Makato ya ushuru wa kuweka au kutoa fedha benki na kutuma na kupokea fedha kielektroniki waanza

Makato ya ushuru wa kuweka au kutoa fedha benki na kutuma na kupokea fedha kielektroniki waanza

Panua ubongo wako kidogo. Tanzania tatizo kubwa siyo fedha ila ni matumizi. Matumizi yasiyo ya lazima na ufisadi ndiyo tanuru linalochoma fedha zetu. Kabla hawajaingia kwenye kumtoza mwananchi kodi mara mbili au hata tatu kwa kitu kile kile ingebidi kwanza wapunguze utitiri wa viongozi wasio na umuhimu wowote na malipo ya anasa. 1. Wabunge wapunguzwe kabisa kwani wengi hawana kazi yoyote. Watu kama ma-DC, maafisa mipango etc waondolewe na ngazi za wilaya na mikoa wabaki viongozi wachache. Mawaziri na makatibu wapunguzwe kabisa. Ununuzi wa magari ufanywe kulingana na hali halisi na siyo kununua magari ya kifahari. Viongozi wasafiri kwenye madaraja ya kawaida na kulala kwenye hotel za kawaida isipokuwa wale viongozi wakuu. Vikao vya kupiga fedha ambavyo Magufuli alikuwa amevipunguza kabisa vimerudi kwa kasi na ufisadi kwa ujumla na pia ukwepaji kodi. Njia za kupata fedha ziko nyingi na siyo kukimbilia kuwakamua wananchi.
Nchi haiendeshwi kwa kwa idadi ya watendaji bali kwa Mipango na Mikakati ya kukuza Maendeleo ya watu na vitu...
Tatizo letu ni kwamba mambo yanaamriwa na wawakilishi wetu(Wabunge) bila sisi kushirikishwa...

In short hakuna uwazi na utoaji wa mawazo kwa wananchi bali kuna maamuzi na maelekezo kutoka kwa Viongozi kwenda kwa wananchi tu...
i.e Top down approach ndo inatuumiza.
 
Nchi haiendeshwi kwa kwa idadi ya watendaji bali kwa Mipango na Mikakati ya kukuza Maendeleo ya watu na vitu...
Tatizo letu ni kwamba mambo yanaamriwa na wawakilishi wetu(Wabunge) bila sisi kushirikishwa...

In short hakuna uwazi na utoaji wa mawazo kwa wananchi bali kuna maamuzi na maelekezo kutoka kwa Viongozi kwenda kwa wananchi tu...
i.e Top down approach ndo inatuumiza.
Yes ni kweli. Ila ili haya uliyosema yafanyike, ni muhimu sana kupunguza mlundikano wa vyeo na viongozi wasio na lazima. Wakipunguzwa fedha nyingi kabisa zitaokolewa na wananchi watashiriki zaidi kwenye maamuzi.
 
Kama mawakala wa Benki nao watakatwa tozo wakati wanatoa pesa Benki kwa ajili ya shughuli zao za uwakala serkali itakuwa imejikata miguu.
 
Yes ni kweli. Ila ili haya uliyosema yafanyike, ni muhimu sana kupunguza mlundikano wa vyeo na viongozi wasio na lazima. Wakipunguzwa fedha nyingi kabisa zitaokolewa na wananchi watashiriki zaidi kwenye maamuzi.
Sawa , lakin tatizo la nchi hii sio vyeo tu kiongozi, Mambo yanafanywa bila uwazi na uwajibikaji,

Tunaweza tukapunguza vyeo, wachache watakaobaki wakajirundikia mali za nchi kuliko kawaida.
Tatizo ni mfumo, kwa mfano je, kuna uwazi katika uwasilishwaji wa Mapato na Matumizi ya Fedha kuanzia ngazi za chini kama vijiji, kata mpaka Serikali kuu?!!

Je, Wananchi wanashirikishwa katika kuibua miradi na kuelezwa ni jinsi gani pesa inatumika?, Je, Matumizi ya fedha yanayofanyika kwa sasa ni rafiki kwa kuleta maendeleo chanya kwa watu wote?

