Tetesi: Makinda kumrithi JK Uenyekiti CCM

Tetesi: Makinda kumrithi JK Uenyekiti CCM

Wana CCM tuna imani na Mama maana alifanya kazi iliyo tukuka pale bungeni kipindi cha uongozi wake, Ni mtu asiyependa ufisadi na ndio maana alisimamia kuwajibika kwa waliohusika na ESCROW
 
CCM tunahitaji mtu makini aina ya mama Mhe. Makinda. ili chama kizoe viti vyote vya ubunge 2020 maana tuna uhakika mgombea urais atashinda kwa asilimia zote
 
Let Magufuli lead any attempt to reduce his authority will indicate the worry of some in CCM "kutumbuliwa"
 
Si JK alisema atamkabidhi Magu mwezi Juni, sasa hiki kiherehere kingine kinatoka wapi?? Wanagwaya nini sasa? SI walimpenda wenyewe???
 
Unaelewa utaratibu wa chama chako ccm kwamba mwenyekiti lazima awe rais
Rais lazima awe mwenyekiti si mwenyekiti lazima awe Rais. Ingekuwa hivyo,Makinda angemnyang'anya Magu ofisi kuu
 
Laiti kama CCM ingekuwa na "haya" japo kidogo mngetafakari yaliyotokea mwaka jana!! Kilichotokea sio ndoto wala hadithi, ni Sawa na kengele ya hatari imepigwa kwenu ili mjitafakari!

Rais Magufuli ndio mtu sahihi wa kushika nafasi ya mwenyekiti ndani ya CCM na hii yote ni kama KARMA tu, reformation ya hali ya juu inahitajika ndani ya chama, majigambo na tambo zisizo na kichwa wala miguu hayatawasaidia tena! Siasa za FITNA zimepitwa na wakati, kama mmechoka au MNAMUOGOPA Rais Magufuli ni kheri mbadirike au mumpishe afanye kazi!!

Mnapoteza muda na kuharibu maisha ya watanzania wa sasa na wajao kwa kuwekeana vikwazo vya kipuuzi!!

**Au ile speech aliyotoa kwa wazee wa darisalama imewakata stimu!

"Ifike mahali watanzania tujiulize tumemkosea nini Mungu?"- Rais Magufuli
 
Katiba inamruhusu Magufuli kuhamia Chama chochote cha siasa, yeye na serikali yake.
 
Wahafidhina wanafanya kila watakalo wamdhibiti Magufuli wanashindwa nawashauri mwambieni bibi Makinda hatumtaki
 
Ukiona hivyo huo mpango upo tayari,dah Jk anamuogopa Magufuli kama paka na panya.na huo mpango hautahishia hapo hiyo kuna misaion kubwa mbele.
 
Hongera sana CCM hongera sana Mwenyekiti kwa kuliona hili
 
Kuna wakati wanachama wa ccm walijaribu kutaka kutenganisha URAIS na UENYEKITI wa chama chao na sababu kubwa iliyowafanya wawe na shauku hiyo ni jinsi Mwenyekiti wao ambaye pia alikuwa Rais wa nchi alivyokuwa anakiweka chama hicho rehani kwa wafanyabiashara na wao hawakuwa na jinsi ya kumthibiti, kwani pia alikuwa mkuu wa vyombo muhimu vya dola!! Walidhania kwa kufanya hivyo wangeweza kuondoa conflict of interest iliyokuwepo; hata hivyo Kikwete akiwa madarakani aliweza kuzima jaribio hilo la kutenganisha kofia ya Rais na mwenyekiti kwani alihisi kuwa hilo lilikuwa jaribio la kutaka kudhoofisha uongozi wake.

Hive sasa Kikwete sio Rais tena lakini bado ni mwenyekiti wa ccm. Rais Magufuli ndiye Rais wa nchi ambae kwa siku za mwanzo wa ungozi wake ameonesha nia ya dhati kabisa ya kutaka kuleta maendeleo ya nchi kwa kasi ya peke yake kwa kuhumiza watu wafanye kazi; kupiga vita ufisadi kwa vitendo na kuweza kukusanya kodi ya kutosha. Utendaji wa serikali ya Magufuli ni tofauti kabisa na utendaji wa awamu ya Kikwete hivyo kuweka wazi kabisa kuwa chama na serikali yake huko nyuma vilikuwa havifanyi kazi ipasavyo. Ni uwekaji hadharani huu wa udhaifu wa awamu zilizopita ndiko kunakowatisha Kikwete na wafuasi wake ndani ya chama kuwa iwapo Magufuli ataachiwa kuwa Mweneyekiti wa ccm na pia rais wa nchi kama ilivyozoeleka huko nyuma , anaweza kuwaumbua na kuwathibiti mafisadi wengi waliojificha kwa mgongo wa chama na ndio maana hivi sasa juhudi kubwa zinafanywa kumzuia asiwe mweneyekiti wa ccm . Vinara wakubwa wanaoongoza juhudi hizo ni Mwenyekiti wa ccm wa sasa anayetaka yeye mwenyewe aendelee ili aweze kutumia ngao hiyo ya uenyekiti kujikinga na maovu yake ama sivyo amsimike kibaraka wake achukue nafasi hiyo; na ndio maana wameanza kupima upepo kwa kuyataja majina ya kina Anna Makinda kuwa mmoja wa prospective wenyeviti wa ccm!!

