Makamba: Sisi tumeamua kuwa wakweli, bwawa la Nyerere linaisha Juni 2024. Adai tarehe ya mwanzo isingewezekana kwa namna yoyote

Makamba: Sisi tumeamua kuwa wakweli, bwawa la Nyerere linaisha Juni 2024. Adai tarehe ya mwanzo isingewezekana kwa namna yoyote

Ah Makamba!!!eeh Ndugu yangu!!!

Kumbe SERIKALI iliyopita walikuwa waongo sio!!?

Nyie ndio wakweli!!

Hivi mnajua kuuendeleza kuponda awamu iliyopita itawafanya wenye DOLA kuwachukia Rasmi na kuwanyang'anya na kijiti akapewa MWINGINE!?

Watawauliza Kwamba wakati awamu iliyopita inadanganya wewe msaidizi wake ulikiwa WAPI kusema kweli!!?ina Maana uliapa kuilinda na kuitetea jamuhuri au kuiangamiza!!?kwanini useme mlidanganya na Sasa tuta aaminije kama hamtudanganyi wakati mlikuwepo NDANI ya utawala!!?

Mtajibu nini eeh makamba!!?

Mtamteteaje namba Moja hapo!!?

NIMEANDIKA tu,ili nichangie uchumi!!
Kuna wenye dola zaidi ya JK, Kinana na Rostam?
 
Haka kajamaa ni zero brain,bado kako vitani na awamu ya tano.

Kama "wao" wametumia mwaka mmoja kujenga 37%, ni nini kinafanya hiyo 26% iliyobaki kuchukua miaka miwili hadi 2024?

Tuki-cross multiplication hapo hiyo spidi yao bwawa lingeisha August 2023.

SGR Dar-Moro nayo nayo wanahamisha magoli tu kuhusu lini itaanza kazi.
 
Ila kweli kabisa hawa jamaa kuwaamini inabidi mtu ujitoe sanaa.

Kila siku akihojiwa anabadiri asilimia ambazo awamu ya tano ilikuwa imejenga bwawa hilo.

Lakini cha ajabu zaidi, kama amelikuta 37%, wao wamefikisha 74%, hilo ni ongezeko la 37% zingine kwa mwaka mmoja...Bwawa hilo kwa sasa limebakiza 26% liweze kukamilika kwa 100%...lakini hizo 26% zilizobaki,zinahitaji miaka miwili kukamilika.

Yaani ni hivi..
37%=mwaka mmoja.

26%=miaka miwili

Ngoja aendelee kutolisikiliza Bunge kama alivohaidi
Yaani huyu jamaa bwana. Anapayuka tu.
 
Akiwa Clouds TV, waziri wa nishati January Makamba amesema bwawa la kuzalisha umeme la mwalimu Nyerere linaisha mwezi Juni mwaka 2024 na wameamua kwenda na uhalisia na hawaoni aibu kusema litaenda miaka miwili mbele kuliko tarehe iliyotarajiwa kwani kwa namna yoyote isingewezekana ile tarehe ilitangazwa awali.

Awali Makamba amesema bwawa limeanza kujengwa Disemba 2018 na mpaka 2021(awamu ya tano) lilikuwa limejengwa kwa asilimia 37 kwa miaka miwili na nusu lakini mwaka mmoja(Awamu ya sita) limefika asilimia 74.

Makamba amesema wameongeza usimamizi na wamebadilisha 'Project Management' na wametumia pesa zaidi kupitia Tanesco kuhakikisha unakamilika kwa viwango na ubora.

Makamba pia amesema wameweka vichwa vyao pale na watapoinua uwe umeisha hivyo mambo ya Bungeni wao hawayasikilizi bali wanasimamia mradi vizuri na hali ilipo ni nzuri.

Awamu iliyopita ilidhamiria kumaliza bwawa la Nyerere Juni mwaka huu wa 2022.

Kuhusu hali ya umeme nchini, Makamba amesema umeme unaozalishwa nchini ni megawatts 1700 na mahitaji ya juu ni megawatts 1500 hivyo nchi inajitosheleza.


February huo ukweli umeupata wapi? Kila siku tunasikia miradi imekamilika Kwa asilimia 80 Leo unatupeleka 2024 ili muendelee kupiga zenu! Yetu macho.
 
Nimesoma hapa nikaona ujinga mtupu, ....
Yaani hawa jamaa kuna wakati wanawatizama watz na kuwaona kama mazuzu na hizi fiksi zao.

Huyu kijana vile tu bila babake tunajua asingekuwa hapo alipo so anamsengenya Magufuri sababu hayupo ila sisi tulio hai we know everything.
 
Kwasababu, Mmmnh! Watanzania wenzangu hebu nisaidieni kuelewa kitu hapa!! Mwaka 2021 ilifikikia 37% sasa tupo 2022 74%. Then tunaambiwa mpaka 2024 ndiyo likamilike!! Sasa hii iko vp ndugu wadau? Kimahesabu imebaki 26% kama nipo sahihi? Swali moja kubwa na kidogo linashangaza kwanini ndani ya mwaka mmoja kazi ifanyike kwa 37% na 26% iliyobakia igarimu muda wa miaka miwili?????() [emoji848] [emoji780]️

Ukweli ni kuwa mwenye bwawa angekuwepo saivi lishawashwa ila Hawa wajanja wanaamua watupige kimya kimya tu!
 
Ni nani huyo kwani alikuwa muongo muongo?🐒🐒🐒
 
Akiwa Clouds TV, waziri wa nishati January Makamba amesema bwawa la kuzalisha umeme la mwalimu Nyerere linaisha mwezi Juni mwaka 2024 na wameamua kwenda na uhalisia na hawaoni aibu kusema litaenda miaka miwili mbele kuliko tarehe iliyotarajiwa kwani kwa namna yoyote isingewezekana ile tarehe ilitangazwa awali.

Awali Makamba amesema bwawa limeanza kujengwa Disemba 2018 na mpaka 2021(awamu ya tano) lilikuwa limejengwa kwa asilimia 37 kwa miaka miwili na nusu lakini mwaka mmoja(Awamu ya sita) limefika asilimia 74.

Makamba amesema wameongeza usimamizi na wamebadilisha 'Project Management' na wametumia pesa zaidi kupitia Tanesco kuhakikisha unakamilika kwa viwango na ubora.

Makamba pia amesema wameweka vichwa vyao pale na watapoinua uwe umeisha hivyo mambo ya Bungeni wao hawayasikilizi bali wanasimamia mradi vizuri na hali ilipo ni nzuri.

Awamu iliyopita ilidhamiria kumaliza bwawa la Nyerere Juni mwaka huu wa 2022.

Kuhusu hali ya umeme nchini, Makamba amesema umeme unaozalishwa nchini ni megawatts 1700 na mahitaji ya juu ni megawatts 1500 hivyo nchi inajitosheleza.


Extremely useless....
 
Back
Top Bottom