KERO Makanisa kupiga kelele usiku kucha na mchana kutwa Kahama/Lugera

KERO Makanisa kupiga kelele usiku kucha na mchana kutwa Kahama/Lugera

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Tatizo ni kwamba hao wafanya Ibada huwa hawapo kanisani na hawaishi mtaa lilipo kanisa lao. Wanachokifanya ni kufungulia tu hizo kelele wao wako makwao mitaa mingine. Afadhali wangekuwepo basi tuwaone wanaabudu, kwani si watachoka tu na kuondoka zao au kupumzika? Lkn badala yake wanamtupa Dj akachafue utulivu wa mtaa wao wanakuja wanaabudu muda mfupi tu lkn kelele za miziki ni kutwa kucha
Na hilo ndilo tatizo kubwa
 
Habari wana JamiiForums, napenda kuiomba Serikali kufuatilia kero na kelele inayosumbua sana maeneo ya (Kahama/Lugera/Mnazi mmoja). Kumekuwa na makanisa mengi maeneo hayo, lakini kuna kanisa ambalo lipo hapo karibu na Mnazi mmoja (la mabati) limekuwa nikero.

Ikifika alasiri wanaweka flash basi inapiga kelele mpaka saa 3 usiku, kisha wanapumzisha SAA moja tu, wanaweka tena saa 4-5 usiku na kupiga kelele usiku kucha mpaka saa mbili asubuhi.

Hii imekuwa ni kero endelevu kwa makanisa haya.

Naiomba Serikali kutoa tamko, watu hawalali kwa kanisa moja tuu kupiga kelele usiku kuchwa, sasa hata kama ni kuabudu sio kwa kupitiliza namna hii.
Hata mimi huwa nashindwa kuwaelewa watu wanaolazimisha tusiohusika tusikilize mahubiri yao.
Kuna kanisa nimewahi kukuta wanapiga kelele yaani linasikika mpaka mtaa wa 4. Kwenda kuwaangalia pale, wapo kama watano hivi na mspika mkuuuuubwa. Yaani spika wanazokuwa nazo sio kwa ajili ya kuhubiriana wao kwa wao bali ni kulazimisha wasiohusika wasikie hata kama wanakereka. Ni mambo ya kishamba sana.

Tunahitaji kubadilika.
Mbona Sir God hahitaji hiyo mispika na mikelele?
 
Habari wana JamiiForums, napenda kuiomba Serikali kufuatilia kero na kelele inayosumbua sana maeneo ya (Kahama/Lugera/Mnazi mmoja). Kumekuwa na makanisa mengi maeneo hayo, lakini kuna kanisa ambalo lipo hapo karibu na Mnazi mmoja (la mabati) limekuwa nikero.

Ikifika alasiri wanaweka flash basi inapiga kelele mpaka saa 3 usiku, kisha wanapumzisha SAA moja tu, wanaweka tena saa 4-5 usiku na kupiga kelele usiku kucha mpaka saa mbili asubuhi.

Hii imekuwa ni kero endelevu kwa makanisa haya.

Naiomba Serikali kutoa tamko, watu hawalali kwa kanisa moja tuu kupiga kelele usiku kuchwa, sasa hata kama ni kuabudu sio kwa kupitiliza namna hii.
Ungeanza kupigia kelele kwanza kwanini barabara ya kupandishia lugela kutokea kibao cha johnson ilichongwa ikaachwa hivo hivo bila kuwekewa moram
 
Ungeanza kupigia kelele kwanza kwanini barabara ya kupandishia lugela kutokea kibao cha johnson ilichongwa ikaachwa hivo hivo bila kuwekewa moram
We nawewe akili zako, kwahio nianze kuongelea barabara nawakati kuna kero katika jamii, kati ya barabara mbovu na makelel yasio na tija kipi ni hoja ya muhimu?
 
