Makamba: Gesi ya Mtwara kuanza kuchimbwa 2025

Makamba: Gesi ya Mtwara kuanza kuchimbwa 2025

Wait a minute 🤔🤔🤔 Mmmhhh okay.

Mkataba unasemaje? Sisi kama nchi tunapata % ngapi? So gharama tu ya uchimbaji ni tril 70? Eti? Gharama hizi kubwa mno wamezipataje kabla hata mradi haujamalizika? Yaani deni la Taifa tokea uhuru hadi sasa ni Tril 78. Sasa gharama za uchimbaji gesi hata pamoja na kujenga LNG plant zote ni tril 70? Hizi gharama kubwa sanaaa, something haiko sawa.

Jamani, nawaza tu, usikute waka zidisha gharama sana tukaanza kupigwa mapemaaaaaa. Nawaza tu, uuwiii, OMG.
Wewe kama nani uambiwe tulia inchi isimame kwanza
 
Hivi kusema gesi itaanza kuchimbwa wana maana gani? Lile bomba lililojengwa enzi za JK kuja Dar kwani halijaanza kusafirisha gesi? Na vipi gesi ya Songo songo haiji Dar kwani?
Hili swali na mimi najiuliza
 
Ni kwa sababu huyo alieuona pia hakutaka na sisi tuuone. Alitaka tu tuamini maneno yake. Angekua mkweli, angetuonyesha!
Hivi kweli kwa raia lay man kuna access kuweza kuona hiyo mikataba ya kiserikali ili kujiridhisha na kinachoongelewa?

Ninavyoelewa, walioko mamlakani ndiyo hufanya hayo mambo kwa niaba yetu bila kulazimishwa na sheria yoyote kuonesha hadharani kila mikataba wanayoiingia kwa niaba ya taifa.

Ninaomba mfano hai, ni mikataba gani serikali iliiingia halafu wewe ukaoneshwa kwamba hii hapa na kisha kutafsiriwa tija yake itakuwaje kwa nchi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi kweli kwa raia lay man kuna access kuweza kuona hiyo mikataba ya kiserikali ili kujiridhisha na kinachoongelewa?

Ninavyoelewa, walioko mamlakani ndiyo hufanya hayo mambo kwa niaba yetu bila kulazimishwa na sheria yoyote kuonesha hadharani kila mikataba wanayoiingia kwa niaba ya taifa.

Ninaomba mfano hai, ni mikataba gani serikali iliiingia halafu wewe ukaoneshwa kwamba hii hapa na kisha kutafsiriwa tija yake itakuwaje kwa nchi!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna niliposema kwamba kuna mikataba mingine tuliwahi kuonyeshwa. Lakini pia, tunalo Bunge ambalo ndio uwakilishi wa wananchi. Kama kuna mkataba mzuri na wenye manufaa kwa wananchi, kuna sababu gani ya kuuficha?

Wanabaki wahuni wachache tu wakitaka kutuaminisha ni mkataba mzuri, na wahuni wengine wanadai ni mkataba mbaya, ila hawataki tuuone. Mtu yeyote mwenye akili, hawezi kuwaamini.
 
Wait a minute [emoji848][emoji848][emoji848] Mmmhhh okay.

Mkataba unasemaje? Sisi kama nchi tunapata % ngapi? So gharama tu ya uchimbaji ni tril 70? Eti? Gharama hizi kubwa mno wamezipataje kabla hata mradi haujamalizika? Yaani deni la Taifa tokea uhuru hadi sasa ni Tril 78. Sasa gharama za uchimbaji gesi hata pamoja na kujenga LNG plant zote ni tril 70? Hizi gharama kubwa sanaaa, something haiko sawa.

Jamani, nawaza tu, usikute waka zidisha gharama sana tukaanza kupigwa mapemaaaaaa. Nawaza tu, uuwiii, OMG.
Magufuli ndio ametufikisha hapa.
 
Kwanini hukubaliani na mimi Chifu?

Hivi una habari ile gesi ya Msimbati ni ONLY 5 Trillion Cubic Feet, out of 57.54 Trillion Cubic Feet of total gas discoveries huku 47 Trillion Cubic zikiwa hazijaguswa?!

Na hadi sasa, kama nilivyosema hapo awali, umeme wa gesi kwenye grid ya taifa ni 57%, na asilimia inayobaki ni kwa vyanzo vingine! Sasa kabla hatujaenda mbali, kama hadi sasa umeme wa gesi ni 57%, na bado tunaendelea kutafuta vyanzo vingine; nini hapo tafsiri yake kama sio hata huo umeme unaokuwa supplied na gas kwa sasa bado hautoshi?

Na kama hautoshi, hivi hiyo si ndo ile Wachumi wanaita Low Supply?! Kitu kikiwa in low supply, bei inakuwaje?!

Ni kweli Muhongo alisema bei itapungua lakini sio katika mazingira ya sasa ambayo hata huo umeme wenyewe bado hautoshi!! Unaweza kupungua endapo utazalishwa umeme mwingi zaidi!! Na umeme mwingi zaidi utazalishwa baada ya kukamilika Bwawa la Nyerere au tukianza kuchimba ile gesi ya kina kirefu!!

