Makamba unampa taarifa za uongo Rais kwa faida ya nani?

Rais Samia walishamgeuza mtu wao wa kumdanganya. Na siyo hilo tu, bali hata usimamizi wa mradi eti January anajifanya alipochaguliwa yeye akashauriwa afuate project managament science, yaani uongo mtupu. January hataki kabisa bwawa liishe ili mgao uendelee. Anapika data kumdanganya rais Samia. Tulishamshauri rais Samia fukuza haraka Mwigulu na January wote hao wanamhujumu ni mijamaa maongo maongo
 
Nitajie Waziri yoyote ndani ya serikali ya JPM na Samia, ambaye ni bold enough angeweza kusema ukweli mchungu kama huu?. Nani angethubutu kuyasema haya?.
P
Wewe ni kaka yangu lakini sikuungi mkono kuwatetea January na Nape!!

Ninavyokufaham, usingeandika haya kama ungebeba maslahi ya taifa na si maslahi yako binafsi.

Hotuba aliyoisema mleta uzi ni ya kipindi Magufuli ashakufa, sasa unataka kusema walikuwa wanajipendekeza kwa marehemu?

Tuweni serious na mambo ya kitaifa, January Makamba hafai kuwa wizarani hapo. Tunafahamu chuki yake binafsi na Hayati Magufuli na WATANZANIA walimjibu kwenye uzinduzi wa bwawa na kumuonyesha jinsi bado wanavyompenda. Throughout his speech, he didn't appreciate and recognize the contribution of his Excellency, the late John Pombe Magufuri. I hate him very much.
 

Pascal naomba nisielezee sana ila sio kweli ukisemacho hapa. Nimetoka kwenye mradi Disemba, 2021 na nilikua naingia kwenye kikao kikubwa kabisa kati ya TANESCO(Client), TECU(Consultant) na JVACEE(Contractor) na tulikua tuko 49%.
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni The late Magufuli did very serious job pale.
 

Kwa kuongezea bwana Pascal ile kazi ina plan of work, so miundombinu mingine tayari ilikuwepo kwenye mpango na tayali shughuli za visibility zilishafanywa na nguzo by Dcember, 2021 zilikua zimeanza kuelekezwa uelekeo ya kituo cha kupokelea umeme.
What I see in your explanation ni kutoa maoni yako ilhali kwa wewe muandishi nguli ulipaswa utafute taarifa ili uwalishe facts audience yako.
Km utataka kupata insider mle ndani nitakusaidia, unaheshimika sana kaka usiongee hisia tafuta taarifa.
 
Shida ya makamba na mwigulu ni wezi sana sasa lzm wawe waongo.
 
Mayalla wewe ni muandishi mkubwa usijivunjie heshima yako kwa kuandika hisia zako badala ya mambo halisi, ukweli tupu.
Enzi za JPM akisema nataka mradi huu ukamilike wakati fulani ni kweli anafuatilia unakamilika muda aliopanga au unapitiliza kidogo sana.
Tumeona hilo kwenye barabara, miradi ya maji, vivuko, flyovers, ndege, mifumo ya kukusanya mapato ya kielektroniki, madaraja, umeme wa REA, umeme haukukatika ovyo, hakukuwa na mgawo wa umeme kwa miaka yake yote aliyokaa Ikulu n.k.
Hii ina maana alipewa taarifa sahihi.
Unafikiri mtu mfuatiliji kama JPM unaweza kumdanganya kwa kukopa bank wakati alikuwa na watu wake kila sehemu? Jinsi alivyo fuatilia mienendo ya kifedha ya bank zote unafikiri itakuwa rahisi taasisi ya umma kukopa kwa kificho bila yeye kujuwa? Hivi mnaijuwa taasisi ya uraisi nyie watu?

Acheni kujipendekeza kiasi hiki mnaangamiza taifa hamsaidii Mh. Raisi Samia kwa kupotosha taarifa au kumponda mtangulizi wake.
 
Yawezekana kaka Pasco aliandikiwa na Steve Nyerere, maana ametiririka kama anavizia fadhila
 
Ungemuuliza pia hivi kwa ile Tumbua tumbua ya JPM mtu angeanzaje danganya.

Kama manager wa mkoa umeme ukikatika tu ulikua unataka wajibishwa. Uje tu mwehu umdanganye mtu aliyefahamika kama dikteta?na kile kicheko chake cha "eeeeeeeeh"
 
Huyo mtu haaminiki na waTanzania wengi sana, ukikaa mitaani muda wa mapumziko ya jioni unawasikia watu wakianza tu kuongelea Serikali na viongozi, vinywa na mawazo ya maongezi yote yanasema vibaya sana kuhusu huyo jamaa, na nibkweli huyu ni dishi limeyumba sana
 
Bro, tafadhari, huyu ndugu haaminiki, kwanza hua anaongea akiwa ni mwenye chuki kubwa sana ndani yake, si mnasemaga wengi wape? Basi mitaani na kundi la waTanzania wengi hawamuamini hata chembe

Sema wewe yamkini unajulikana kwao na unaweka mazingira ya faida zako za baadae kwao, lakini unajua wazi kabisa hao ndugu na hasa huyo mmojawapo siyo mtu mwema kwa waTanzania, hii nchi inataka watu wenye uchungu na kufanya kazi yenye matokeo yanayoonekana kwa wananchi wengi kama nyakati za JPM ambaye anapondwa kila Kona, lakini waTanzania wengi tuliona kwa macho.