Ach
Malalamiko mengine ni ya kipuuzi na yasisikilizwe, huko ni kuingilia uhuru wa kuabudu. Watu wanamuabudu Mungu wao kwa shangwe, vifijo, nderemo na nyimbo we unaona ni kero. Sasa kila mtu akianza kuona kelele na shangwe za mwenzake kuna ambaye atabaki bila kumkera mwenzake? Hata ukienda kujenga porini kuna kelele za milio ya wanyama na ndege watakukera tu. Tujifunze kuanisha zipi kelele ni kero na zipi kelele si kelele. Kelele zingine ni ibada kwa wengine na shangwe za furaha
A ujingaa ungekua wewe masaa yote makelele ungeluzika,mim mkristo lakini spendagi hata maswalaa swalaa maspika ya waislamu natamanigi wasitumie.

Mungu sio mwenye usikuvu hafifu mpaka makelele ndo asikie ni ushamba tu.
 
Ach
A ujingaa ungekua wewe masaa yote makelele ungeluzika,mim mkristo lakini spendagi hata maswalaa swalaa maspika ya waislamu natamanigi wasitumie.

Mungu sio mwenye usikuvu hafifu mpaka makelele ndo asikie ni ushamba tu.
mkristo gani mpuuzi namna hii? Kelele za shangwe kwa wengine ni ibada wewe, unajua ukuta wa yeriko ulianguka kwa kupigiwa kelele? Elewa maana ya falsafa kelele huwa zina maana gani katika mukhtadha wake. Ni kelele tu? Za namna gani? Kenge wewe!
 
Maeneo flani ubungo kuna kanisa wanapiga matowazi yao usiku kucha lkn cha ajabu nalala usingizi mnono kabisa na wapo hatua mbili toka ninapolala.
 
Changamoto iliyopo maeneo ya kujenga nyumba za Ibada yako karibu na makazi ya watu!
Wakristo nao wakianza sasa kulalamika yale mavipaza sauti alfajiri yanayopiga kelele!
 
Hili suala limekua kero sana kote Tanzania si Kahama tu. Makanisa haya hasa ya kilokole ambayo mtaani yanaweza kua hata manne matano yote ya aina moja, kwa mfano TAG. Hawana muda maalumu wa kupiga nyimbo zao. Usiku wanaweza wakaweka flashi inapiga nyimbo wao wakasepa na spika nzito zinaangalia dirishani.
Huku niishiko kila saa kumi alfajir lazma waingie kwenye maombi na wanatumia Maiki. Sielewi kwa nini maombi binafsi wanatumia Mic.
Hiyo inaenda mpaka saa kumi na mbili na nusu asubuhi. Then wanaweka nyimbo zao za kwenye flashi.
Imekua ni lazma wakiamka wao na sisi tuamke maana kelele zile huwezi pata usingi tena.
Kuna haja ya elimu zaidi kutolewa kwa wachungaji hawa maana hata sisi nyimbo wanazopiga tunazo, hatuhitaji kuzisikia kutoka kwao. Maombi na sisi huwa tunafanya lakini hayawasumbui wengine. Kwa nini wao tu.
Pia haya makanisa yakilokole sijui kwa nini yanafunguliwankwa kasi sana, naona kama yanashindana na shule za kata.
Serikali iingilie kati, waabudu wanavyotaka lakini isiwe kero kwa wengine.
Na kama kuna wachungajibwa makanisa hayo humu ndani na wanasoma post hii, wajirekebishe. Pia waache tamaa, wafungue kanisa moja kubwa kwa ajili ya watu wao. Sasa mtaa mmoja kua na makanisa mawili ya aina moja yote yanapiga nyimbo full time as if hawana kazi nyingine, sio poa kabisa.
 
nyie ndio wadini wakubwa, mkiguswa dini yenu mnakuwa very sensitive infiriority complex, pelekeni udini wenu kule mnakoabudu

Kelele za nini! Si Ungepita kimya kimya, waislamu wanakukosesha raha sio?? Pole sana loth,
 
Kuna watu wana mapepo hayataki kusikia kelele za kusifu na kuabudu Mungu, wanajisikia vibaya
 
Back
Top Bottom