Nasisitiza kitu kimoja ambacho najua kimesha zungumziwa!!! Lengo kuu sio kupata likes, mizigo ya likes ambayo tumepata leo ni matokeo tu ya hali iliyokuwepo, lengo kuu ni usawa kwa JF nzima! MAKAPUKU TUNATAKA USAWA!
Usinitreat low eti kwasababu nimejiunga jana, hakuna uhusiano wa siku ya mtu kujiunga na kutoa mchango wake humu JF.
Arrogance
Selflifting
Ujuaji uliopitiliza
Kujitwika umiriki wa majukwaa
Hayo na mengine mengi ndio tunayotaka yabadirike, na movement hii haitakoma mpaka pale tutakapoona deliberate efforts za Mamods wetu wapeeendwa katika kuyafanyia kazi hayo, tunajua yako ndani ya uwezo wenu na ndio maana tunayabwaga mbele yenu.
Moderator mna nafasi kubwa ya kuibadiri JF na kuwa sehemu nzuri kwa kila mwanamtandao, muifanye JF kiwe ni kisiwa cha elimu na mijadara yenye balance katika yote.
Mnaweza mkaset standards mpya, hamjachelewa, muda ni huu, muda ni sasa.
Makapuku ni jeshi kubwa, hii inamaanisha movement hii si ya kupuuzia bali suruhu yenye tija ni kuyafanyia kazi tunayoyapigia kelele.
Mwishoni lakini si mwisho, kwa niaba ya founder members, napenda kutoa shukrani kwa woooote waliochukua dakika mbili au hata moja, au zaidi kufanikisha vuguvugu hili. Mdogo si dogo😱