Makampuni ya Tanzania ya usafirishaji yanakwama wapi, maana yanasababisha nchi inaingia kwenye migogoro na majirani wote

Makampuni ya Tanzania ya usafirishaji yanakwama wapi, maana yanasababisha nchi inaingia kwenye migogoro na majirani wote

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Ni dhahiri kwenye hili la corona, Tanzania imeamua kutoendana na mataifa mengine duniani, yenyewe imeamua kupuuza hiki kirusi na kuendelea na maisha kama kawaida, bado wanasongamana kwenye vilabu vya pombe, kwa hili hakuna taifa lenye uhuru wa kuingilia maamuzi yao Watanzania maana wenyewe ni taifa huru. Hivyo hata wakijifia huko watajua wenyewe na kuzikana. Lakini changamoto inaibuka pale kwamba Tanzania sio kisiwa, ni taifa lenye ujirani na mataifa mengine, linachangia hata baadhi ya makabila kwenye mipaka yake.

Kwa hiyo, ina maana kwa namna moja au nyingine lazima raia wake wataingia na kutoka kwenye baadhi ya haya mataifa ambayo yameizunguka, hususan madereva wanaofanya kazi za usafirishaji wa mizigo. Lakini changamoto inakuja pale, kila mojawapo wa haya mataifa wameweka bayana lazima yeyote anayeingia apimwe, hamna njia ya mkato kwa hili., iwe kule SADC au EAC, lazima upimwe, na imetokea kwamba madereva wengi wa Tanzania wanagunduliwa kuwa na kirusi, kitu ambacho kinasababisha aibu kwa uongozi wa Tanzania maana huko kwao walishaaminisha raia wao hamna kitu kama corona.

Viongozi wao waliomba Kenya isiwe ikitaja uraia wa madereva wao kila inapowagundua na kirusi, Kenya ilizingatia hili na kuweka siri, kila ikipima na kumgundua muathirika wa Tanzania, imekua inampokeza kwenye mamlaka husika kimya kimya. Kingine walichokubaliana ni kwamba madereva wawe wanapimwa kwenye taifa wanakotokea na kupewa vyeti, ili ipunguze msongamano pale mpakani, kwamba akiibuka na cheti, hana haja ya kupimwa tena, anapita tu, ila wakakubaliana hata hawa wenye vyeti watakua wanapitiwa mara moja moja (random tests), sio wote ila anaibukiwa mmoja kati ya kama kumi vile na kupimwa.

Hii hapa ndio imeibua changamoto, maana madereva wanaibuka na vyeti, wengi wanaoshtukizwa na kupimwa wanakutwa na kirusi ilhali wana vyeti, sasa hapo inabidi wapimwe wote, hata kama una cheti chenye mihuri ya hadi ikulu, lazima upimwe tena, na ndio wanakutwa na kirusi balaa.

Rais wetu Uhuru ana jukumu la kuhakikisha usalama wa afya ya Wakenya, haijalishi nini wala nini, Tanzania wanune, walipuke, wabwatuke, wang'ake ukweli utabaki pale pale, lazima tuhakikishiwe usalama wetu, wao wafanye yao huko watakavyo, lakini kila anayeng'ang'ania kuvuka mpaka kuja Kenya lazima afuate sheria zetu na masharti.

Sasa sielewi makampuni yao ya usafirishaji yanakwama wapi, mbona wasiajiri madereva pande zote mbili, gari linafika na kupokezwa kwa dereva wa nchi ya pili, wanatupiana funguo, linapulizwa madawa na kila hatua zinachukuliwa. Hapo mbona tutaendelea kuheshimiana tu. Ni bayana Kenya ndiye jirani muhimu sana kwa Tanzania, ukipitia takwimu zao za biashara baina yao na majirani wote, utakuta Kenya ndiko wanauza mazao yao mengi, na ndio maana wao hupiga makelele sana kila pakiibuka mzozo, maana hata ukiangalia leo hii Uganda bado wanataja madereva wa Tanzania wanaogunduliwa na kirusi, ila hautaskia Watanzania wakililia Uganda, wanawaacha waendelee kutaja, ila kwetu wanalia sana.

Njia itafutwe ya kumaliza hii issue kabisa, aidha tuwekeane bandari kavu mipakani kila mtu abaki kwao, au madereva waajiriwe kwenye kila taifa la pili, lakini ukweli utabaki pale pale, lazima upimwe upimwe upimwe, hapiti mtu...kwa cheti au makaratasi ya kariokoo lazima upimwe.
 
Hivi kwanini Magufuli asifunge kabisa mpaka na Kenya angalau kwa mwaka mmoja kama Nyerere

Tafuta mzee yeyote akuelimishe kuhusu umaskini uliokuwepo Tanzania kipindi cha Nyerere na sera zake, wengi walipitia mateso makubwa na mpaka leo hamjapona kabisa, Kenya ndio mshirika mkubwa wa Tanzania likija kwenye suala la biashara baina yenu na mataifa majirani. Siku tukifungiana kabisa mtarudi nyuma mpaka mjihurumie.

Tunachokitegemea kikubwa kutoka kwenu ni mazao ya shambani, kitu ambacho kwa jeuri ya hela zetu tunawaeza tukaagiza kwingine, ila nyie mtakosa soko na kukoma umaskini ukizingatia hata sasa nyie bado maskini wa kutupwa, sasa ukija kuongeza umaskini mwingine wa kukosa soko, ndio mtalia kwa kusaga meno.
 
Hivi kwanini Magufuli asifunge kabisa mpaka na Kenya angalau kwa mwaka mmoja kama Nyerere
Kenya hawawezi kuhimili kufunga mipaka na Tanzania hata kwa wiki moja, sasa hivi uchumi wa Kenya unaitegemea Tanzania kuliko wakati wowote ule.

Tatizo la Kenya ni kukosekana kwa nidhani na utawala wa pamoja. Viongozi wao wakuu wanatoa maelekezo, lakini watendaji wanafanya tofauti. Haiwezikani rais wa nchi anajaribu kusuluhisha, waziri anatoa maelekezo lakini watendaji wanafanya kinyume chake.

Unaweza kuona jinsi ambavyo hata uongozi wa Ikulu ulivyoparagantika, rais na naibu wake hawaelewani kiasi cha rais kupokonya mamlaka ya ofisi wa Naibu wake na kuyaweka katika utendaji wake ili kujaribu kurudisha utii. Imefikia hatua rais na naibu wake kila mtu ana kundi lake na watumishi wake.
 
Tafuta mzee yeyote akuelimishe kuhusu umaskini uliokuwepo Tanzania kipindi cha Nyerere na sera zake, wengi walipitia mateso makubwa na mpaka leo hamjapona kabisa, Kenya ndio mshirika mkubwa wa Tanzania likija kwenye suala la biashara baina yenu na mataifa majirani. Siku tukifungiana kabisa mtarudi nyuma mpaka mjihurumie.

Tunachokitegemea kikubwa kutoka kwenu ni mazao ya shambani, kitu ambacho kwa jeuri ya hela zetu tunawaeza tukaagiza kwingine, ila nyie mtakosa soko na kukoma umaskini ukizingatia hata sasa nyie bado maskini wa kutupwa, sasa ukija kuongeza umaskini mwingine wa kukosa soko, ndio mtalia kwa kusaga meno.
Soko la bidhaa gani ambalo Tanzania hutegemea Kenya ukiacha vyakula ambavyo vinahitajika na nchi Jirani kuliko uwezo wetu wa kuzalisha?. Zimbabwe na Msumbiji pekee wanahitaji mahindi na mchele kuliko uwezo wetu wa kuwatimizia.

Biashara kati ya Kenya na Tanzania jumla haizidi $500M kwa mwaka, Tanzania tunawauzia bidhaa za $270M, wakati biashara na nchi za SADC tunauza bidhaa za $740M, nani kasema Tanzania tunahitaji Kenya.

Kenya haina bidhaa zozote muhimu inayouza kwa Tanzania zaidi ya Sigara, Sabuni, mafuta ya kula na maziwa, bidhaa ambazo zote tunazitengeneza hapa nchini na tunajitoshekeza, tukipungukiwa tunaagiza toka majirani wetu wa kusini.
 
Kenya hawawezi kuhimili kufunga mipaka na Tanzania hata kwa wiki moja, sasa hivi uchumi wa Kenya unaitegemea Tanzania kuliko wakati wowote ule.

Tatizo la Kenya ni kukosekana kwa nidhani na utawala wa pamoja. Viongozi wao wakuu wanatoa maelekezo, lakini watendaji wanafanya tofauti. Haiwezikani rais wa nchi anajaribu kusuluhisha, waziri anatoa maelekezo lakini watendaji wanafanya kinyume chake.

Unaweza kuona jinsi ambavyo hata uongozi wa Ikulu ulivyoparagantika, rais na naibu wake hawaelewani kiasi cha rais kupokonya mamlaka ya ofisi wa Naibu wake na kuyaweka katika utendaji wake ili kujaribu kurudisha utii. Imefikia hatua rais na naibu wake kila mtu ana kundi lake na watumishi wake.
Mpaka wa Kenya na Tanzania ulifungwa kwa mda mrefu kutoka 1977, Kenya ilisonga mbele. Endeleeni na huu ujinga wenu.
 
