Makonda aamuru kukamatwa mara moja wezi wa millioni 478

Makonda aamuru kukamatwa mara moja wezi wa millioni 478

Tuache siasa kwenye mambo ya msingi..wezi wakamatwe,wafikishwe mahakamani ili watendewe haki yao.
Tutakwama kama taifa kama tunaanza kuangalia nani anakamata mwizi au kusema mkamataji anatuhumiwa kwa wizi mwingine.
 
Kuna watu watapinga kwasababu tu wanamchukia Makonda.
Hapingwi sababu ya kuchukiwa, anapingwa Sababu hana moral authority ya kufanya hayo afanyayo.
Muovu anapotakatisha uovu wake kwa kujifanya unashughulikia waovu hiyo haiwezi kukubalika.
Hicho anachokifanya ni utakatishaji wa tabia zake za hovyo, za kijinai na kitapeli.
 
Itakuwa bwana Mlay,hakuwaona WAZEE..alibugia pekee yake SEHEMU kubwa ya keki
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ametaka kufikishwa mahakamani haraka kwa watumishi wanaodaiwa kuhusika na upotevu wa shilingi Milioni 428 ambazo ni fedha za Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

Makonda ameyasema hayo mkoani Arusha wakati akizungumza na waandishi wa habari na kuongeza kuwa watumishi wanaodaiwa kuhusika na upotevu wa fedha hizo wafikishwe mahakamani kwa kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) tayari imekamilisha uchunguzi wake.

"Vyombo vimeridhika kwa uchunguzi uliofanyika mtu anaingiziwa shilingi Milioni 428 kwenye akaunti yake sio msambazaji wala sio mkandarasi waliomuingizia hizo fedha wanazunguka upande wa pili na kwenda kuzichukua wanagawana na kumuachia fedha katika akaunti yake kama kishika uchumba kwa kazi ya kuficha fedha za wananchi wa hali ya chini". amesema Makonda
HIVI WALE WANAOTAJWA KWA UPOTEVU WA MABILIONI YA FEDHA UPELELEZI WAO UNACHUKUA MIAKA MINGAPI?
 
Kw mpalange panakujusu ngoja nimjulishe mbowe
Kinywa hunena yaujazao moyo. Unaonekana mchezo wa kuzibuliwa mtaro umefanyiwa Sana Hadi umekuwa addicted na unautumja Kama njia ya kupata mlo wa siku!
Katafute mteja mwingine Mimi situmii bali nawahidumia walioathirika Kama wewe ili kuwaponya! Karibu kwa therapy nikuponye!
 
Ni kichaa pekee ataamini kuwa kuna mtu atachukuliwa hatua
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ametaka kufikishwa mahakamani haraka kwa watumishi wanaodaiwa kuhusika na upotevu wa shilingi Milioni 428 ambazo ni fedha za Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

Makonda ameyasema hayo mkoani Arusha wakati akizungumza na waandishi wa habari na kuongeza kuwa watumishi wanaodaiwa kuhusika na upotevu wa fedha hizo wafikishwe mahakamani kwa kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) tayari imekamilisha uchunguzi wake.

"Vyombo vimeridhika kwa uchunguzi uliofanyika mtu anaingiziwa shilingi Milioni 428 kwenye akaunti yake sio msambazaji wala sio mkandarasi waliomuingizia hizo fedha wanazunguka upande wa pili na kwenda kuzichukua wanagawana na kumuachia fedha katika akaunti yake kama kishika uchumba kwa kazi ya kuficha fedha za wananchi wa hali ya chini". amesema Makonda
Duu huo ndiyo urefu wa Kamba yao au wameongezea urefu wa kamba
 
Hapingwi sababu ya kuchukiwa, anapingwa Sababu hana moral authority ya kufanya hayo afanyayo.
Muovu anapotakatisha uovu wake kwa kujifanya unashughulikia waovu hiyo haiwezi kukubalika.
Hicho anachokifanya ni utakatishaji wa tabia zake za hovyo, za kijinai na kitapeli.
Alikutapeli ?kuna aliyetapeliwa amejitokeza kulalamika? Kuna wakati makonda alikuwa rais wa kawaida bila cheo chochote kwanini wasijitokeze?usilishwe habari za vijiweni ,nimesikia makonda kafanya hili unabeba.
 
Back
Top Bottom