Hivi nyakati za JPM hata kama kulikopwa pesa lakini zilipoelekezwa watu hatukuona? Nyakati hizi Kuna kinachoeleweka?

waTanzania wengi wanapenda kuona Kwa macho utendaji wa viongozi kama nyakati iliyo pita, na siyo maneno. Na ukweli matokeo yanayoonekana ndiyo yanayoweza kumtetea mtu.

Popote leo akitamkwa JPM watu wanapiga kelele za furaha
 
Ndugu Unadanganya tena bila aibu. Hakuna awamu tokea awamu ya Mkapa hapakuwa na mgao wa umeme. Awamu ya 5 tulipata matatizo hayo.
Bila ya kuongeza vyanzo vya uzalishaji wa umeme kama Gas,Hydro ama Makaa ya Mawe, tutaendelea kupata shida, Bwawa la Nyerere litatuongezea MW2100 tuu, na hizo hazitoshi, Tanzania ina uwezo wa kuzalisha MW 10000 kwa Makaa ya Mawe na Gesi 10000, bila Matatizo, sema shida itakuwa pesa za kujenga

Tanzania Coal

Summary Table

TonsGlobal Rank

Coal Reserves

296,521,39050th in the world

Coal Production

304,23856th in the world

Coal Consumption

327,86187th in the world

Yearly Deficit

-23,623

Coal Imports

84,992

Coal Exports

53,522

Net Imports

31,470

(Data shown is for 2016, the latest year with complete data in all categoreies)
 
Tanzania Coal

Summary Table

TonsGlobal Rank

Coal Reserves

296,521,390 50th in the world

Coal Production

304,238 56th in the world

Coal Consumption

327,861 87th in the world

Yearly Deficit

-23,623

Coal Imports

84,992

Coal Exports

53,522

Net Imports

31,470

(Data shown is for 2016, the latest year with complete data in all categoreies)
 
Shida yenu mnapenda kusikia habari mnazopenda kuzisikia au mnazoaminishana hata kama za uongo. Lakini huo ndio ukweli kulikuwa na upishi wa data kwa kiwango kikubwa kumdanganya mzee kuwa kazi inafanyika. Hizo taarifa za kuongopa idadi ya vijiji vilivyounganishwa umeme hazikutolewa ili kumuharibia mtu bali ni uhalisia.

Je uliwahi kusikia wakati wa JPM kukisainiwa mkataba wa kujenga miundombinu ya kuutoa umeme huko Rufiji kuja kwenye gridi?

Hii ya Trillioni 1.5 kwanini mnapenda kulishana ujinga? Mikataba haiandaliwi kizembe hivyo. Nani hajui kama kulikuwa na breakdown ya supply ya kila kitu duniani wakati wa Corona. Au wewe unaona mambo yalienda sawa tu wakati wa Corona! Ungekuwa unajihusisha na masuala ya biashara za kimataifa ungejua hali ilivyokuwa wakati wa Corona. Everything just paralyzed, sasa utatumiaje hicho kifungu kwa sababu zilizo nje ya uzembe wake? Kama mna risiti kuwa mkandarasi alilipa hicho kiasi na zikaliwa ziletwe hapa. Msiishi kwa kupenda kuyasikia mtakayo, wakati mwingine yapeni masikio yenu taarifa mbadala.
 
Team Kalemani hawatakuelewa mkuu. Umeongea the naked truth.
 
Team Kalemani hawatakuelewa mkuu. Umeongea the naked truth.
Ndio tatizo kubwa walilo nalo. Wanaleta utimu kila sehemu na bahati mbaya wanaamini wao tu ndo watu sahihi na wenye uwezo wa kuwa viongozi wa nchi yetu. Taifa lina watu 60m kila mmoja ana nafasi ya kuwa kiongozi kulingana na utanzania wake, sifa zake, kipaji chake na network yake, ukiwa kiongozi then ukiondolewa just sepa acha wengine wafanya sehemu yao. Hili jambo ni gumu sana kwa waliokuwa viongozi wa awamu ya 5.
 
Wamezoea kudanganyana.
 
Kabisa, kutwa kucha kuwasimanga viongozi wa awamu ya sita. Na wanamchukia kila mtu aliyepata nafasi katika awamu ya sita ambaye si wa circle yao ya awamu iliyopita.
 
Watu wanaamini eti siasa ni uongo uongo unaofanana na ukweli. !!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…