Kenya hawawezi kuhimili kufunga mipaka na Tanzania hata kwa wiki moja, sasa hivi uchumi wa Kenya unaitegemea Tanzania kuliko wakati wowote ule.

Tatizo la Kenya ni kukosekana kwa nidhani na utawala wa pamoja. Viongozi wao wakuu wanatoa maelekezo, lakini watendaji wanafanya tofauti. Haiwezikani rais wa nchi anajaribu kusuluhisha, waziri anatoa maelekezo lakini watendaji wanafanya kinyume chake.

Unaweza kuona jinsi ambavyo hata uongozi wa Ikulu ulivyoparagantika, rais na naibu wake hawaelewani kiasi cha rais kupokonya mamlaka ya ofisi wa Naibu wake na kuyaweka katika utendaji wake ili kujaribu kurudisha utii. Imefikia hatua rais na naibu wake kila mtu ana kundi lake na watumishi wake.
Na ukabila pia unachangia government kuwa dismantled, Kenya wamekosa moral and order yaani kila mtu kambale

Yule Mike sonko pamoja na kufanya ufisadi wa kutisha lakini bado karudishwa offisini na anaenda mpaka ikulu hahaha kweli kuna nchi zililaanika
 
Soko la bidhaa gani ambalo Tanzania hutegemea Kenya ukiacha vyakula ambavyo vinahitajika na nchi Jirani kuliko uwezo wetu wa kuzalisha?. Zimbabwe na Msumbiji pekee wanahitaji mahindi na mchele kuliko uwezo wetu wa kuwatimizia.

Biashara kati ya Kenya na Tanzania jumla haizidi $500M kwa mwaka, Tanzania tunawauzia bidhaa za $270M, wakati biashara na nchi za SADC tunauza bidhaa za $740M, nani kasema Tanzania tunahitaji Kenya.

Kenya haina bidhaa zozote muhimu inayouza kwa Tanzania zaidi ya Sigara, Sabuni, mafuta ya kula na maziwa, bidhaa ambazo zote tunazitengeneza hapa nchini na tunajitoshekeza, tukipungukiwa tunaagiza toka majirani wetu wa kusini.
Haya , ambieni Magufuli afunge mpaka... Kenya isambaratike.
 
Mbona tulipofunga mpaka wetu ni balozi wenu aliyeanza kujipendekezai na kulialia kuwa sisi ni majirani pia sisi ni ndugu?

Mbona tulipofunga mpaka Rais wenu ndiye aliyepiga simu na sie wetu!!

Dawa yenu ni kuwafungia mpaka na kupandisha bei ya vyakula, akili zitawarudi tuu.

Hakuna cha bandari kavu wala cha bandari bubu, tufunge mipaka yetu yote tutafute masoko mengine, hakuna Mkenya atakayeingia Tz wala Mtz atakayeingia kenya then tutaona nani atakuwa wa kwanza kubeg.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpaka wa Kenya na Tanzania ulifungwa kwa mda mrefu kutoka 1977, Kenya ilisonga mbele.
endeleeni na huu ujinga wenu..
Wakati huo Kenya manufacturing industry ilikua mikononi mwa wazungu by 80%, bidhaa zao zote walizozalisha walikua wakizipeleka kuuzwa Ulaya na mataifa mengine waliyokuwa wakiyatawala kama Zimbabwe na Namibia, sasa hivi uhusiano wenu na nchi hizo haupo tena, Mnategemea kufanya biashara na nchi za Afrika zaidi kuliko kipindi kile, na nchi nyingi zipo kusini mwa Afrika, hamuwezi kuzifikia bila kupitia Tanzania.
 
Wakati huo Kenya manufacturing industry ilikua mikononi mwa wazungu by 80%, bidhaa zao zote walizozalisha walikua wakizipeleka kuuzwa Ulaya na mataifa mengine waliyokuwa wakiyatawala kama Zimbabwe na Namibia, sasa hivi uhusiano wenu na nchi hizo haupo tena, Mnategemea kufanya biashara na nchi za Afrika zaidi kuliko kipindi kile, na nchi nyingi zipo kusini mwa Afrika, hamuwezi kuzifikia bila kupitia Tanzania.
Ha ha Nchi za Africa ni "Tanzania" peke yake?
unadhani nchi zingine za Africa zina ujinga kama huo wenu?

Tanzanians are insecure and full of jealousy. Kenya will move on without you.

Kenya's biggest export markets are

Main export partners
  • 23px-Flag_of_Uganda.svg.png
    Uganda 10.8%
  • 23px-Flag_of_Pakistan.svg.png
    Pakistan 10.6%
  • 23px-Flag_of_the_United_States.svg.png
    United States 8.1%
  • 23px-Flag_of_the_Netherlands.svg.png
    Netherlands 7.3%
  • 23px-Flag_of_the_United_Kingdom.svg.png
    United Kingdom 6.4%


Unaona Tanzania hapo... ???
 
