Makonda: Atakayenunua makontena yangu atalaaniwa yeye na kizazi chake! Atoa onyo kwa atakayethubutu kununua

Makonda: Atakayenunua makontena yangu atalaaniwa yeye na kizazi chake! Atoa onyo kwa atakayethubutu kununua

Huyu RC si alisema mbele ya waandishi wa habari yale makontena sio yake.Eti Mpango sasa na yeye aonekane wa maana kwenye huu upuuzi.Anyway, ni maigizo na sarakasi zao za kila siku, kuna jipya? Watu wajifunze kuwa ignore
 
Yaani unasema RC wetu ni mpinzani?? Waziri wa shilingi naye alipofungua na kutuonesha vyombo vya mahotelini naye ni mpinzani uchwara?? Naona unatafuta kupopolewa mawe wewe
Punguza muhemko kwanza ili tujadiliane.
 
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda jana alifanya ibada maalum kanisani kwa ajili ya makontena yake yenye samani za shule yanayoshikiliwa na TRA

Katika ibada hiyo Makonda alionya watakao nunua makontena yake watapata laana kali

Pia aliwarushia dongo TRA akisema ni watu wabaya wasio na huruma na kudai kuwa wanamchukia Makonda

"Kama wanachukia Makonda waondoe nembo ya majina yangu kwenye makontena hayo" alisema Makonda

Ni mara nyingine viongozi wa serikali wanasuguana na taasisi za serikali katika kutekeleza majukumu yake huku kiongozi huyo wa mkoa akihisi anaonewa na ni wivu unaofanywa na TRA kisa anafanya vizuri katika mkoa wake

Juzi Paul Makonda alikaririwa na vyombo vya habari kuhusu kupigwa mnada makontena yake,akisema yeye hatishiki na ni mlima hawezi kuyumbishwa na wale wasiomtakia mema katika harakati zake za maendeleo ya Dar es salaam

Kwa hali ilivyo sasa ni dhahiri kuwa Makonda analaumu serikali kumhujumu na hakubaliani na TRA na mambo inayomfanyia
Rc Makonda kama ulijua huo ni msaada kwa nini uliruhusu waandike jina lako? Nadhani hawakuchukii ni sheria ya Kodi inafuatwa. Jina binafsi Kodi inakuhusu wee lipa tuu. Sheria Msumeno
 
Nimeupenda msisitizo aliotoa waziri wa fedha,, anamwambia kamishna wa ushuru wa forodha "naomba sheria ifuate mkondo wake, na asipatikane mtu wa kukutisha,, sisi tunakusanya kodi kwa ajili ya maendeleo ya watanzania hivyo watu wote walipe kodi". Safi sana Mh. Mpango,, ila naona kama umepewa support na Jiwe vinginevyo sasa hivi ungekuwa umesharudi Buhigwe ukiugulia maumivu!!
 
Kumbe simpo tuu. Agiza bidhaa kotoka nje. Tiaraei wakikutokea, unawahi church fasta! Mengine yatajisolve yenyewe
 
Juu in mchezo was kuigiza kutaka kushawishi wananzego kuwa hakuna aliye juu ya sheria. Hata awe bashite(mwana was pekee wa mkuu wa kaya) fix tupu!
 
Ngoja tusubiri tu, once dust has settled down lazima tutasikia tamko toka kwa boss wake. Anamcheki sio kwamba hajui yanayoendelea, na amini usiamini kwa ninavyomjua boss wake hapendagi mambo ya hovyo yatokee na tumeona wote jinsi anavyochukuaga maamuzi ya kutokumwangalia mtu usoni. So, lets wait. "Msema kweli ni mpenzi wa Mungu".
 
Sielewi, kwa nini kiongozi mkuu kama rc ashindwe kujua na kutafsiri sheria ambazo anatakiwa kuzisimamia. Kama anakwepa kodi atawezaje kusimamia wengine wakusanye kodi ya serikali katika eneo lake? Kuna tatizo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
30d163f7-842f-43fe-9c10-8701a9316e15.jpg
3539ac61-4091-4e26-9356-ff33f5dd944c.jpg
da8698eb-44c5-487b-ac08-9b9263e077d7.jpg
7c99bc35-4f7e-4d3e-9067-ea1b52312021.jpg
 
Mkuu ina maana wewe vitu vyako vikipigwa mnada utakaa kimya?
Vitu vyake!?? Mbona wabongo mnakuwa wajinga na wapumbavu kiasi hiki....!?? Inamaana wakati vinaagizwa hata kama alipewa msaada hakujua kuna swala la kodi..!?? Na aliviagiza kwa jina la nani...la mkoa au la kwake...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kwa nini barua ya tra ya February haikujibiwa mapema ili rc ajue kama ombi lake la msamaha wa kodi ya container 20 limekubaliwa au limekataliwa? Waziri atueleze ucheleweshaji wa jibu la barua ya tra ni wa nini ama ajipime.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom