Make Kilimo Great Again: Tunahitaji Movement ya Vijana kurudi Vijijini, maana hii miji inazaa kizazi maskini

Make Kilimo Great Again: Tunahitaji Movement ya Vijana kurudi Vijijini, maana hii miji inazaa kizazi maskini

Rorscharch

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2013
Posts
878
Reaction score
2,014
Kila ninapofikiria taswira ya mkulima, mara nyingi namwona mtu aliyechoka, akiwa na mavazi yaliyochakaa. Hii inatokana na jinsi kilimo kimekuwa kikichukuliwa kama kazi ya watu wa kipato cha chini. Hata matangazo ya pembejeo za kilimo mara nyingi huwahusisha watu wenye lafudhi nzito za vijijini, kama Kisukuma au lugha nyingine za mashambani, na hivyo kudumisha mtazamo hasi kuhusu sekta hii muhimu. Hapa ndipo changamoto kubwa inaanzia.

Asilimia kubwa ya kizazi kilichozaliwa kuanzia mwaka 1998 kimekulia mijini, lakini bila mipango madhubuti ya kiuchumi, kizazi hiki kitakumbana na umaskini uzeeni. Mfumuko wa bei uliojitokeza kwa miongo miwili iliyopita haujaendana na ongezeko la kipato, huku biashara nyingi za mijini zikitoa faida ndogo inayoshindwa kufidia gharama za maisha. Vijana hawa, ambao wanatarajiwa kuwa nguzo za familia zao na kuwahudumia wazazi wao waliozeeka, wanakosa fursa za kujiimarisha kiuchumi.

Suluhisho? KILIMO. Kama taifa, tunayo nafasi kubwa ya kubadilisha mtazamo kuhusu kilimo. Tukianza kwa kuboresha taswira ya sekta ya kilimo, tunaweza kuwahamasisha vijana kuacha kushikilia maisha magumu ya mijini na kuhamia vijijini, ambako kuna fursa kubwa za kiuchumi.

Mfano wa Utekelezaji: Mashirika kama NHC, yakishirikiana na Wizara ya Kilimo, yanaweza kuanzisha mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu vijijini, zikiambatana na miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji. Mpango huu utalenga tabaka la kati mijini ambalo linakabiliwa na changamoto za kipato. Mfano, mtu anayepata mshahara wa shilingi laki tano mjini anaweza kuchukua mkopo wa shilingi milioni tano chini ya masharti maalum, na kutumia fursa hiyo kuwekeza katika kilimo cha umwagiliaji.

Hatua hii haitasaidia tu kupunguza changamoto ya upatikanaji wa nyumba za gharama nafuu, bali pia itafungua milango ya mafanikio kwa kizazi kipya. Ni wakati wa kufufua maana ya methali ya Kiswahili: “Ukitaka mali, utaipata shambani.”

Badala ya kutegemea mapato ya mauzo ya madini—sekta inayotoa ajira kwa watu wachache sana—tunapaswa kuwekeza katika kilimo. Je, unafahamu kuwa parachichi tunalonunua kwa shilingi 1,000 hapa nchini linaweza kuuzwa kwa hadi shilingi 10,000 nchini Marekani? Hii ni fursa kubwa inayosubiri kutumiwa!
 
It's simple make Kilimo profitable watu watalima bila hata kukumbushwa..., Ila kwa mwendo huu mara hatuwazuii kuuza nje mara muuze nje yaani ngojera zisizo mwisho usitegemee kuna mtu atafanya hii betting...

 
Sema siku hizi nimekuwa mvivu wa kuandika maneno mengi sio kama zamani.

Nilikuwa Simanjiro Langai na Monduli Lolkisale..
Matokeo? Funguka usaidie wengine angalau boss. Hapa tunapoongea kuna mtu anafikiria kufanya kilimo Mondoli Lolkisale au atafikiria. Ukieleza uzoefu wako ni elimu kwa jamii hiyo ya watu.
 
Asilimia kubwa ya kizazi kilichozaliwa kuanzia mwaka 1998 kimekulia mijini, lakini bila mipango madhubuti ya kiuchumi, kizazi hiki kitakumbana na umaskini uzeeni. Mfumuko wa bei uliojitokeza kwa miongo miwili iliyopita haujaendana na ongezeko la kipato, huku biashara nyingi za mijini zikitoa faida ndogo inayoshindwa kufidia gharama za maisha. Vijana hawa, ambao wanatarajiwa kuwa nguzo za familia zao na kuwahudumia wazazi wao waliozeeka, wanakosa fursa za kujiimarisha kiuchumi.

Suluhisho? KILIMO. Kama taifa, tunayo nafasi kubwa ya kubadilisha mtazamo kuhusu kilimo. Tukianza kwa kuboresha taswira ya sekta ya kilimo, tunaweza kuwahamasisha vijana kuacha kushikilia maisha magumu ya mijini na kuhamia vijijini, ambako kuna fursa kubwa za kiuchumi.
Nimekupenda sana kwa hii mistari hapa, ubarikiwe, hii inawahusu hata baadhi ya wazee
 
Nazani ni mtazamo wa kijana mwenyewe kuamua kurudi kijijini kulima, kilimo sio rahisi kama tunavyofikiri, mfano me mwenye ndiyo mara yangu ya kwanza kuanza kulima msimu huu ila mpaka sasa zimekatika si chini ya 600k.
 
Nazani ni mtazamo wa kijana mwenyewe kuamua kurudi kijijini kulima, kilimo sio rahisi kama tunavyofikiri, mfano me mwenye ndiyo mara yangu ya kwanza kuanza kulima msimu huu ila mpaka sasa zimekatika si chini ya 600k.
Suluhisho ya hii sintofahamu ni kuhakikisha kilimo kinachofanyika sio cha kubahatisha; kijana anapohamia kijijini baada ya kukopa anakutana na miundombinu yote iliyowekwa kuminimize losses ikiwemo kama system ya umwagiliaji ili kama tatizo mvua basi hilo suala linakuwa sio pasua kichwa tena, kingine ni kijana huyu huyu anakutana na class mpya ya maafisa kilimo ambao wamefundwa kwelikweli mahususi kwa mradi kama huu
 
Suluhisho ya hii sintofahamu ni kuhakikisha kilimo kinachofanyika sio cha kubahatisha; kijana anapohamia kijijini baada ya kukopa anakutana na miundombinu yote iliyowekwa kuminimize losses ikiwemo kama system ya umwagiliaji ili kama tatizo mvua basi hilo suala linakuwa sio pasua kichwa tena, kingine ni kijana huyu huyu anakutana na class mpya ya maafisa kilimo ambao wamefundwa kwelikweli mahususi kwa mradi kama huu
Ni kweli unachosema, swala jingine ambalo nimeliona ni soko linamuangusha sana mkulima.
 
Ni mada nzuri sana na namshukuru mtoa hoja.. shida tunaongozwa na wapu/mbafu, wasiofahamu namna ya kufanya..

Mfano, gharama za uzalishaji ni kubwa sana kwa sababu nishati inayotumika kwenye kilimo ni ya ghali sana(dizeli/umeme) kutokana na kodi za ajabu (punitive)
Nguvu ndogo ya kiuchumi ya wananchi.. husababisha bidhaa zitokanazo na kilimo kuuzwa bei ya chini hivyo kuwakatisha tamaa wakulima.. hapa nataka kusema kwamba, uchumi wa nchi umedumaa vibaya mno tena kwa miaka mingi. Bei za mkulima haziongezeki wakati inflation imeongezeka kupindukia asilimia 120 kwa miaka michache iliyopita.. kwa hiyo kuwekeza kwenye kilimo ni jambo lisilovutia kiuchumi..

Viwanda vya kuchakata mazao ya wakulima havipo.. hapa ni sawa na kuku na yai (vianze viwanda ili vivutie wananchi walime kwa wingi au wananchi walime kwa wingi ndo viwanda vijengwe)..
Kwa ufupi hatuna uongozi wenye vision bali wenye illusion..

Tuendelee kujadili
Shukrani sana
 
Only way hapa ni kukamata vijana waliojaa mijini bila kazi na kuwarudisha makwao, kataza redio za kijinga kupiga bongo fleva la sivyo tutakuwa tunakuza vijana wenye asili ya ushoga wanaopenda kwenda Marekani kupakatwa na P. Diddy na kupakwa mafuta ya watoto mkunduni.
 
kilimo hakina faida kwa sasa (unatumia gharama kubwa kulima unakuja kuuza mazao kwa bei ndogo!) au kutokuvuna kabisa kwa ukosefu wa mvua!!!.
 
Back
Top Bottom