Hata hivyo, napo kupungua kwenyewe kwa bei kutategemeana na principle ipi ya kiuchumi itatumika! Kwa bahati mbaya sana, watu wanaamini kwenye kuongeza bei ili kuongeza mapato, wakati mtu kama mimi naamini kwenye kuongeza mauzo kama njia bora ya kuongeza mapato, wakati factors zingine zinabaki constant!!

Maana yake ni nini?! Hata Bwawa la Nyerere likishakamilika, ndio umeme utakuwa mwingi sana lakini hapo hapo taifa litakuwa limeingia gharama kubwa za uwekezaji kwenye hilo bwawa!!

Sasa basi, kwenye hizo principle nilizotaja hapo juu, Serikali inaweza ku-opt kubakisha bei ya umeme kama ilivyo ikidhani bei kubwa inawaongezea mapato ya ku-finance gharama walizoingia kwenye ujenzi wa bwawa, huku wakisahau ukifanya hivyo unakuwa una-discourage matumizi ya umeme!

Tafsiri ya haraka ya ku-discourage matumizi ya umeme inafanya TANESCO wauze units chache!! Kwa mazingira ya sasa, LAZIMA u-discourage matumizi kwa sababu watu wakianza kutumia umeme kadri watakavyo, umeme uliopo hautatosha! Lakini kama tayari una umeme wa kutosha, hapatakuwa na sababu ya ku-discourage matumizi ya umeme!!

Yaani, ningekuwa mimi ningeshusha bei ili ku-encourage matumizi ya umeme! Ukishusha bei, hata wale wanaoogopa kutumia majiko ya umeme hatimae wataanza kutumia! Watu watapiga pasi hadi sidiria na boksa, na hivyo kupelekea TANESCO kuuza units nyingi zaidi ya umeme, na hatimae kupata mapato makubwa zaidi... win win game!!

Ninachotaka kusema hapo ni kwamba, Muhongo sio mjinga wa kudhani kwamba ile gesi iliyoanza kuchimbwa peke yake ingeleta umeme wa ziada na hivyo kusababisha bei ipungue!! Lakini pamoja na hayo, bado alikuwa na matumaini in the future tutazalisha umeme mwingi zaidi kwa sababu imegundulika gesi nyingi zaidi, na ndo maana hata lile bomba, ni kubwa maradufu kuliko hata gesi inayosafirishwa hivi sasa!!

View attachment 2010039
Mkuu, Naona kabisa unaongea unachokijua...Big up Mkuu Chige.
 
Hiyo 70 Trillion is ONLY for Gas Processing Plant ambayo itajengwa pale Lindi!!

Kama ulivyosema, uchimbaji unafanyika offshore... several kilometers away from the shore! Ikishachimbwa huko offshore, inasafirishwa in raw form na ma-impurity yake hadi nchi kavu kwenye hiyo plant ya 70 Trillion!!

Pesa ni ndefu sana kwa sababu...

1. Serikali ilikataa kujenga kiwanda baharini
2. Vitalu vipo zaidi ya 100km from nchi kavu
3. Gesi yenyewe nayo ipo kwenye kina kirefu... hapa tunazungumzia kilometers!!

Sasa kutandaza mabomba umbali wote huo, hadi nchi kavu kwenye processing plant, anyway, inawezekana ni kweli tunapigwa lakini sio kazi nyepesi! Hii ni tofauti na gesi kama ile ya Mkambakofi ambayo ipo nchi kavu, au hata ile ya Songosongo!!

Kwamba kusambaza kwenye nyumba chache sana... uchache utatokana na ama sisi wenyewe kushindwa kusambaza miundombinu kwa watu wengi zaidi, au kama priority yetu itakuwa kwenye export ingawaje ukisoma Sheria ya 2015 kuhusu Matumizi ya Fedha za Mafuta na Gas, inasema priority ya kwanza iwe for domestic use, na ziada ndipo isafirishwe!!

Ni kutokana na hilo ndo maana TPDC walitangaza tenda ya kusambaza miundombinu ya gesi nchi mzima, na kwahiyo inawezekana kabisa kuwafikia wananchi wengi kwa sababu, as of now, kuna roughly 47 Trillion Cubic Feet of gas ambazo hazijaguswa kabisa!!


Bravo mkuu, nimekosa tu kitufe cha kukupigia makofi
 
Hii nchi kuna watu wameumbwa kulalamika na kuwa na mashaka dhidi ya watu fulani walioamua tu kuwa nao na mashaka milele daima. Hakuna kitakachopangwa kisiache miguno ya wasiwasi. Ajabu pia ni kuwa wahusika wakikaa kimya watu haohao haraka huja humu na mathreads, '.....atatembelea lini wananchi?', 'mbona hatuoni jipya?', 'hivi gesi ya asili itanufaisha lini wananchi?' n.k

Makamba piga kazi baba, kafaida kadogo utakachokapata wewe kama wewe ndiyo maana ya kuwa waziri.....kila mmoja angekapata kafaida hako, tena walalamikaji na wenye mashaka wa humu wangefanya jitihada ya kukapata kakubwa zaidi. Maana yake haya malalamiko na mashaka meeeengi ni matokeo ya wivu tu na husda. Ukisema uwasikilize wabongo basi utajikuta umesimama hapo hapo bila kupiga hatua yoyote ile
hii gesi ya mtwara haikuanza leo.
Sasa sijui ni muendelezo au NI uchimbaji mpya.
NI matrilioni ya fedhwa.
KULIPA FADHILA NDO MWENDO
 
Back
Top Bottom