Huu "mchepuko" Kenya unahitaji kupigwa chini kama alivyofanya baba wa taifa ili ukae sawa.

Tunamichepuko mingi tu huyu anataka kujiona kama mke na ilihali ni "mchepuko" tuwapige chini miezi mitatu kwanza tukiona bado tena tuwapige chini mwaka mzima.[/b]
 
haya , ambieni Magufuli afunge mpaka... Kenya isambaratike.
mko na ushenzi wa hali ya juu...
Tatizo lenu wakenya ni kwamba mpo na matatizo ya siasa zenu za ndani "internal politics", nchi yenu imepoteza mwelekeo kutokana na makundi yanayotaka urais wa 2022, sasa matatizo yenu hayo yanasababisha kutokuwepo na utii wa amri zinazotolewa na viongozi wenu.

Haiwezikani Uhuru Kenyatta anajitahidi kutafuta suluhisho la mgogoro wa mpaka wa Kenya na Tanzania, tena kwa kujishusha kwa kumpigia magoti Magufuli, James Macharia anatoa maelekezo kwamba kila dereva atapimwa nchini kwao, watendaji wa chini wanafanya tofauti na amri ya waziri Macharia, huko ni kukosa nidhamu.
 
ha ha Nchi za Africa ni "Tanzania" peke yake?
unadhani nchi zingine za Africa zina ujinga kama huo wenu?

Tanzanians are insecure and full of jealousy. Kenya will move on without you.

Kenya's biggest export markets are

Main export partners


Unaona Tanzania hapo... ???
Jumla ya Exports kwa hizo nchi ulizotaja ni 44% ya total Exports, the remaining 66% zinakwenda katika nchi za Africa, mainly katika nchi za SADC, hamuwezi kuzifikia bila kupitia Tanzania. Bila Tanzania uchumi wa Kenya utasambaratika.
 
Tatizo lenu wakenya ni kwamba mpo na matatizo ya siasa zenu za ndani "internal politics", nchi yenu imepoteza mwelekeo kutokana na makundi yanayotaka urais wa 2022, sasa matatizo yenu hayo yanasababisha kutokuwepo na utii wa amri zinazotolewa na viongozi wenu.

Haiwezikani Uhuru Kenyatta anajitahidi kutafuta suluhisho la mgogoro wa mpaka wa Kenya na Tanzania, tena kwa kujishusha kwa kumpigia magoti Magufuli, James Macharia anatoa maelekezo kwamba kila dereva atapimwa nchini kwao, watendaji wa chini wanafanya tofauti na amri ya waziri Macharia, huko ni kukosa nidhamu.
Siasa zetu tunazifanya tutakavyo,
 
Hakikisheni haziathiri utendaji wa kazi wa Serikali yenu, vinginevyo mtakorofishana na majirani wenu wote. Amri ikitokea kwa rais lazima itekelezwe kama ni amri halali, asitokee mtu kufanya vinginevyo.
In Kenya the govt does not issue vendettas in the public, rarely will you find a minister talking of how they will treat a neighbor state.

things are decided in cabinet meetings and other high level meetings..

So what is done on the ground is what was agreed officially.

Forget about the PR...na hapo ndiyo WaTanzania wanapotoshwa, Magufuli na viongozi wa TZ ni kutupa maneno wafurahishe watu kwenye media.

Rais mzima anasimama kujigamba eti amepigiwa simu na rais mwingine, ili wananchi wamwone ana nguvu?
 
In Kenya the govt does not issue vendettas in the public, rarely will you find a minister talking of how they will treat a neighbor state..
things are decided in cabinet meetings and other high level meetings..

So what is done on the ground is what was agreed officially.

Forget about the PR, na hapo ndiyo WaTanzania wanapotoshwa, Magufuli na viongozi wa TZ ni kutupa maneno wafurahishe watu kwenye media.

Rais mzima anasimama kujigamba eti amepigiwa simu na rais mwingine, ili wananchi wamwone ana nguvu?
Huu ndio ujinga wenu, ninyi ni wapumbavu sana. Juzi mawaziri wa uchukuzi wa Kenya na Tanzania walikutana pale Namanga, wakatoka na maazimio ya pamoja waliyokubaliana katika MoU waliyokubaliana, wakazungumza na vyombo vya habari kuitangazia dunia na wananchi wa hizi nchi mbili yaliye yaliyokubalika ili kumaliza mgogo uliokuwepo, unasema ile ilikua ni PR?, ninyi wakenya ni wapumbavu kuliko maelezo.
 
Back
Top Bottom