Makapuku Forum

Makapuku Forum

Jaji Mkuu wa zamani nchini Liberia, Gloria Musu Scott pamoja na watu wengine watatu wa familia yake, wamehukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kukutwa na hatia ya kutekeleza mauaji.

Tovuti ya RFI imeripoti kuwa, wanne hao walikamatwa na kufunguliwa mashtaka Juni mwaka jana kwa kuhusishwa na kifo cha Charlotte Musu, ambaye ni mpwa wa jaji huyo.

Charlotte aliuawa Februari mwaka jana, katika makazi ya Scott, mjini Brewerville, Kaskazini Magharibi wa Liberia.

Jaji Mkuu huyo wa zamani amekuwa akisisitiza kwamba watu wasiojulikana walivamia makazi yake ambapo walitekeleza mauaji ya mpwa wake.

Baada ya miezi minne ya kusikilizwa kwa kesi hiyo Mahakamani katika mji mkuu wa Monrovia, mwezi uliopita walipatikana na kosa la kumuua Charlotte japo wamekuwa wakikana mashtaka hayo. Hata hivyo, mahakama imesema ilipata ushahidi wa kutosha.

Scott alihudumu katika nafasi ya Jaji Mkuu wa Liberia kati ya mwaka 1997 hadi 2003.

Screenshot_20240111_153205_InstaPro%20.jpg
 
Gavana wa zamani wa Jmbo la New Jersey nchini Marekani, Chris Christie ameghairi kugombea urais kupitia chama cha Republican.

VOA imemnukuu akisema: “Lengo langu halijawahi kuwa sauti tu dhidi ya chuki na mgawanyiko pamoja na ubinafsi wa kile ambacho chama chetu kimekuwa, chini ya Donald Trump,” Christie alisema katika mkutano huko New Hampshire. “Siku zote nimekuwa nikisema kwamba kama sitaon njia ya kufanikisha lengo hilo, hivyo ningejitoa."

“Ni wazi kwangu hivi leo usiku kwamba hakuna njia ya mimi kushinda uteuzi, ndio maana nasitisha kampeni yangu usiku wa leo kuwania nafasi ya rais wa Marekani.”

Haikubainika wazi iwapo Christie atamuunga mkono mmoja wa wapinzani wake, lakini alisikika akimkosoa balozi wa zamani wa Umoja wa Mataifa Nikki Haley, katika mazungumzo ya moja kwa moja yalioandaliwa na kampeni yake kabla ya tukio hilo.

Screenshot_20240111_153311_InstaPro%20.jpg
 
Jamani babu asante sana kumbe huwa unapita huku nimefurahi sana na karibu mnooo [emoji847]
Huwa napita na kusoma kimya kimya almost kila siku, kuna siku nimepita saa 10 alfajiri nikakuta umepost tayari.... unajitahidi sana kwa kweli

Sio wote wanaweza kufanya hicho unachofanya, na ingekuwa tupo jirani ungekunywa soda kwa bili yangu leo 🤗

Very proud of you 👏
 
Back
Top Bottom