Tatizo ni Mfumo Wa nchi lakin pia na Ufatiliaji wa Wananchi uko chini kwa kuiogopa mamlaka
 
Panua ubongo wako kidogo. Tanzania tatizo kubwa siyo fedha ila ni matumizi. Matumizi yasiyo ya lazima na ufisadi ndiyo tanuru linalochoma fedha zetu. Kabla hawajaingia kwenye kumtoza mwananchi kodi mara mbili au hata tatu kwa kitu kile kile ingebidi kwanza wapunguze utitiri wa viongozi wasio na umuhimu wowote na malipo ya anasa. 1. Wabunge wapunguzwe kabisa kwani wengi hawana kazi yoyote. Watu kama ma-DC, maafisa mipango etc waondolewe na ngazi za wilaya na mikoa wabaki viongozi wachache. Mawaziri na makatibu wapunguzwe kabisa. Ununuzi wa magari ufanywe kulingana na hali halisi na siyo kununua magari ya kifahari. Viongozi wasafiri kwenye madaraja ya kawaida na kulala kwenye hotel za kawaida isipokuwa wale viongozi wakuu. Vikao vya kupiga fedha ambavyo Magufuli alikuwa amevipunguza kabisa vimerudi kwa kasi na ufisadi kwa ujumla na pia ukwepaji kodi. Njia za kupata fedha ziko nyingi na siyo kukimbilia kuwakamua wananchi.
Huu utitiri wa viongozi wasio na tija ndio hawanifanyi nishawishike kulipa kodi. Unakutana utitiri wa viongozi wezi wanatumia fedha watakavyo huku wakiiba ili kufaidisha familia zao, katika mazingira hayo unalipa kodi ili iwe nini?
 
Panua ubongo wako kidogo. Tanzania tatizo kubwa siyo fedha ila ni matumizi. Matumizi yasiyo ya lazima na ufisadi ndiyo tanuru linalochoma fedha zetu. Kabla hawajaingia kwenye kumtoza mwananchi kodi mara mbili au hata tatu kwa kitu kile kile ingebidi kwanza wapunguze utitiri wa viongozi wasio na umuhimu wowote na malipo ya anasa. 1. Wabunge wapunguzwe kabisa kwani wengi hawana kazi yoyote. Watu kama ma-DC, maafisa mipango etc waondolewe na ngazi za wilaya na mikoa wabaki viongozi wachache. Mawaziri na makatibu wapunguzwe kabisa. Ununuzi wa magari ufanywe kulingana na hali halisi na siyo kununua magari ya kifahari. Viongozi wasafiri kwenye madaraja ya kawaida na kulala kwenye hotel za kawaida isipokuwa wale viongozi wakuu. Vikao vya kupiga fedha ambavyo Magufuli alikuwa amevipunguza kabisa vimerudi kwa kasi na ufisadi kwa ujumla na pia ukwepaji kodi. Njia za kupata fedha ziko nyingi na siyo kukimbilia kuwakamua wananchi.
Kwahiyo magufuli wenu alidhibiti ufisadi au? Mazezeta kweli nyie
 
Viwango vidogo, ila sio kwa kipindi hiki ambako kuna mfumuko wa bei Duniani.

Waiahirishe mpaka pale mambo yatakaporudi sawia.
 
Kwahiyo magufuli wenu alidhibiti ufisadi au? Mazezeta kweli nyie
Ni masikitiko kuwa na watu wasiojua kusoma kwa ufahamu. Nionyeshe nimeandika wapi Mafufuli alidhibiti ufisadi. Toa kithibitisho kuwa Magufuli alikuwa wangu! Unajitolea conclusion zako za hisia zinazoongozwa na ubishi wa kibongo-bongo bila facts! Magufuli hakudhibiti ufisadi hata kidogo. Narudia tena, HAKUDHIBITI! Alihamisha tu ufisadi kutoka kwa kundi moja kwenda kwa kundi jingine, na sasa umerudi tena kwenye kundi la mwanzo! Nadhani mapaka hapa umeshajua kati yetu ni nani zezeta!
 
Back
Top Bottom