Makinda amekuwa mwanachama wa siku nyingi na kusema kweli amekulia ndani ya ccm; huwezi kumtenganisha na uozo wote ulikuwa unatendeka ndani ya chama hicho. Kumuweka Makinda kama mwenyekiti wa chama hicho utakuwa mwendelezo wa mambo yale yale yaliyokuwa yanafanyika miaka nenda miaka rudi ambayo sasa hivi ndio majipu yanayotubuliwa na Rais Magufuli. Jinsi alivyolelewa na kukuzwa Anna Makinda ndani ya chama ni lazima atajaribu kuyaficha majipu hayo hivyo ili Magufuli afanikiwe kuyatumbua nilazima apewe uenyekiti wa ccm; iwapo itatokea watamyima na kumpa mtu ambaye atajaribu kuyaficha hayo majipu kwa kutumia mgongo wa chama hapo ni lazima kutatokea mgongano ambao kwa vyovyote vile Magufuli ambaye ndio ana dola atashinda, na ili kuepusha mgongano huo ni vyema Rais Magufuli akawa pia mwenyekiti wa ccm!

MKAPA alipoingia tu magogoni aliweza kubadili majenali wate wa majeshi aliweka wapya, KIKWETE Alipoingia pia aliweka wakwake, tena alimludisha mwema alikua intapol na kumteua kua IGP, kwa mifano hiyo hapo inaonyesha jinsi JK na BMW waliingia magogoni wakiwa waziefu wa system hizi muhimu kwenye nchi, lakini JPM hadi leo bado anatumia system za JK, hii inaonyesha kua jpm ameingia magogoni akiwa mgeni, kwahiyo inahitaji muda kidogo hadi awe mwenyeji, utumbuaji wa majipu kwenye ofisi za uma ni tofauti kidogo na utumbuaji kwa wanachama wenzio usipokua makini utajikuta unakua bize na wanachama unasahau serkali na wananchi wako, na kama unakumbuka hata jk mwenyewe walishawahi kumtaka asiwe mwenyekiti wa chama kalbu mala2 hii ni kwasababu ingawa kunasababu zingine lakin kubwa ni BADHI YAO WALIHISI ANATAKA KUUA CHAMA NA HII NI KUTOKANA NA TABIA YAKE YA KUWAACHA HURU SAANA WAPINZANI WAROPOKE, NA KUSEMA WANACHOTAKA. na ngoja huyo muheshimiwa apate uzoefu, akabidhiwe na chama, UPONZANI UJIANDAE KUDODA kama sio kuzimika kabisa MAANA HAWATAPATA UHURU KAMA WALIOKUA WANAUPATA KWA MIAKA 10.
 
Kuna kila dalili kuwa Spika Mstaafu, Mhe. Mama Anne Makinda kumrithi Dr. JK uenyekiti wa chama Tawala, hii inajidhirisha wazi kutokana na uzoefu wa mwanamama huyu shupavu katika medani za kisiasa hapa nchini.

Chanzo kinasema, Katika kuhakikisha hoja jinsia inazingatiwa Chamani ni wakati muafaka UENYEKITI kushikiliwa na Mwana Mama kaka ilivyo kwa Chama rafiki cha AFRICAN NATIONAL CONGRESS (ANC) nchini Afrika kusini kinachoongozwa na mwanamama mahiri Mhe. Baleka Mbete. Kwa CCM Hongera mama yetu mpendwa Mhe. Makinda.

Chama kimekupa heshima iliyotukuka. Kama mwanachama wa CCM nakaribisha mabadiliko haya kwa mikono miwili.

Maana tutakuwa tumefungua ukurasa mpya katika eneo la kuhakikisha Usawa wa kijinsia
Mumeshaanza,wacha huyo bibi alee wajukuu zake,atastaafu mara ngapi?
 
Kwa CCM kila kitu kinawezekana
Mtamuua mama yetu Makinda kwa ugonjwa wa Moyo. Kwanza alishasema hataki tena siasa. Mwacheni mama apumzike. Kama ishu ni Gender mbona CCM ina MIGUBELI mingi tu? Mama Makinda Muungwana sana mwacheni heshma yake ijitunze
 
Back
Top Bottom