Ushauri: Msisubiri tena ahadi kutoka kwa yeyote, fanyeni maamuzi magumu ya kuhama hilo eneo.
Maji yana nguvu hasa kwenye njia yake.
Najua uchumi mgumu, kuhama ni njia ya uhakika zaidi
Kwa mtazamo wangu sioni kama hilo ni tatizo la kudumu bali la msimu. Huo mtu si wa kudumu bali wa msimu hivyo maswali ya msingi ni kwa nini wakati si wa mvua serikali isitengeneze mfumo wa kuudhibiti huo mto?
Nimeona maeneo mbali mbali ya nchi mito ya msimu inavyodhibitiwa.Maana kwa mujibu wa picha zilizowekwa, huo mto ni wa msimu kupeleka maji mto Msimbazi. Maana yake wakati si wa masika kuna fursa kubwa sana ya kutengeneza njia hiyo ya maji kuwa salama.
Kama viwanja hivyo vilipimwa na kuidhinishwa na serikali kwa makazi ya watu, kwa hilo serikali inawajibika kwa kugawia wananchi viwanja vya kujenga maeneo hatarishi.
Lakini kama ujenzi ni wa holela kwa kuvamia maeneo kwa kupimiana viwanja kwa hatua za miguu ninyi kwa ninyi, serikali haitabeba mzigo huo, kwani mlijitakia wenyewe na hivyo mnabeba mizigo mliyojibebesha wenyewe.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.