Pre GE2025 Arusha: RC Makonda aiagiza TAKUKURU kumhoji Mrisho Gambo upotevu wa Tsh. Milioni 400 zilizochangwa na wadau kwa ajili ya kusaidia bodaboda

Pre GE2025 Arusha: RC Makonda aiagiza TAKUKURU kumhoji Mrisho Gambo upotevu wa Tsh. Milioni 400 zilizochangwa na wadau kwa ajili ya kusaidia bodaboda

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda, ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Arusha kufanya uchunguzi wa upotevu wa kiasi cha fedha shilingi milioni 400 zilizochangwa na wadau kwa ajili ya kusaidia waendesha pikipiki maarufu bodaboda.

Fedha hizo zimepotea na hazijapata majibu kuanzia mwaka 2016, baada ya harambee iliyoongozwa na Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo, wakati akiwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Makonda ameelekeza TAKUKURU kumuhoji Mbunge Gambo kwa kuwa alikuwa ni miongoni mwa waasisi wa ukusanyaji wa fedha hizo.

Maelekezo haya ameyatoa leo kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichowakutanisha wadau mbalimbali na taasisi za serikali.

"Fedha ni ngumu, tulishachangiwa hapa na matajiri shilingi milioni 400, iliwekwa kwenye akaunti, lakini ilipowekwa tukaambiwa kuwa hizi fedha ni za bodaboda na wametuchangia matajiri zetu hapa mjini. Tulipochaguliwa kuwa viongozi wa bodaboda na kwenda kuangalia kwenye akaunti hatukukuta hata shilingi mia moja, sasa tunauliza zimeliwa na nani? Mimi nilipambana hadi TAKUKURU," alisema mmoja wa viongozi wa waendesha bodaboda na kuongeza,

"Mbunge (Gambo) alielekeza shilingi milioni 120 iende kwa akina mama kwenye kikundi kinachoitwa UWAWAJA."

Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda, amesema kwamba, alikumbana na madai ya upotevu wa fedha hizo hata alivyokuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi pindi alipofanya ziara katika mkoa huo.

"Hata nilipokuja hapa niliambiwa kuna hela za boda, sasa hivi mkiniambia kuwa mna milioni 20 ambazo Mheshimiwa Rais amechanga na mnatakiwa milioni 100 ili mpewe pikipiki, najiuliza hizi fedha zinazochangwa sasa zitakuwa salama vipi wakati zile milioni 400 hazijulikani ziko wapi?" aliongeza Makonda.

Kwa sasa, wananchi wanajiuliza ni nani alihusika na upotevu wa fedha hizo, huku matumaini yakielekezwa kwa TAKUKURU kufanya uchunguzi wa haki na kutoa majibu kwa umma.
Pia soma:
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda, ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Arusha kufanya uchunguzi wa upotevu wa kiasi cha fedha shilingi milioni 400 zilizochangwa na wadau kwa ajili ya kusaidia waendesha pikipiki maarufu bodaboda.

Fedha hizo zimepotea na hazijapata majibu kuanzia mwaka 2016, baada ya harambee iliyoongozwa na Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo, wakati akiwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Makonda ameelekeza TAKUKURU kumuhoji Mbunge Gambo kwa kuwa alikuwa ni miongoni mwa waasisi wa ukusanyaji wa fedha hizo.

Maelekezo haya ameyatoa leo kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichowakutanisha wadau mbalimbali na taasisi za serikali.

"Fedha ni ngumu, tulishachangiwa hapa na matajiri shilingi milioni 400, iliwekwa kwenye akaunti, lakini ilipowekwa tukaambiwa kuwa hizi fedha ni za bodaboda na wametuchangia matajiri zetu hapa mjini. Tulipochaguliwa kuwa viongozi wa bodaboda na kwenda kuangalia kwenye akaunti hatukukuta hata shilingi mia moja, sasa tunauliza zimeliwa na nani? Mimi nilipambana hadi TAKUKURU," alisema mmoja wa viongozi wa waendesha bodaboda na kuongeza,

"Mbunge (Gambo) alielekeza shilingi milioni 120 iende kwa akina mama kwenye kikundi kinachoitwa UWAWAJA."

Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda, amesema kwamba, alikumbana na madai ya upotevu wa fedha hizo hata alivyokuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi pindi alipofanya ziara katika mkoa huo.

"Hata nilipokuja hapa niliambiwa kuna hela za boda, sasa hivi mkiniambia kuwa mna milioni 20 ambazo Mheshimiwa Rais amechanga na mnatakiwa milioni 100 ili mpewe pikipiki, najiuliza hizi fedha zinazochangwa sasa zitakuwa salama vipi wakati zile milioni 400 hazijulikani ziko wapi?" aliongeza Makonda.

Kwa sasa, wananchi wanajiuliza ni nani alihusika na upotevu wa fedha hizo, huku matumaini yakielekezwa kwa TAKUKURU kufanya uchunguzi wa haki na kutoa majibu kwa umma.View attachment 3252445
 
Hivi TAKUKURU na Makonda Mkuu wa Mkoa nani ametangulia kufika Arusha? Ni nani anayo pua ya kunusa harufu ya rushwa kambla ya mwingine?
Yaani ikifikia hatua mwalimu anakumbushiwa kuingia darasani kufundisha wanafunzi kila wakati japo ni kazi yake, huyo mwalimu hastahili kuendelea kuwa na sifa ya mwalimu.

TAKUKURU NYIE NI MZIGO KWA TAIFA. Inastahili TAKUKURU ivunjwe inaleta hasara kubwa kuliko faida.
 
Back
Top Bottom