Makapuku Forum

Makapuku Forum

Magazeti ya leo November 19, 2023.
Screenshot_20231119_070637_Opera%20Mini.jpg
 
Shahidi wa tatu katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara wa madini, Mussa Hamis inayowakabili maofisa Saba wa Polisi mkoani Mtwara; Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Yustino Mgonja amehitimisha ushahidi wake huku akichambua jinsi baadhi ya washtakiwa wanavyohusika katika tuhuma hizo.

ACP Mgonja ametoa uchambuzi huo wakati akijibu maswali ya dodoso kutoka kwa mawakili wa utetezi na maswali ya ufafanuzi kutoka kwa mwendesha mashtaka, kuhusiana na maswali hayo ya dodoso, akihitimisha ushahidi wake leo jioni baada ya kusimama kizimbani kwa siku tatu.

Wakati wa tukio la mauaji hayo ACP Mgonja alikuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa (RCO) wa Mtwara na kwa sasa ni Kamanda wa Polisi Mkoa (RPC) wa Kipolisi Ilala jijini Dar es Salaam.

Washtakiwa katika kesi hiyo ni aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Mtwara (OC- CID), Mrakibu wa Polisi (SP), Gilbert Sostenes Kalanje; na aliyekuwa Mkuu wa Kituo Kikuu cha Polisi Mtwara (OCS), Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Charles Maurice Onyango.

Screenshot_20231119_072251_Instagram.jpg
 
Wanafunzi 88 waliojiunga na Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli (TMA) mkoani Arusha, wameshindwa kumaliza mafunzo kwa sababu mbalimbali ambapo kati yao, 14 wadaiwa kuyakimbia ambapo mhitimu hutunukiwa “Shahada ya Kijeshi.”

Hayo yamebainishwa katika mahafali ya leo Jumamosi Novemba 18, 2023 ambapo maofisa wanafunzi 575, wametunukiwa Kamisheni na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Samia Suluhu Hassan na hivyo kuvishwa vyeo vya Luteni Usu.

Akitoa taarifa ya mafunzo hayo, Mkuu wa chuo hicho, Brigedia Jenerali Jackson Mwaseba amesema kulikuwa na makundi mawili wa wanafunzi ambapo katika kundi la 04/20 la maofisa wa wanafunzi wa shahada ya Sayansi ya Kijeshi, waliojiunga na chuo walikuwa 73 huku 62 ndiyo walifanikiwa kuhitimu.

Screenshot_20231119_072422_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom