadaye. Kukubaliana na viti maalum ni inconsistency kwa madai yao ya uchaguzi kuvurugwa.
 
#@ Pascal Mayalla ,
Tunatambua huna ulichobakiza kwenye kichwa chako zaidi ya uchonganishi, unafiki na kujikomba ili upate cheo...

Platform hii unaitumia ipasavyo kipropaganda na kupata ujira usio na haki
Kwa kusaliti harakati za watanzania kujikomboa na kujiletea maendeleo

Legacy umeipoteza punde utabaki kama takataka ccm tunawajua waulize wenzio kina nape makonda wamepotea kwenye mioyo ya watanzania
 
Umeongea jambo la mhimu sana na unatumia akili nyingi sana, niwakumbushe tu hawa chadema wakijidanganya kuwafukuza jamii haitakaa iwaamini tena, hapo jamii itaanza kuyaamini yale maneno yaliyo semwa na Lijua likali na wenzake, pia watakosa uwanja wa kusikika ndani ya miaka 5 hivyo watakua na wakati mgumu sana, maana huenda wakasahaliuka masikioni mwa watu. Niushauri tu wawaache kabisa hao wakina mama walitumikie taifa.
 
Mkuu,
Hichi ulichosema ndicho hasa niniachokiona kikiendelea.
Chadema wanahitaji kupata ushauri, washauri wawe watu wanaojitambua na wanaojuwa nje ndani ya kinachoendelea kwenye siasa za Tanzania. Washauri wasiwe bias na upande wa chama chochote including chama chao wenyewe! Washauri wasiwe wana CCM kama kina Pascal Mayalla. Washauri wawe smart na analytical people.
CHEDEMA wasitowe uamuzi kwa kufuata pressure ya wanasiasa au pressure ya wanachama wenye hasira. Hakuna asiejuwa kwamba ni kweli CHADEMA wamebamikizwa na ukuta na kwa kweli ni ngumu hata kuvuta pumzi! Ni wakati wa wao kujikusanya upya kuona hali inayowakabili na kuamua kitakachookoa jahazi.
 
Ngugu yetu Njaa yaani Mayala , huu ndyo uzi mbovu umewahi kuandika ktk kuumaliza mwka huu 2020 , ila nisiseme mengi nikakengeuka kama wewe.
 
Although I haven't read your now familiar lengthy and boring comment, I think it's an utter rubbish and ask myself since when did you become a prophet.

You don't speak of your karma to the one who is responsible for the disappearance, kidnapping, torture and wounding of other innocent lives but you speak of the traitors who've been bribed to betray the people's cause.

You've resorted to writing nonsensical articles ostensibly to appease the dictator to remember you when he will be making political appointments. Surely you've been a poor excuse for a journalist.
 
Ushauri wenu kaeni nao. Mlishindwaje kumsamehe Membe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…