Makamba: 89.7% ya wananchi bado wanatumia Kuni na Mkaa kupikia

Makamba: 89.7% ya wananchi bado wanatumia Kuni na Mkaa kupikia

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1665595474182.png


Akizungumza leo Oktoba 12, 2022 jijini Dar es Salaam Waziri wa Niashati, January Makamba amesema, “Kupika ni moja ya tukio pekee linalounganisha watu wa hali zote kuanzia wa juu, kati na chini, lakini Watanzania wengi hawajui na wala hawahoji aina ya nishati inayotumika katika kupika vyakula wanavyokula kila siku.

Makamba amesema 72% ya nishati yote inayozalishwa nchini Tanzania inatumika majumbani na uchafuzi wa mazingira hasa hewa kwa njia moshi unachangiwa na 89.7% ya Nishati yote inayotumika majumbani.

Amefafanua kuwa 63.5% ya kaya nchini zinatumia Kuni kupikia, 26.2% hutumia Mkaa, 5.1% ya kaya zinatumia Gesi za Mitungi, 3% Umeme na 2.2% ikiwa ni nishati nyingine.

Waziri Makamba amesema hayo kwenye mkutano wa kuandaa Kongamano la Nishati Safi Ya Kupikia ‘Clean Cooking Conference’ ili kuchunguza vikwazo vinayodumaza matumizi ya nishati za kisasa za kupikia. Kongamano hilo linalenga kupendekeza mikakati ya kufanikisha upatikanaji wa nishati safi, za bei nafuu na endelevu nchini Tanzania.

Litafanyika Novemba 1 na 2 2022 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam na kuwakutanisha watunga sera, wadau wa maendeleo, wajasiriamali, wawekezaji, wafadhili, wanataaluma na wananchi kwa ujumla.

Siku ya ufunguzi wa kongamano itahudhuriwa na Rais Samia Suluhu Hassan, akiwa Mgeni Rasmi. “Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi wa Kongamano la Nishati safi ya Kupikia yaani ‘Clean Cooking Conference’ ili kuchunguza vikwazo vinavyodumaza matumizi ya nishati za kisasa za kupikia”- amesema Waziri Makamba
 
Yaani moshi unaotoka kwenye hivi vijiko vya mkaa huku mtaani vinachangia 89% ya uchafuzi wa hali ya hewa nchini 🤔 mm sio mtaalamu wa haya masuala ili hio takwim itakuwa na walakini
 

Wakati January akiwa waziri wa Mazingira, Kigwangala alisema January hana anachofanya zaidi ya kuandaa makongamano.

sijui kama alikuwa au hakuwa sahihi.
 
Hayo pia ni mafanikio ya ccm kwa miaka 61 tangu uhuru maana kipindi kile watu walikuwa wanakula vyakula bila kuvipika.
 
Hizi ni habari zilizoniskitisha toka twitter handle ya MMM kama ni kweli watu wanalamba asali namna hii basi hatuna budi kuomba katiba mpya.
Screenshot_20221012-191631.jpg
 
Sisiem tumlaumu nani jama sio nyie? Punguza kodi kwa gas bei ishuke
 
Waruzuku hiyo Gesi ya kupikia iwe affordable.
Ndugu yangu hawa wanasiasa bana! Hakuna mtu anayependa upikaji unaohatarisha afya yake, kutokana na moshi wa kuni au mkaa bt the issue ni 'affordability' ya nishati mbadala..... Je watz wangapi walio na uwezo na nishati mbadala???? Unless iwe na bei rafiki....
Waruzuku hiyo Gesi ya kupikia iwe affordable.
 
Back
Top Bottom